Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 3/1 kur. 7-14
  • Wakusanyikaji Wasifiwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakusanyikaji Wasifiwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Makusanyiko Yetu ya Wilaya—Ushuhuda Wenye Nguvu wa Ile Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Siku Tatu za Kuburudishwa Kiroho
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • “Wajumbe wa Amani ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1996
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 3/1 kur. 7-14

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

Wakusanyikaji Wasifiwa

“ENDELEA kufanya mema, nawe utapata sifa kutokana nayo,” akasema mtume Paulo katika Warumi 13:3, NW. Ndivyo ilivyokuwa kwenye “Ongezeko la Ufalme” mikusanyiko ya 1984 katika Brazili.

Kwa mfano, baada ya mkusanyiko katika João Pessoa, mkurugenzi wa klabu aliiambia hivi halmashauri ya mkusanyiko: “Mimi nawapongeza kwa sababu ya njia nzuri kabisa ambayo kusanyiko lilifanywa na kwa tabia iliyo nzuri sana yenu na ya watoto wenu. Hakuna tengenezo jingine la kidini linaloonyesha mwenendo mwema hivyo. Tunapowakodishia ninyi, hatuna wasiwasi. Milango ya klabu iko wazi wakati wo wote ninyi mnapotaka kutumia vifaa vyetu.”

Maelezo yanayofanana na hayo yalisikiwa kutoka kwa wengine wengi:

◻ “Mimi nimefanya kazi miaka mingi pamoja na makutano makubwa ya watu, lakini ninyi ndio mnaopanga mambo vizuri zaidi kitengenezo, ninyi ndio safi zaidi, na ninyi ndio mnaofanya ushirikiano mwingi zaidi pamoja nasi.”​—Mwenye kusimamia Maracanãzinho Stadium katika Rio de Janeiro.

◻ “Mimi nimevutiwa kweli kweli na chama chenu. Kama Yesu Kristo angekuja sasa, nina hakika dini ambayo angeikubali ni hii yenu.”​—Mzima moto aliyekuwa kazini kwenye mmoja wa mikusanyiko ya Rio de Janeiro.

◻ “Ninyi hamtusumbui sisi [polisi] hata kidogo. Ningetamani kama kila mtu angekuwa kama ninyi. Lingekuwa jambo la kupendeza sana. Wakati mimi ninapopuliza filimbi yangu, najua kwamba mtanitii bila ubishi.”​—Polisi wa kuongoza magari aliyegawiwa kazi kwenye mkusanyiko katika Curitiba.

◻ “Tunataka kutumia nafasi hii tuwapongeze kwa sababu ya utaratibu wenu na nidhamu nzuri ajabu iliyofuatwa kwa kujipendea, nasi tunawatakia mafanikio katika mikutano ya wakati ujao, nayo Manispaa hii itakuwa tayari sikuzote kuwatumikia.”​—Barua iliyopokewa na mwangalizi wa mkusanyiko kutoka afisi ya meya katika Santo André.

◻ “Palikuwa na tofauti kubwa kati ya tabia yenu na ya wengine ambao wametumia vyumba vyetu vya hotelini. Watu wenu walitunza usafi wa vifaa vyote na kuviweka katika utaratibu, na mwenendo wao ulionyesha wanawaheshimu kabisa watu wale wengine.”​—Meneja wa hoteli katika Novo Hamburgo.

◻ “Bila shaka ninyi mnalipwa vizuri.”​—Ndivyo alivyosema mwenye duka la mikate aliyekuwa akipeleka bidhaa zake zikatumiwe na mkusanyiko katika Sorocaba, baada ya kuona jinsi akina ndugu walivyojibidiisha huko. Alipopata habari kwamba wote ni wafanya kazi wa kujitolea, wasiolipwa, alirudia duka lake la mikate na kuleta wafanya kazi wake wote kwenye uwanja huo ili waone bidii na kujitoa kwao!

Mikusanyiko ya Brazili hata ikakaziwa fikira na vyombo vya habari. Gazeti Triburta da Bahia lilitoa ripoti hii: “Wakiwa wameshika Biblia mkononi, wakichunguza mistari iliyomo ili wapate maelezo juu ya sababu ya kuwako kwa jeuri na udanganyifu unaofanywa na wanadamu, Mashahidi hawazungumzi siasa, hawajitii katika mahubiri yanayohusu utetezi wa mambo ya kijamii, nao hawajui hata kidogo kufanya uchaguzi wa moja kwa moja. Jambo linalowatetea katika kuepuka kufanya uchaguzi ni kwamba hata mtawala awe ni nani, hawezi kamwe kuwa na usawaziko, kwa kuwa ni Mungu tu anayeweza kuusimamia ulimwengu kwa ukamilifu. . . . Msingi wa imani yao ni kuja kwa ulimwengu mpya ambao njia ya pekee ya kuupata ni kujifunza Biblia na kubadili tabia mbovu kisha kuwa na moyo uliotakata.”

Bila shaka, Mashahidi wa Yehova hawadai kwamba wao ni watu wakamilifu bali wanaamini kuwa Ufalme wa Mungu utaleta utaratibu mpya ulio mkamilifu. Hata hivyo, wao wamejitahidi kutumia shauri la Biblia lililo katika 1 Petro 2:12, NW: “Dumisheni mwenendo wenu ukiwa mwema miongoni mwa mataifa, ili, katika lile jambo ambalo wanasema kinyume chenu kuwa watenda mabaya, wapate kumtukuza Mungu.”

[Picha katika ukurasa wa 14]

Mwenendo wa Kikristo unamtukuza Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki