Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 3/1 kur. 4-6
  • Usiache Ukweli Ukuponyoke

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Usiache Ukweli Ukuponyoke
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Kupata Maarifa’
  • Kuacha Kiburi
  • Kuyatendesha Maarifa Kazi
  • Wakristo Huabudu kwa Roho na Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kwa Nini Utafute Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • “Inunue Kweli Wala Usiiuze Kamwe”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • “Nitatembea Katika Kweli Yako”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 3/1 kur. 4-6

Usiache Ukweli Ukuponyoke

LABDA Pontio Pilato alitambua kwamba kuukubali ukweli kungemgharimu kitu. Kuwa mfuasi wa Kristo kungalimaanisha kuukubali Umaliki wa Kristo na bila shaka kugeuka haraka aache kuwa mkosefu wa maadili. Hata hivyo, hivi ndivyo alivyosema Sulemani, mwandikaji wa Mithali 23:23: “Inunue kweli, wala usiiuze; naam, hekima, na mafundisho, na ufahamu.”

‘Ati ukweli?’ unauliza kwa dhihaka. Ndiyo, kwa maana hapa Biblia inatusaidia tuthamini kwamba mtu anapata ukweli, hekima na ufahamu kwa kugharimiwa tu! Lakini, ukweli ndiyo bidhaa yenye thamani kubwa zaidi inayoweza kuwazika. Naam, Sulemani alishauri kwamba, “Usiiuze.” Ni kama kwamba alitaka kusema hakuna kitu kinginecho chote kingeweza kulingana nao katika thamani!

‘Lakini ukweli ni nini hasa?’ watu wengi wanauliza, wakirudia ulizo la Pilato. Kwa maoni ya wengi, ‘ukweli’ leo ni wazo lenye kutatiza. Kwa mfano, fikiria aliyoyasema Albert Einstein wakati mmoja: “Ni vigumu hata kushikamanisha maana halisi kwa usemi huu ‘ukweli wa kisayansi.’ Ziko maana nyingi sana za neno ukweli, ziwe zinahusu tukio lililopata mtu binafsi, pendekezo la kihesabu, au nadharia ya sayansi. ‘Ukweli wa kidini’ haueleweki kwangu hata kidogo.” (Ideas and Opinions, cha Albert Einstein) Lakini je, jambo la kwamba Einstein alishindwa kufahamu maana ya ukweli linamaanisha kwamba ni lazima ukuponyoke wewe? Hata kidogo.

Yesu alisema waziwazi hivi: “Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima.” (Yohana 14:6) Ndiyo, ‘ukweli’ huo unamtegemea Kristo Yesu na cheo chake katika makusudi ya Yehova Mungu akiwa ndiye Mtimizaji wa mambo ya unabii, Mkombozi wa wanadamu wenye dhambi, Mfalme aliyewekwa rasmi wa Ufalme wa Mungu, Kuhani Mkuu, na Mfishaji wa waovu. (Warumi 15:8; 1 Timotheo 2:5, 6; Yohana 3:16; Waefeso 1:20-22; Danieli 7:13, 14; Mathayo 6:9, 10; Waebrania 4:14; Ufunuo 19:11-21; 2 Wathesalonike 1:7-9) Ingawa hivyo, mtu anaweza ‘kununuaje’ ukweli huo?

‘Kupata Maarifa’

Mtu anaanza kununua ukweli kwa kufuata maneno ya Yesu katika Yohana 17:3, NW: “Hii ndiyo maana ya uzima wa milele, wapate maarifa ya kukujua wewe, Mungu wa kweli mmoja tu, na ya yeye uliyemtuma, Yesu Kristo.” Hiyo ingekuwa kazi kubwa kweli kweli kama ingempasa mtu kuifanya peke yake. Kule nyuma katika karne ya kwanza, alikuwako “towashi,” au afisa wa mahakamani, aliye Mwethiopia ambaye alijaribu kufanya hivyo. Lakini mwevanjeli Filipo alipomwona towashi akijaribu kujifunza unabii mgumu wa Biblia, yeye alimuuliza, “Je! yamekuelea haya unayosoma?” Naye mwanamume huyo akajibu, “Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza?” (Matendo 8:28-31) Labda wewe unajisikia ivyo hivyo.

Basi Mashahidi wa Yehova wanakupa toleo wajifunze Biblia pamoja nawe katika nyumba yako.a Vipindi hivyo vinafanywa bila malipo. “Mmepata bure, toeni bure,” akasema Yesu. (Mathayo 10:8) Lakini kununua ukweli ‘kutakugharimu’ kwa njia nyingine​—kutataka wakati na jitihada yako. Ingawa hivyo, kumbuka kwamba Yesu Kristo​—ambaye yungali hai na ni mtendaji mbinguni​—anataka kukusaidia ujifunze ukweli. (Linganisha Luka 5:13.) Yeye aliwaahidi wanafunzi wake wa kwanza kwamba roho ya Mungu ingewaongoza ‘iwatie kwenye kweli yote.’ (Yohana 16:13) Maneno hayo yanaweza kufanyiwa urefusho yakuhusu wewe pia. Kwa hiyo usijisikie kwamba kujifunza ukweli kutakuwa jambo gumu mno kwako.

Kujifunza Biblia kwa uzito kumefanywa kuwe rahisi zaidi pia na misaada ya kujifunzia Biblia inayochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Mifano michache tu ya vichwa vya vichapo hivyo vinatia hamu ndani ya wenye kuutafuta ukweli kwa moyo mweupe: Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele, Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya, na Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli, Life​—How Did It Get Here? By Evolution or By Creation?b kutaja vichache tu.

Vichapo hivyo vinaeleza habari za Maandiko bila kukosa shabaha vikitumia maneno yanayoeleweka kwa urahisi, yenye kuvuta uwezo wako wa kufikiri na pia moyo wako. Ukweli uliomo unaonekana kutokana na unyofu wavyo, habari za uchunguzi zilizomo, na mashauri yavyo yenye mafaa. Unapojifunza kweli za Biblia kwa msaada wa vichapo hivyo, utapata kuthamini jambo ambalo hasa Yesu alimaanisha aliposema: “Mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.” (Yohana 8:32) Hapa neno “kweli” linatia ndani ujumla wote wa mafundisho ya Kikristo yanayopatikana katika Neno la Mungu la ukweli ambalo limeandikwa​—Biblia. (2 Timotheo 2:15; Waefeso 1:13) Ingawa hivyo, kwa sababu gani kujifunza ukweli kunampa mtu uhuru mwingi?

Kwa mfano, fikiria jambo la kwamba “hofu ya mauti” imeweka wanadamu ‘maisha yao yote katika hali ya utumwa.’ (Waebrania 2:15) Ndivyo ilivyo ujapokuwa uhakika wa kwamba watu walio wengi wanadai kwamba ni wenye tumaini fulani wasilolifahamu wazi la kuishi katika raha nyingi ya kimbingu baada ya kufa. Lakini, kweli za Biblia zinamweka mtu huru na woga huo usio na afya. Mtu anajifunza kwamba wafu hawataabiki mahali fulani penye moto wa mateso, kwa maana “wafu hawajui neno lo lote.” (Mhubiri 9:5, 10; ona pia Zaburi 146:4 na Mhubiri 3:19, 20.) Pia Biblia inaonyesha kwamba mwanadamu hakurithi tamaa ya kufa na kwenda mbinguni. Bali, Mungu ‘ameiweka milele ndani ya mioyo ya wanadamu’; mtu aliye timamu anatamani kuishi milele!—Mhubiri 3:11, NW; ona pia Warumi 5:12; 6:23.

Tamaa hiyo itatimizwa katika ile ambayo Biblia inaiita “dunia mpya.” (2 Petro 3:13, NW; linganisha Mathayo 6:9, 10.) Yesu alionyesha kwamba wenye kufikia uzima katika “dunia mpya” wangefurahia “Paradiso.” (Luka 23:43, NW) Maandiko mengine yanatusaidia tuthamini kwamba huo utakuwa ulimwengu usio na maumivu wala machozi! (Ufunuo 21:4; Isaya 11:6-9) Ebu fikiria jinsi tumaini hilo lingeweza kugeuza maisha yako wewe! Lakini kwanza ni lazima upate maarifa.

Kuacha Kiburi

Katika Zaburi 25:9 Biblia inasema: “Wenye upole atawaongoza katika hukumu, wenye upole atawafundisha njia yake.” Hakika Mungu hatawapa ukweli watu walio na kiburi na moyo wa kujiinua. “Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.” (1 Petro 5:5) Inaweza kuwa kwamba Pilato angalau alidadisi apate kujua mambo fulani juu ya ukweli. Lakini waandikaji wa kale wanamsimulia Pilato kuwa mwanamume mwenye majivuno mengi. Machoni pa Waroma, Wayahudi walikuwa watu wa kudharaulika wenye dini ya kushangaza, nao walifurahia kuendelea kuwagandamiza! Inaonekana kwamba mambo yaliyomkwaza Pilato asiujue ukweli ni kiburi na makuu ya kisiasa.​—Mithali 16:18.

Vivyo hivyo watu wengi leo wanadadisi wakitaka kujua mambo fulani juu ya ujumbe ulio na Mashahidi wa Yehova. Lakini, huenda wakaona kwamba mara nyingi Mashahidi wa Yehova wanakuwa ni watu wa maisha ya chini, kwamba mahali pao pa mikutano (Majumba ya Ufalme) pasipokuwa na vifaa vya bei-bei hapalingani kamwe na makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yenye mapambo mengi, kwamba ni wachache kati yao walio na elimu ya juu. Lakini angalia inavyosema Biblia katika 1 Wakorintho 1:26-29: “Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa; bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu.”

Basi huenda ukahitaji kukiondoa kiburi chako ndipo uweze kufunzwa na watu hao ‘walio dhalili.’ Lakini je, ni gharama kubwa mno kufanya hivyo kwa ajili ya ukweli?

Kuyatendesha Maarifa Kazi

Kujipatia tu maarifa​—hata ukweli​—hakutoshi. Ndiyo sababu tunahimizwa ‘tununue hekima.’ (Mithali 23:23) Hekima ni kutumia maarifa! Kwa kweli Sulemani alisema kwamba “hekima ndilo jambo kuu zaidi.” (Mithali 4:5-7, NW) Ndiyo, maarifa yana faida gani ikiwa hayatendeshwi kazi? Kwa hiyo baada ya kujifunza njia za Mungu, amri, sheria, vikumbusho, na mashauri yake, jifunze kuyatumia maishani mwako. “Hekima inathibitishwa kuwa adilifu na kazi zake,” akasema Yesu.​—Mathayo 11:19, NW.

Pontio Pilato aliukataa ukweli. Lakini, haikupasi wewe ufanye kosa hilo. Kuuacha ukweli ukuponyoke kwa sababu ya kiburi au kujitakia makuu au kwa sababu ya uovu fulani usiopatana na Maandiko kungekuwa jambo la upumbavu kweli kweli. Uwe kama mtunga zaburi aliyesali akisema, “Unifanye nielewe, ili nipate kuendelea kuishi.” (Zaburi 119:144, NW) Ndiyo, mtu aliye na nia ya kuilipa bei inayohitajiwa ili kupata ukweli na hekima anaweza ‘kuendelea kuishi.’ Kwa maana mtu anayenunua mambo hayo “hakika ataona uzima, naye anapata nia njema kutoka kwa Yehova.”​—Mithali 8:34, 35, NW.

Mwanamume mmoja aliyeanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova alisema hivi: “Ni baraka kusema kwamba ukweli umegeuza maisha zetu.” Unaweza kugeuza yako pia. Kwa hiyo usiuache ukweli ukuponyoke! Itumie nafasi hii isiyo na kifani ununue ukweli, hekima, na ufahamu. Hutajuta kamwe kwamba ulifanya hivyo.

[Maelezo ya Chini]

a Jione huru kuandikia wachapishaji wa gazeti hili ikiwa unatamani funzo la Biblia la jinsi hiyo. Sisi tutafurahia kukupangia mhudumu anayestahili akutembelee nyumbani kwako.

b Vimechapishwa na Sosaiti yetu.

[Picha katika ukurasa wa 4]

Huenda ni kiburi kilichomfanya Pontio Pilato aache ukweli umponyoke

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki