Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 5/1 kur. 10-14
  • Je, Jicho Lako Ni “Rahisi”?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Jicho Lako Ni “Rahisi”?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Taa ya Mwili”
  • Uvutano wa Jicho
  • Kuendeleza Jicho Likiwa “Rahisi,” Si “Ovu”
  • Baraka za Kuliendeleza Jicho Likiwa “Rahisi”
  • Tumia Jicho kwa Hekima
    Amkeni!—2012
  • Ni Nini Maana ya “Jicho kwa Jicho”?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Uwe na Jicho Rahisi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 5/1 kur. 10-14

Je, Jicho Lako Ni “Rahisi”?

“Ikiwa, basi, jicho lako ni rahisi, mwili mzima wako utakuwa mwangavu.”—MATHAYO 6:22, NW.

1. Kwa sababu gani inaweza kusemwa kwamba jicho ni ajabu la uumbaji wenye akili?

KUONA ndiko kwa ujumla kunakohesabiwa kuwa hisia iliyo ya thamani na yenye maana zaidi ya zote—hasa na wale ambao wamekwisha kuipoteza. Wanasayansi wanatuambia kwamba kila nukta, viale vidogo sana vya nuru trilioni kumi vinapita katika mboni za macho yetu. Vinapofikia kioo cha jicho, vinapokewa na chembe milioni mia moja za kurekebishia nuru zenye maumbo kama ya fito na pia. Kwa kuchochewa na nuru, chembe hizo za mishipa ya fahamu zinaanza kuupelekea ubongo viishara vya umeme. Humo, sehemu kubwa ya vichembe vya mishipa vinaanza kazi ya kufasiri habari zilizopokewa na kuamua ni itikio gani linalohitaji kufanywa. Yote hayo yanafanyika kwa muda wa kisehemu kidogo tu cha sekunde. Kwa kweli, jicho ni mfano mmoja wa kustaajabisha mno juu ya ajabu ya uumbaji wenye akili.—Zaburi 139:14.

2. Ni upande gani wa kuona ambao ungali haujafahamika kwa wanasayansi?

2 Ingawa wanasayansi wanajua mengi juu ya kazi za jicho na ubongo, wanajua machache juu ya jinsi na sababu sisi tunakuwa na maitiko yale tunayoonyesha tunapoona vitu. Kwa mfano, haieleweki kwa ukamili ni kwa sababu gani mtu mmoja anapendelea rangi nyekundu badala ya buluu hali mwingine huenda akapendelea buluu badala ya nyekundu, au ni kwa sababu gani rangi mbalimbali zinakuwa na matokeo tofauti tofauti juu yetu. Uhusiano uliopo kati ya kuona na kuitikia ungali haujafahamika. Lakini Yehova, mfanyi wa jicho, na mwanaye aliye mfanyi kazi mwenzi Yesu Kristo, wanajua yale mambo yenye kutatanisha yenye kuhusiana na jicho la kimwili na pia jinsi jicho linavyoongoza vitendo vyetu na maisha zetu.

“Taa ya Mwili”

3. Ni kwa njia gani jicho ndilo “taa ya mwili”?

3 Yesu alisema kwamba “taa ya mwili ni jicho.” (Mathayo 6:22) Taa inatumiwa kuangaza mahali penye giza ili tujue tulipo, jinsi ya kutenda, njia ya kuendea, na kadhalika. Kwa kuingiza nuru ndani ya mwili wetu, macho yetu yanafanya kazi moja na taa. Yanatuwezesha kupashana habari na ulimwengu unaotuzunguka na kuitikia kwa njia yenye akili na ya wazi badala ya kupapasa-papasa, kujikwaa, na labda kujiumiza wenyewe.

4. Tunapatwaje na matokeo ya hali la jicho?

4 Lakini, kadiri ambayo jicho linaweza kutumika likiwa taa ya mwili inategemea sana sana hali ya jicho lenyewe. Kwa sababu hiyo, Yesu aliendelea kusema: “Ikiwa, basi, jicho lako ni rahisi, mwili mzima wako utakuwa mwangavu; lakini ikiwa jicho lako ni ovu, mwili mzima wako utakuwa na giza. Ikiwa kwa hakika nuru iliyo ndani yako ni giza, giza hilo ni kubwa kama nini! ” (Mathayo 6:22, 23, NW ) Kutokana na hilo, tunaweza kuona kwamba jicho linatia uvutano mkubwa sana juu ya mwendo wote wa maisha yetu, kwa mema au kwa mabaya.

Uvutano wa Jicho

5. Ni kwa kadiri gani jicho lilihusika katika kishawishi ambacho Shetani alimfanyia Hawa?

5 Fikiria kisa cha yule mwanamke wa kwanza, Hawa. Kadiri ambayo jicho lilivuta vitendo vyake inaweza kuonekana kutokana na usimulizi wa Biblia juu ya kukutana kwake na Mdanganyi, Shetani Ibilisi. (2 Wakorintho 11:3; 1 Timotheo 2:14) Kwanza, Shetani alidokeza kwamba ‘yeye angefunguliwa macho’ kama tu angepuuza amri ya Mungu na kutwaa ale lile tunda kutokana na “mti wa ujuzi wa mema na mabaya.” Mwanamke huyo aliitikiaje? Biblia inatuambia: “Mwanamke [aliona] ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho.” Yeye aliruhusu macho yake yaendelee kutazama kitu alichokuwa amekatazwa. Hayo yalikuwa matumizi mabaya ya jicho. Matokeo yalikuwa nini? “Basi alitwaa katika matunda yake akala.”—Mwanzo 2:17; 3:4-6.

6. Macho yetu yanavutaje vitendo vyetu?

6 Bila shaka huu haukuwa ndio wakati wa kwanza Hawa alipoona “mti wa ujuzi wa mema na mabaya” au matunda yake. Lakini jambo tofauti lilikuwa likitendeka. Safari hii, mti huo ulionekana kuwa “wapendeza macho” na “ni mti wa kutamanika.” Kwa kawaida kutaka sana kitu na kukitamani ni sifa ambazo si za jicho bali za moyo. Lakini kinachoonwa na jicho kinazidisha ile hali ya kutaka sana na tamaa ya moyoni, sana hivi kwamba kitendo kinaweza kufanywa. Katika kisa cha Hawa, kitendo hicho kilimletea yeye mwenyewe na mumeye Adamu msiba, na pia wazao wao wote waliotazamiwa kuzaliwa, kutia na sisi leo.—Warumi 5:12; Yakobo 1:14, 15.

7. Jicho lilihusikaje katika jitihada ya tatu ya Shetani ya kutaka kumpoteza Yesu, na matokeo yalikuwa nini?

7 Lakini, ili kuonyesha kwamba inawezekana kupinga uvutano wo wote wa kututendesha mabaya ambao waweza kupitia kwenye jicho, tunaweza kuufikiria mfano wa Yesu Kristo. Tena, Mshawishi yule yule Shetani, alihusika. Katika jitihada yake ya tatu ya kumvuta Yesu aache kufanya mapenzi ya Mungu, “Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake.” Angalia kwamba Shetani hakumtolea Yesu kwa maneno tu uweza na utukufu wote wa ulimwengu kwa kubadilishana naye kitendo kimoja cha ibada. Yeye ‘alimwonyesha’ vitu hivyo, akiutumia uvutano wenye nguvu nyingi wa jicho. Hata hivyo, kwa sababu jicho la Yesu halikuvutwa kando na toleo hilo lenye kushawishi bali lilikuwa limekazwa sana juu ya uhusiano wake na baba yake wa kimbingu, Yehova, yeye alifanikiwa kuipinga hila ya Shetani.—Mathayo 4:8-10.

8. Tunaweza kujifunza masomo gani kutokana na mifano ya Hawa na Yesu?

8 Sisi tunaweza kujifunza nini kutokana mifano iliyotangulia? Kwanza, kwamba mambo ambayo tunakazia macho yetu yanaweza kuzitia nguvu tamaa njema au mbaya za moyo wetu. Jambo hilo linaweza kuongoza kwenye kitendo kitakachotuletea sisi wenyewe na wengine ama baraka ama msiba. Pili, ni wazi kwamba jicho ni njia ambayo Shetani anapendelea sana kutumia ili kudaganya anaotaka kudanganya. Kati ya ‘mbinu’ ambazo Shetani anatumia kupoteza wanadamu, njia hii ya kuvutia jicho inaonekana kuwa ndiyo yenye nguvu zaidi ya zote.—2 Wakorintho 2:11, NW.

9. Shetani anatiaje moyo leo watu wawe na “tamaa ya macho”?

9 Leo, Shetani bado anatumia njia ile ile katika mipango yake ya kuvuta watu wote waache kufanya mapenzi ya Mungu. Kwa kutumia umeremeti na marembo ya ulimwengu, Shetani anaendeleza “tamaa ya mwili na tamaa ya macho na kujionyesha kwa mtu mali yake.” (1 Yohana 2:16, NW ) Jambo hilo linaonekana wazi katika mipango ya utangazaji wa bidhaa inayotumiwa na ulimwengu wa kibiashara. Je, si kweli kwamba matangazo ya bidhaa yaliyo na mafanikio makubwa zaidi ni yale yanayotumia uwezo mwingi wa kuvutia macho? Yale maelfu ya matangazo ya bidhaa yenye rangi-rangi na ishara zinazowaka-waka kwa njia ya kupendeza, zile picha zenye rangi nyingi katika magazeti, miwako-wako ya werevu sana katika televisheni—na mabilioni ya shilingi zinazotumiwa kuyatokeza—yote yanashuhudia kwamba kusudi la utangazaji bidhaa ni kusisimua “tamaa ya macho” ya wanunuzi.

10. Kwa kweli ulimwengu wa kibiashara unatia moyo jambo gani?

10 Ingawa mengi ya matangazo hayo hayamwachii mtu nafasi ya kufikiri vizuri, jambo lililo la ujanja zaidi ni kwamba matangazo hayo ya kibiashara hayawi yakitia moyo ununuzi wa bidhaa tu bali pia ufuataji wa mitindo. Mara nyingi sana bidhaa hizo zinaonyeshwa kuwa zikitumiwa na watu walio na mapendeleo makubwa zaidi, walio mashuhuri zaidi, wenye furaha zaidi, na walio warembo zaidi. Ujumbe wa matangazo hayo ni kwamba mnunuzi akitumia bidhaa hiyo, njia yake ya maisha itaonyesha wazi yeye ni mmoja wa watu hao mashuhuri. Watangazaji wanajua kwamba mtu akiisha kukubali namna fulani ya maisha, si vigumu sana kumshawishi akubali bidhaa na vitu vinavyoambatana nayo. Basi, jinsi lilivyo jambo la hekima Wakristo walio wakfu kutii shauri linalopatikana kwenye Waebrania 13:5! Hapo tunasoma hivi: “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo.”

Kuendeleza Jicho Likiwa “Rahisi,” Si “Ovu”

11. Eleza maana ya maneno “rahisi” na “ovu” katika maneno ya Yesu juu ya jicho.

11 Kwa sababu ya kukabiliwa kila siku na namna nyingi hizo za vivuta macho vinavyoondosha fikira kando, tunaweza kuthamini zaidi ni kwa sababu gani Yesu Kristo alituonya kwa upole tuendeleze jicho letu likiwa “rahisi” wala si “ovu.” (Mathayo 6:22, 23 NW ) Hiyo inamaanisha nini? Neno “rahisi” hapa limetafsiriwa kutokana na neno la Kigiriki ha·plousʹ. ambalo kwa msingi linamaanisha umoja wa akili au kujitoa kwa ajili ya kusudi moja. Kwa upande mwingine, neno “ovu” katika kigiriki cha awali ni po·ne·rosʹ nalo linamaanisha kitu kibaya, kisichofaa kitu, kiovu. Hivyo, ‘jicho rahisi’ linakaza fikira juu ya jambo moja tu badala ya kuvutwa kando na kila jambo linaloendelea. Tofauti na hilo, ‘jicho ovu’ ni kigeugeu, lenye ujanja, na lenya kutamani vitu visivyo vyalo, nalo linavutwa kwenye mambo yenye hila ya udanganyifu na ya giza.

12. Rudia na ueleze habari zilizozunguka mazungumzo ya Yesu.

12 Lakini jicho linapaswa kukazwa juu ya nini ili ‘mwili mzima uwe mwangavu’? Kuzifikiria habari zenye kuzunguka maneno hayo kutatusaidia kupata jibu. Katika mistari iliyotangulia, Yesu alikuwa akisema habari za “hazina duniani” na “hazina mbinguni.” Alisema kwamba “hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.” Basi, baada ya kulizungumza jicho, alikazia tena uhitaji wa kuonyesha umoja wa kusudi kwa kusema: “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili,” Mungu na Mali. Katika mistari inayofuata, Yeye alitoa mashauri juu ya maoni ya mtu kuhusu riziki kisha akamalizia kwa onyo hili la upole: “Bali utafuteni kwanza ufalme, na haki yake: na hayo yote mtazidishiwa.”—Mathayo 6:19-34.

13. Inatupasa tukaze jicho letu juu ya nini ili ‘mwili mzima wetu uwe mwangavu’? Kwa sababu gani?

13 Twaelewa nini kutokana na hilo? Basi, hapa Yesu anaongea juu ya miradi katika maisha, akionyesha wazi kwamba ni kazi bure kufuatia vitu vya kimwili na ni baraka kusitawisha upendezi katika mambo ya kiroho. Kwa wazi, anatuambia kwamba kwa kukaza macho yetu juu ya faida za ufalme tu, ‘mwili mzima wetu utakuwa mwangavu.’ Kwa sababu gani? Kwa sababu tukiufanya mradi maishani uwe ni kutenda mapenzi ya Mungu, tutatafuta kuiangaza nuru ya zile habari njema tukufu katika kila upande wa maisha zetu. Si kwamba tunaweza kutazamia tu wakati ujao ulio mwangavu bali pia kukombolewa katika mambo ya kichini-chini yenye giza yanayotokezwa na maisha yenye kufuatia shughuli za kichoyo.—2 Wakorintho 4:1-6.

14. Kukaza jicho juu ya mali za kimwili kunatokezaje “giza”?

14 Mtume Paulo aliyatilia nguvu maneno ya Yesu alipoeleza: “Hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu.” (1 Timotheo 6:9) Hakika maneno hayo ni kweli! Habari zimejawa na hadithi kuhusu maseneta, mameya, mahakimu, wanabenki, wakuu wa mashirika, na watu wengine ambao wamenaswa katika uhalifu wakutumia udanganyifu ambao kulingana na ripoti moja, “unafagia kiasi kisichopungua dola bilioni 200 kila mwaka” katika United States peke yake. ‘Majaribu na tanzi’ ya kuwa tajiri yamefanya watu waliokuwa wakiheshimika hapo kwanza wawe majambazi na wahalifu. Kwa uhakika, tunataka kuepuka ‘kutoswa katika upotevu na uharibifu,’ tusije tukapatwa na lile “giza” ambalo Yesu alionya juu yake.—Ona pia Mithali 23:4, 5.

15, 16. (a) Ni “tamaa ya macho” gani nyingine ambayo ni lazima tuiepuke? (b) Wewe ungelitumiaje shauri lililo katika Mithali 27:20 kuhusu mazungumzo yetu?

15 Lakini, je, ni wale tu wanaoweka jicho lao juu ya kuwa matajiri wanaokabiliwa na hatari ya kutembea katika giza? Hapana, kwa maana “tamaa ya macho” inatia ndani pia mambo mengine mengi. Yakumbuke maneno ya Yesu kwenye Mathayo 5:28: “Kila mtu anayeendelea kutazama mwanamke ili awe na nyege kwa ajili yake amekwisha kufanya uzinzi pamoja naye katika moyo wake.” (NW ) Kwa hakika onyo hilo linaweza kutumiwa pia juu ya mtu kuachilia macho yake yaendelee kuangalia habari ambazo zimebuniwa ili kusisimua au kuamsha nyege na tamaa zisizofaa.

16 Halafu Yesu alisema juu ya mahangaikio kuhusu chakula, vinywaji, na mavazi. (Mathayo 6:25-32) Ingawa vitu hivyo vinahitajiwa, tamaa inayopita kiasi ya kutaka kuwa na vilivyo wa karibuni zaidi, vilivyo vya utajiri mwingi zaidi, vinavyotafutwa na watu wengi zaidi, inaweza kutumikisha akili na moyo wetu. (Warumi 16:18; Wafilipi 3:19) Hata katika tafrija, shughuli tunazofanya wakati wa starehe, michezo, mazoezi, na kadhalika, inatupasa tudumishe usawaziko unaofaa na kujilinda tusije tukanaswa katika mitindo na visisimuaji vya ulimwengu. Katika maeneo haya yote, ingekuwa vizuri tuyazingatie maneno yenye hekima yanayopatikana kwenye Mithali 27:20, New World: “Sheoli na mahali pa uharibifu wenyewe havitosheki; wala “macho ya mwanadamu hayatosheki.” Kwa kweli, tunahitaji kujizoeza kujiweza ili hali yetu ya kiroho isihatirishwe tunapojaribu kuyatosheleza macho yetu.

Baraka za Kuliendeleza Jicho Likiwa “Rahisi”

17. Kuliendeleza jicho likiwa “rahisi” kumesaidiaje wengine wafuatie faida za Ufalme?

17 Wale ambao wameliendeleza jicho lao likiwa “rahisi” na wakalikaza sana juu ya ufalme wa Mungu na ahadi za Mungu wamepokea baraka nyingi kutoka kwa Yehova. Jambo hilo linaonyeshwa vizuri na maono ya watu wa kutoka sehemu zote za ulimwengu katika tabaka zote za maisha. Fikiria mifano hii:

“Nilipokuwa nikitumikia mahali ambapo uhitaji ni mkubwa katika Kolombia, Amerika ya Kusini, nililazimika kuishi kwa kutegemea mapato ya karibu dola 100 kwa mwezi. Nilikuwa nimeanza kupainia, lakini wakati wa siku chache za kwanza za mwezi, nilianguka nikavunja kifundo cha mguu wangu. Gharama za kitiba zilizoletwa na jambo hilo zilikamua pesa zangu, nami singepata pesa zaidi mpaka mwisho wa mwezi. Lakini, wakati wangu ulikuwa umefika wa kutoa mchango wa Jumba la Ufalme, na kama ningezichanga pesa hizo, singekuwa na kitu cha kununua bidhaa za kula juma ambalo lingefuata. Baada ya kufikiria jambo hilo kwa siku chache, nikaamua kwamba ni lazima kodi ya Jumba ilipiwe, kwa hiyo nikaziingiza pesa zangu katika sanduku la mchango. Asubuhi ile ile iliyofuata, nilipokea barua kutoka kwa dada mmoja katika United States aliyekuwa amenitembelea katika Kolombia. Alikuwa ametia ndani ya barua yake pesa fulani za Kolombia alizobakiza wakati wa ziara yake. Kilikuwa ni kiasi kinacholingana barabara na kile nilichokuwa nimetumbukiza sandukuni.”

Katika alasiri yenye joto jingi siku ya Jumanne, mwanamume Ki, anayeendesha kihospitali kimoja katika Taechun, Korea, alialikwa na wafanya kazi wenzake watatu wakatumie alasiri hiyo wakiwa kwenye ufuo wa bahari. Ingawa wazo hilo lilikuwa lenye kushawishi, Ki, alijua kwamba kama angeenda, hangerudi katika wakati unaofaa ahudhurie Funzo la Kitabu la Kundi jioni hiyo. Kwa hiyo akaukataa mwaliko huo. Dakika kadha baadaye, wale watatu walirudishwa kwenye kihospitali—wakiwa wamekufa! Walipatwa na aksidenti ya kifo iliyo mbaya sana ya gari mara tu baada ya kuondoka kwenye kihospitali. Ki, alihuzunika kuhusu aksidenti hiyo lakini akafurahi kwamba aliponya maisha yake kwa sababu ya kushikamana na ile tabia njema aliyokuwa amesitawisha muda wa miaka mingi.—Waebrania 10:24, 25.

18. Watoto wanaweza kufundishwaje waendeleze jicho lao likiwa “rahisi”?

18 Hata watoto wanaweza kufundishwa waendelee kukaza macho yao juu ya faida za Ufalme, kama inavyoonyeshwa na jambo lililoonwa lifuatalo:

“Tulipopashwa habari na wageni wawili kwamba akina ndugu katika makundi matatu ya Ufilipino walipaswa kuchanga dola 1,000 katika kila kundi—ambacho ni kiasi kikubwa sana kwao—ili wajenge upya Jumba la Ufalme lao lililoteketezwa na moto, mume wangu na mimi tuliamua kutoa mchango. Namna gani watoto wetu wanne, wenye umri wa kuanzia miaka sita mpaka miezi minne? Kila juma mume wangu alipolipwa mshahara alikuwa akinunulia kila mtoto dola ya fedha. Mume wangu alizigawa sarafu hizo ili kila mtoto aweze kuona alikuwa na ngapi. Sisi tuliwatajia watoto pia baadhi ya vitu walivyokuwa wamekusudia mioyoni kuvinunua kwa pesa hizo. Lakini siku zote jibu lilikuwa lile lile—walitaka kuwapa akina ndugu pesa hizo.” Watoto walipeleka pia barua fupi pamoja na dola zao 99. Upendo na ukarimu wao uliwagusa sana akina ndugu katika Ufilipino hivi kwamba wengi wao wakatoa machozi barua hiyo iliposomwa.

19. Tunaweza kuhakikishiwa kupata wakati ujao ulio mwangavu tukiendelea kukaza macho yetu juu ya nini?

19 “Macho yako yatazame mbele, na kope zako zitazame mbele yako sawasawa.” (Mithali 4:25) Ni jambo la hekima kama nini tutii shauri hilo wala tusiruhusu macho yetu yatangetange au kuvutwa kando! “Angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima,” Paulo akasihi, “Mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.” Alihimiza hivi pia: Mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya [Yehova].” (Waefeso 5:15-17) Kwa kufanya hivyo, tunaweza kuwa na uhakika wa kwamba tutafanikiwa katika kuliendeleza jicho letu likiwa “rahisi” na tunaweza kutazamia kwa tumaini thabiti wakati ujao ulio mwangavu—uzima wa milele katika Utaratibu Mpya wa Mungu ulioahidiwa.—Linganisha 2 Wakorintho 4:17, 18.

Wewe Unaweza Kueleza?

◻ Ni kwa njia gani jicho ndilo “taa ya mwili”?

◻ Macho yetu yanavutaje vitendo vyetu, kama ilivyoonyeshwa na Hawa na Yesu?

◻ Ni kwa njia zipi Shetani anatumia “tamaa ya macho” leo?

◻ Ni lazima tufanye nini ili kuliendeleza jicho letu likiwa“rahisi”?

◻ Inatupasa tukaze macho yetu juu ya nini sasa?

[Picha katika ukurasa wa 12]

Jambo tunalokazia macho yetu linaweza kuizidisha tamaa ya moyo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki