Yubile ya Kikristo Yafikia Upeo Katika Mileani
1. Wayahudi katika Jamhuri ya Israeli hawajafanya jitihada ya kuanzisha tena kitu gani, na kwa sababu gani?
HATA katika Jamhuri ya Israeli (iliyoanzishwa katika 1948), Wayahudi walio wengi wanaojifikiria kuwa wako chini ya Torati la Musa hawajaanzisha tena kusherehekea mwaka wa Yubile. Na kungekuwa na vitatanishi vingi kama wangejaribu. Matatizo mengi sana ya uchumi yangetokea, kwa maana haki za umaskini zinahusika. Jamhuri ya Israeli siyo yenye nchi yote iliyokaliwa na makabila yale 12 ya kale. Pia hakuna hekalu lenye kuhani mkuu wa kabila la Lawi, kwa kuwa vitambulishi vya makabila ya watu vilipotezwa.
2. Ni jinsi gani Wakristo wengine tayari wamekwisha kuanza kusherehekea Yubile iliyotolewa na kivuli ile ile ya Israeli wa kale?
2 Ingawa hivyo, jambo hilo linatuacha sisi wapi kwa habari ya baraka za sherehe ya Yubile? Tunakumbuka kwamba Yubile ya kale ilikuwa mwaka wa uhuru wenye shangwe—Waisraeli waliokuwa wamejiuza kuingia utumwani waliwekwa huru na wakarudishiwa mashamba yao ya urithi. (Walawi 25:8-54) Katika makala iliyotangulia tuliona kwamba mpango huo ulikoma pamoja na agano la torati la Musa katika 33 W.K. (Warumi 7:4, 6; 10:4) Ndipo lilipoanzishwa kutenda agano jipya ambalo kwalo Mungu angeweza kusamehe dhambi za waamini, awapake mafuta kwa roho takatifu, na kuwachukua wawe wana wa kulelewa ambao wangepelekwa mbinguni. (Waebrania 10:15-18) Hata hivyo wale wenye kufaidika kwa njia hiyo kutokana na mpango huo wa agano jipya ni “kundi dogo” la watu 144,000 ‘ambao wamenunuliwa katika dunia.’ Kwa hiyo mamilioni ya Wakristo wengine washikamanifu wanaweza kupataje ukombozi ambao Yubile ilikuwa kivuli chao? —Luka 12:32; Ufunuo 14:1-4.
Dhabihu kwa Ajili ya Wote!
3. Dhabihu ya Yesu ni yenye matokeo na udumifu wa kadiri gani?
3 Katika nyakati zilizotangulia Ukristo faida za Siku ya Upatanisho ya kila mwaka zilidumu kwa mwaka mmoja tu. Faida za dhabihu ya ukombozi wa Bwana Yesu Kristo ni za kuendelea, za daima. Hivyo Yesu, Kuhani Mkuu mfananishwa, si lazima awe mwanadamu tena, na ajidhabihu, ndipo arudi mbinguni, akaonyeshe thamani ya dhabihu hiyo mwaka baada ya mwaka katika Patakatifu Zaidi Sana pa Yehova Mungu. Ni kama vile Maandiko yanavyosema: “Kristo, sasa kwa kuwa yeye ameinuliwa kutoka kwa wafu, hafi tena; kifo si bwana mkubwa juu yake tena.”—Warumi 6:9; Waebrania 9:28, NW.
4, 5. (a) Ni nini yamekuwa matokeo ya matumizi ya dhabihu ya Yesu kuanzia Pentekoste 33 W.K.? (b) Tuna kionyesho gani cha kwamba dhabihu yake itatumiwa kwa upana zaidi?.
4 Kwa sababu hiyo, katika miaka iliyofuata Pentekoste ya 33 W.K., waamini wameanza kusherehekea Yubile ya Kikristo wakiisha kuwa wafuasi waliozaliwa kwa roho wa Bwana Yesu aliyetukuzwa. Wakiisha ‘kuwekwa huru watoke katika sheria ya dhambi na kifo,’ wao wamefurahia uhuru wenye kuwatia nguvu. (Warumi 8:1, 2, NW) Wameutangaza pia ujumbe wa Kikristo ili watu wengine zaidi waweze kusamehewa dhambi zao, wapakwe mafuta, na wawe wana wa kiroho v Mungu. Ingawa hivyo, hiyo inamaanisha kwamba ikiwa mtu si wa kikundi hicho ambacho ni cha watu 144,000 tu, hawezi kupata ukombozi wenye kufurahisha sasa?
5 Yaliyo ya maana katika habari hii ni m, neno ya mtume Paulo kwenye Warumi 8:19-21: “Viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu. Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili [vikiwa vyenye dhambi na visivyoweza kuondolea mbali dhambi kabisa].” Ndipo Paulo alipokazia kwamba kuna “tumaini; kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru w utukufu wa watoto wa Mungu.” Basi, uhuru huo si kwa wale tu wanaokuwa “watoto wa Mungu” mbinguni. Maneno yaliyozoeleka kwenye Yohana 3:16 yanathibitisha jambo hilo. Na, kama ilivyotajwa, mtume Yohana mpakwa-mafuta alisema kwamba Kristo alikufa “kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.’—1 Yohana 2:2.
1919—Ukombozi wa Kwanza-kwanza
6, 7. Tangu 1919 ni ukombozi wa namna gani umetangazwa, na kwa sababu gani hasa tangu wakati huo?
6 Katika nyakati za kisasa wapakwa-mafuta wanaosherehekea Yubile ya Kikristo wamekuwa wakitangaza habari njema zinazokomboa, hasa tangu 1919 W.K. ‘Kwa sababu gani kuanzia wakati huo?’ huenda wewe uke taka kujua ikiwa umezaliwa majuzi zaidi. Acheni tuone, huku tukizingatia kwamba jambo hili linahusu kufurahia kwako ukombozi.
7 Kwa miongo ya miaka kabla ya tarehe hiyo wapakwa-mafuta wa Yehova walichapisha kweli za Kibiblia, kama vile katika mfululizo unaojulikana sana wa vichapo Studies in the Scriptures (1886-1917). Waligawa pia kati ya watu vijitabu na trakti nyingi zenye kuwaarifu mambo. Wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza upinzani ulitokea, kujaribu na kupepeta, na kupungua mwendo kwa utendaji wao mbalimbali. Lakini katika 1919, mabaki wapakwa-mafuta walijitokeza wakiwa na bidii iliyofanywa upya ili kutangaza kweli za Biblia. Kama vile Yesu angeweza kusema katika 30 W.K. kwamba yeye alipakwa mafuta awahubirie ‘wafungwa kufunguliwa kwao na vipofu kupata kuona tena,’ ndivyo wapakwa-mafuta hao wa kisasa wangeweza kufanya. Baada ya mkusanyiko wa kusisimua katika Septemba 1-7, 1919,a wao walisonga mbele kwa nguvu nyingi wakizitangaza kweli zilizokomboa watu wasiohesabika.—Luka 4:18.
8, 9. Ni katika maana gani watu wengi wamewekwa huru, na ni misaada gani imetumiwa katika kutangaza ukombozi huo?
8 Kwa mfano, fikiria msaada ule wa kujifunzia Biblia The Harp of God (1921), uliotokeza kweli za muhimu kama kwamba zilikuwa nyuzi kumi katika kinubi. Kitabu hicho kilikiri kwamba “watu wengi wameogopeshwa wasijifunze Biblia” na fundisho lile la kwamba “adhabu kwa waovu . . . ni mateso ya milele au kuteswa-teswa katika mahali panapowaka moto na kiberiti usiozimika.” Wasomaji wa nakala zile karibu 6,000,000 za kitabu hicho walijifunza kwamba fundisho hilo ‘halingeweza kuwa kweli kwa angalau sababu nne mbalimbali na zenye kutokeza sana: (1) kwa sababu halipatani na kufikiri kuzuri; (2) kwa sababu linahitilafiana sana na haki; (3) kwa sababu ni kinyume cha kanuni ya upendo; na (4) kwa sababu lote kabisa halipatani na maandiko.” Unaweza kuwazia jinsi jambo hilo lilivyokomboa watu waliokuwa wamekua katika woga wa mateso ya milele katika mahali penye moto au ya maumivu makali sana katika purgatori!
9 Ndiyo, mahubiri yenye bidii ya ukweli wa Biblia yaliyofanywa na wapakwa-mafuta hao yaliwaweka huru kila upande wa dunia watu waliokuwa wamefanywa kuwa watumwa wa mafundisho ya uwongo, mambo ya ushirikina, na mazoea yasiyo ya kimaandiko (kama vile kuabudu wazee wa ukoo waliokufa, kuogopa mizuka au roho waovu, na kunyonywa kifedha na viongozi wa kidini). Vichwa vyenyewe vya misaada fulani ya kujifunza Biblia vinaonyesha jinsi ilivyokuwa na nguvu nyingi za kuvuta mamilioni ya watu wakombolewe.b Hivyo maneno ya Yesu yamethibitika kuwa kweli, wakati aliposema kwamba wafuasi wake ‘wangefanya kazi kubwa kuliko’ alizofanya yeye. (Yohana 14:12) Kwa kulinganishwa na kazi ile ya utangulizi ya ukombozi wa kiroho ambayo Yesu alifanya kwa kuhubiri ‘kufunguliwa kwa wafungwa,’ watumishi wa kisasa wa Mungu wamefanya kiasi kikubwa zaidi—wakifikia mamilioni mengi ya watu kila upande wa dunia.
10. Kwa sababu gani tunaweza kutazamia kwamba ukombozi wa ziada na ulio mkubwa zaidi utaonwa na watu?
10 Ijapokuwa hivyo, kumbuka kwamba katika karne ya kwanza ukomboaji mwingine zaidi ulianza katika Pentekoste 33 W.K. Huko Yubile ya Kikristo ilianza kwa ajili ya “kundi dogo” ambao wangesamehewa dhambi zao, na jambo hilo liwaongoze kuwa “wana wa Mungu” mbinguni. Namna gani katika wakati wetu? Je! mamilioni ya Wakristo wengine wenye kujitoa wangefunguliwa watoke katika kifungo cha dhambi na hivyo washerehekee Yubile kuu? Ndiyo, na mtume Petro alionyesha hivyo aliposema juu ya “zamani za kufanya upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu [wa kale].”—Matendo 3:21.
Yubile kwa Mamilioni
11. Walawi sura ya 25 inadokezaje kwamba tunaweza kutafuta ukombozi unaopanuka kufikia wengi zaidi ya Israeli wa kiroho tu?
11 Inastahili kuangaliwa kwamba katika Walawi sura ya 25, Waisraeli walikumbushwa mara mbili kwamba kwa maoni ya Yehova wao walikuwa “watumwa” wake aliokuwa amewakomboa kutoka Misri. (Mistari 42 na 55, NW) Sura hiyo ya Yubile inataja pia “walowezi” na ‘wakaaji wa kigeni kati yao.’ Watu hao leo wana ulinganifu na “mkutano mkubwa” wanaoshiriki pamoja na Waisraeli wa kiroho katika kuzitangaza habari njema za Kikristo.
12. Tangu 1935 ni tukio gani lenye kufurahisha ambalo limekuwa likiendelea?
12 Tangu 1935 “mchungaji mwema” Yesu Kristo amewaingiza wale wanaotaka kuwa: “kondoo wengine” ndani ya ushirika wenye utendaji pamoja na mabaki wapakwa-mafuta Ilikuwa lazima ‘awalete’ hao, nao walipaswa kuwa “kundi moja” chini ya “mchungaji mmoja.” (Yohana 10:16) Sasa “kondoo wengine” ni mamilioni. Ikiwa wewe ni wa umati huo wenye furaha, tayari unahesabiwa kuwa mwadilifu ukiwa rafiki ya Mungu. na ukiwa sehemu ya uumbaji wa kibinadamu unaotazamia ‘kuwekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu’ wakati wa “zamani [zinazokuja] za kufanywa upya vitu vyote” duniani. Hilo si tumaini lililowekwa pasipofaa.—Warumi 8:19-21; Matendo 3:20, 21.
13. Ni baraka gani hasa tunayopasa kuangalia kuwa inatukia baada ya dhiki kubwa?
13 Baada ya mtume Yohana kuona 144,001 wanaofurahia Yubile ya Kikristo ambao tu maini lao ni kuwa mbinguni, alieleza juu ya “mkutano mkubwa,” akisema: “Hao ndio ambao wanatoka katika dhiki kubwa, na wao wamefua kanzu zao na kuzifanya nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo. Hiyo ndiyo sababu wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu nao wanamtolea utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake.”—Ufunuo 7:14, 15, NW.
14, 15. Kwa sababu gani wale wa “mkutano mkubwa” wana sababu ya pekee kufurahi sana sasa?
14 Hata sasa, kabla ya ile dhiki kubwa, hao wanajizoeza imani katika damu iliyomwagwa ya Kristo, na hivyo wanafaidika na kifo chake cha dhabihu. Wanafurahi sana pia juu ya kukombolewa kutoka katika Babuloni Mkuu, juu ya kuwa na dhamiri njema mbele za Yehova Mungu, na katika pendeleo lao la kushiriki katika utimizo wa Mathayo 24:14 kwa kuzihubiri habari njema za Ufalme kabla mwisho haujaja.
15 Ijapokuwa hivyo, namna gani taraja la mkutano mkubwa la kukombolewa kutoka katika dhambi na kutokukamilika walikozaliwa nako? Je! wakati huo uko karibu? Kuna sababu nzuri ya kushikilia kwamba bado wangali pamoja nasi wengine wa kizazi cha wanadamu ambacho Yesu Kristo alitabiri hakingepita mpaka mambo yote yaliyotabiriwa yatimizwe. (Mathayo 24:34) Kwa sababu hiyo, mwisho mkuu wa “umalizio wa mfumo wa mambo” bila shaka uko karibu sana.—Mathayo 24:3.
Vipeo vya Yubile ya Kikristo
16. Sisi tunasimama wapi katika kutimilizwa kwa kusudi la Mungu, na ni jambo gani lililo mbele?
16 “Vita ya siku ile kuu ya Mungu mwenyezi” inakuja mbio mbio, na mabaki ya “kundi dogo,” na pia ule “mkutano—mkubwa” wa waandamani waaminifu na washikamanifu watashika ukamilifu kuelekea Yehova Mungu na wanatazamia kupata ulinzi wa kimungu. Wao wanatazamia kwa hamu nyingi Yehova ashinde kabisa majeshi yote ya adui, ili yeye Kuu ya Ulimwengu Wote. Hicho kitakuwa kipeo cha ajabu kitakachofanya wafurahie uhuru wa Kikristo!—Ufunuo 16:14; 19:19-21; Habakuki 2:3.
17. Ni jinsi gani bado mamilioni ya watu watapokea ukombozi katika Yubile kuu na yenye utukufu?
17 Ndipo utakapofuata juu ya dunia utawala wa Mfalme Yesu Kristo aliye mshindi, huku enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote ikiwa imethibitishwa kwa mara nyingine tena, na Yesu Kristo akiwa ndiye mwenye uongozaji kamili wa dunia akiwa Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. Ndipo yeye atakapotumia moja kwa moja ustahili wa dhabihu yake kwa mamilioni ya wanadamu, kutia ndani watakaofufuliwa, wanaojizoeza imani na wanaokubali kwa nia msamaha wa dhambi ambao Mungu ataandaa kupitia Kristo. Ushuhuda wa jambo hilo utaonyeshwa kwa Mungu kufuta “kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena.” (Ufunuo 21:3, 4) Ikiwa huo si ukomboaji wa kweli, kuna mwingine gani?
18. Kwa njia inayoweza kulinganishwa na jambo moja la Yubile ya kale, ni nini litakalotukia kuhusu dunia katika mfumo mpya?
18 Zaidi ya hivyo, dunia haitaongozwa tena, ichafuliwe tena, wala iharibiwe tena na watu mmoja mmoja wenye pupa, mashirika, na serikali za kibinadamu. (Ufunuo 11:18) Bali, itarudishwa kwa waabudu wa kweli. Wao watakabidhiwa ile kazi yenye kufurahisha ya kushiriki katika utimizo halisi wa unabii wa Isaya: “Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake. Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine, . . . Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na [Yehova].” (Isaya 65:21-25) Kufikia mwisho wa Utawala wa Mileani vidalili vyote vya dhambi na kutokamilika kulikorithiwa vitakuwa vimefutiliwa mbali na washikamanifu wa Mungu duniani watakuwa wakisherehekea upeo kamili utakaokuwa kikomo cha Yubile. Kwa hiyo ukombozi uliotolewa kivuli na ile Yubile utakuwa umetimilika.—Waefeso 1:10, NW.
Baada ya Upeo wa Kimileani wa Yubile
19, 20. Shetani na mashetani watajaribuje kukatiza baraka zenye kutokana na Yubile ya Mileani, lakini matokeo yatakuwa nini?
19 Andiko la Ufunuo 20:1-3 linatabiri kwamba Shetani Ibilisi, mtawala wa vikosi vya mashetani, atakuwa ameondoshwa uwanjani kwa muda wa ile miaka elfu ya utawala wa Kristo juu ya wanadamu. Mwishoni mwa ile Mileani, wakati Ibilisi na mashetani wake watakaporuhusiwa kwa muda mfupi wajitokeze, roho hao waovu wataiona dunia, si ikiwa katika hali walimoiacha ikiwa, bali ikiwa paradiso ya duniani pote yenye uzuri usioelezeka. Wataiona dunia ikiwa imekaliwa na ule “mkutano mkubwa” wenye uaminifu na mabilioni ya wafu wa kibinadamu watakaokuwa wamefufuliwa ambao Yesu Kristo alifia akiwa dhabihu ya ukombozi. Kufikia mwishoni mwa Mileani ile Yubile ya Kikristo itakuwa imetimiza kusudi layo la kufungua wanadamu kwa ukamili katika matokeo ya dhambi. (Warumi 8:21) Lingekuwa tendo la kiibilisi na lenye aibu sana kama nini mtu ye yote akijaribu kuharibu hali hiyo nzuri sana! Lakini kwa ruhusa ya Mungu Mwenye Nguvu Zote, Ibilisi atafanya jaribio la mwisho la kutenda hivyo, naye atapiga kwa dharuba akiwa na uchungu wenye kasirani. Kwa sababu hiyo imeandikwa hivi kwenye Ufunuo 20:7-10, 14.
20 “Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake; naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari. Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala. Na yule Shetani, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto.
21. Baada ya Yubile ya Kikristo kukoma pamoja na Mileani, ni itikio gani lenye kufanywa na wana wa Mungu wa kimbingu litakalokumbusha maneno ya Ayubu 38:7.
21 Uhuru wa kweli, utakaokuwa umetokezwa na mpango wa Yubile, utaendelea kufurahiwa kila mahali; viumbe wote watakuwa huru na watakuwa wakiheshimu yule ambaye pekee yake ndiye mwenye lile jina Yehova. (Zaburi 83:18) Ndivyo itakavyokuwa Yehova anapoendelea kutekeleza makusudi yake katika ulimwengu wote mzima. Wakati wa kuumbwa kwa dunia, kabla wanadamu hawajawekwa juu yayo, ‘nyota za asubuhi ziliimba pamoja, na wana wote wa Mungu walipiga kelele kwa furaha’ wakishangilia kwa kuona urembo huo. (Ayubu 38:7) Watafanya hivyo hata zaidi kwa kuona dunia ikiongezeka wanaume na wanawake ambao wameonyesha n kuthibitisha wakfu wao wote kabisa na ukamilifu wao kwa Mungu Mwenye Nguvu Zote.
22. Mwelekeo wetu unapasa kuwa nini, kupatana n himizo linalopatikana kwenye Zaburi 150:1-6?
22 Mambo yote yakiwa yanafikiriwa kulingana na mng’aro wa kustaajabisha unaoangazwa juu ya Maandiko, sisi hatuna la kufanya isipokuwa kutokeza shangwe ya Yubile kwa hiari pamoja na mbingu na kusema, Haleluya! Hili ndilo himizo kwetu ambalo kwalo kitabu cha Zaburi kinamalizika: “Haleluya. Sifuni Mungu katika patakatifu Pake sifuni Yeye katika anga, ngome Yake. Sifuni Yeye kwa vitendo Vyake vyenye nguvu; sifuni Yeye kwa ukuu Wake unaozidi. Sifuni Yeye kwa mipulizo ya mbiu; sifuni Yeye kwa kinubi na zeze. Sifuni Yeye kwa kigoma na dansi; sifuni Yeye kwa udi na filimbi. Sifuni Yeye kwa matoazi yenye kuvuma; sifuni Yeye kwa matoazi yenye kugongana kwa sauti kubwa. Acheni vyote vipumuavyo vimsifu Bwana. Haleluya.”—Zaburi 150:1-6 Tanakh Bible (1985), Sosaiti ya Amerika ya Uchapishaji wa Kiyahudi.
[Maelezo wa Chini]
a Gazeti jipya lilitolewa kule ambalo lingekuwa “kama sauti katika jangwa la mvurugo, kazi ya gazeti hilo [likiwa ni] kutangaza kuingia kwa Kipindi cha Ufanisi Mkubwa (“Golden Age”).” Leo linaitwa Amkeni!
b Millions Now Living Will Never Die (1920); Deliverance (1926); Freedom for the Peoples (1927); Liberty (1932); “The Truth Shall Make You Free” (1943); What Do the Scriptures Say About “Survival After Death”? (1955); Life Everlasting—In Freedom of the Sons of God (1966, kwa Kiswahili ni 1976); The Truth That Leads to Eternal Life (1968, kwa Kiswahili ni 1969); The Path of Divine Truth Leading to Liberation (1980).
Wewe Ungejibuje?
◻ Wafuasi wa Yesu walifunguliwa kutoka nini siku ya Pentekoste 33 W.K., na hiyo ilikuwa alama ya mwanzo wa nini kwao?
◻ Kwa nini kuna sababu ya kutazamia ukombozi mkubwa zaidi ya ule uliotukia katika karne ya kwanza?
◻ Ni ukombozi wa namna gani ambao umekuwa ukiendelea tangu 1919?
◻ Ni jinsi na wakati gani i ati gani a ukiendelea tangu 1919?9? tangu 1919? uliotukia
◻ Baada ya upeo wa Yubile, dunia itakuwa namna gani?
[Picha katika ukurasa wa 25]
Uhuru watangazwa Seda Pointi, 1919 W.K.
[Picha katika ukurasa wa 26]
“Kondoo wengine” washiriki Yubile ya Mileani