Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 1/1 uku. 29
  • “Mkusanyiko wa Wilaya Wenye Kushangaza”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mkusanyiko wa Wilaya Wenye Kushangaza”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Habari Zinazolingana
  • “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1988
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • “Njia ya Mungu ya Maisha” Mkusanyiko wa Wilaya na wa Kimataifa wa 1998
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Panga Sasa Kuhudhuria “Wapendao Uhuru” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1991
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 1/1 uku. 29

Ripoti ya Watangaziji Ufalme

“Mkusanyiko wa Wilaya Wenye Kushangaza”

MANENO hayo yalikuwa katika kichwa kikuu cha gazeti moja katika Martinez De La Torre, Veracruz, Meksiko, juu ya mkusanyiko mmoja wa Mashahidi wa Yehova uliofanywa katika mji huo. Gazeti hilo lilieleza hivi: “Lile hudhurio kubwa kwenye mkusanyiko wa wilaya wa [Mashahidi wa Yehova] uliofanywa kwenye Wanja za Mawonyesha ya Bidhaa ndio wonyesho wenye kuvutia zaidi wa tukio la kutokeza lenye kufanyika katika sehemu zote za ulimwengu siku zetu: ongezeko la ukosefu wa kutoamini ambalo watu wanalo katika mafundisho ya yale yanayoitwa makanisa ‘ya Kikristo’ ati, na usadiki thabiti wa kwamba ukubwa wa matatizo yaliyopo unapita kwa mbali uwezo wa serikali wa kuyatatua.

“Hatujapata kamwe kuwa na wakati mwingine ambapo mkutano wa kisiasa au tukio la kijamii limekusanya watu wengi hivyo likiwa na utaratibu na usafi kama huo. Lilikuwa jambo la kushangaza kabisa kuona watu 5,000 wakifuata kwa uangalifu programu iliyotegemezwa juu ya habari zilizotoka katika Biblia tu na zenye kushughulika na pande za maisha za kila siku tangu kulea watoto na kuishi pamoja watu wakiwa jamaa mpaka kufuata maadili ya afya ya kiroho, pamoja na mchezo wa kuigiza hadithi wa Biblia na matumizi yao katika nyakati za kisasa.”

Baada ya kutoa maelezo juu ya “wonyesho mkubwa ajabu wa uratibu na tengenezo la kazi lenye kuendelea vizuri sana zaidi,” ripoti hiyo ya habari ilitoa maoni haya: “Umaana wa utendaji unaoendeshwa na Mashahidi wa Yehova wa nchi hiyo unaweza kupimwa kwa matokeo ambayo yamepatikana katika muda wa miaka michache tu. Leo hilo ni shirika linalokua kwa haraka sana, ambalo halitiwi wasiwasi hata kidogo na maelezo mabaya ambayo kwa kawaida yanasemwa na watu wanaowazunguka. Jambo lo lote baya ambalo mtu angeweza kuwahesabia wao linapotea kabisa wakati anapoona msimamo wao juu ya mambo yanayowazunguka, njia sahihi wanayotumia katika kufanya mpanuko, heshima yao kwa mamlaka, na uthamini mkubwa walio nao kwa unyofu na usemi mzuri.

“Wanafunzi wa Biblia hao wamejulikana kuwa hivyo kutokana na karibu asilimia 100 ya watu waliokuwa wanaharakati wa dini mbalimbali, sana-sana Wakatoliki, ambao wameona dini ikipeperuka kuelekea kwenye siasa na kuidhinisha na kukubalia mazoea yasiyopatana na Biblia ya mchangamano wa imani mbali-mbali, ukosefu wa adili, na jeuri. Wao wamepata uradhi kwa kujipatanisha na kanuni za Kimaandiko juu ya mwenendo bila kufuatia ibada ya sanamu wala mapokeo yasiyojulikana asili. Kufanya hivyo kumewapa umoja wa imani unaostahili sifa ambao unaonekana kuwa unawatofautisha na wengine ko kote waliko.”

Maelezo hayo yanatukumbusha juu ya kanuni ambayo Yesu alitaja: “Mtawatambua kwa matunda yao.” (Mathayo 7:16) Watu wengi wenye mioyo minyofu katika Meksiko wanaendelea kutambua kwamba mafundisho ya Mashahidi wa Yehova yanapatana na Maandiko, wanashirikiana nao, na wanabarikiwa sana kiroho na Yehova Mungu.

[Picha katika ukurasa wa 29]

Tamasha iliyo kawaida ya mkusanyiko katika Meksiko

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki