Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 3/15 kur. 21-23
  • Watu Wenye Furaha—Kwa Sababu Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watu Wenye Furaha—Kwa Sababu Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kupata Furaha Katika Kazi ya Kueneza Evanjeli
  • Kupata Furaha Katika Ongezeko la Ufalme
  • Kushinda Vipingamizi Vinavyozuia Furaha
  • Kuvumilia Tukiwa Watu Wenye Furaha
  • Mtumikie Yehova kwa Moyo Wenye Kujaa Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Shangwe
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Shangwe​—Sifa Inayotoka kwa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Tumikia Yehova kwa Shangwe ya Moyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 3/15 kur. 21-23

Watu Wenye Furaha—Kwa Sababu Gani?

WAKIRISTO wa kweli leo ni watu wenye furaha. Ingawaje, sisi tunatumikia “Mungu mwenye furaha,” Yehova. (1 Timotheo 1:11, NW) Yeye anatutolea roho yake, na tunda moja la roho hiyo ni furaha.—Wagalatia 5:22.

Furaha hiyo yenye kina kirefu ina nguvu za kujirudisha na inastahimili mkazo. Kwa mfano, Yesu Kristo alitiishwa kwenye maumivu ya kutundikwa mtini na kwenye aibu ya kuuawa kama mkufuru. Hata hivyo, “kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake yeye alivumilia mti wa mateso.” (Waebrania 12:2, NW) Yesu alijua kwamba mbele yake kulikuwa na nafasi na mapendeleo makubwa kuhusiana na utumishi wake kwa Yehova. Kukaza fikira juu ya mapendeleo hayo wakati ujao kulimsaidia adumishe furaha yake katikati ya taabu.

Yesu anataka wanafunzi wake wawe wenye furaha pia. Yeye alisema: “Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe.” (Yohana 15:11) Imethibitika kuwa hivyo kwa Mashahidi wa Yehova leo. Ziko sababu nyingi zinazotufanya sisi tuwe watu wenye furaha. Sisi tunaujua ukweli, ambao unatuweka huru tuache kukabwa na ushirikina na itikadi za dini ya uwongo. (Yohana 8:32) Ndipo, pia, sisi tumejua mahali tulipo katika mkondo wa wakati na tunafurahia tumaini la wokovu litakalotimizwa karibuni. (Luka 21:28) Tunalindwa pia tusipatwe na mengi ya matatizo yanayokabiliwa na wale wasiozoea adili inayotegemea Biblia, miongoni mwa hayo yakiwa ni magonjwa ya kuambukizana kupitia ngono. Sisi tunafurahia ushirika ulio bora zaidi—pamoja na watu wanaopendezwa na kufanya mapenzi ya Yehova. Na, ndiyo, sisi tuna pendeleo kubwa la kushiriki katika kuzihubiri habari njema za Ufalme na kufanya wanafunzi kutoka watu wenye mfano wa kondoo.—Mathayo 24:14; 28:19, 20.

Lakini ingawa hivyo ndivyo ilivyo kuhusu Mashahidi wa Yehova kwa ujumla, namna gani wewe ukiwa mtu mmoja? Kwa sababu gani unaweza kusema kwamba wewe una sababu ya kufurahi sana pamoja na wale wengine wa watu wa Mungu?

Kupata Furaha Katika Kazi ya Kueneza Evanjeli

Wengine wanaona ni vigumu kujitia katika kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. Labda wao wanahisi wasiwasi wa kufikia watu wasiojuana nao na kuanzisha maongezi. Au huenda wakahisi tu kwamba wao si watoshelevu sana katika kufundisha wengine. Je! wewe unahisi hivyo nyakati nyingine? Ikiwa ndivyo, unaweza kupataje furaha katika kazi ya kueneza evanjeli?

Kwanza kabisa, endeleza mwelekeo wa kutazamia mema. Kwani, watu wengi wangesisimuka kuajiriwa kazi na mtu fulani mashuhuri au mwanasiasa anayejulikana sana! Lakini ni furaha iliyo kubwa zaidi kama nini tunayopaswa kupata kwa kutumiwa na yule “Mfalme wa umilele,” Yehova Mungu mwenyewe!—1 Timotheo 1:17, NW.

Kumbuka, pia, kwamba hii ni kazi ambayo haitarudiwa tena kamwe. Ebu wazia! Malaika wenyewe wanaongoza na kuelekeza Wakristo hapa duniani katika jitihada zao za kutafuta wenye mfano wa kondoo. (Ufunuo 14:6) Je! jambo hilo halileti furaha moyoni mwako?

Kupata Furaha Katika Ongezeko la Ufalme

Sababu nyingine ya kuwa na maoni ya kutazamia mema katika kazi ya kuhubiri ni tokeo zuri ambalo kazi hiyo inapata. Biblia ilitabiri hivi: “Mdogo atakuwa elfu, na mnyonge atakuwa taifa hodari; mimi [Yehova], nitahimiza hayo wakati wake.” (Isaya 60:22) Ahadi hiyo ya Yehova imekuwa kweli katika nyakati za karibuni. Kwa mfano, wakati wa mwaka wa utumishi wa 1986 watu 225,868 walibatizwa kuonyesha wakfu wao wa nafsi yote kwa Yehova Mungu. Kulikuwa ongezeko la asilimia 6.9 katika hesabu ya wastani ya wenye kushiriki kueneza kweli za Biblia kwa wengine.

Bila shaka ongezeko hilo linaonekana wazi katika kundi au mzunguko wenu wenyewe. Wapya wanakuja kwenye mikutano na kufanya mabadiliko yanayohitajiwa kabisa katika maisha zao ili waweze kutumikia Mungu. Je! jambo hilo halionyeshi kwamba kazi ya kuhubiri ina baraka ya Yehova? Kuwa na ushiriki katika ongezeko hilo kunaweza hivyo kuwa chanzo cha furaha kubwa kwako. Ni kweli kwamba huenda ukawa wewe binafsi hujajifunza na mtu fulani kufikia ubatizo. Lakini hata ikiwa hivyo, sisi hatuwezi kujipatia sifa kwa kuleta mtu ndani ya ukweli. ‘Mungu anafanya ikue,’ akasema Paulo. (1 Wakorintho 3:6-9) Washiriki wote wa kundi wana ushiriki fulani katika kusaidia wapya. Jinsi gani? Kwa kuwapo mikutanoni, kutoa maelezo, kusalimu wapya kwa njia ya ukaribishaji, na kujiendesha wenyewe kwa njia inayofanya ukweli uvutie wengine.

Hata hivyo, furaha kubwa zaidi inaweza kupatikana ukiwa na ushiriki wa moja kwa moja zaidi katika kazi ya kuhubiri na kufanya mafunzo ya nyumbani ya Biblia. Mwaka jana, kwa wastani, mafunzo ya Biblia ya kila juma 2,726,252 yaliongozwa. Mbona usifanye jitihada zaidi kushiriki katika kazi hiyo yenye furaha? Tolea mtu fulani unayejua funzo la Biblia, labda jirani au mtu fulani ambaye umemwangushia kitabu fulani. Mwombe Yehova msaada upate mtu fulani wa mfano wa kondoo.

Kushinda Vipingamizi Vinavyozuia Furaha

Bila shaka, ikiwa mtu anahisi si mtoshelevu juu ya kufundisha wengine, jambo hilo linaweza kuwa kipingamizi kweli kweli cha kuzuia asipate furaha katika huduma ya shambani. Ingawa hivyo, kumbuka kwamba “utoshelevu wetu watoka kwa Mungu.” (1 Wakorintho 3:5) Na kupitia tengenezo lake Yehova ameandaa misaada mingi mizuri sana kutusaidia tustahili kuwa wahudumu wenye matokeo mazuri.

Kwanza kabisa, kuna wengi miongoni mwetu ambao wamekuwa wakitumikia Mungu kwa muda mrefu na wana ujuzi mwingi katika huduma ya shambani. Tunaweza kujiunga na wahudumu hao wenye ujuzi katika utendaji wao na kujifunza kutokana nao. Tena, kila mwezi madokezo mazuri sana yanatokea katika Huduma ya Ufalme Yetu. Halafu kuna kile kichapo Reasoning From the Scriptures, kilicho na utajiri mwingi wa habari za kunoa ustadi wetu wa kuhubiri. Tumia vyombo hivyo na ujitayarishe kwa ukamili zaidi kwa ajili ya huduma ya shambani. Fikiria njia mpya na za kupendeza za kujitolea utangulizi mlangoni. Au ufikirie njia mbalimbali za kuvuta wenye nyumba katika maongezi. Unapozidi kuwa mwenye matokeo mazuri katika shamba, shauku yako na furaha katika kuhubiri bila shaka vitaongezeka.

Huduma inakuwa yenye kufurahika zaidi wakati tunapoweza kusema na watu. Katika maeneo fulani ni wazi kwamba hilo ni tatizo. Je! unaweza kupanga kushiriki katika utumishi wa shambani wakati ambao watu wengi zaidi wako nyumbani, kama vile mapema jioni? Wengi wanaona kwamba kufanya hivyo kuna matokeo mazuri sana. Unaweza pia kuchukua hatua ya kwanza na kusema na watu ko kote wanakopatikana—barabarani, wanaoketi katika viti vya bustani za mji, wanaosafisha magari yao. Kumbuka kwamba watu wanahitaji ukweli na maisha zao zinahusika. Jambo hilo linaweza kusaidia kukusukuma wewe uyashinde maelekeo ya kuona haya. Ingawa ni kweli kwamba walio wengi kati ya watu hawataitikia kwa njia inayofaa, wale wanaoitikia wanatuletea furaha nyingi.

Hata hivyo, mmoja wa misaada iliyo mikubwa zaidi ya kudumisha furaha yetu ni sala. Omba Yehova akupe roho yake ikupe nguvu na kukutia moyo. Paulo alisema: “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.” (Wafilipi 4:13) Sisi tunaweza kuhisi hivyo, pia, tunapojifunza kumtegemea Yehova.

Kuvumilia Tukiwa Watu Wenye Furaha

Watu wengi mmoja mmoja hawathamini kazi yetu. Yesu alijua kwamba ndivyo ingekuwa. Kwa hiyo wakati alipotuma wafuasi wake waende kuhubiri, yeye aliwashauri hivi: “Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu. . .. Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwamwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.” Yesu alisema hivi pia: “Hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope basi.”—Mathayo 10:11-16, 30, 31.

Maneno hayo yanatusaidia tuvumilie kwa furaha. Yanatusaidia tutambue kwamba wakati tunapokutana na watu wasiothamini jitihada zetu kwa ajili yao, bado sisi tunakuwa tukijulisha jina la Yehova; bado tunakuwa tukimsifu yeye. (Zaburi 100:4, 5) Jambo la kupendezwa ni kwamba, nyakati nyingine wenye nyumba wanaokataa kufungua mlango wanaweza kusikiwa wakiambia wengine hivi: “Waliokuwa hapa ni Mashahidi wa Yehova.” Ndiyo, bila ya sisi kusema neno lo lote, jina la Yehova linakuwa limetukuzwa, na watu wanakuwa wamepokea nafasi ya kuukubali au kuukataa ukweli. (Mathayo 25:31, 32) Kwa hiyo hata maeneo yasiyo na itikio yanaweza kuvumiliwa kwa furaha.

Zaidi ya hilo, hatujui kamwe ni wakati gani watu hao mmoja mmoja huenda wakawa na badiliko la mwelekeo. Siku moja, mwanamke mmoja aliyekuwa amefukuza dada mmoja Mkristo mlangoni pake katika pindi kadha alimwuliza dada huyo kama ana vitabu vyo vyote vipya. Dada yule alishangaa na kusema kwamba mwanamke huyo hakuwa amewahi kukubali kitabu cho chote cha Kibiblia. Mwanamke yule akamweleza kwamba mumeye alifanya kazi na mwanamume anayekuwa akijifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Mwanamume huyo alikuwa amempa yeye na mumeye kimoja cha vichapo vya Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi. Kwa sababu ya udadisi, mwanamke yule akawa amekisoma na kuutambua ujumbe huo kuwa ukweli. Kwa hiyo ndipo akaamua pale pale kwamba safari ile nyingine Shahidi akimtembelea nyumbani angekubali kumkaribisha. Funzo la nyumbani la Biblia lilianzwa, na mwanamke huyo baadaye akawa shahidi aliye wakfu wa Yehova!

Hivyo sisi tuna pendeleo kubwa—pendeleo lenye furaha la kuutangaza ujumbe ule mmoja tu wa tumaini katika ulimwengu. Na kazi ya kuhubiri ni mgawo ambao Mungu ametupa sisi katika hizi siku za mwisho. Ni lazima ufanywe kabla ya mwisho kuja. (Mathayo 24:14) Ni muda gani utakaopita kabla mwisho wa mfumo mbovu wa Shetani haujaja? Tunajua mwisho hautakuja kwa kuchelewa. (Linganisha Habakuki 2:3.) Kwa wakati uliopo, kungali kuna wakati wengine wajifunze ukweli. Acheni sisi tutumie kwa faida wakati uliobaki na tuwe wenye bidii kwenye kazi yetu ya kuhubiri. Na acheni sisi tuwe na mwelekeo unaofaa, tukifanya kazi kwa bidii ili ‘tujiokoe sisi wenyewe na wale wanaotusikiliza.’ (1 Timotheo 4:16) Katika kufanya hivyo, sisi tutabaki tukiwa jamii ya watu wenye furaha wanaoshiriki katika ongezeko la Ufalme.

[Picha katika ukurasa wa 23]

Kazi yetu ya kueneza evanjeli ni chanzo cha furaha ya kweli—hata wakati watu wanapokuwa hawaitikii ujumbe wa Ufalme

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki