Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 7/1 kur. 3-4
  • Hasira—Ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hasira—Ni Nini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kuonyesha Hasira
  • Visababishi vya Hasira
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Hasira?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je! Ni Vibaya Nyakati Zote Kuwa na Hasira?
    Amkeni!—1994
  • Hasira
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Kuweza Hasira Yako na ya Wengine
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 7/1 kur. 3-4

Hasira​—Ni Nini?

“KWA KUZUIA kipawa chako ulichopewa na Mungu cha hasira, unajiua mwenyewe.” Ndivyo ilivyoonya makala moja iliyonakiliwa katika jarida Newsweek. Kwa miaka mingi, kwa wazi, madaktari wengi wa magonjwa ya akilini wamefanya likubaliwe na wengi wazo la kwamba hasira isiyoonyeshwa huenda ikatokeza matatizo kama mkazo wa juu wa damu, ugonjwa wa moyo, kushuka moyo, wasiwasi, na uzoevu wa kileo.

Biblia, kwa upande mwingine, imeonya kwa maelfu ya miaka hivi: “Ukomeshe hasira, uache ghadhabu.” (Zaburi 37:8) Uchunguzi wa Biblia wa tatizo hili unalenga jambo lenyewe: “Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.”—Mhubiri 7:9.

Ni nani anayesema ukweli, wataalamu wa kilimwengu au Biblia? Hasira ni nini hasa? Je! kuonyesha hasira ni jambo linalotufaa sisi?

Kuonyesha Hasira

“Hasira” ni neno la ujumla linaloeleza hisia yenye nguvu au tendo la udhiko na ushindani. Kuna maneno mengine, pia, ambayo hufunua kadiri ya hasira au jinsi inavyoonyeshwa. Kasirani hudokeza hasira kali sana. Kiruu kinaweza kuwa chenye kuharibu. Ghadhabu huenda ikaelekeza kwenye hasira kwa ajili ya kusudi la uadilifu. Na hasira kali mara nyingi inaweza kuwa na maana ya kulipa kisasi au adhabu.

Kwa kawaida hasira inakuwa dhahiri: Sisi tunakuwa na hasira juu ya jambo fulani. Lakini namna tunavyoonyesha hasira au kushughulikia nayo hufanya tofauti kubwa.

Jambo la kupendeza ni kwamba, ingawa wataalamu fulani wanasisitiza kwamba kuonyesha hasira ni jambo lenye mafaa, machunguzi ya karibuni yanayohusu magonjwa ya akilini yanaonyesha kwamba watu wengi wanaojiruhusu wenyewe waonyeshe hasira wanapata hali ya chini zaidi ya kujiheshimu wenyewe, kushuka moyo, kuhisi ukiwa na hatia, uadui ulioongezeka, au wasiwasi. Isitoshe, kuonyesha hasira, pengine kukiambatana na mifoko ya hasira, kupiga makelele, kulia, au hata kushambulia wengine kimwili, kwa kawaida kunatokeza matatizo mengi zaidi ya kuyatatua. Yule mtu mwenye hasira anakuwa na hasira zaidi, na hisia zilizoumizwa zingeongezeka ndani ya wengine.—Mithali 30:33; Mwanzo 49:6, 7.

Wakati tunapopiga makelele na mayowe kwa hasira, kwa kawaida hatupati yale matokeo tuliyotumainia kwa sababu yule mtu mwingine kwa kawaida anachochewa alipe kisasi. Kwa mfano, tuseme kwamba unapoendesha gari lako, dreva mwingine anafanya jambo linalokuudhi. Katika kuitikia, wewe unapiga kelele na kupiga honi ya gari lako. Mfoko wako ungeweza kwa urahisi kumchochea yule uliyeelekezea kasirani yako alipe kisasi. Nyakati nyingine msiba umetokea katika hali kama hiyo. Kwa mfano, mwanamume mmoja katika Brooklyn, New York, aliuawa alipokuwa akitoa ubishi juu ya mahali pa kuegesha gari barabarani. Biblia inakazia tatizo hilo inaposema: “Mtu wa hasira huchochea ugomvi; na mtu mwenye ghadhabu huasi sana.” (Mithali 29:22) Jinsi lilivyo jambo la hekima kufuata shauri hili: “Msimlipe mtu ovu kwa ovu. . . . Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote”!—Warumi 12:17, 18.

Kwa sababu hiyo, kuonyesha kwetu hasira hakutusaidii kijamii. Lakini je! kunatufaa kimwili? Hesabu fulani ya matabibu wamekata maneno kwamba sivyo. Machunguzi yameonyesha kwamba watu wanaoelekea sana kuonyesha hasira wana mkazo wa juu zaidi wa damu. Wengine waliripoti kwamba hasira hutokeza mishtuko ya moyo, maumivu ya kichwa, kutokwa damu puani, kizunguzungu, au kutoweza kutoa sauti yenye kusikika. Kwa upande mwingine, Mpaji wa uhai wetu anaeleza hivi: “Moyo uliotulia ndio uzima wa mwili wenye nyama.” (Mithali 14:30, NW) Yesu alisema: “Wenye furaha ni wenye kuamanika, kwa kuwa wataitwa ‘wana wa Mungu.’ “—Mathayo 5:9, NW.

Visababishi vya Hasira

Baadhi ya visababishi vya hasira ni mashambulio juu ya kujiheshimu kwetu, uchambuzi wa kibinafsi, kutukanwa, kutendwa isivyo haki, na kuvurugika akili kusiko haki. Watu wanapokuwa na hasira, wanapeleka ujumbe huu wenye mkazo: “Wewe unahatirisha furaha na usalama wangu! Unaumiza fahari yangu! Unaninyang’anya hali yangu ya kujiheshimu! Unanitumia vibaya ili ujifaidi mwenyewe!”

Nyakati nyingine watu wanatumia hasira ili kufunika jambo jingine. Kwa mfano, mvulana mmoja wa miaka 14 katika Mji wa New York alikuwa katika hali ya kukasirika daima na sikuzote akijiingiza katika vita. Kwa msaada wa daktari, mwishowe mvulana huyo alikubali hivi: “Mimi singesema kamwe, ni sawa, mimi nahitaji msaada, nataka mtu wa kuzungumza naye . . . Hofu yako ni kwamba watu hawatakupenda.” Kwa hiyo, jambo alilotaka kweli kweli ni kukaziwa fikira na kuonyeshwa shauku ya upendo.

Watu wawili waliooana katika Kalifornia walijitia katika mifoko ya hasira kila mara mke alipoenda kutembelea rafiki yake msichana. Mwenendo wa hasira wa mumeye ulitokeza tendo-kisasi kama lake katika mkeye. Katika kikao cha kushauriwa, mume huyo hatimaye alimwambia mkeye jambo ambalo hakuwa ameambia mtu mwingine kamwe mbeleni. Wakati mkeye alipoenda mbali bila yeye, hata kwa kitambo kidogo, ndani ndani sana alihofu kwamba mkeye angeweza kumwacha kabisa kwa sababu baba yake alikuwa amemwacha kabisa alipokuwa mchanga. Wakati mke huyo alipofahamu sababu iliyo asili ya hasira ya mumeye—hofu ya kuachwa kabisa—ilimsaidia mkeye kuondoa hasira yake mwenyewe kuelekea mumeye na kumhakikishia upendo wake.

Hivyo, huenda hasira ikawa dalili. Katika visa kama hivyo, kwa kutambulisha visababishi vilivyo asili ya hasira, tunaweza kujifunza kushughulika nayo ifaavyo.

[Picha katika ukurasa wa 4]

Hesabu fulani ya matabibu wamekata maneno kwamba kuonyesha hasira hakuleti afya

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki