Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 8/15 kur. 10-15
  • Vijana Mtafanya Nini na Maisha Zenu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vijana Mtafanya Nini na Maisha Zenu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Vielelezo Vinavyoigwa na Wengi
  • Shauri la Kufuata
  • Vielelezo vya Kutazama
  • Ishi kwa Ajili ya Ulimwengu Mpya wa Mungu
  • Timotheo—“Mtoto Halisi Katika Imani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Timotheo Anapata Mashauri kwa Mwanamume Mzee
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Timotheo—Alikuwa Tayari na Mwenye Nia ya Kutumikia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Vijana—fuatieni Miradi Inayomletea Mungu Heshima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 8/15 kur. 10-15

Vijana Mtafanya Nini na Maisha Zenu?

“Ili walio hai wasiwe hai tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa akafufuka kwa ajili yao.”—2 WAKORINTHO 5:15

1. Watu wamesema maneno gani ya shukrani, na kwa sababu gani?

1‘ASANTE! Ninakuwia uhai wangu!’ Watu ambao wanaokolewa kutoka nyumba inayoteketea au kufa maji wamewaambia hivyo wale waliowaokoa. Na vijana Wakristo wenye kuthamini wamewaambia wazazi wao maneno kama hayo. Hawakuwa wakielekeza tu kwenye maisha ya kimwili ambayo wamepokea kutoka kwa wazazi wao bali hasa utunzaji wenye upendo na agizo ambalo limewaweka vijana hao katika njia ya kupokea “ahadi aliyotuahidia, yaani uzima wa milele.”​—1 Yohana 2:25.

2. Ni kwa ufahamu wa habari gani inawapasa kulifikiria ulizo hili, Mtafanya nini na maisha zenu?

2 Upendo ndio uliosukuma Yehova Mungu kufanya uzima wa milele, “uzima ulio kweli kweli,” upatikane kwa kila mmoja wetu. “Yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu.” (1 Timotheo 6:19; 1 Yohana 4:10) Ebu fikiria, pia, upendo ambao Mwana wake Yesu alionyesha kwa kufa kifo chenye maumivu ili sisi tupate uzima wa milele! (Yohana 15:13) Kwa sababu ya mambo hayo yanayotangulia, Mtafanya nini na maisha zenu?

3. Ni kitu gani ambacho mara nyingi kinaamua yale ambayo watu watafanya na maisha zao?

3 Washauri wa wanafunzi shuleni au watu wanaopendezwa na wakati wao ujao, mara nyingi wanawauliza vijana ulizo hili, katika njia moja au nyingine. Ni nini kitakachoamua jibu lenu? Je! litaamuliwa tu na mambo mnayopendelea kibinafsi? Je! jambo litakaloamua litakuwa shauri la wale ambao wanawataka ninyi mpate cheo salama katika ulimwengu usio wa kidini? Au je! yale ambayo mtafanya na maisha zenu yataamuliwa na makusudio bora zaidi? Kikumbusho kilichoongozwa na roho kinasema: “Tena alikufa kwa ajili ya wote, ili walio hai wasiwe hai tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa akafufuka kwa ajili yao.” (2 Wakorintho 5:15) Ndiyo, jinsi lilivyo jambo zuri wakati njia tunayotumia maisha zetu inapoonyesha shukrani kwa yale ambayo Yesu Kristo na Baba yake wa kimbingu wametufanyia sisi!

Vielelezo Vinavyoigwa na Wengi

4. Ni nani walio vielelezo vinavyoigwa na walio wengi sana leo?

4 Hata hivyo, ni watu gani wanaopendwa na wengi zaidi sana leo, wale ambao kwa kawaida vijana wanachagua kama vielelezo vya kuiga? Je! si watu walio matajiri na mashuhuri katika ulimwengu, bila kujali viwango vyao vya adili? Unapotazama katika vyumba vya vijana wengi, ni picha za nani unazoona zikiwa zinaning’inia ukutani? Mara nyingi ni za wanamuziki, wachezaji sinema mashuhuri, na wanariadha. Kwa kawaida vijana wanaota ndoto za kupata siku moja mafanikio ya kilimwengu yanayofanana na hayo au labda kumwoa au kuolewa na mtu ambaye ana sifa za kimwili za watu hawa. Namna gani wewe? Unataka nini maishani?

5, 6. (a) Kwa sababu gani inaweza kusemwa kwamba mafanikio ya kilimwengu yanashindwa kuleta uradhi wa kweli? (b) Chanzo cha uradhi wa kweli ni nini?

5 Ikiwa ungepata mafanikio ya kilimwengu ya watu mashuhuri wanaosifiwa, je! ungekuwa kweli na furaha na uradhi? Mmoja wa wanamke waigizaji michezo wenye mafanikio zaidi sana wa Hollywood alisema: ‘Nimepata mwonjo wangu wa mali na vitu vyote vya kimwili. Haimaanishi cho chote. Katika kila jamaa yenye utajiri wa kutosha kuwa na dimbwi la kuogelea kuna mikazo na matatizo ya akili, bila kutaja talaka na watoto wanaowachukia wazazi wao.’—Mhubiri 5:10; 1 Timotheo 6:10.

6 Mwanafunzi mmoja mwanariadha mwenye kutokeza, aliyekuwa mshindi wa mbio kubwa za wanawake za kilometa 10 katika New York katika 1981, alipata kukatishwa tumaini sana hivi kwamba alijaribu kujiua. “Nimejifunza kweli nyingi kuhusu maisha katika miezi michache iliyopita,” akaandika mwanamke huyo baadaye. ‘Ukweli mmoja ni kwamba uradhi wa kweli haupatikani katika njia ambazo watu wengi wanajitahidi kupata usitawi na ufaulu. Kwangu, uradhi haukutokana na kuwa mwanafunzi aliyepokea maksi za A, mkimbiaji shujaa wa mkoa au mwenye umbo la kuvutia.’ Ndiyo, watu wanahitaji kujifunza kwamba uradhi wa kweli unatokana tu na kuwa na uhusiano wa kibinafsi pamoja na Mungu, ambaye peke yake ndiye anaweza kutoa amani na furaha ya kweli.​—Zaburi 23:1, 6; 16:11.

7. Kuhusu kupata uradhi wa kweli, elimu ya koleji na mafanikio ya kilimwengu ni ya muhimu kadiri gani?

7 Kwa wazi, basi, haikupasi utake kuwaiga wale ambao wanang’ang’ana ili wapate umashuhuri na mali tu. Hata waandikaji wa ulimwengu wanaona kwamba mafanikio ya kilimwengu yanashindwa kuleta uradhi wa kweli. Mchangiaji habari za safu za magazeti Bill Reel aliandika hivi: “Unahitimu kutoka kwenye koleji ukiwa na ndoto za wakati ujao. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, yaliyo mengi zaidi ya matazamio yako yatakosa kutimia. Sitaki kukuvunja moyo, lakini unaweza kuusikia ukweli pia: Unapopata mali unazotamani, ukizipata, unapopata mafanikio unayofuatia, ukiyapata, hayataridhisha. Badala yake, wakati ule ule unapotazamia kujifurahisha kwa ushindi wenye shangwe, unahisi ukiwa tupu badala ya kuwa umetimiza jambo, umeshuka moyo badala ya kutiwa moyo, umefadhaika badala ya kuwa na amani.”—New York Daily News, Mei 26, 1983.

8. Kuna sababu gani yenye nguvu ya kutokufuatia kazi ya maisha ya kilimwengu?

8 Lakini kwetu sisi ambao tu macho kuhusu maana ya matukio ya ulimwengu kwa msaada wa unabii wa Biblia, kuna sababu zenye nguvu sana za kutotanguliza maishani kazi ya maisha ya kilimwengu. (Mathayo 24:3-14) Tunaweza kujilinganisha sisi wenyewe na mtu anayeona jengo lenye ishara: “Kampuni Hii Inafilisika.” Je! tungetafuta kazi humo? Bila shaka la! Na ikiwa tungefanya kazi katika kampuni kama hiyo, kwa hekima tungetafuta kazi mahali pengine. Basi, ishara hiyo inaonekana wazi kila mahali katika taasisi za ulimwengu huu: “Zinafilisika —Mwisho Umekaribia!” Ndiyo, “Ulimwengu unapitilia mbali,” ndivyo Biblia inavyotuhakikishia. (1 Yohana 2:17, NW) Kwa hiyo, kwa hekima, hatutataka kuchagua wale ambao wanahusika sana nao kuwa vielelezo vya kuigwa.

Shauri la Kufuata

9. Wale ambao wanaonekana kuwa wanakutakia mema huenda wakatoa shauri gani la kilimwengu?

9 Maisha yako yanaongozwa si na wale ambao unaheshimu tu bali pia mara nyingi na watu wa ukoo na marafiki ambao, kama wanavyosema, ‘wanakutakia mema.’ ‘Lazima ujiruzuku,’ huenda wakasema. Kwa hiyo huenda wakakushauri kupata elimu ya koleji au ya chuo kikuu ili ujitayarishe mwenyewe kupata kazi ya ustadi. ‘Mwandikaji wa Biblia Luka alikuwa tabibu,’ huenda wakasema, ‘na mtume Paulo alifundishwa na mwalimu wa Torati Gamalieli,’ (Wakolosai 4:14; Matendo 5:34; 22:3) Hata hivyo, changanua kwa uangalifu sana shauri hilo.

10. Luka na Paulo walitoa shauri gani, na ni jambo gani linaloweza kusemwa kuhusu utendaji wao kabla ya kuwa Wakristo?

10 Tabibu Luka hakuwatia moyo kamwe Wakristo wafuate kiolezo cha kazi yake ya kwanza kwa kuwa daktari, bali Luka alionyesha maisha ya Yesu na mitume yaigwe. Kwa wazi Luka alipata kuwa tabibu kabla yeye hajajifunza juu ya Kristo lakini baadaye aliweka huduma ya Kikristo yake kwanza maishani. Ndivyo hali ilivyokuwa na Paulo. Badala ya kuwatia moyo wengine wamwige yeye kama vile yeye alivyokuwa amemwiga Gamalieli, Paulo aliandika hivi: “Mnifuate mimi kama mimi ninavyomfuata Kristo.” Paulo alithamini sana maarifa ya Kristo hivi kwamba kwa kulinganisha yeye alisema kwamba aliyafikiria mambo yake aliyofuatia kwanza “kuwa kama mavi.”—1 Wakorintho 11:1; Wafilipi 3:8.

11. (a) Petro alimwambia nini Yesu, na kwa sababu gani? (b) Yesu aliitikiaje?

11 Kumbuka, kusukumwa na hisia za moyoni kunaweza kuwafanya hata wale wanaokupenda watoe shauri baya. Kwa mfano, Yesu alipozungumuza juu ya yale yaliyomngojea yeye wakati wa huduma yake katika Yerusalemu, mtume Petro alijibu hivi: “Ujifadhili, Bwana; hutapatwa na jambo hili hata kidogo.” Petro alimpenda Yesu naye hakutaka Yesu ateseke. Hata hivyo Yesu alimkemea Petro kwa sababu Yeye alitambua kwamba kutimiza mapenzi ya Mungu kungetia ndani kuteseka na pia kuuawa na wapinzani,—Mathayo 16:21-23, NW.

12. Ni shauri gani ambalo watu wenye makusudio mazuri wanaweza kuwapa vijana, na kwa sababu gani?

12 Vivyo hivyo, wazazi fulani au marafiki huenda wakakuvunja moyo utoke kwenye mwendo wa kujidhabihu. Kwa sababu ya kusukumwa na hisia za moyoni zisizofaa, huenda wakasitasita kukutia moyo uchukue mgawo katika huduma ya painia wa wakati wote, kutumikia kama mmisionari, au kujitolea ufanye kazi katika afisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova. Huenda wakasema: ‘Badala yake, mbona, usioe au kuolewa kisha utulie karibu nasi.’ Au, ‘Unajua, kazi ni ngumu sana huko Betheli. Labda ni afadhali ukae nasi.’ Kwa maneno mengine, kama vile Petro alivyosema, “Ujifadhili.”

13. (a) Ni maoni gani yaliyorekebishwa ambayo Petro alisema? (b) Ni nini kinachohusika katika kuwa Mkristo wa kweli?

13 Hata watumishi wa Yehova wanahitaji kurekebisha kuwaza kwao nyakati nyingine. Petro alihitaji kufanya hivyo, na akiwa na maoni yaliyorekebishwa, yeye aliandika hivi: “Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.” (1 Petro 2:21) Kuishi maisha ya Kikristo ya kweli kunahusu kujidhabihu, ndiyo, hata kuteseka. Siyo mwendo rahisi, lakini ndio tulioitiwa tukiwa Wakristo. Kuukubali kunahusu ‘kutokuwa hai tena kwa ajili ya nafsi zetu wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa akafufuka kwa ajili yetu.’ (2 Wakorintho 5:15) Kufikiria vielelezo vizuri kutatusaidia sisi tutumie maisha yetu katika njia hii ya kujidhabihu.

Vielelezo vya Kutazama

14. Yesu aliandaa mfano gani?

14 Kielelezo ambacho unahitaji kufikiria sana ni kile ambacho Yesu alitoa. Akiwa mtu mkamilifu, yeye angeweza kuwa mwanariadha, mwanamuziki, tabibu, au mwanasheria mkubwa zaidi sana ambaye ulimwengu umepata kujua. Lakini fikira zake zilikaziwa kupendeza Baba yake wa kimbingu, hata alipokuwa kijana. (Luka 2:42-49) Baadaye yeye alisema: “Imenipasa kuihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu katika miji mingine pia; maana kwa sababu hiyo nalitumwa.” (Luka 4:43) Kiangazi kilichopita barua moja katika Ministry gazeti la kanisa ilieleza hivi: “Mwokozi wetu alipenda kujiondoa katika umati, kisha Yeye akaenda nyumba kwa nyumba —kuwinda nafsi. Furaha yake ilikuwa kusikilizwa na nafasi moja moja. Kisha Yeye angeweza kuumimina ukweli—upendo wa Mungu.”—Luka 10:1-16.

15. (a) Kwa sababu gani kuhubiri nyumba kwa nyumba ni mwito wa ushindani? (b) Ni jambo gani linaloonyesha kwamba huduma ya nyumba kwa nyumba ya vijana ni yenye matokeo mazuri?

15 Imekubaliwa kwamba, kuhubiri nyumba kwa nyumba si rahisi. Kunahitaji funzo la bidii ili kufahamu habari njema za Ufalme na kazi nyingi sana ili kutayarisha utoaji wenye maana. Pia, utumishi huu unahitaji ushujaa, kwa kuwa wenye nyumba walio wengi hawapendezwi, na hata wengine ni wenye uhasama. Hata hivyo, huduma ya nyumba kwa nyumba inayofanywa na ninyi vijana ina matokeo ya ajabu, kama ilivyosemwa katika gazeti la kimtaa wa kanisa la Kiitalia La Voce. Mwandikaji alisema hivi: “Mimi binafsi, nawapenda Mashahidi wa Yehova,” ambao, yeye alieleza, “wanakuja na kukutembelea wewe nyumbani.” Yeye alitoa maelezo hivi: “Wale ninaowajua wana tabia isiyolaumika, wenye kusema kwa njia nyororo; pia ni watu wazuri na sana sana vijana. Uzuri na ujana unapoonyeshwa, unakuwa wenye kushawishi sana.”

16. (a) Vijana wanastahili kusifiwa kwa ajili ya utendaji gani? (b) Tengenezo la Mashahidi wa Yehova linalinganaje na makanisa katika kufanya kazi iliyo ya maana zaidi duniani?

16 Hakika, ninyi vijana mnaokubali Kristo awe kielelezo chenu mnahitaji kusifiwa sana! Vijana zaidi ya 12,000 wenye umri wa 25 na chini wamo katika kazi ya painia katika United States, na bila shaka makumi ya maelfu zaidi wanapainia sehemu nyinginezo. (Zaburi 110:3) Mnahakikishiwa kwamba, hakuna kazi nyingine ambayo ninyi mngefanya ambayo ni ya muhimu zaidi! Hata mwandikaji wa gazeti la kanisa aliyetajwa juu alisema: “Mungu anasema kwamba kazi yenye maana kabisa ni kuzuru nyumba kwa nyumba—kuwinda nafsi,” hata hivyo anaendelea, “Unasema nini juu ya jambo hili? Ni ziara ngapi ambazo wewe na mimi tunafanya? Sijaona kazi ya aina hii ikitajwa sana katika “HUDUMA.” Je! hatuwezi kuwa wenye shukrani kwamba tunashirikiana pamoja na tengenezo linalokazia takwa la kuiga mfano wa Yesu wa kuhubiri?

17. Timotheo alitimiza nini akiwa pengine bado tineja, na ni jambo gani linaloonyesha kwamba huenda ikawa yeye alikuwa mchanga kadiri hiyo wakati huo?

17 Kwa kuwa yale utakayofanya na maisha yako yataongozwa sana na wale unaosifu mno, kuza sifa kubwa pia kwa kielelezo kinachotolewa na kijana Timotheo. Timotheo aliyezaliwa muda mfupi kabla ya kifo cha Yesu, aliiacha jamaa yake akiwa kijana na akajiunga pamoja na mtume Paulo kwenye safari yake ya pili ya umisionari. Miezi michache baadaye watu wenye ghasia waliwalazimisha Paulo na Sila kutorokea Thesalonike, lakini si kabla wao hawajafanya wanafunzi fulani. (Matendo 16:1-3; 17:1-10, 13-15) Muda mfupi baadaye Paulo alimtuma Timotheo kwenye eneo hilo hatari ili awafariji wanafunzi hao katika majaribu yao. (1 Wathesalonike 3:1-3) Labda Timotheo alikuwa katika miaka yake ya kumalizia utineja wakati huo, kwa kuwa Paulo bado alizungumza juu ya “ujana” wake Timotheo miaka 12 hadi 14 baadaye. (1 Timotheo 4:12) Je! wewe husifu sana kijana kama huyo mwenye ushujaa, na mwenye kujidhabihu?

18. Kwa sababu gani Paulo alikuwa akitayarisha kumtuma Timotheo kwa Wakorintho?

18 Miaka mitano baada ya mgawo wa Timotheo wa kuwatia nguvu ndugu katika Thesalonike, Paulo aliwaandikia Wakorintho kutoka Efeso: “Mnifuate mimi. Kwa sababu hii nimemtuma Timotheo kwenu,. .. atakayewakumbusha njia zangu zilizo katika Kristo, kama vile nifundishavyo kila mahali.” (1 Wakorintho 4:16, 17) Tayari akiwa amefanya kazi pamoja na Paulo kwa miaka mitano, kijana Timotheo, alifahamiana vizuri sana na njia za Paulo za kufundisha. Yeye alijua jinsi Paulo alivyokuwa amewatolea Waefeso ujumbe, kutia na jinsi alivyokuwa amewafundisha “waziwazi, na nyumba kwa nyumba.” (Matendo 20:20, 21) Akiwa amezoezwa vizuri katika njia hizo za kuhubiri, Timotheo alikuwa msaada bora kama nini kwa makundi!

19. Paulo alisema nini juu ya Timotheo zaidi ya miaka kumi baada ya wao kuanza kutumikia pamoja?

19 Miaka mingine mitano au sita inapita, na Paulo yumo gerezani katika Roma. Timotheo ambaye amefunguliwa kutoka gerezani hivi majuzi, yu pamoja naye. (Waebrania 13:23) Ebu wazia tamasha hiyo: Labda akimtumia Timotheo kama mwandishi wake, Paulo anawaandikia Wafilipi barua. Akizungumza kwa makusudi, Paulo anaendelea hivi: “Natumani katika Bwana Yesu kumtuma Timotheo afike kwenu karibu . . . maana sina mtu mwingine mwenye nia moja nami, atakayeiangalia hali yenu kweli kweli . . . mwajua sifa yake, ya kuwa ametumika pamoja nami kwa ajili ya Injili, kama mwana na baba yake.”—Wafilipi 1:1; 2:19-22.

20. Ni jambo gani linalomfanya Timotheo awe kielelezo cha cheo chenye kusifika sana kwa vijana?

20 Hakika, kijana Timotheo ni mfano wenye kusifika sana! Yeye alikuwa mwandamani wa Paulo mwenye kutegemeka, mwaminifu, akishikamana naye nyakati nzuri na mbaya, akimtegemeza katika kazi ya kuhubiri, na akiwa na nia ya kutumikia mahali po pote alipotumwa. Yeye alidhabihu yanayoitwa maisha ya kawaida ya nyumbani, hata hivyo, utumishi wa Mungu ulimletea uradhi na utosheki ulioje katika maisha yake! Hakika Timotheo hakuwa ‘hai tena kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, bali kwa ajili ya Kristo aliyekuwa amekufa kwa ajili yake.’ (2 Wakorintho 5:15) Je! wewe unasukumwa kuiga mfano wake?

Ishi kwa Ajili ya Ulimwengu Mpya wa Mungu

21. Kwa nini tunaweza kusema kwamba Timotheo alikuwa mtu mwenye fikira za kiroho?

21 Kweli, Timotheo alikuwa akiishi kwa ajili ya ulimwengu mpya wa Mungu. Yeye hakuwa akifikiria tu mambo ya sasa hivi, bali alikuwa akifikiria kuyatumia maisha yake kutokeza manufaa yenye kudumu. (Mathayo 6:19-21) Kwa kuwa baba yake Timotheo alikuwa Mgiriki na ni wazi kwamba hakuwa mwamini, huenda alimsihi Timotheo afuatie elimu ya juu na kazi ya maisha ya kilimwengu. Lakini kama matokeo ya maagizo ya kimungu kutoka kwa mama na nyanya yake, maisha ya Timotheo yalikuwa yamefungamana pamoja na kundi la Kikristo. Yeye alifuatia mapendezi ya kiroho, yaelekea aliendelea kuwa mseja angaa kwa wakati fulani, na alistahili kutumikia pamoja na mtume Paulo.—2 Timotheo 1:5.

22. Broshua Shule inakaziaje mwendo wa maisha unaofanana na ule wa Timotheo kwa vijana leo?

22 Namna gani wewe? Je! wewe utatumia ujana wako katika njia aliyoutumia Timotheo? Broshua Shule na Mashahidi wa Yehova ilikuwa ikielekeza kwenye njia hiyo ya maisha ilipoeleza hivi kuhusu vijana Mashahidi: “Mradi wao mkubwa katika maisha ni kutumikia vya kufaa wakiwa wahudumu wa Mungu, na wanathamini masomo ya shule kuwa msaada wa kutimiza mradi huo. Basi, kwa ujumla wanachagua mitaala inayofaa ili wajipatie riziki katika ulimwengu wa sasa. Hivyo, huenda wengi wakajifunza mitaala ya kikazi au wakahudhuria shule zinazotoa mafundisho ya kazi. Wanapomaliza shule wanatamani kutafuta kazi itakayowaruhusu wakaze fikira zao juu ya kazi yao kuu, yaani, huduma ya Kikristo.”

23. Kwa sababu gani halipaswi kuwa jambo gumu kwa vijana Wakristo kujibu ulizo hili, Mimi nitafanya nini na maisha yangu?

23 Kwenu ninyi mnaothamini sana yale ambayo Yehova Mungu na Mwana wake wamewafanyia, halipasi kuwa jambo gumu kujibu ulizo hili: “Mimi nitafanya nini na maisha yangu? Badala ya kuishi kwa ajili yako mwenyewe na raha ya kibinafsi, utayatumia maisha yako kufanya mapenzi ya Mungu. Utaishi, kama alivyoishi Timotheo, akiwa mtu wa kiroho.

Maswali kwa Ajili ya Kurudia

◻ Kwa nini haiwapasi Wakristo wa kweli kutanguliza kazi ya maisha ya kilimwengu maishani?

◻ Wengine wametoa shauri gani lenye kosa, hata hivyo tunaweza kujifunza nini kutokana na jibu la Yesu kwa Petro?

◻ Ni katika njia zipi Yesu na Timotheo waliandaa vielelezo bora vya kuigwa na vijana?

◻ Ni nini linalohusika katika kuwa mtu mwenye fikira za kiroho?

[Picha katika ukurasa wa 12]

Luka, ingawa alikuwa tabibu aliyezoezwa, yeye alitanguliza mambo ya Kikristo maishani

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki