Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 9/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Huchukia Mwenendo wa Hila
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kitabu Cha Biblia Namba 39—Malaki
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Wakati wa Kujaribu na Kupepeta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Mungu Huchukia Talaka ya Aina Gani?
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 9/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Ni nini “uzao wa Mungu” unaotajwa kwenye Malaki 2:15, NW?

Mstari huu wenye kutatanisha unasema hivi kwa sehemu: “Na kulikuwa na mmoja ambaye hakufanya jambo hilo, kwa maana yeye alikuwa na kile kilichokuwa kimebakia cha ile roho. Na huyo mmoja alikuwa akitafuta nini? Ule uzao wa Mungu.” “Ule uzao” kwa wazi unamaanisha taifa la Israeli la kale, ambalo wakati mstari huo ulipoandikwa lilikuwa katika hatari ya kuchafuliwa kidini.

Malaki alitoa unabii wakati wa kipindi cha mchakao wa adili za kitaifa. Wanaume fulani Waisraeli si kwamba tu walikuwa wakichukua ‘binti za mungu wa kigeni wawe bibi-arusi’ bali pia walikuwa wakitaliki wake zao asilia wa Kiyahudi, ‘wake wa ujana wao,’ ili wachukue labda wake wachanga zaidi wa kipagani. Hata hivyo, si wanaume wote Waisraeli waliofanya hilo “jambo la kuchukiza sana.” (Malaki 2:11, 13, 14; Kumbukumbu 7:3, 4, NW) Kwa wazi akimaanisha watu mmoja mmoja waliokataa kuvunja agano lao la ndoa pamoja na mwabudu mwenzao wa Yehova, Malaki aliandika hivi: “Na kulikuwa na mmoja ambaye hakufanya jambo hilo, kwa maana yeye alikuwa na kile kilichobakia cha ile roho.”

“Roho” hiyo ni roho takatifu ya Mungu, ambayo yeye alikuwa amemimina juu ya taifa. Hata hivyo, Waisraeli wasiotii walikuwa wakipinga, na kwa sababu hiyo wakihuzunisha, roho hiyo. (Isaya 63:10; Matendo 7:51-53; Linganisha Waefeso 4:30.) Wayahudi fulani mmoja mmoja walikuwa washikaminifu kwa sheria za Mungu, na kwa utii wao walikuwa wamebaki na kile “kilichokuwa kimebaki cha ile roho.” Waabudu hao waaminifu hawakutafuta furaha yao wenyewe ya ubinafsi. Juu ya mtu wa namna hiyo, Malaki aliandika hivi: “Huyo mmoja alikuwa akitafuta nini? Ule uzao wa Mungu.” “Uzao” huo ulikuwa taifa la Israeli la kale, ambalo Malaki alisema ‘liliumbwa na Mungu.’ ‘Uumbaji’ huo ulitokea wakati Yehova alipovuta Waisraeli waingie katika agano pamoja naye kwenye Mlima Sinai, akiwafanya wawe “mali ya pekee” na “taifa takatifu.” “Uzao” ule wa kweli wa Abrahamu ambao ungebariki watu wa dunia yote ungekuja kupitia taifa hilo.—Malaki 2:10; Kutoka 19:5,6; Mwanzo22:18, NW.

Hata hivyo, Waisraeli walipaswa kuendelea kuwa safi kidini kwa kutofunga ndoa za mchanganyiko pamoja na watu wa mataifa ambao hawakumwabudu Yehova. Kutotii Mungu kwa watu hao kungewachafua, kama inavyoweza kuonwa kutokana na hali iliyokuwako wakati wa Ezra. Wakati huo Waisraeli ‘walikubali hesabu fulani ya binti [za mataifa yaliyowazunguka] kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya wana wao; na wao, ule uzao mtakatifu [wakawa] wamechangamana-changamana na jamii za watu wa nchi zile.” (Ezra 9:2, NW) “Ubaya mkubwa” uo huo ulitukia siku za Nehemia, aliyeishi wakati mmoja na Malaki. Wanaume Wayahudi waliokuwa washikamanifu kwa Mungu waliiona hatari ya kiroho iliyokuwapo kwao wenyewe na kwa watoto waliozaliwa kutokana na mwungano huo. Ilikuwapo hatari ya kuvutwa waondolewe katika ibada ya Yehova na mke asiyekuwa amejitolea Yeye. Nehemia hata aliripoti kwamba miongoni mwa Wayahudi hao waliokuwa wamefunga ndoa ya mchangamano, ‘hakuna ye yote wa watoto wao aliyejua jinsi ya kusema Kiyahudi.’—Nehemia 13:23-27, NW.

Wayahudi wasio washikamanifu walikuwa wakitafuta raha yao wenyewe bila kujali madhara mazito ya kidini yaliyokuja juu ya taifa lao, ule “uzao wa Mungu.” Si ajabu kwamba Malaki alionya hivi kwa upole: “Na ninyi watu lazima mjilinde wenyewe kwa habari ya roho yenu, na mtu ye yote asishughulike pamoja na mke wa ujana wake kwa ukorofi!” (Malaki 2:15, NW) Wayahudi waaminifu walilinda roho au mwelekeo wao, ili wabaki wakiwa washikaminifu kwa wake zao Wayahudi. Wanaume hao walithamini sana usafi wa kidini wa “taifa takatifu” lao. Walitamani kwamba watoto wao wasome Neno la Mungu na kukua wampende Yehova, wakichangia nguvu za kidini za taifa hilo.

Wakristo waliojitoa wakfu leo wanahitaji kujizoeza bidii ile ile ya kutawala roho yao, au mwelekeo wao mkuu. Ikiwa wamefunga ndoa, watu hawa mmoja mmoja wanahitaji kuepuka kutaliki wenzi wao wa ndoa kwa uhaini. Na Mkristo mseja anapaswa kutii shauri la mtume Paulo kufunga ndoa “katika Bwana tu,” akiingia katika kifungo hicho cha ndoa pamoja na shahidi mwingine tu aliyejitoa wakfu na kubatizwa wa Yehova.—1 Wakorintho 7:39.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki