Kunyoosha Mambo Kati ya Mungu na Wewe
“Ingawa dhambi za ninyi watu zipase kuwa kama wekundu-mwangavu, hizo zitafanywa nyeupe sawasawa na theluji.”—ISAYA 1:18, NW.
1, 2. (a) Wewe ungeweza kuwazia nini kama mtu fulani angesema: ‘njoo sasa, na acha sisi tusababu mambo pamoja’? (b) Kwa sababu gani haitupasi sisi kutazamia kufanya pamoja na Mungu mashauriano ya nipe nikupe?
KAMA uhusiano wenye migogoro ungekuwa kati ya wewe na mtu mwingine kwa sababu ya kosa au tendo la kukosa fadhili la wakati uliopita, wewe ungeitikiaje maneno haya: ‘Njoo sasa, na acha sisi tusababu mambo pamoja’? Huo ungeweza kuwa mwaliko wa kuketi kwa ajili ya mashauriano ya nipe nikupe, huku kila upande ukikubali kuacha mambo fulani na kuridhiana na upande ule mwingine. Kila mmoja angeweza kudokeza maoni yake, halafu kila mmoja angeweza kukubali kwamba kwa kadiri fulani ni mwenye kosa au ufahamu wake wa jambo haukuwa sawa.
2 Lakini je! wewe ungewazia kwamba katika maana hiyo Muumba angesihi hivi, “Njooni sasa, na mwache sisi tusababu mambo pamoja [tusemezane, UV],” kama vile Isaya 1:18 inavyosomwa katika Biblia nyingi? Sivyo hata kidogo. Hakuna ye yote kati yetu angeweza kutazamia ‘kujadiliana jambo’ (The New English Bible) au kuwa na mashauriano ya nipe nikupe pamoja na Yehova, kama kwamba yeye angeweza kuhitaji kukubali alikuwa na kosa na kuridhiana. Ingawa hivyo, ikiwa sisi tunataka amani pamoja na Mungu, Isaya 1:18 inataka nini?
3. Ni nini maana inayofaa ya neno la Kiebrania ambalo nyakati fulani linatafsiriwa ‘kusababu mambo pamoja’ [‘kusemezana,’ UV] kwenye Isaya 1:18?
3 Neno la Kiebrania lililofasiriwa “kusababu mambo pamoja” linamaanisha kwa msingi “amua, toa hukumu rasmi, thihitisha.” Hilo lina ladha ya kisheria, likigusia maana ambayo haihusu tu kusababu mambo pamoja kwa watu wawili. Uamuzi fulani ulihusika.a (Mwanzo 31:37, 42; Ayubu 9:33; Zaburi 50:21; Isaya 2:4) Wilson’s Old Testament Word Studies inatoa maana ya “kuwa sawa; kusababu, kuonyesha jambo ambalo ni sawa na kweli.” Mungu alikuwa anaamuru hivi: “Njooni sasa, na mwache sisi tufanye mambo yawe sawa” (The New American Bible) au, “Acheni sisi tunyooshe mambo.”
4-6. Isaya alikuwa nani, na ni wakati gani yeye alitumikia akiwa nabii?
4 Yehova Mungu alitumia nabii Isaya kutoa ujumbe huo wenye nguvu. Isaya alikuwa nani? Na kwa sababu gani ujumbe wake ulifaa katika wakati wake? Zaidi ya hilo, ni jinsi gani sisi tunaweza kunufaika kutokana na huo?
5 Kwa kutaja “nabii,” wengi leo wangeweza kutunga fikira za kwamba yeye alikuwa kijana mwanamume mwenye kujinyima mno raha ambaye alikuwa akitangaza maoni yake yaliyopotoshwa juu ya jinsi maisha yalivyo hasa. Wengine wangeweza kufikiri kwamba alikuwa kizee cha kiajabu-ajabu chenye kujifanya hakimu wa hali zilizokuwako. Mwanamume Isaya mwenye usawaziko na mwenye uwezo wa kusababu mambo, ambaye Yehova Mungu alitumia kuandika kitabu kile cha Biblia chenye jina lake, alikuwa tofauti kama nini na fikira kama hizo!
6 “Isaya mwana wa Amozi” aliishi katika Yuda na alitumikia Yehova kwa vitendo sana “katika zile siku za Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda”—zaidi ya miaka 40. Kwa kuwa mwenye kiasi, Isaya hakuandaa habari nyingi kuhusu yeye mwenyewe. Pokeo linasema kwamba yeye alikuwa wa ukoo wa jamaa ya kifalme ya Yuda. Sisi tunajua kwa uhakika kwamba yeye alikuwa mwanamume mwenye jamaa ambaye mke wake alimzalia wana wawili. Huenda yeye akawa alifunga ndoa upya baada ya mwanamke huyo kufa, akawa baba kwa mwana mwingine, ambaye kwa unabii aliitwa Imanueli.—Isaya 1:1; 7:3, 14; 8:3, 18, NW.
7. Kwa sababu gani sisi tunapaswa kupendezwa na unabii wa Isaya?
7 Kuna mifanano kati ya wakati wa Isaya na wetu. Wewe umeona kwamba sisi tunaishi katika wakati wa mkazo wa kimataifa, wa vita au matisho yanayotokana na mambo hayo. Ingawa viongozi wa kidini na kisiasa ambao wanadai kuabudu Mungu wanajitokeza mbele kama mifano ya kufuatwa, sisi kwa ukawaida tunaona ripoti za magazetini juu ya matendo yao ya kashifa zinazohusu pesa na adili. Mungu anaonaje viongozi hao, hasa wale walio na ukamatano pamoja na Jumuiya ya Wakristo? Ni nini kilicho mbele yao na ya wale wanaowafuata? Katika kitabu cha Isaya, sisi tunapata .maelezo ya kimungu ambayo yanahusu sana mambo hayo ya wakati wa sasa. Sisi pia tunapata masomo kwa kila mmoja wetu wakati sisi tunapojitahidi kibinafsi kutumikia Mungu.
Nabii kwa Taifa Lenye Hatia
8. Kitabu cha Isaya kina mambo gani, na kiliandikwa kwa namna gani?
8 Unaposoma kitabu cha Isaya, wewe utaona ujumbe mbalimbali juu ya hatia ya Yuda na Yerusalemu, maelezo marefu ya kihistoria juu ya mivamio iliyofanywa na adui, matangazo rasmi ya ukiwa wa mataifa yenye kuzunguka, na matabiri yenye kutia moyo ya kurudishwa na kupewa wokovu kwa Israeli. Mambo hayo yameandikwa kwa uwazi wenye kuvuta sana, wenye kunasa fikira. Dakt. I. Slotki anasema: “Wanachuo wanatoa sifa ya moyo wote kwa jinsi Isaya alivyokuwa na fikira za hali ya juu sana na kwa mifafanuo yake yenye kufanya maumbo ya vitu yadhihirike wazi kabisa katika akili, ufundi wake wa kutumia semi zinazovutia za ukarina, usanifu wa kuanzisha maneno kwa herufi ile ile moja, ustadi wa kupatanisha milio ya maneno, na usawaziko ule mzuri na mtitiriko wa vina vya sentensi zake.” Acheni tuchunguze hasa ujumbe wa utangulizi wa Isaya—unaopatikana katika sura ya 1.
9. Sisi tunajua nini juu ya wakati na hali za kuandikwa kwa Isaya sura ya 1?
9 Nabii hasemi barabara ni wakati gani yeye aliandika sura hiyo. Isaya 6:1-13 ni ya tarehe ya kuanzia mwaka ule ambao Mfalme Uzia alikufa. Kwa hiyo ikiwa Isaya aliandika sura zake za utangulizi mapema kidogo, huenda hizo zikawa zinaonyesha hali iliyokuwa ikiendelea chinichini wakati wa umaliki wa Uzia. Kwa msingi, Uzia (829-777 K.W.K.) “aliendelea kufanya mambo yaliyokuwa wima katika macho ya Yehova,” kwa hiyo Mungu alibariki utawala wake kwa ufanisi. Hata hivyo, sisi tunajua kwamba si mambo yote yaliyokuwa sawa, kwa maana “watu bado walikuwa wakitoa dhabihu na kufanya moshi wa kidhabihu juu ya mahali-mahali pa juu” kabla Mungu hajapiga Uzia (au, Azaria) kwa ukoma kwa sababu ya kufanya kimbelembele kutoa uvumba katika hekalu. (2 Nyakati 26:1-5, 16-23; 2 Wafalme 15:1-5, NW) Ubaya uliokuwa chinichini katika wakati wa Uzia huenda ukawa ndio ulioongoza kwenye wingi wa uovu tunaosoma ambao ulihusu Mfalme Ahazi mjukuu wake (762-745 K.W.K.), ambao pia labda ndio ule Isaya alikuwa akisimulia. Lakini ni jambo la maana kuliko tarehe fulani ya wazi kuhusiana na sura ya kwanza lililofanya Mungu aseme: “Acheni sisi tunyooshe mambo kati yetu.”
10. Wakati wa utawala wa Mfalme Ahazi, ni hali gani iliyokuwa imeenea sana katika Yuda, hasa miongoni mwa viongozi?
10 Isaya alitangaza hivi kwa kutoboa mambo wazi: “Ole kwa lile taifa lenye dhambi, wale watu walio na uzito wa makosa, mbegu inayotenda maovu, wana wenye kufanya uharibifu! Wao wameacha Yehova, wao wametenda yule Mmoja Mtakatifu wa Israeli kwa ukosefu wa staha, wao wamegeuka kuelekea nyuma. . . . Kichwa kizima kimo katika hali ya ugonjwa, na moyo mzima ni dhaifu. Kutoka wayo wa mguu hata kwenye kichwa hapana mahali penye afya katika huo.” (Isaya 1:4-6, NW) Utawala wa miaka 16 wa mfalme Ahazi ulijawa sana na ibada ya sanamu iliyokuwa mbaya sana. Yeye aliteketeza “wana wake [kama dhabihu] katika moto, kulingana na mambo ya kuchukiza sana ya mataifa yale . . . Na yeye kwa ukawaida... alifanya moshi wa kidhabihu katika pale mahali-mahali pa juu na juu ya vilima na chini ya kila namna ya mti wenye kusitawi sana.” (2 Nyakati 28:1-4; 2 Wafalme 16:3, 4, NW) Matendo ya ukosefu wa haki, rushwa, na ukosefu wa adili yalienea sana miongoni mwa wana-wafalme, ambao walifaa zaidi kuwa watawala katika Sodoma wa kale. (Isaya 1:10, 21-23; Mwanzo 18:20, 21) Kwa uhakika, Mungu hangeweza kuwakubali. Tena watu wangeendeleaje wakiwa na viongozi kama hao?
11. Ni jinsi gani sisi tunapaswa kufahamu Isaya 1:29, 30?
11 Nabii Isaya alitoa mfano wa hali yenye kusikitisha sana ya watu kwa kutaja miti mitakatifu na bustani ambako wao walifanya matoleo ya dhabihu za kuabudu sanamu na wakafukiza uvumba kwa miungu ya kipagani. Hiyo “miti hodari kwa nguvu” ingekuwa kisababishi cha aibu. Akigeuza usemi wake wa mifano uelekee waabudu sanamu wenyewe, Isaya aliandika: “Ninyi mtakuwa kama mti mkubwa ambao majani yao yananyauka, na bustani ambayo haina maji.” (Isaya 1:30, NW) Ndiyo, watu wanaoacha Yehova ‘wangekuja kwenye kikomo chao’ wao wangekuwa kama makumbi yenye kuchomeka ya kitani, na sanamu zao zingekuwa kama cheche ya moto —vyote viwili viteketezwe.—Isaya 1:28, 31.
12, 13. Ni mambo gani yanayofanana yanayoweza kuonyeshwa kati ya wakati wetu na wa Isaya?
12 Sasa linganisha hali hiyo na ile ya leo. Katika muda usiozidi mwezi mmoja magazeti katika United States yaliripoti hivi: Mtu mmoja mashuhuri mwenye kugombea cheo cha urais aliacha kugombea kwa kuhusika katika kashifa iliyohusu ripoti za kwamba yeye alikuwa mtembeana-wanawake; kiongozi wa kidini aliye mashuhuri aliondolewa cheo kikachukuliwa na mwingine baada ya kuungama uzinzi na kushtakiwa juu ya ugoni-jinsia-moja, juu ya tendo la kubadilishana mke, na utumizi mbaya wa pesa kwa kuwalipa watu ili wasiseme mambo hayo. (Yeye “alisemekana kwamba alikuwa amechomoa kiasi kikubwa ajabu cha dola milioni 4.6 kulipia makosa yake tangu 1984.” Time Mei 11, 1987) Katika Austria mwaka uliopita, yule Mtawa Mkuu wa Rein ‘aliondoshwa kazini na kuwekewa shtaka la kutapanya-tapanya dola milioni 6 akiwa mashambani katika nyumba za starehe za kuwinda wanyama na kuwafanyia karamu-karamu washiriki wa ile jamaa iliyokuwa yenye utawala na kuhusiana na wanawake wenye malezi yasiyo ya kisharifu sana.’ Labda wewe ungeweza kutoa mifano mingine ya viongozi kama hao. Je! wewe unafikiri maoni ya Mungu ni nini juu yao?
13 Kuhusu watu kwa ujumla, kuna ongezeko la kuwa na maoni ya kupita kiasi kabisa kuhusiana na dini, upande mmoja au mwingine. Watu fulani wanageuka kutoka kwenye dini kwa kuchukizwa au kutojali. Kwa mfano, ni asilimia 3 tu ya idadi ya watu wa Uingereza ambao wanahudhuria kanisa lile la tangu zamani. Kwa upande ule mwingine, tunapata uanadini wa kupita kiasi. Jambo hilo linaonekana wazi katika makanisa yanayokua ya kikarisma, ambayo yanatumia njia yao ya kusisimua-sisimua maoni ya watu ili “waokolewe,” njia ya kusema lugha, au kuona wagonjwa “wakiponywa.” Makutano ya watu yanamiminika kwenye sehemu zinazoonwa kuwa takatifu wakitumaini kuona miujiza. Wengine wanafanya dhabihu kama vitendo vya “imani,” kama vile kutambaa chini huku magoti yakitokwa na damu ili wakaone yule Bikira wa Guadalupe [Mji wa Meksiko]. Karatasi moja yenye habari ilisema: “Ingawa huenda kwa watu wa nje kuwako kwa bikira huyo na ile bidii ambayo kwayo yeye anaabudiwa kukaonekana kuwa ni kuchanganya vibaya sana Ukristo na upagani, Bikira huyo pasipo ubishi wo wote ndiye kitu cha maana zaidi katika Ukatoliki wa Meksiko.”
Ni Jinsi Gani Wewe Unaweza Kupata Upendeleo Wake?
14. Kupitia Isaya, ni jinsi gani Yehova alionyesha wazi kwamba Yeye hakubali watu wote ambao wanadai kuabudu Yeye?
14 Yehova Mungu haachi kuwe na mvurugo wo wote juu ya maoni yake kuhusu wale ambao wanadai kuwa upande wake lakini ambao hawataki ‘kuabudu Baba kwa roho na ukweli.’ (Yohana 4:23, NW) Ikiwa taifa fulani, kikundi fulani cha kidini, au mtu fulani hatendi kulingana na viwango vya Mungu vilivyofunuliwa, mwonyesho wo wote wa kidini ni bure. Mathalani sikukuu na dhabihu za kidini zilikuwa sehemu ya matakwa ya ibada ya kweli katika Israeli wa kale. (Walawi, sura za 1-7, 23) Hata hivyo, Isaya alionyesha wazi maoni ya Mungu—kuchukizwa na Wayahudi wasio waaminifu wenye kushika miadhimisho hiyo. Mungu alisema: “Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia.” (Isaya 1:11-15) Hivyo ndivyo ilivyo leo. Badala ya kutaka sherehe tupu za kidini au mitajo ya itikadi na sala za kukariri tu, Mungu anataka sala na matendo yanayofaa ambayo yanatoka kwenye moyo.
15. Kwa sababu gani Isaya 1:18 inatupa sisi sababu ya tumaini, na ni nini maana ya maneno ‘Njooni na mwache sisi tunyooshe mambo’?
15 Kujua kwetu jambo hilo kunaandaa msingi wa tumaini. Wanadamu wanaweza kupata upendeleo wa Mungu. Jinsi gani? Isaya alihimiza: “Jiosheni ninyi wenyewe; jifanyeni safi ninyi wenyewe; ondoeni ubaya wa shughuli zenu kutoka mbele ya macho yangu; acheni kutenda mabaya. Jifunzeni-kutenda mema; tafuteni haki.” Kufikia hapo Isaya alitokeza amri ya Mungu: “Njooni, sasa, ninyi watu, na mwache sisi tunyooshe mambo kati yetu.” Kwa hiyo Yehova hakuwa akiomba kuwe na kipindi kati ya watu wa cheo kimoja ambao wangeketi wafanye mashauriano ya nipe nikupe. Mungu alijua jambo ambalo lilikuwa la kufaa, au la kunyooka. Hukumu yake ilikuwa: Mabadiliko yo yote ambayo, yanahitajiwa yatapasa kuwa kwa upande wa wanadamu,.. ambao .walihitaji kujipatanisha na viwango vyake vya haki na uadilifu. Ndivyo ilivyo leo pia. Badiliko linawezekana, matokeo yakiwa kupata upendeleo. Hata mtu ambaye mwendo wake umekuwa mbaya kweli kweli anaweza kubadilika. Isaya aliandika: “Ingawa dhambi za ninyi watu zipase kuwa kama wekundu mwangavu, hizo “zitafanywa nyeupe sawasawa na theluji”—Isaya 1:16 18, NW.
16. Ni jinsi gani watu fulani wameitikia shauri lenye msingi wa Biblia kuhusu kufanya makosa?
16 Hata hivyo, kuna elekeo la kuangalia shauri kama hilo lakini kufikiri kwamba linatumika kwa wengine. Kwa wazi, wengi katika siku za Isaya walifanya hivyo. Kwa kweli, kila mtu mmoja mmoja anapaswa kujichunguza mwenyewe. Ikiwa Mkristo ana hatia ya dhambi nzito, iwe ni kusema uwongo, kupunja, kukosa adili ya ngono au makosa mazito mengine, toba na kazi zinazoifaa toba ni za muhimu. (Matendo 26:20) Jambo la kusifika ni kwamba watu fulani wamechukua hatua kunyoosha mambo kati yao na Yehova.’ Kwa mfano Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 1985 na Oktoba 15, 1985, lilizungumzia jambo la kurekebisha makosa ambayo yangeweza kuwa ya siri kwa watu wa nje lakini yanaonwa na Mungu. (Mathayo 6:6; Wafilipi 4:13) Maeneo matatu ya kuelekezewa fikira yalitajwa, kukubali kisiri kutiwa damu mishipani, kupiga punyeto, na utumizi mbaya wa kileo. Baada ya kufikiria habari hizo, hesabu kubwa ya wasomaji waliandika barua za uthamini; wao walikiri kwamba walikuwa wamekuwa na makosa hayo, lakini wao walikuwa wamesukumwa na moyo kutubu na kubadilika.
17. Hata ikiwa sisi hatutendi makosa mazito, ni jinsi gani Isaya 1:18 inaweza kutumika kwetu sisi na kutusaidia?
17 Bila shaka, Wakristo walio wengi wanaofikiria jambo hili hawana hatia ya mwenendo mbaya sana. Hata hivyo, ujumbe wa Isaya bado unapasa kusukuma sisi tufanye uchunguzi wa kujipekua-pekua moyoni. Je! sisi tungeweza kuwa tunahitaji kunyoosha jambo fulani pamoja na Mungu? Jambo moja la maana kabisa la ujumbe wa Isaya lilikuwa kuwa na kusudio linalofaa la moyoni. Kwa habari ya sala, mtu angeweza kuuliza: ‘Je! sala zangu zinatoka katika moyo wangu, na je! ninapatanisha vitendo vyangu na sala zangu kwa kadiri ya uwezo wangu wote?’ Watu fulani wanaofanya uchunguzi huo wameona nafasi ya maendeleo. Wao walikuwa wamekuwa wakisali wapate maarifa yaliyoongezeka ya mapenzi ya Mungu, na bado wao walitumia wakati mdogo wakijifunza Biblia na vichapo vya Kikristo. Wengine walikuwa wamekuwa wakisali kuwa na ushiriki mkubwa zaidi katika huduma, lakini wao walifuatia namna ya maisha ambayo haikuruhusu wakate mapato yao kwa kupunguza kazi yao ya kimwili. Au je! wewe umesali kwamba Mungu abariki kazi yako ya kufanya wanafunzi? Basi, ni kwa kadiri gani wewe unajitahidi ili uwe mwalimu mwenye matokeo? Je! wewe kwa dhamiri umeongezea kufanya ziara za kurudia na kuwa mwenye nia ya kutoa wakati fulani uwe wa kuongoza funzo la ukawaida la Biblia pamoja na mwingine? Kujitahidi mwenyewe kupatana na sala zako kutaonyesha kwamba wewe unataka kwa moyo mweupe Mungu asikilize.
18. Kwa sababu gani sisi tunapaswa kuelekeza fikira juu ya kunyoosha mambo kati yetu na Mungu?
18 Inafaa kabisa kwamba kila mmoja wetu ajitahidi ‘kunyoosha’ pamoja na Mungu, Muumba wetu, pande zote za maisha yetu. Angalia jinsi Isaya alivyosababu mambo kuhusiana na hilo: “Ng’ombe amjua bwana wake, na punda ajua kibanda cha bwana wake; bali Israeli hajui, watu wangu hawafikiri.” (Isaya 1:3) Hakuna ye yote kati yetu ambaye angependa kufananishwa kuwa aliyepungukiwa kujua au kuthamini mambo kuliko ng’ombe au punda. Ingawa hivyo, elezo hilo lingetumika kama sisi tungehisi kwamba sisi hatuhitaji kujitahidi kujifunza juu ya Mpaji-Uzima wetu na matakwa yake halafu tujaribu kwa bidii kuishi kulingana nayo.
19. Ni taraja gani ambalo Isaya alieleza kwa ajili ya wale wanaonyoosha mambo pamoja na Mungu, na jambo hilo lina maana gani kwetu?
19 Isaya alitolea watu wake sababu ya kutazamia mazuri. Yeye alisema kwamba msimamo wao mbele za Yehova ungeweza kugeuzwa uwe mmoja uliotakata. Ungeweza kuwa kama nguo iliyo nyekundu kama damu ambayo ingekuwa nyeupe kama sufi au kama theluji inayofunika kilele cha Mlima Hermoni. (Isaya 1:18, NW; Zaburi 51:7; Danieli 7:9; Ufunuo 19:8) Hata ikiwa walio wengi zaidi hawakuitikia, na hivyo lile taifa likapewa kwenye upanga na katika ya utekwa, baki lenye uaminifu lingeweza kurudi. Vivyo hivyo, sisi tunaweza kupata upendeleo wa Yehova, labda kwa usaidizi wa waangalizi wanaodhamiria kufanya mambo kwa bidii, ambao wanatumikia katika kundi wakiwa ‘waamuzi na washauri’ wenye upendo. (Isaya 1:20, 24-27; 1 Petro 5:2-4; Wagalatia 6:1, 2) Kwa hiyo uwe na uhakikisho, wewe unaweza kunyoosha mambo kati ya wewe na Mungu. Au, ikiwa wewe tayari una upendeleo wa Mungu, wewe unaweza kuutia nguvu uhusiano wako pamoja na yeye. Kwa kweli jambo hilo linastahili ulifanyie kila jitihada.
[Maelezo ya Chini]
a Dakt. E. H. Plumptre anaeleza: “Ile [fasiri katika King James Version] inadokeza wazo la mazungumzo kati ya watu wa cheo kimoja. Badala ya hivyo neno la Kiebrania linagusia maana ya mmoja ambaye anatoa amri-mkataa ya kimamlaka, kama lile lenye kutoka kwa hakimu kuambia mshtakiwa.”
Mambo ya Kurudia
◻ Ni jambo gani ambalo lilimaanishwa na ile amri ‘njooni kunyoosha mambo’ pamoja na Mungu?
◻ Ni jinsi gani wakati wa Isaya ulifanana na wetu?
◻ Ni nini ambalo Isaya alionyesha lilihitajiwa kwa watu mmoja mmoja ili kupata upendeleo wa Mungu
◻ Kando na dhambi nzito, ni katika maeneo gani sisi tungeweza kuhitaji kunyoosha mambo kati yetu na Mungu?
[Picha katika ukurasa wa 10]
Mainamizi yenye theluji ya Mlima Hermoni, kutazama upande wa kusini-magharibi ng’ambo ya sehemu ya juu ya bonde la Yordani kwenye vilima vya Galilaya
[Credit Line]
Photos, pages 10, 31: Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.
[Picha katika ukurasa wa 13]
Isaya alisema kwamba “punda ajua kibanda cha bwana wake.” Mna somo gani katika jambo hilo?