Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 12/1 kur. 25-27
  • Thamani ya Kuimba Katika Ibada ya Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Thamani ya Kuimba Katika Ibada ya Kweli
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Ni Mungu wa Wimbo
  • Kuimba Katika Nyakati Zilizotangulia Zile za Ukristo
  • Kuimba Katika Nyakati za Kikristo
  • Tumia kwa Ukamili Uimbaji wa Kitheokrasi
  • Sisi Sote Tunaweza Kufanya Maendeleo
  • Manufaa Ni Nyingi
  • Imba kwa Shangwe na Sauti Kubwa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Mahali pa Muziki Katika Ibada ya Kisasa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Mwimbie Yehova Sifa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Kumsifu Yehova kwa Wimbo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 12/1 kur. 25-27

Thamani ya Kuimba Katika Ibada ya Kweli

E! WEWE unaweza kuwazia kuwa katika ulimwengu bila nyimbo? Usisikie tena kamwe kuimba kwa watoto wenye furaha au ile sauti tamu ya ndege-mwimba-usiku au ndege-mpiga-kengele? Usisikie tena kile kicheko chenye kuambukiza wengine cha ndege anayeitwa magpai au kicheko kinachojitokeza kooni mwa ndege anayeitwa kookaburra? Kwa furaha, jambo hilo halitatukia kamwe. Lakini kufikiria jambo hilo kunakazia moja ya zawadi nyingi ambazo Mungu amempa mwanadamu: ile zawadi ya wimbo.

Yehova Ni Mungu wa Wimbo

Kwa sababu gani kuimba kunatuletea sisi sote raha na furaha? Kwanza, Yehova mwenyewe anafurahia na anapendezwa na nyimbo za sifa kutoka kwa viumbe wake. Je! wewe unaweza kuwazia ile pindi ambayo malaika wote walipaaza sauti kwa furaha kwa sababu ya uadimu wa uumbaji wa kidunia wa Yehova? Au je! wewe unaweza kujiwazia ukiwa umesimama kwa kuduwaa sana miongoni mwa wachungaji usiku wa majira ya vuli ambapo uzawa wa Yesu wa kibinadamu ulitukia, huku ukisisimuliwa na sauti ya kikosi kikubwa cha malaika wakiimba hivi: “Atukuzwe Mungu juu mbinguni”?​—Luka 2:13, 14; Ayubu 38:7.

Njia moja ambayo Yehova alionyesha kwamba yeye ni Mungu wa wimbo ni kwa kufanya kuimba kuwe sehemu ya ibada ya kweli katika Israeli. Baadaye, Mungu alifunua tena kifungo cha karibu kilichoko kati ya kuimba na ibada ya kweli katika njozi ya Ufunuo aliyopewa mtume Yohana. Katika tamasha moja ya kiunabii kundi la waimbaji wengi ajabu—144,000 barabara—linaimba wimbo mpya ulio adimu mbele ya kiti cha Mungu.​—Ufunuo 14:3.

Kuimba Katika Nyakati Zilizotangulia Zile za Ukristo

Fahari ya Mungu na vitendo vyake vya kustaajabisha sana viliingiza roho pia katika watumishi wake wa kidunia ya kufungulia hisia zao za moyo kwa wimbo. Ebu hisi matokeo yenye kuchochea ambayo kuimba kulikuwa nayo kwa Waisraeli mara tu baada ya wao kukombolewa kwa muujiza katika utumwa wa Misri. Mioyo ya Musa na wanaume wenzake Waisraeli ilisukumwa na hisia za moyoni walipokuwa wakiimba wimbo wa ushindi wenye kusimulia yale ambayo Yehova alikuwa ametenda Farao na vikosi vyake.—Kutoka 15:1-21.

Baadaye katika historia ya Israeli, ile siku ya maana sana ilifika wakati, chini ya mwelekezo wa mfalme Daudi, sanduku la agano lilipaswa kuwekwa ndani ya hema lalo lililokuwa limepigwa chini kwa njia ya pekee. Hilo lilikuwa tukio la kihistoria kama nini! Si uimbaji tu wenye kutokeza bali pia mfuatanisho wa vyombo vingi vya kimuziki uliongezea utukufu wa siku hiyo.—1 Nyakati 16:4-36.

Upendo wa Daudi kwa muziki na ustadi wake wa kutumia kinubi uliongezea kuonyesha juhudi yake ya kuendeleza muziki na uimbaji katika ibada ya kweli. Kwenye Zaburi 33:1, 3, NW, sisi tunasikia ombi lake lenye harara kwa waabudu wa Yehova waimbie Mungu kwa sauti kubwa kwa moyo wao wote: “Pazeni mlio kwa furaha nyingi, E ninyi waadilifu, kwa sababu ya Yehova. . . . Fanyeni yote mwezayo katika kupiga zile nyuzi pamoja na mpazo wa sauti wenye kujaa furaha.”

Kuimba Katika Nyakati za Kikristo

Katika nyakati za mapema za Kikristo, kuimba kulikuwa na mahali penye kutokeza pia katika ibada ya kweli. Yesu na mitume wake waliimba pamoja baada ya chakula cha jioni kabla tu ya kifo cha Yesu. (Marko 14:26) Katika gereza Paulo na Sila waliimba kwa sauti kubwa hivi kwamba watu wote wangeweza kusikia. (Matendo 16:25) Kama Daudi, mtume Paulo alikuwa na idili juu ya utumizi wa wimbo. Zaidi ya mara moja, yeye aliwatia moyo waitikadi wenzake waimbie Yehova nyimbo za sifa.—Waefeso 5:18, 19; Wakolosai 3:16.

Katika ibada ya kisasa ya Kikristo, uimbaji una sehemu ya kutokeza pia. Katika 1905 kitabu Hymns of the Millennial Dawn kilichapishwa. Ukurasa wenye kichwa unaeleza nyimbo zacho 333 kuwa “Mkusanyo Bora wa Zaburi na Tenzi na Nyimbo za Kiroho za Kuwasaidia Watu wa Mungu Katika Kumwimbia na Kumsifu Bwana Katika Mioyo Yao.”

Halafu katika 1928 kitabu kilichosahihishwa chenye nyimbo 337 kiliandaliwa. Kiliitwa Songs of Praise to Jehovah, (Nyimbo za Sifa kwa Yehova), na dibaji yacho ilisema: “Nyimbo hizi zitaonwa kuwa zimepatana na kweli za kimungu ambazo sasa zitafahamika.” Hata hivyo, miaka ilipoendelea kupita na nuru ya ukweli ikaongezeka, ilikuwa wazi kwamba nyingine za nyimbo hizo ziliongozwa na mawazo yalitokana na dini isiyo ya kweli. Kuongezea hilo, zilihitajiwa nyimbo za Ufalme za kutia moyo kuhubiri habari njema, kwa kuwa tangazo la waziwazi lilianza kukaziwa zaidi.​—Mathayo 24:14; Waebrania 13:15.

Katika 1944 Kingdom Service Songbook (Kitabu cha Nyimbo cha Utumishi wa Ufalme) kiliandaliwa, kikiwa na nyimbo 62. Miongo miwili baadaye, katika 1966, (kwa Kiingereza) kitabu Kuimba na Kufuatana Wenyewe na Muziki Katika Mioyo Yenu kilitolewa. Kitabu hicho kilikuwa na nyimbo za Ufalme 119 ambazo zilihusu kila upande wa maisha na ibada ya Kikristo, kutia na kutolea wengine ushuhuda na kusifu Yehova Mungu na Kristo Yesu.

Karibu miongo mingine miwili ilipita wakati ambapo nuru ya ukweli iliendelea kuongezeka. (Mithali 4:18) Uhitaji ulionekana wa kitabu kingine cha nyimbo. Kwa hiyo katika 1984 (katika Kiingereza) kilitolewa kitabu cha nyimbo chenye kichwa Mwimbie Yehova Sifa. Kina nyimbo za Ufalme 225, zenye maneno na midundo mitamu ambayo yote yote kabisa imetungwa na watumishi wa Yehova waliojitoa wakfu kutoka sehemu zote za dunia.

Tumia kwa Ukamili Uimbaji wa Kitheokrasi

Mfano ulionyeshwa katika karatasi mbili za mwisho upande wa nyuma wa kitabu cha nyimbo hicho cha karibuni unatuchochea sisi kutumia uimbaji wa kitheokrasi kwa ukamili kwenye mikutano ya Kikristo. Waimbaji wa hekaluni waliopewa mazoezi ambao wameonyeshwa humo wanaonekana kwa wazi kuwa wanainua mioyo yao na sauti zao kwa kuimbia Mungu.—1 Nyakati 25:7.

Vile vile sisi tunaweza kuimba kwenye mikutano yetu ya Kikristo, tukifungua vinywa vyetu na kuimba kutoka mioyoni mwetu. Hata hivyo, si sisi sote tunaofanya hivyo. Labda kiburi kinasababisha sisi tukose furaha ya kuimbia Yehova bila kuona haya, hata kama tuna sauti ya namna gani. Huenda ikawa sisi tunahangaikia kupita kiasi wazio ambalo tunawapa wale waliosimama karibu nasi. Musa alikuwa na tatizo linalofanana na hilo—si kuhusu kuimba, bali kusema. Jibu ambalo Yehova alimpa yeye lingeweza kutusaidia sisi ikiwa tuna elekeo la kusita-sita kuimba kwa sababu ya ukosefu wa uwezo. Yehova alimwuliza Musa: “Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? . . . Si mimi, BWANA [Yehova, NW]?” (Kutoka 4:11) Kwa uhakika, Yehova atasikiliza kwa furaha wakati sisi tunapotumia uwezo wo wote ambao yeye ametupa sisi kuimba sifa zake kwa sauti kubwa!

Pia, fikiria jinsi Paulo na Sila walivyoimba kwa sauti kubwa walipokuwa gerezani. Hakukuwa na haya hapo, na hawakuwa na mfuatanisho wa vyombo vya kimuziki, hata hawakuwa hata na kitabu cha nyimbo cha kufuatia. Ebu piga akilini picha ya pindi hiyo: “Lakini yapata katikati ya usiku Paulo na Sila walikuwa wakisali na kusifu Mungu kwa wimbo; ndiyo, wale wafungwa walikuwa wakiwasikia wao.” (Matendo 16:25, NW) Je! hiyo ilikuwa kwa sababu ama Paulo ama Sila alikuwa na sauti iliyopata mazoezi rasmi? Si kwa lazima. Hangaikio lao kuu lilikuwa kuimba kwa sauti kubwa na kutoka moyoni! Ni nini hangaikio letu kuu wakati tunapoimba nyimbo za sifa?

Sisi Sote Tunaweza Kufanya Maendeleo

Shauri la mwanamuziki Daudi linafaa hapa: “Fanyeni yote mwezayo katika kuzipiga zile nyuzi pamoja na mpazo wa sauti wenye kujaa furaha.” (Zaburi 33:3, NW) Hilo ndilo jambo ambalo Yehova anatazamia kutoka kwa watumishi wake wote—si zaidi, wale si kidogo kuliko kwamba sisi ‘tufanye yote tuwezayo.’ Tukifanya lilo hilo, sisi tunaweza kutazamia Yehova abariki jitihada zetu, na kwa furahio letu—na nyakati nyingine kwa mshangao wetu—inaelekea sisi tutafanya maendeleo.a

Hapa pana madokezo fulani yanayofaa ambayo huenda yakasaidia kufanyia maendeleo ubora wa uimbaji wako: Jaribu kusikiliza mara kwa mara ile midundo mitamu ya Ufalme iliyo mipya zaidi, ukitumia kanda za kimuziki au sahani za santuri inapowezekana. Kwa watu fulani, kuziimba nyimbo nyumbani au kwenye vikusanyiko pamoja na waitikadi wenzetu kumethibitika kuwa jambo lenye manufaa na pia lenye kufurahisha. Kwenye mikutano ya kundi ni jambo la maana kwamba mfuatanisho wa kimuziki upigwe kwa sauti kubwa kutosha kusikiwa na wote wale wanaoimba. Jambo hilo linafanya iwe rahisi zaidi kufuata sauti ya wimbo na linaongeza uhakika upande wa wale wanaoimba. Yule mmoja anayetangaza wimbo anapaswa kusema kichwa chao, labda hata akitaja unafaa kwa njia gani, wala si kusema namba tu.

Wazazi, je! ninyi mnawatia moyo watoto wenu waimbe nyimbo za Ufalme kwa idili na kutoka mioyo yao? Jamaa ambazo zimewatia moyo watoto wazo waimbe kutoka moyoni, na kwa ufahamu, mara nyingi zinapata kwamba huu ni msaada mzuri sana kwa ukuzi wa kiroho.

Manufaa Ni Nyingi

Kuna manufaa nyingi zinazopatikana kwa kuimba kwa sauti kubwa na kutoka moyoni. Kuhusika kwetu kibinafsi katika ibada ya waziwazi kunakuwa kwenye nguvu zaidi. Wale ambao wanasimama karibu wanatiwa moyo kuimba kwa sauti kubwa zaidi wanaposikia tukiimba bila haya. Kundi lote pia linanufaika, kwa maana sauti iliyoongezwa inaambukiza wengine!

Kwa kuongezea, kuimba kwa sauti yenye nguvu kunatoa ushuhuda mzuri kwa wale wanaohudhuria mkutano kwa mara ya kwanza. Wale wanaopita karibu na Majumba ya Ufalme yetu, vilevile majirani wanaoishi karibu, wanavutiwa na kuimba kwetu kuzuri sana, sawasawa na vile walivyovutiwa bila shaka wale wanagereza wengine ambao walisikia Paulo na Sila. Jambo hilo hata limefanya wasikiaji fulani watake kujua mengi zaidi juu ya ukweli.

Jambo la maana zaidi, kuimba kwetu kulikofanyiwa maendeleo kutamletea sifa kubwa zaidi Yehova, yule Mwanzilishi wa muziki na kuimba, yule mmoja anayestahili kusifiwa kwa wimbo juu ya wengine wote.

[Maelezo ya Chini]

a Nyingine za nyimbo zilizo za karibuni zaidi huenda zikawa ngumu kidogo kuimba mara ya kwanza, lakini baada ya kuzizoea, huenda zikathibitika kuwa ndizo tunazopenda zaidi. Mathalani, wakati kitabu cha nyimbo kilichotangulia kilipotokea, wimbo 88, “Kutembea kwa Ukamilifu,” haukupendwa katika nchi moja, lakini baadaye ukawa ndio wimbo wao wenye kupendwa zaidi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki