Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 12/15 kur. 4-7
  • Malaika—Je! Wao Wanaathiri Maisha Yako Wewe?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Malaika—Je! Wao Wanaathiri Maisha Yako Wewe?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Malaika Ni Halisi?
  • Malaika Katika Kusudi la Mungu
  • Malaika Wanakuathiri Wewe Jinsi Gani?
  • Malaika Katika Wakati Ujao Wako
  • Namna Malaika Wanavyoweza Kukusaidia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Malaika—Jinsi Wanavyohusika Katika Maisha Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Malaika—“Roho kwa Ajili ya Utumishi wa Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Malaika Ni Nani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 12/15 kur. 4-7

Malaika—Je! Wao Wanaathiri Maisha Yako Wewe?

JE! KWELI kuna malaika? Au wao ni kitu cha kuwaziwa tu? Ikiwa wako, je! wao wanaweza kuathiri maisha yako wewe?

Kuna chanzo kimoja tu chenye kutegemeka cha majibu kwa maswali hayo. Hicho ndicho Maandishi yaliyovuviwa ambayo Mungu amewapa wanadamu—Neno lake, Biblia Takatifu. Juu ya hilo mtume Paulo aliandika: “Andiko lote liliongozwa na Mungu na ni lenye manufaa . . . kwa kunyoosha mambo.”—2 Timotheo 3:16, NW.

Hivyo, sisi tunaweza kuwa na uhakika kwamba Biblia itatupa majibu yenye kunyooka juu ya kuwako kwa malaika na kama wao wanatuathiri sisi. Kwa uhakika Muumba wa ulimwengu wote mzima anaweza kutuambia kama malaika walikuwa miongoni mwa viumbe vyake.

Je! Malaika Ni Halisi?

Biblia inasema kwa uwazi hivi: “Yeye [Mungu] hufanya malaika zake wawe roho.” (Waebrania 1:7, NW) Kwa hiyo Muumba ana viumbe wa kiroho katika makao ya kimbingu. Hao hawaonekani kwetu sisi, na wao ni wenye nguvu nyingi.—Zaburi 104:4; 2 Petro 2:11.

Je! Mungu alikusudia malaika wawe vitu tu visivyo na utu? Kama hivyo ndivyo ilivyo, kwa sababu gani Biblia inatoa taswira ya malaika wakiwa wenye hisia? Kwa mfano, hiyo inatuambia kwamba wakati msingi wa dunia ulipowekwa, malaika “walipaaza mlio pamoja kwa shangwe, na wana wa Mungu wote [malaika] walianza kupaaza sauti kwa kupiga makofi.”—Ayubu 38:4-7, NW.

Inaonekana kwamba, kama viumbe wa Mungu wa kidunia wenye uelewevu, viumbe wa kiroho wenye uelewevu, malaika, wana utu wao wenyewe. Ingawa Biblia inataja majina ya malaika wawili tu (Mikaeli na Gabrieli), uhakika wa kwamba malaika wana majina unaongezea jambo la kwamba kila mmoja ni mtu peke yake. (Luka 1:11, 19, 26; Yuda 9) Biblia inashutumu vikali kuabudu malaika, na hiyo inatia ndani kuwapelekea sala. Badala ya sisi kupelekea malaika sala, mtume Paulo anatushauri hivi: “Katika kila jambo kwa sala na kusihi pamoja na shukrani, Mungu na ajulishwe maombi yenu.”—Wafilipi 4:6; Ufunuo 19:10; 22:8, 9, NW.

Lakini je! malaika walipangiliwa muundo wa kutokuwa na nguvu za uchaguzi wa kibinafsi kati ya yanayofaa na yasiyofaa kama mashine-watu ambazo hazina akili? Sivyo, malaika ni mawakili walio na uhuru wa hiari, sawa na vile wanadamu walivyo. Kwa mfano, wakati malaika fulani walipovunja sheria za Mungu katika siku za Noa, Mungu aliwakataa, na wameoondoshwa katika nyua za kimbingu za Mungu. Kujiendesha kwao kwa njia ya kutotii kulikuwa wonyesho wa wazi kwamba malaika ni watu ambao kila mmoja ana utu wake peke yake.—Mwanzo 6:1, 2; 2 Petro 2:4; Mathayo 25:41.

Hivyo, Biblia inatuandalia habari zenye msaada juu ya asili, kuwako na umbile la malaika. Kupita mpaka wa mambo ambayo Neno la Mungu linasema juu yao kungeweza kufanya mtu afikirie bure tu maswali ambayo Biblia haijibu. Kungeweza hata kuongoza kwenye mwelekezo usiofaa wa fikira au ibada kwa malaika. (Wakolosai 2:18) Biblia inatukumbusha ‘tufanye uhakika wa mambo yaliyo ya maana zaidi’ na ‘tusipite mpaka wa mambo ambayo tayari yamekwisha kutangazwa kuwa habari njema.’—Wafilipi 1:10; Wagalatia 1:8, NW.

Malaika Katika Kusudi la Mungu

Ingawa huenda wengi wakakubaliana juu ya asili na vitabia vya malaika, ni wachache ambao wanajua kweli kweli sababu ya kuwako kwao na jinsi malaika wanavyoathiri maisha zetu leo.

Katika Biblia, yale maneno mawili yaliyotumiwa kwa “malaika” ni mal·’akhʹ (Kiebrania) na agʹge·los (Kigiriki). Yote hayo mawili yanamaanisha “mjumbe.” Hayo yanatuambia jambo fulani juu ya moja ya kazi za malaika. Malaika wanatumikia wakiwa wajumbe, au matarishi, kati ya Mungu na wanadamu.

Kwa mfano, malaika mmoja alitumwa kupeleka ujumbe kwa Abrahamu kuhusu Isaka mwana wake na baraka ambayo ingekuja kupitia yeye, baraka ambayo sisi tunaweza kupokea. (Mwanzo 22:11-17) Malaika mmoja alitumwa kuwasiliana pamoja na Musa. (Matendo 7:37, 38) Mungu alituma pia malaika mmoja akiwa na maagizo kwa nabii Eliya. (2 Wafalme 1:3) Na malaika mmoja alimtokea Yusufu, baba-mlezi wa Yesu, akiwa na maagizo maalum kuhusu kile kitoto kichanga.—Mathayo 2:13.

Malaika wametumwa pia kuwapa himaya watu wa Mungu: “Malaika wa Yehova anapiga kambi kuwazunguka kote kote wale wanaogopa yeye, na yeye anaokoa hao.” (Zaburi 34:7, NW) Mathalani, malaika mmoja alifungua mtume Petro kutoka gerezani. (Matendo 12:6-11) Malaika wawili walisaidia Loti na binti zake kuokoka uharibifu wa Sodoma na Gomora kwa kuwasindikiza watoke katika eneo hilo. Hata hivyo, mke wa Loti hakutenda kwa kupatana kabisa na malaika hao, kwa hiyo yeye aliangamia katika uharibifu pamoja na miji hiyo.—Mwanzo 19:1-26.

Biblia inataja visa vingine vingi vya msaada wa kimalaika, ikitilia nguvu yale ambayo Waebrania 1:7 na 14 (NW) husema: “Kwa habari ya wale malaika yeye anasema: ‘Na yeye hufanya malaika zake wawe roho, na watumishi wake kwa watu wote anawafanya wawe mwali wa moto.’ Je! wao wote sio roho kwa ajili ya utumishi kwa watu wote, ambao wametumwa waende kuhudumu kwa ajili ya wale ambao watarithi wokovu?”

Malaika mmoja aliletea Yesu faraja kubwa. Usiku uliotangulia kifo chake, Yesu alijua mambo yaliyokuwa mbele yake—kwamba yeye angesalitiwa, angepigwa, na kuuawa kwa ukatili. Yeye alihitaji nguvu za kuvumilia jaribu hilo la ukamilifu wake. Kwenye wakati huo wa maana sana, malaika mmoja alimtokea yeye ‘kumtia nguvu.’ Lo, bila shaka faraja hiyo ya kimalaika ilikuwa baraka sana kwa Yesu! Tokeo ni kwamba, ingawa yeye alipatwa na masumbuko makubwa sana ya fikira hata ‘jasho lake likawa kama matone ya damu yakianguka chini,’ yeye aliweza kuvumilia kwa uaminifu mpaka kifo.—Luka 22:43, 44, NW.

Mungu ametumia malaika pia kuangamiza adui za watu wake. Wakati Serikali Kubwa Ulimwenguni ya Ashuru ilipotisha waabudu wa kale wa Mungu, jambo linalofuata lilitukia: “Ikawa usiku uo huo malaika wa BWANA [Yehova, NW] alitoka, akakiingia kituo cha Waashuri, akawapiga watu mia na themanini na tano elfu. Na watu walipoondoka asubuhi na mapema, kumbe! hao walikuwa maiti wote pia.” (2 Wafalme 19:35) Wewe unaweza kuona nguvu za kutia hofu ambazo malaika wanazo—ilichukua malaika mmoja tu kufisha wapinzani 185,000 wa Mungu na watu wake!

Herode mwenye kukufuru alikabiliwa pia na nguvu za malaika mmoja. Wakati Herode alipoanza kujifikiria mwenyewe kuwa ni mfano wa mungu, “Mara malaika wa Bwana [Yehova, NW] akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho.”—Matendo 12:21-23.

Sisi tunapashwa habari kwamba karibuni, wakati Mungu atakapoleta mfumo wa mambo wote mbovu kwenye mwisho wao, malaika watatumiwa tena kuwa wafishaji: “Mwana wa binadamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka ufalme wake vitu vyote vinavyoleta kukwaza na watu wanaovunja sheria, nao watawatupa katika tanuri lenye moto.”—Mathayo 13:41, 42, NW.

Hivyo, malaika ni tofauti kabisa na vile ambavyo huenda watu wengi wakawazia. Mtungaji wa kidini Mjeremani Dak. Manfred Barthel alisema: “Ikiwa sisi tunataka kuwazia malaika za Bwana kuwa kama vile ambavyo walionwa na watungaji wa Agano la Kale, kwanza tutalazimika kusahau wale makerubi wenye vibonyeo usoni . . . ambao wanapamba kadi zetu za salamu.”—What the Bible Really Says.

Malaika Wanakuathiri Wewe Jinsi Gani?

Hata hivyo, lile swali linabaki: Malaika wanafanya nini leo? Je! wao wanatuathiri sisi sasa hivi? Ndiyo, kwa uhakika wanafanya hivyo!

Kumbuka kwamba katika unabii wake kuhusu “ule umalizio wa mfumo wa mambo” Yesu alitabiri: “Wakati Mwana wa binadamu atakapofika katika utukufu wake [akitoa nguvu za Ufalme], na malaika wote wakiwa pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti cha ufalme chake chenye utukufu. Na mataifa yote yatakusanywa mbele yake, naye atatenga watu mmoja mmoja, kama vile mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi.”—Mathayo 24:3; 25:31, 32, NW.

Ni jinsi gani mtenganisho huo wa watu utakavyofanywa? Yesu alitabiri hivi: “Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia nzima yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.” (Mathayo 24:14, NW) Ndiyo, Mungu anatumia watu wake duniani kufanya kazi hiyo ya kuhubiri .duniani pote.

Ufalme wa Mungu ndio serikali ambayo italeta utatuzi ule mmoja tu kwa matatizo ya wanadamu. Leo, ujumbe juu ya serikali hiyo unatangazwa katika sehemu zote za ulimwengu na Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni tatu ambao malaika wanawategemeza. “Hivyo ndivyo itakavyokuwa katika ule umalizio wa mfumo wa mambo: wale malaika wataenda nje na kuwatenganisha waovu kutoka miongoni mwa waadilifu.”—Mathayo 13:49, NW.

Kazi hiyo ya kuhubiri yenye kuelekezwa na malaika leo inapokea itikio-mchanganyiko kutoka kwa watu. Watu fulani wanasema wao ni wenye shughuli mno wasiweze kusikiliza au wanakataa tu kufanya hivyo. Wengine wanasita-sita au hawafanyi uamuzi. Hata hivyo, watu wengi wenye mioyo minyofu, kwa kuhangaika juu ya wakati ujao wao, wameitikia kwa nia ya kupenda. Jinsi gani?

Katika bara 208, Mashahidi wa Yehova wanaongoza mafunzo ya nyumbani ya Biblia na mamilioni ya watu ambao ‘wanaona uhitaji wao wa kiroho’ na ambao ‘wanaona njaa kwa ajili ya uadilifu.’ (Mathayo 5:3, 6, NW) Mambo mengi yaliyoonwa yanaonyesha kwamba mara nyingi malaika wanaelekeza watumishi wa Mungu kufikia watu hao wenye mioyo minyofu wakiwa na ujumbe wa wokovu. Ufunuo 14:6 unaeleza kwa ishara ya mfano ‘malaika akiruka katikati ya mbingu’ akiwa na “Injili ya milele, awahubiri hao wakaao juu ya nchi.” Kwa uhakika jambo hilo linatukia sasa hivi! Hili litaathirije wakati ujao wako?

Malaika Katika Wakati Ujao Wako

Biblia inatambulisha waziwazi nyakati zetu kuwa ndizo “siku za mwisho” za mfumo huu uliopo. (2 Timotheo 3:15) Biblia inatupasha habari pia kwamba malaika sasa “wamesimama katika pembe nne za nchi, wakizizuia pepo nne.” (Ufunuo 7:1) Maneno hayo ya mfano yanamaanisha nini?

Wakiwa kwenye zile “pembe” za dunia, malaika hao wamo katika kikao cha kufungulia “pepo” zenye uharibifu kutoka pande zote. Hakuna eneo la dunia litakaloachiliwa, na hiyo itamaanisha ‘dhara,’ au uharibifu, kwa mfumo mbovu huu na wategemezaji wayo wote. Hivyo, malaika za Mungu wanaelezwa kuwa wako tayari kwenda kuchukua hatua wakati kiishara kinapotolewa!—Ufunuo 7:3; 19:11-21.

Ingawa hivyo, lile “dhara” lenye uharibifu litakuwa juu ya wale tu ambao hawaitikii ujumbe unaotegemezwa na malaika ambao sasa unahubiriwa duniani pote. Dhara hilo halitadhuru wale ambao wanatafuta Mungu na ambao wanasikiliza ule ujumbe wa Ufalme. Wao watahifadhiwa, kama Neno la Mungu linavyosema: “Tafuteni Yehova, ninyi nyote wasikivu wa dunia . . . Tafuteni uadilifu, tafuteni usikivu. Inaelekea huenda mkafichwa katika ile siku ya kasirani ya Yehova.”—Sefania 2:3, NW.

Ni nini basi litakalokuwa fungu la “wasikivu” hao? Zaburi 37:11, NW inasema: “Wasikivu wenyewe watamiliki dunia, nao kwa kweli watapata upendezo mzuri sana wao katika wingi wa amani.” Kwa muda mrefu jinsi gani? “Waadilifu wenyewe watamiliki dunia, nao watakaa milele juu yayo.” (Zaburi 37:29, NW) Hiyo inamaanisha kwamba uzima wa milele utawezekana katika dunia ambayo itageuzwa umbo iwe paradiso, kama vile Yesu alivyoonyesha.—Luka 23:43.

Kwa hiyo, basi, lile swali ambalo wewe unahitaji kuuliza ni: Wakati ujao wangu utakuwa nini?’ Jibu linategemea jinsi wewe unavyoitikia mwelekezo wa kimalaika. Je! wewe utasikiliza na kukubali wakati wewe unapotolewa ujumbe ambao wao wanategemeza? Wewe ukifanya hivyo, wewe utakuwa miongoni mwa wale ambao wanaweza kutazama mbele kwenye wakati ujao wakiwa na uhakika, wakiwa na ahadi hakika ya Mungu: “Ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hubaki milele.”—1 Yohana 2:17, NW.

[Picha katika ukurasa wa  7]

Malaika sasa ‘wanazizuia pepo nne.’ Kwa sababu gani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki