Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 12/15 kur. 10-15
  • Tumaini Katika Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumaini Katika Yehova
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tangu Mapema—Tumaini!
  • Tumaini Laendelezwa Likiwa Hai
  • Wakati wa Kuwa na Tumaini Sasa
  • Kumfurahia “Mungu wa Tumaini”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Tumaini la Viumbe—Latazamia Kutimizwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Upatano wa Biblia Yote
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Mtumaini Yehova na Uwe Hodari
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 12/15 kur. 10-15

Tumaini Katika Yehova

“Tumaini katika Yehova na shika njia yake, naye atakweza wewe umiliki dunia. Wakati waovu wanapokatiliwa mbali, wewe utaona hilo.”—ZABURI 37:34, NW.

1, 2. Aina ya wanadamu wanaonekana kuwa wamesimama wapi, na ni jinsi gani Umoja wa Mataifa unavyohusika?

KWA UWEZO wa kujua mambo, jamaa ya kibinadamu imefikia hatua ya ukuzi iliyo na maendeleo makubwa zaidi ya yote. Kwa sababu ya jitihada yayo, hatimaye imewasili kwenye kile kizazi cha nyukilia. Nguvu za kiatomi zinaonekana kama zinaweza kuandaa nishati nyingi sana na hivyo kufungulia mambo makubwa duniani pote. Kwa kinyume, hizo zimetayarisha njia pia ya kuleta umizo lililo kubwa zaidi ya yote kwa jamii ya kibinadamu.

2 Ni nini kinachozuia jamaa ya kibinadamu isijiharibu yenyewe katika maangamizi yenye moto wa nyukilia? Ingeweza kuonekana kuwa kizuizi hicho ni Umoja wa Mataifa, ambao unajisifia kuwa na mataifa-washiriki wapatao 159 walio na namna nyingi za serikali. Kisiasa, serikali hizo hazikubaliani moja na nyingine, huku kila moja ikiwa na itikadi ya kwamba namna yayo yenyewe ya utawala ni bora, naam, ndiyo bora zaidi. Kwa hiyo, ndani yao wenyewe, UM ni baraza lisilo na masikilizano. Fahari ya kitaifa na tamaa ya kujitegemea ni mambo ambayo yameuenea kila sehemu. Zaidi ya hilo, hesabu fulani ya mataifa yameacha kushikamana na itikadi katika Mungu, yakawa yasiyoamini kuwako kwa Mungu.

3. Ni jinsi gani maoni ya Jumuiya ya Wakristo juu ya Mungu yalivyo tofauti na yale ambayo Mungu mwenyewe anayo?

3 Jina Jumuiya ya Wakristo bado linatumika kwa mataifa ambayo hayataki kutiwa katika tabaka la kuwa yasiyotii Mungu bali yanayojidai kuwa yenye imani katika Yesu Kristo aliye katika muungano pamoja na “Mungu yule Baba” katika ukamatano wa utatu pamoja na Yesu na pamoja na roho takatifu yenye utu. Kauli inashikiliwa kwamba washiriki wa ule Utatu wana usawa wa cheo. Lakini Baba ya Yesu aliagiza nabii Isaya aandike maneno haya ya utambulishi: “Mimi ni BWANA [Yehova, NW]; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.” (Isaya 42:8) Yehova huyu, au Yahweh (The Jerusalem Bible), amejifanyia mwenyewe kumbukumbu lisilolinganika la kihistoria.

4. Umoja wa Mataifa unakengeusha aina ya wanadamu kutoka kwenye nini?

4 Bila kujiletea sifa kwa njia yo yote, Umoja wa Mataifa umeepuka kutolea jina la Mungu heshima na utambuzi. Huo hautii moyo aina ya wanadamu, ambayo sasa inahangaika katika taabu iliyo kubwa zaidi, imtumaini mwenye jina hilo. Hata hivyo, Mmoja huyo kwa kufaa anaitwa “yule Mungu wa tumaini,” kwa kuwa yeye ameweka msingi wa tumaini moja tu halali ambalo aina ya wanadamu inaweza kuwa nalo sasa. (Warumi 15:13, King James Version) Tumaini ambalo yeye anatoa limewatia nguvu na kuendeleza wanaume na wanawake wengi.

Tangu Mapema—Tumaini!

5. Ni wakati gani msingi wa kuwa na tumaini ulipowekwa?

5 Msingi wa kuwa na tumaini hilo uliwekwa mapema katika historia ya jamaa ya kibinadamu. Ndiyo, uliwekwa mara tu kabla ya mwondosho wa wazazi wetu wa kwanza kutoka katika kao lao la bustani ya Kiedeni katika Mashariki ya Kati. Maandishi ambayo yaliandikwa katika lugha ya Kiebrania juu ya bustani hiyo, au paradiso, si hekaya tu, wala hadithi ambayo imetungwa na jamii za watu waliokengeuka wakaacha kuabudu Muumba wao.—Mwanzo 2:7–3:24.

6. Ni jinsi gani aina ya wanadamu ilivyokuja kuhitaji tumaini?

6 Zaidi ya miaka 4,000 baadaye, mtume Mkristo Paulo alivuviwa na Mungu kuandika: “Kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.” (Warumi 5:12) Katika mingine ya miandiko yake, yeye alitambulisha mtu huyu mmoja mwenye hatia: “Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa.” (1 Wakorintho 15:22) Tabibu mmoja jina lake Luka, katika sura ya 3 ya Injili yake, alifululiza mrudio wa mstari wa ukoo wa Yesu mpaka kwa Adamu, ambaye, kabla ya kufukuzwa katika Edeni, alisikia ujumbe wa Yehova wa tumaini.—Luka 3:23-38.

7. Ni jambo gani la kutia moyo ambalo Mungu alifanya wakati Adamu alipokuwa angali hai?

7 Ni jambo la kawaida kutazamia kwamba, wewe ungepaswa kutaka kujua yaliyo katika ujumbe huu. Lakini kabla ya kuusoma, angalia uhakika wa kwamba kwa muda mrefu Yehova amekuwa mpaji tumaini. Hapo mwanzo Adamu alikuwa mwana wa kidunia wa Mungu, na Mungu alimruhusu yeye kuzaa uzao. Kama wewe ungetangulia kuona hali ya kutia hofu, labda ungetaka kuwatia moyo au kuwapa tumaini wazao wako. Mungu alifanya jambo kama hilo. Baada ya Adamu kusikia maneno ya Mungu ya shutumu kali yakitangazwa rasmi juu yake binafsi, yeye alisikia maneno ya tumaini kwa wazao wake.

8. Ni jinsi gani Mwanzo 3:15 ulivyoandaa msingi wa kuwa na tumaini?

8 Maneno hayo yenye kutoka kwa Mungu huyu anayekaza sana tumaini katika watu yalikuwa nini? Kwa “nyoka” aliyehusika katika dhambi ya Adamu, Mungu alisema: “Nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.” (Mwanzo 3:14, 15) Labda wewe utashangaa uulize ni jinsi gani maneno hayo yangeweza kusemwa kuwa yanatokeza tumaini. Kwanza, sisi tunajifunza kwamba, “nyoka” angepaswa kupondwa kichwa chake.

9. Ni nani yule “nyoka” anayetajwa kwenye Mwanzo 3:14, 15?

9 Katika Ufunuo 12:9 imeandikwa: “Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.” Ndiyo, “nyoka” ambaye alihusika katika Edeni hakuwa mwingine ila yule kiumbe-roho mwovu anayejulikana kuwa Shetani Ibilisi. Si kwamba nyoka wa mfano huyo alikuja tu kuwa na malaika zake katika mbingu bali yeye amekuwa pia na “uzao” hapa chini duniani, “uzao” ambao katika wakati unaofaa utasetwa-setwa pamoja naye uache kuwako.

10. Ni jinsi gani Yesu alivyohakikisha utambulisho wa yule “nyoka”?

10 Akihakikisha utambulishi huo wa Ibilisi kuwa ndiye “nyoka” ambaye alileta angamizo la wazazi wetu wa asili, Yesu Kristo aliwaambia hivi viongozi wa kidini Wayahudi katika karne ya kwanza: “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli . . . Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo [uongo]. (Yohana 8:44) Pia Yesu aliwaita wapinzani hao wa kidini “wazao wa nyoka.”​—Mathayo 12:34; 23:33.

Tumaini Laendelezwa Likiwa Hai

11. Ni sababu gani ya ziada ya kuwa na tumaini ambayo Mwanzo 3:15 unaandaa?

11 Ile ahadi ya kimungu ya kuponda kichwa cha yule nyoka wa mfano kwa kweli iliweka tumaini lenye kuchangamsha moyo mbele ya jamaa yote ya kibinadamu ambayo ingekuja kuwako baadaye. Tunaweza kuona sababu kwa kuchunguza mambo mengine ya Mwanzo 3:15. Ule “uzao” wa mwanamke unatajwa. Huo utambulisho wa “uzao” huo uliachwa kwa muda mrefu ukiwa umefichika katika fumbo. Lakini ilikuwa wazi kwamba Yehova Mungu angetia “uzao” huo uliokuwa bado haujatambuliwa katika uadui pamoja na yule nyoka wa mfano na “uzao” wake wenye kupinga Mungu. Ushindi uliahidiwa, ndiyo, ukathibitishwa kikamili, kwa ajili ya “uzao” wa “mwanamke”! Ushindi wa uzao huo uliwekwa uwe tumaini mbele ya aina ya wanadamu. Kwa hiyo washiriki wa jamaa ya kibinadamu wangeweza kutumainia kuja kwa ule “uzao” wa “mwanamke.”

12. Baada ya wakati fulani, ni mambo gani zaidi ambayo yalifunuliwa juu ya ule “uzao” wa “mwanamke”?

12 Katika muda wa karne ambazo zimepita, Mungu alifunua kwamba “uzao” huo ulikuwa Mwana wake mzaliwa-pekee, ambaye alitumwa duniani awe ndiye Masihi na kutoa uhai wake uwe dhabihu ya ukombozi. (Mwanzo 22:17, 18; Wagalatia 3:16; 1 Yohana 2:2; Ufunuo 5:9, 10) Kwa sababu hiyo tumaini la Mashahidi wa Yehova haliegemei juu ya Umoja wa Mataifa. Hilo linaegemea juu ya Yesu Kristo anayeishi, Mneni Mkuu wa Yehova Mungu. Sisi tunaweza kuwa na uhakika kwamba Kristo anaishi, kwa kuwa yeye aliinuka kutoka kwa wafu akaketishwa mkono wa kiume wa Yehova katika mbingu. Ni kama Paulo anavyosema: “Ikiwa tumemtumaini Kristo katika maisha haya tu [maisha ambayo yanatia ndani karne yetu ya 20], sisi ni wa kusikitikiwa zaidi ya watu wote. Hata hivyo, sasa Kristo ameinuliwa kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo.” (1 Wakorintho 15:19, 20, NW) Kama vile ambavyo imethibitishwa Kibiblia mara nyingi katika kurasa za gazeti hili, leo Yesu Kristo amekwisha kuketishwa cheoni akiwa Mfalme wa kimbingu.—Ufunuo 11:15.

13, 14. Ni wapi ambapo Mashahidi wa Yehova wanaweka tumaini lao, na wao wanafanya nini juu yalo?

13 Bila shaka. Yesu hajachukua mahali pa Yehova akiwa tumaini la aina ya wanadamu. Zaburi 37:34, NW bado inabaki ikitumika: “Tumaini katika Yehova na shika njia yake, naye atakweza wewe umiliki dunia. Wakati waovu wanapokatiliwa mbali, wewe utaona hilo.” Bado inahitajiwa kabisa kuendelea kutumaini katika Yehova na kutia moyo jamii zote za watu ziache kutumaini katika mashirika ya kibinadamu.

14 Kupatana na uhakika huo, Mashahidi wa Yehova ni watendaji katika nchi 208, wakihubiri zile habari njema za Ufalme. Wao hawawezi kukomeshwa kufanya hivyo. Mashirika ya kisiasa, yikisaidiwa na kusukumizwa na matengenezo ya kidini, hayana haki ya kimungu katika kujaribu kuwakomesha. Sisi tunaweza kuendelea kuwa mashahidi wa Yehova na kutumaini katika yeye, kama alivyofanya Daudi wa Bethlehemu, ambaye aliandika:

15. Ni tumaini la namna gani ambalo Mfalme Daudi alikuwa nalo katika Yehova?

15 “BWANA [Yehova, NW] ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu. Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, kando ya maji ya utulivu huniongoza. Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya; kwa maana Wewe upo pamoja nami, gongo lako na fimbo yako vyanifariji. Waandaa meza mbele yangu, machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, na kikombe changu kinafurika. Hakika wema na fadhili zitanifuata siku zote za maisha yangu; nami nitakaa nyumbani mwa BWANA [Yehova, NW] milele.”—Zaburi 23.

16. Kwa sababu gani inaweza kusemwa kwamba Yesu alikuwa na mtazamo wa mambo unaofanana na ule ambao Daudi alikuwa nao?

16 Mfalme Daudi alikuwa mchungaji wa kiroho wa Yehova kwa yale makabila ya Israeli wa kale, na yeye ndiye alitayarisha njia ili Yerusalemu uwe mji mkuu wa taifa hilo, ambapo Sulemani mwana wake alitawala kwa miaka 40. Kwa sababu nzuri, Yesu Kristo alinenwa kuwa ndiye ‘mwana wa Daudi.’ (Luka 1:31; 18:39; 20:41) Ikiwa Daudi alitumaini katika Yehova Mungu, Yesu Kristo mzao wake wa kidunia angefanya vivyo hivyo. Na alifanya.

17. Kuna ithibati gani kwamba Yesu alitumaini katika Yehova?

17 Kama ithibati ya kwamba mzao wa Daudi wa kidunia mwenye sifa zaidi ya wote, Yesu Kristo, alifuata shauri la Zaburi 37:34 wakati alipokuwa akipumua mpumuo wake wa mwisho juu ya mti wa mateso, Yesu alisema: “Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.” (Luka 23:46) Yeye alikuwa akitaja na kutimiza maneno ya Daudi kwenye Zaburi 31:5, ambayo yalielekezwa kwa Mungu: “Mikononi mwako naiweka roho yangu.” Tumaini la Yesu halikutamaushwa, kama vile la Mfalme Daudi halikutamaushwa. Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu siku ya tatu. Siku 40 baadaye yeye alirudi kwa Baba yake wa kimbingu. Kwenye mwisho wa Nyakati za Mataifa katika 1914, Yehova alikweza Mwana wake awe Mtawala wa dunia.

Wakati wa Kuwa na Tumaini Sasa

18. Kwa sababu gani leo ni wakati unaofaa wa kuwa na tumaini?

18 Leo, wakati ule mwaka mpya 6,014 A.M. (katika ule Mwaka wa Ulimwengu) unaposogeza jamaa ya kibinadamu mbele kuingia wakati ujao, ni tumaini gani linaloweza kuwapo kwa ajili ya jamaa ya kibinadamu? Swali hilo linafaa sana sasa kwa sababu karibu miaka 1,900 sisi tumo ndani ya ile pindi ya baada ya Biblia kuandikwa. Umekuwa muda mrefu tangu Daudi aandike Zaburi 37:34.

19. Yehova alifanya nini kwa ajili ya Yesu, kwa njia hiyo akitupa sisi tumaini?

19 Yehova Mungu, yule Mungu Mweza Yote ambaye alifufua Yesu kutoka kwa wafu, ana fungu la kazi lililo kubwa zaidi ya lile linalowaziwa na wanadamu wenye akili chache. Kwa kufufua na kukweza Mwana wake mzaliwa-pekee kwenye mkono wa kiume wake katika mbingu, Yehova Mungu ameongeza sababu zaidi kwetu za kumtegemea Yeye tukiwa na tumaini lisilo na upungufu, tumaini letu la kabisa kabisa. Hilo linaweza kumaanisha kwetu uzima wa milele katika furaha, sawa na vile mwandikaji Paulo mwenye kuvuviwa na Mungu anavyosema: “Sisi [tunaokolewa] katika tumaini hili.”—Warumi 8:24.

20. Kwa sababu gani sisi tunaweza kusema kwamba bado Yehova ndiye “yule Mungu wa tumaini”?

20 Mtume anaendelea kusema: “Lakini tumaini ambalo linaonwa si tumaini, kwa maana wakati mtu anapoona kitu, je! yeye anatumainia hicho? Lakini ikiwa sisi tunatumainia kile ambacho sisi hatuoni, sisi tunaendelea kungojea hicho kwa uvumilivu.” (Warumi 8:24, 25, NW) Kwa hiyo tumaini hilo la asili bado linaendelea kuishi, ndiyo, linakaribia utimizo mtukufu juu ya jamii ya kibinadamu. (2 Petro 3:13; Ufunuo 21:4, 5) Kwa sababu ile ile ya kwamba hilo ni tumaini kwa ajili ya aina ya wanadamu wote, hilo linastahili kujulishwa kwa wote. Hilo ndilo wazo la “Mungu wa tumaini” wetu.

21, 22. Sisi tunaweza kutazamia mataifa yafanye nini katika wakati ujao ulio karibu?

21 Sasa ndio wakati wake unaozidi nyakati zote kwa wazo hilo kutekelezwa. Hata katika pindi yetu ambapo mataifa fulani ya UM yameweza kupata ujuzi mwingi wa kisayansi juu ya kiini chenyewe cha mata (ambayo ndiyo asili ya maumbo yote) viongozi wa serikali hizi hawahisi uhitaji wa kuachia mtu fulani mwenye uelewevu mkubwa zaidi utatuzi wa matatizo.—Linganisha Mwanzo 11:6.

22 Kuliko wakati wo wote uliotangulia, dini inayopendwa na watu wengi sana imesukumwa katika hali ya kujitetea, ikiwa imebanwa sana. Uvutano wayo wenye kuleta migawanyiko lazima uondolewe mbali kabisa. Biblia inaonyesha kwamba sehemu zinazotawala zitajidaia ukuu wazo na kujipa talaka kutoka zile dini za unyonyaji ambazo zimekuwa zikijaribu kwa muda mrefu sana kunyonya mfumo wa mambo ya kilimwengu ili zipate vitu vyote ambavyo zinaweza. Basi, si mshangao kwamba ile sehemu ya kisiasa itachukua mwendo huo. Kuponyoka salama kwa sehemu hizo za kisiasa bila kupatwa na dhara baada ya shambulio hilo juu ya dini kutaonyesha, kutokana na maoni yazo, kwamba hakuna Mungu ambaye anastahili kuabudiwa na kutumikiwa. Dalili inayoonyeshwa na unabii ni kwamba sehemu hizo ndipo zitakapogeuka dhidi ya mashahidi wa Mungu, ambao wanabaki. Hizo zitatafuta kupata ushindi ulio rahisi zaidi ya maushindi yote juu ya Mashahidi wa Yehova katika kufikia ukomo wa kampeni yao ya kupinga Mungu.—Ufunuo 17:12-17; Ezekieli 38:10-23.

23, 24. Ni jinsi gani Yehova atakavyotenda kwa sababu ya shambulio la mataifa juu ya watu wake?

23 Hata hivyo, wao hatimaye watapata kuujua ushinde wenye kiaibu ambao lazima ujilie mmoja anayethubutu kuingia katika pambano pamoja na Yehova wa majeshi, ambaye hajapata kamwe kushindwa pigano. Hilo litaonyesha kwa uwazi usioweza kukosewa kwamba wao wamekuwa wakitumikia makusudio ya yule mpinzani mkuu wa yule Mungu wa kweli, yaani, “nyoka,” Shetani, “mungu wa huu mfumo wa mambo.”—2 Wakorintho 4:4, NW.

24 Huo utakuwa mnyenyekezo ulio kama nini kwao! Mambo ambayo wao walikuwa wametumaini kuonyesha yatathibitika kuwa kipeo cha ufidhuli, yakichochea yule yule Mungu wa mbingu na dunia kwenye ghadhabu ya uadilifu. Kwa wanadamu duni tu yeye angeweza kusema: “Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA [Yehova, NW]. Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu. Maana kama vile mvua ishukavyo, na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; bali huinywesha ardhi, na kuizalisha na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.”—Isaya 55:8-11.

25. Basi, kwa sababu gani, sasa sisi tuna sababu nzuri ya kutegemea Yehova akiwa ndiye “Mungu wa tumaini” wetu?

25 Muumba huyo wa mwanadamu ametia ndani ya moyo wa kibinadamu wepesi mwingi sana wa kugusika hisia, kama vile yeye mwenyewe alivyo nao. “Kwa maana BWANA [Yehova, NW] wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake.” (Zekaria 2:8) Kwa hiyo, basi, Mashahidi wa Yehova watalazimika kutumaini katika Yehova. Yeye atajiwekea kipimo cha kutimiza tumaini hilo mpaka enzi kuu yake ya ulimwengu wote mzima ifikie uzuri uliotiwa madoido yaliyo bora zaidi. Yeye atathibitisha kwa njia isiyoweza kufanyiwa tena ubishi wo wote kwamba yeye ndiye yule Mungu aliye juu zaidi, mweza yote, wa umilele, ambaye ametimiza yaliyo bora zaidi kati ya matumaini ya viumbe wake katika mbingu zote na dunia yote. Haleluya!—Zaburi 150:6.

Wewe Ungejibu Jinsi Gani?

◻ Kwa sababu gani lile tumaini la mataifa ni la udanganyifu?

◻ Ni jinsi gani ambavyo Mungu aliandaa msingi wa kuwa na tumaini katika Mwanzo 3:15?

◻ Maoni ya Yesu yalikuwa nini kuhusu Zaburi 37:34?

◻ Kwa sababu gani sisi tuna sababu ya kuwa na tumaini?

[Picha katika ukurasa wa 10]

Kama vile kondoo wanavyofuata mchungaji wao, ndivyo Daudi alimtegemea na kutumaini katika Yehova

[Credit Line]

Jumba la Kuhifadhi Picha (Historia ya Mashariki ya Karibu)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki