Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 12/15 kur. 15-20
  • Kuheshimu Yule Mungu wa Tumaini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuheshimu Yule Mungu wa Tumaini
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Binadamu Wanaheshimu Mungu
  • Je! Wewe Utaheshimu “Yule Mungu wa Tumaini”?
  • Kwa Vitu Vyetu Vinavyothamanika
  • Heshimu Yehova, Kwa Nini Na Kwa Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Onyesha Wengine Heshima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Heshimu Wanadamu Wa Namna Zote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Mpe Heshima Yule Anayestahili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 12/15 kur. 15-20

Kuheshimu Yule Mungu wa Tumaini

“Tamko la Yehova ni: . . . ‘Wale ambao wanaheshimu mimi nitaheshimu, na wale ambao wanadharau mimi watakuwa wa hesabio ndogo.’”​—1 SAMWELI 2:30, NW.

1. Ni sababu gani ambayo sisi tunayo ya kutaka kuheshimu Yehova? (1 Timotheo 1:17; Ufunuo 4:11)

KWA SABABU ya matazamio ya mbele ambayo sisi tunaweza kuwa nayo, yakiwa yanategemea msingi wa Biblia, inafaa na ni jambo la kiakili kabisa kwetu kuheshimu “yule Mungu wa tumaini,” “yule Mungu apaye tumaini.” (Warumi 15:13, King James Version; New World Translation) Kwa sababu gani? Ni jinsi gani sisi, ambao ni binadamu duni tusio na ukamilifu tunaweza kuheshimu yule Muumba Mwadhamu wa ulimwengu wote mzima? Na je! yeye ataheshimu sisi kwa kurudisha?

2. Yesu alihisi jinsi gani juu ya Mungu kupewa heshima?

2 Sisi tunaweza kujifunza kutokana na yaliyotukia kwa Yesu. Hakuna ye yote wetu ambaye angekana kwamba Yesu sikuzote alitaka Baba yake aheshimiwe, atukuzwe. (Yohana 5:23; 12:28; 15:8) Kwa hakika Yesu alichambua Mafarisayo na waandishi ambao ‘huheshimu Mungu kwa midomo yao lakini mioyo yao ilikuwa imeondolewa mbali kutoka kwake.’ Tafadhali ona hapo, ukosefu wao wa heshima kwa Mungu ulihusu makusudio na vitendo visivyofaa. (Mathayo 15:7-9, NW) Ingawa hivyo, je! sisi tunaweza kusema kwamba kwa kuheshimu Mungu, tumaini la Kristo lilihusika? Na Yehova aliitikia jinsi gani kwa kuheshimiwa hivyo?

3. Ni jinsi gani sisi tunavyojua kwamba Yesu alitumaini katika Yehova?

3 Yesu alithamini moyoni maneno ya Daudi kwenye Zaburi 16:10, NW: “Wewe hutaacha nafsi yangu katika Sheoli. Wewe hutaruhusu mshikaminifu wako aone shimo.” Kwa sababu Yesu Kristo alikuwa na tumaini hilo la kufufuliwa, yeye angeweza kusema maneno yenye kugusa sana hisia kama nguvu za umeme na kumwambia mtenda maovu aliyetudikwa mtini kando yake: “Kweli kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja na mimi katika paradiso.” (Luka 23:39-43, NW) Mtenda maovu huyo alikufa baada ya muda mfupi, kwa hiyo yeye hakuweza kushuhudia siku chache baadaye uhakikisho wa tumaini la Yesu wa kuinuliwa. Lakini shahidi mmoja aliyeona kwa macho aliripoti hivi: “Yesu huyo Mungu alimfufua, uhakika ambao juu yao sisi sote ni mashahidi.” (Matendo 2:31, 32, NW) Huo ulikuwa uhakika.

4. Ni heshima gani ambayo Yesu alistahili na kupokea? (Ufunuo 5:12)

4 Wengi wa watu wa kawaida ambao Yesu alihudumia walijua kwamba yeye alistahili kupewa usharifu, au heshima. (Luka 4:15:19:36-38; 2 Petro 1:17, 18) Ndipo yeye alipokufa kama mhalifu. Je! hilo lilibadili mambo? Sivyo, kwa maana Yesu alikuwa na ukubali wa yule Mungu ambaye katika huyo yeye alitumaini. Hivyo, Yehova alimleta tena kwenye uzima. Uhakika wa kwamba “yule Mungu wa tumaini” aliinua Mwana wake kwenye uzima na kumvisha kutokufa katika makao ya roho unathibitisha kwamba Baba huyo alikuwa akiendelea kuheshimu Mwana wake. Paulo anasema: “Sisi tunaona Yesu . . . amevishwa taji la utukufu na heshima kwa sababu ya kuwa alipata taabu ya kifo, kwamba yeye kwa fadhili isiyostahiliwa ya Mungu aweze kuonja kifo kwa ajili ya kila mwanadamu.”—Waebrania 2:7, 9; Wafilipi 2:9-11, NW.

5. Ni katika njia gani ya pekee ambayo Yesu aliheshimiwa, hiyo ikitokeza heshima gani ya ziada kwa Mungu?

5 Yesu, ambaye alikuwa ameheshimu Yehova, alitaja njia moja ya pekee ambayo katika hiyo Baba aliheshimu yeye. Katika mtokeo mmoja kwa mitume wake waaminifu, yeye alisema: “Mamlaka yote imepewa kwangu mimi katika mbingu na katika dunia. Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu . . . Tazama! mimi nipo pamoja na ninyi siku zote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 28:18-20, NW) Kwa hiyo yule Baba alimheshimu zaidi yule Mwana kwa kumpa mamlaka isiyo na kifani. Hiyo ilipasa kutumiwa kwa ajili ya wanadamu ambao wangefanya kazi fulani ambayo inaleta heshima kwa yule Mmoja ambaye Yesu anajitahidi kuheshimu. Basi, hiyo inamaanisha kwamba sisi wanadamu tusio wakamilifu tunaweza kwa njia fulani kuheshimu yule Baba na kuheshimiwa naye kwa kurudisha?

Binadamu Wanaheshimu Mungu

6. Je! inafaa kutamani kuheshimiwa, lakini ni hatari gani iliyo katika jambo hilo? (Luka 14:10)

6 Inakuwa vigumu binadamu walio wengi kufikiria kuheshimu Mungu kwanza, na wao wanapendezwa zaidi na kupata heshima kwa ajili yao wenyewe. Watu fulani hata wangeweza kusema kwamba ni jambo la kawaida kwetu kutaka tuheshimiwe. Kuna kipimo fulani cha ukweli katika jambo hili, kwa kuwa ni jambo la kawaida kutamani sifa njema, pamoja na kipimo fulani cha kupata heshima kutokana na jambo hilo. (1 Timotheo 3:2, 13; 5:17; Matendo 28:10) Hata hivyo, tamaa ya kutaka heshima kutoka kwa wanadamu inaweza kwa urahisi kuongezewa chumvi nyingi mno. Jambo hilo linaonekana wazi kwa jinsi watu wengi wanavyotafuta-tafuta jina lenye sifa kwa gharama yo yote au kufanya lo lote lile ili walinde heshima yao.

7. Kwa sababu gani kuheshimiwa na wanadamu ni kwenye thamani kidogo sana?

7 Wakati unapofikiria hilo, inaonekana kuwa hata heshima iliyo kubwa zaidi ya zote kutoka kwa wanadamu inapitilia mbali mbio-mbio, kwa maana baada ya muda mfupi wote wanakufa. Eh ndiyo, huenda lile kumbukumbu la majogoo wachache likaheshimiwa kwa muda, lakini walio wengi kati ya wafu wanasahauliwa. Ni watu wangapi wanaojua majina ya wazazi wa babu na nyanya zao au wanaojua wale waliokuwa viongozi wa taifa lao miaka mia moja iliyopita? Kwa kweli, kama mtu fulani aliishi au hakuishi, hiyo haibadili mambo. Yeye ni kavumbi katiti kadogo juu ya mizani ya wakati, kijitone katika mtiririko wa uzima. Na hata kama yeye anaheshimiwa kwa muda mfupi baada ya kifo, yeye hajui jambo hilo. (Ayubu 14:21; 2 Nyakati 32:33; Mhubiri 9:5; Zaburi 49:12, 20) Jambo lile moja tu ambalo linaweza kufanyiza tofauti ni kuwa na tumaini ambalo Mungu anaandaa, kumheshimu yeye, na kuheshimiwa kwa kurudisha. Sisi tunaweza kuona jambo hilo katika maisha za watu wawili walioishi katika pindi ile ile moja katika Israeli ya kale.

8. Eli alianguka ndani ya mtego gani unaohusu kutoa heshima?

8 Eli alikuwa mmoja. Yeye alitumikia Mungu katika kile cheo kisicho na kifani cha kuhani mkuu kwa miaka 40 na alipendelewa pia kuhukumu Israeli. (1 Samweli 1:3, 9; 4:18) Hata hivyo, baada ya wakati fulani yeye alionyesha udhaifu kwa habari ya Hofni na Finehasi, wana wake. Ingawa walikuwa makuhani, wao walitumia vibaya cheo chao kwa kuiba sehemu za zile dhabihu na kujitia katika ngono isiyo ya adili. Wakati baba yao alipowachambua kidogo-kidogo tu kwa upole, Mungu alitangaza rasmi kwamba Eli ‘aliendelea kuheshimu wana wake zaidi ya mimi.’ Yehova alikuwa ameahidi kuendeleza ukuhani wa Kiharuni, lakini yeye angeikatalia mbali nyumba ya Eli kutoka cheo cha ukuhani mkuu. Kwa sababu gani? Mungu alieleza: “Wale ambao wanaheshimu mimi nitaheshimu, na wale ambao wanadharau mimi watakuwa wa hesabio ndogo.”—1 Samweli 2:12-17, 29-36; 3:12-14, NW.

9. Ni jinsi gani Samweli alivyopewa nafasi ya kuheshimu Yehova?

9 Katika utofauti alikuwako Samweli. Inaelekea wewe unajua kwamba wazazi wake walileta yeye katika umri mchanga atumikie kwenye ile tabernakulo katika Shilo. Usiku mmoja Yehova alisema kwa kivulana yule. Huenda wewe ukafurahia kusoma usimulizi huo kwenye 1 Samweli 3:1-14, ukiwazia kuamshwa kwa mvulana huyo, si na mgurumo wenye kututuma sana, bali na sauti ya chini ambayo yeye aliichukua kimakosa kuwa ya Eli mzee-mzee. Ndipo fikiria kwamba lazima liwe lilikuwa jambo la kuogopesha sana kwa Samweli mchanga kulazimika kuambia yule kuhani mkuu wa umri mkubwa kwamba Mungu alikuwa amepiga moyo konde kuiadhibu nyumba ya Eli. Na bado Samweli alifanya hivyo; yeye aliheshimu Mungu kwa utii.—1 Samweli 3:18, 19.

10. Katika kuitikia kuheshimiwa, ni jinsi gani Mungu alivyoheshimu Samweli?

10 Samweli aliheshimu Yehova kwa miaka kadha akiwa nabii, na Mungu aliheshimu yeye. Angalia hilo kwenye 1 Samweli 7:7-13. Yehova alijibu kwa haraka sala ya Samweli ya kuomba msaada ili kushinda Wafilisti. Je! wewe hungehisi kuwa umeheshimiwa kupata utambuzi kama huo wa kimungu? Wakati wana wa Samweli hawakufuata uongozi wake, Mungu hakumkataa yeye kama vile alivyokuwa amekataa Eli. Kwa uwazi hiyo ilikuwa kwa sababu Samweli alifanya yote ambayo yeye angeweza ili kuheshimu Mungu. Kuonyesha hivyo zaidi, Samweli alikataa kutolea kwa ukubali lile ombi la watu la kutaka mfalme wa kibinadamu. (1 Samweli 8:6, 7) Mungu alitumia Samweli kuwapaka mafuta wote wawili Sauli na Daudi. Wakati Samweli alipokufa, Israeli ilimheshimu yeye kwa kuomboleza. Hata hivyo, jambo la maana zaidi ni kwamba Mungu aliheshimu yeye kwa kumtaja katika Biblia miongoni mwa wanaume wa imani ambao watabarikiwa kwa ufufuo na yale mambo mema ambayo Mungu ameweka akibani kwa ajili yao. (Zaburi 99:6; Yeremia 15:1; Waebrania 11:6,16, 32, 39, 40) Je! hiyo haionyeshi kwamba kuheshimu “yule Mungu wa tumaini” ni jambo la thamani kubwa?

Je! Wewe Utaheshimu “Yule Mungu wa Tumaini”?

11, 12. Ni jambo gani ambalo sisi tunahitaji kufikiria juu ya kuheshimu Yehova, na ni nini njia moja ya sisi kufanya hilo?

11 Kutoa vielelezo viwili tu, visa vya Yesu na Samweli, vinathibitisha kwamba wanadamu wanaweza kufanya kuheshimu “Mungu wa tumaini” wao kuwe ndilo jambo kubwa zaidi la kutangulizwa katika maisha. Na visa viwili hivyo vinaonyesha kwamba kwa kufanya hivyo sisi tunaweza kwa kufaa kutafuta na kupokea heshima kutoka kwa Mungu. Lakini ni jinsi gani wewe unavyoweza kufanya hivyo ukiwa na uhakikisho wa kiasi kwamba wewe utafurahisha Mungu, utaheshimiwa na yeye, na utafikia tumaini lako lenye msingi wa Biblia?

12 Njia moja ni kuwa na woga wa kweli na wenye kujaa staha ya kutochukiza Mungu. (Malaki 1:6) Inaelekea sisi tunakubaliana kwa utayari na taarifa hiyo. Hata hivyo, kumbuka wana wa Eli. Kama wewe ungalikuwa umewauliza wao kama walitaka kuheshimu Mungu wakimwogopa yeye kwa staha, inaelekea sana wao wangalisema ndiyo. Tatizo linakuja katika kuifasiri katika uhalisi wa vitendo katika maisha ya kila siku tamaa yetu ya kuheshimu Mungu kwa kumwogopa yeye.

13. Toa kielezi juu ya jinsi tamaa ya kuheshimu Mungu kwa kumwogopa yeye inavyoweza kutusaidia sisi.

13 Ikiwa sisi tunaelekeana na hali yenye kushawishi ambayo katika hiyo sisi tungeweza kuiba au kujitia katika tendo fulani lisilofaa la ngono bila ya hilo kujulikana na watu wengi, je! tamaa yetu ya kuheshimu Mungu ingeathiri vitendo vyetu? Sisi tunapaswa kusitawisha ile hisia ya kwamba, ‘Hata ikiwa lile kosa lingeweza kubaki limefichika, kule kujiachilia kwangu kwenyewe niingie katika dhambi kama hiyo ni utovu wa heshima kwa “yule Mungu wa tumaini” ambaye mimi nachukua jina lake.’ Na uhakika ni kwamba kosa hilo halitabaki daima limefichika, sawa na vile hayakufichika mambo ambayo wana wa Eli walifanya. Jambo hilo linatokezwa wazi na maneno ya Paulo kuhusu “hukumu yenye uadilifu ya Mungu”: “Yeye atatolea kila mmoja kulingana na kazi zake: uzima wa milele kwa wale ambao wanatafuta utukufu na heshima na kutofisidika kwa kuwa na uvumilivu katika kazi ambayo ni njema; hata hivyo, kwa wale ambao ni wenye kutokeza mashindano na ambao hawatii ule ukweli bali wanatii ukosefu wa uadilifu kutakuwa na hasira-kisasi na kasirani.”—Warumi 2:5-8, NW.

14. Ni njia gani nyingine ambayo katika hiyo sisi tunaweza kuheshimu Mungu, na ni jambo gani ambalo sisi tungeweza kujiuliza wenyewe?

14 Kwa upande ule mwingine, Paulo anataja ushiriki “katika kazi ambayo ni njema,” ambayo inaheshimu Mungu na kutokeza “utukufu na heshima” kutoka kwake. Kazi moja ya msingi ya aina hiyo leo ni ile ambayo Yesu alitaja kwenye Mathayo 28:19, 20, NW: ‘Fanyeni wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mkiwabatiza na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo mimi nimewaamuru ninyi.’ Duniani pote, mamilioni ya Mashahidi wa Yehova ni watendaji katika kazi hiyo yenye kuheshimu Mungu ya kuhubiri na kufundisha. Wengi hata wanajikaza wenyewe kuwa wahudumu wa wakati wote wakiwa mapainia, ama kwa msingi wa kudumu ama wakati wa likizo kutoka kazi ya kimwili au shule. Kwa kutia hilo katika akili, kila mmoja wetu anaweza kufikiria kwa njia yenye manufaa jinsi yeye anavyosimama kuhusiana na kazi hiyo. Mathalani, wewe ungeweza kuuliza, ‘Je! mimi ninaheshimu “yule Mungu wa tumaini” kwa kuwa na ushiriki kamili katika ile kazi ya kuhubiri?’

15. Ni jambo gani ambalo limetukia kwa Wakristo fulani kuhusu kuheshimu Yehova kupitia ile huduma ya peupe?

15 Wakristo fulani ambao kwa miaka kadha walikuwa wahubiri watendaji wamepunguza mwendo kidogo kidogo. Wao wamelowea ndani ya kiolezo cha kuwa na ushiriki mdogo au usio wa mara nyingi katika ile kazi ya maana ya kufanya wanafunzi. Sisi hatumaanishi watu mmoja mmoja ambao wana mipungukio ya kimwili na wanapunguza mwendo kwa sababu ya matokeo ya umri wa uzee. Mbali kabisa na mambo kama hayo, mpunguzo-mwendo unaonekana miongoni mwa Mashahidi wa umri mbali-mbali. Jambo linalofaa kuangalia ni kwamba Paulo hakuwa akirejeza kwenye kikundi cha umri fulani wakati alipoonya Wakristo dhidi ya ‘kuchoka na kuacha.’ Badala ya hivyo, hata kama mtu ana umri gani, kiini cha tatizo lenyewe ni kwamba ushiriki wa ukawaida katika huduma unataka jitihada. Kama inavyoonekana wazi kwamba ilitukia katika siku ya Paulo, watu fulani leo wanafikiria sababu ya kwamba, ‘Mimi nimefanya fungu langu la ushiriki muda wa miaka ile, kwa hiyo sasa Wakristo wapya zaidi wanaweza kujitahidi wenyewe.’—Wagalatia 6:9, NW; Waebrania 12:3.

16. Kwa sababu gani sisi tungeweza kunufaika kutokana na kujichunguza wenyewe katika habari hii?

16 Wale ambao wameathiriwa kwa njia hiyo kwa uhakika ni walio wachache zaidi, lakini wewe ungeweza kuuliza. ‘Je! mimi najitambulia waziwazi kwamba katika kisa changu mna elekeo lo lote kama hilo? Ushiriki wangu katika huduma unalingana jinsi gani na ule wa wakati uliopita?’ Kama mpunguzo-mwendo wo wote umetukia au haujatukia, sisi sote tunapaswa kuzingatia katika akili kwamba “Mungu wa tumaini” wetu anaahidi kuandaa “utukufu na heshima na amani kwa ajili ya kila mtu ambaye anafanya kazi ya yaliyo mema.” (Warumi 2:10, NW) Paulo alitumia neno la Kigiriki ambalo linamaanisha “kufanya kazi kutokeza jambo fulani, kutokeza zao, kutimiza.” Jinsi ilivyo muhimu kwamba sisi tuepuke mambo ambayo yaliangukia Mafarisayo na waandishi, ambao waliheshimu Mungu kwa namna ya utumishi wa midomo tu! (Marko 7:6; Ufunuo 2:10) Kwa kinyume, wakati sisi tunaposhiriki kiutendaji katika huduma ya peupe kutoka moyoni, sisi tunahakikisha kwetu wenyewe na kwa wengine kwamba sisi tuna tumaini halisi. Sisi tunaheshimu Muumba na Mpaji-uzima wetu. Na tunakuja ndani ya mstari wa kuheshimiwa na yeye, sasa na kwa wakati usio na mwisho.—Luka 10:1, 2, 17-20.

Kwa Vitu Vyetu Vinavyothamanika

17, 18. Ni njia gani nyingine ambayo katika hiyo sisi tunaweza kuheshimu Mungu, na kwa sababu gani si halali kutopenda kufanya hivyo?

17 Kwa habari ya njia nyingine moja ambayo katika hiyo sisi tunaweza kuheshimu “Mungu wa tumaini” wetu, Mithali 3:9, NW, inasema: “Heshimu Yehova kwa vitu vyako vinavyothamanika na kwa yale matunda ya kwanza ya zao lako lote.” Spurrell anafasiri mstari huo hivi: “Tukuza Yehova kwa utajiri wako, na kwa lililo bora zaidi la ongezeko lako lote.”—A Translation of the Old Testament Scriptures from the Original Hebrew.

18 Kwa kuwa viongozi wa kidini mbalimbali wamekuwa na sifa mbaya ya kula pupa isiyo na mipaka na kuwa na mtindo wa maisha wa utajiri mwingi, watu wengi wanasita-sita kuyatolea upaji makanisa na matengenezo ya kidini ambayo shabaha yao inaonekana waziwazi ni kama kupata tu utajiri. (Ufunuo 18:4-8) Hata hivyo, matumizi mabaya hayo hayauondoi uhalali wa Mithali 3:9. Kulingana na shauri hilo lililovuviwa na Mungu, ni jinsi gani sisi tunavyoweza kutumia “vitu vinavyothamanika” vyetu ili ‘kuheshimu Yehova,’ “Mungu wa tumaini” wetu?

19. Toa kielezi cha jinsi watu fulani wametumia Mithali 3:9.

19 Mashahidi wa Yehova wanapata kwamba ile hesabu inayoendelea kuongezeka ya watu wanaoitikia ujumbe wa Ufalme inataka kuwe na mpanuko wa Majumba ya Ufalme au kuwe na ujenzi wa mapya. Hapo, basi, ipo njia moja ya ‘kutukuza Yehova kwa utajiri wako.’ Vijana na wazee wameshiriki katika kufanya hivyo, kama kwa kuazimia kibinafsi kuchangia hiyo mifuko ya ujenzi. Kushikilia maazimio hayo ya siri bila kuyaacha huenda kutahitaji nidhamu ya kibinafsi au hata kujidhabihu kwa kadiri fulani, hususa kama uchoraji ramani na mpango wa kumaliza mradi wa ujenzi unaendelea kwa kipindi kirefu. (2 Wakorintho 9:6, 7) Hata hivyo, kutumia pesa kwa njia hiyo kunaheshimu Yehova kweli kweli, kwa maana Majumba ya Ufalme ni mahali ambapo Wakristo wanamwabudu yeye na ambapo wao na washirika wao wanapata maarifa ya kujua Mungu. Maneno ya Yesu kwenye Mathayo 6:3, 4 yanatupa sisi sababu nzuri ya kuwa na itibari kwamba Mungu ataheshimu wale ambao wanamheshimu yeye hivyo.

20. (a) Kwa sababu gani uchunguzi mwingi sana wa kibinafsi unafaa kufanywa katika kutumia Mithali 3:9? (b) Ni maswali gani ambayo sisi tungeweza kujiuliza wenyewe?

20 Ingawa hivyo, hapa pana tahadharisho: Mafarisayo na waandishi, ambao Yesu alisema hawakuwa wakitanguliza mbele kabisa kumheshimu Mungu, walihakikisha kwamba wao ndio walikuwa wa kwanza kunufaika kutokana na utajiri wao. Kwa hiyo lile shauri kwenye Mathayo 15:4-8 linapendekeza kwamba sisi tujitie chini ya uchunguzi mwingi sana wa kibinafsi juu ya ‘kuheshimu Yehova kwa vitu vyetu vinavyothamanika.’ (Yeremia 17:9, 10) Mathalani, labda Mkristo ambaye amekuwa tajiri kidogo kupitia biashara yake angeweza kutafutia-tafutia visababu kuendelea kwake kufanya kazi ya wakati wote ili achume pesa nyingi hata zaidi. Labda yeye angeweza kufikiri kwa kutoa sababu ya kwamba, ‘Wengine wanaingia huduma ya painia au wanahama kutumikia mahali ambako wahubiri wanahitajiwa kwa njia ya pekee, lakini njia yangu ya pekee ya kutumikia Mungu ni kwa kuchuma pesa zaidi ndipo niwe na nyingi za kutoa kama mchango.’ Huenda michango yake ikafanya mema mengi. Lakini yeye angeweza kujiuliza pia, ‘Je! mtindo wa maisha yangu ya kibinafsi unaonyesha kwamba kutumia pesa katika kuheshimu Mungu ndilo kusudio langu la msingi ambalo linanifanya nichume pesa zaidi na zaidi?’ (Luka 12:16-19; linganisha Marko 12:41-44.) Na, ‘Je! mimi ningeweza kupanga mambo yangu ili niwe na ushiriki mkubwa zaidi wa kibinafsi katika ile kazi iliyo ya maana zaidi kwa siku yetu—kutangaza zile habari njema?’ Kwa uhakika, hata hali zetu katika maisha ziwe nini, sisi tunaweza kuchunguza makusudio na vitendo vyetu na kuuliza, ‘Ni jinsi gani mimi naweza kumheshimu kwa ukamili zaidi Mpaji-uzima wangu na “Mungu wa tumaini”?’

21. Ni tazamio gani ambalo sisi tunakuwa nalo ikiwa tunaheshimu Yehova sasa?

21 Yehova hatatutamausha sisi. Ni tazamio la kufurahisha kama nini kwamba, sasa na mpaka ndani ya wakati ujao, labda yeye atasema juu yetu kama alivyosema juu ya Israeli waaminifu: “Kwa sababu ya uhakika wa kwamba ninyi mmekuwa wenye thamani kubwa katika macho yangu, ninyi mmehesabiwa kuwa wa kuheshimika, na mimi mwenyewe nimependa ninyi”! (Isaya 43:4, NW) Mmoja uyo huyo anaahidi “uzima wa milele kwa wale ambao wanatafuta utukufu na heshima.” Yeye anaelekeza ahadi hiyo kwa wale ambao wanavumilia “katika kazi ambayo ni njema.” Ni “Mungu wa tumaini” kama nini!

Wewe Ungejibu Jinsi Gani?

◻ Kwa habari ya wanadamu kuheshimu Yehova, sisi tunaweza kujifunza nini kutokana na kielelezo cha Yesu?

◻ Ni jinsi gani Eli na Samweli walivyotofautiana kuhusu kuheshimu Mungu?

◻ Ni baadhi ya njia gani ambazo katika hizo wewe unaweza kuongeza heshima ambayo wewe unaletea Mungu, na ni itikio gani ambalo huenda wewe ukapokea?

◻ Ni wakati ujao gani unaoongoja wale ambao wanatanguliza kuheshimu “Mungu wa tumaini wetu”?

[Sanduku katika ukurasa wa 20]

BARUA ZINAZOHUSU MICHANGO

Hapa pana madondoo fulani kutokana na barua zilizopokewa na afisi ya Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi ya Brooklyn, New York:

“Jina langu ni Abijah. Mimi nina umri wa miaka tisa. Mimi nataka kuwapa ninyi dola 4 kwa ajili ya wale ndugu wanaofanya kazi kuhusiana na Majumba ya Ufalme. Wao wanaweza kuzitumia kwa kununua mbao au kununua peremende, mimi sijali watakachonunua.”—Oregon.

‘Ninyi mtapata nimetia ndani ya bahasha hundi yangu binafsi. Mimi nimepita umri wa miaka 96 na mimi nina shida ya kusikia, lakini nafurahia kweli kweli kuokoa pesa zangu kwa ajili ya jambo hili. Ndiyo, mimi najua, ninaendesha gari lililokwisha kutumiwa na wengine, na nyakati za majira ya baridi mimi huwa siendi Florida au California. Kadiri ambayo mimi naweza kufanya ni kidogo tu kuhusu kufanya habari njema za Ufalme zihubiriwe kwa kupiga hodi milangoni. Lakini kwa kuokoa pesa zangu na kuwapelekea ninyi kiasi fulani, mimi nahisi kwamba bado ninakuwa na sehemu fulani katika jambo hilo.’—Ohio.

‘Asanteni kwa kila jambo ambalo ninyi mmefanya kwa ajili ya Jumba la Ufalme. Pesa hizi [dola 5] ni za kuwasaidia ninyi kuhusiana na vitabu na Minara ili sisi tusome. Pesa hizi zimetoka katika nguruwe-bandia ambaye mimi natumia kama benki ya kutumbukiza pesa zangu. Asante kwa broshua Shule kutuambia sisi juu ya dawa za kulevya.’

“Tafadhali pateni hundi ikiwa imetiwa ndani ya bahasha. Dola mia mbili kati ya hizo ni kwa ajili ya Mfuko wa Ujenzi wa Jumba la Ufalme. Zile ambazo zimebaki ni za kutumiwa kwa njia yo yote ambayo ninyi mnaona inafaa kuiendeleza kazi ya kuhubiri.”—Missouri.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki