Ni Nani Ambao Ndio Waeneza-Evanjeli wa Kweli
HATA kama wewe unaishi wapi, katika njia moja au nyingine ile harakati ya kueneza evanjeli ambayo ilianzwa na Yesu Kristo imegusa maisha yako. Lakini si kila mtu ambaye anadai kuwakilisha Kristo ameeneza ule ujumbe wa kweli wa neno la Mungu. Si waeneza-evanjeli wote—wa sasa au wa wakati uliopita—ambao wamewaka juhudi ya umisionari ambayo ilikuwa tabia ya wanafunzi wa Kristo wa karne ya kwanza.
Ni kweli, makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yana wamisionari wanaokadiriwa kuwa 220,000 wakifanya kazi katika ulimwengu leo, lakini je! wamisionari hao wanapita ule mtihani wa kuwa waeneza-evanjeli wa kweli? Uenezaji-evanjeli wa Kikristo haukukusudiwa uwe namna ya ukoloni wa kiroho, ambapo wahubiri wangefanya kazi wakiwa mawakili wa serikali kubwa-kubwa za ulimwengu zenye kufanyiza makoloni. (Linganisha Yakobo 4:4.) Wala uenezaji-evanjeli wa kweli wa Kikristo haungetetea ile inayoitwa theolojia ya ukombozi ati na kusukuma-sukuma mambo ili kutokeza mabadiliko makubwa katika mifumo ya kisiasa na kijamii. (Yohana 17:16) Wala katika akili yake Yesu hakuwa na fikira ya wahubiri wenye kuhubiri Biblia kwa vishindo vingi katika vyombo vya kielektroni ambao wanapiga mayowe kutangaza namna yao ya “theolojia ya ufanisi” katika mawimbi ya televisheni na redio. (Mathayo 6:24) Basi, je! mweneza-evanjeli ni nani?
Ni Nini Uenezaji-Evanjeli wa Kweli?
Katika zile lugha za awali za Biblia, Kiebrania na Kigiriki, mweneza-evanjeli ni mtangazaji wa habari za kupendeza, au habari njema.a Habari njema za nini? Za wokovu, za utawala wenye uadilifu, na za amani. Mathalani, Isaya 52:7 inasema: “Jinsi ilivyo mizuri juu ya milima miguu yake aletaye habari njema, yeye aitangazaye amani, aletaye habari njema ya mambo mema, yeye autangazaye wokovu, auambiaye Sayuni, Mungu wako anamiliki!”
Zaidi ya hilo, kwenye uzaliwa wa Mwana wa Mungu, malaika alitangazia wachungaji hivi: “Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote; maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.” (Luka 2:10, 11) Hivyo, zile habari njema ziko hasa juu ya Yesu Kristo.
Yapata miaka 30 baadaye, Yesu aliingia katika lile Sinagogi katika mji wa Nazareti siku ya sabato na akasimama kusoma. “Ile hatikunjo ya nabii Isaya ilipokezwa kwake, na yeye akafungua ile hatikunjo na kupata pale mahali ambapo palikuwa pameandikwa: ‘Roho ya Yehova iko juu yangu mimi, kwa sababu yeye alinipaka mimi mafuta kutangaza habari njema.’” Baada ya yeye kumaliza kusoma, “alikunja ile hatikunjo akampokeza yule mtumishi kumrudishia hiyo na akaketi; na macho ya wote katika lile sinagogi ilikazwa kwa kukodolewa juu yake. Ndipo yeye akaanza kuwaambia hao: ‘leo andiko hili ambalo mmesikia sasa hivi limetimizwa.’” Kwa wazi Yesu alikuwa mhubiri wa habari njema, na zile habari njema ambazo yeye alitangaza zilikazwa hasa juu ya “ufalme wa Mungu.”—Luka 4:17-21; 8:1, NW.
Yesu aliwazoeza na kuwapa utume wafuasi wake wawe waeneza-evanjeli pia. (Mathayo 10; Luka 10) Kama ilivyokuwa kwa Mwalimu wao, ule moyo wa kuhubiri kwao ulikuwa “ufalme wa mbingu.” (Mathayo 10:7, NW) Hata hivyo, kuuhubiri Ufalme hakukuwa kwa mitume wa Yesu tu.
Wakati mnyanyaso dhidi ya lile kundi changa la Kikristo ulipofoka katika mji wa Yerusalemu, usimulizi wa kihistoria katika Matendo 8:1 unasema kwamba “wote isipokuwa wale mitume walitapanywa katika sehemu zote za yale majimbo ya Yudea na Samaria” Je! wanafunzi hao waliotawanywa walijificha na kujikunyata kwa woga? Sivyo! Kwa maana mstari 4 unaendelea kusema: “Hata hivyo, wale ambao walikuwa wametapanywa walienda kupitia ile nchi wakitangaza zile habari njema za lile Neno.” (NW)
Na ni kwa akina nani wao walitangaza zile habari njema? Kwa kupendeza, kitabu A Theological Word Book of the Bible kinasema: “Katika lile AJ [Agano Jipya] kuhubiri hakuhusiani hata kidogo na kuwatolea mahubiri wale ambao wameongolewa, jambo ambalo ndilo kwa kawaida linafanywa leo, lakini sikuzote kunahusiana na lile tangazo la ile ‘Habari nzuri ya Mungu’ kwa ulimwengu usio wa Kikristo.” Hivyo, Wakristo wote ni waeneza-evanjeli, na uenezaji-evanjeli wao hauwi wa kusema na wanaitikadi wenzao tu.
Lakini ni nini kilicho kichwa cha uenezaji-evanjeli wa ki-siku-hizi? Yesu alitabiri kwa siku yetu kwamba “habari njema hizi za Ufalme zitahubiriwa katika dunia nzima yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.” (Mathayo 24:14, NW) Na Yesu aliamuru si wale tu ambao waliona kupaa kwake bali wafuasi wake wa wakati ujao pia wawe “mashahidi [wake] katika Yerusalemu na katika Yudea yote na katika Samaria na kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.”—Matendo 1:8; ona pia Mathayo 28:19, 20, NW.
Hivyo, kiini cha ujumbe wa mweneza-evanjeli ni zile habari njema za Ufalme wa Yehova Mungu ulio katika mikono ya Mtawala mwekwa-rasmi wake Yesu Kristo, yule mwana-mfalme wa amani. (Isaya 9:6, NW) Na ujumbe huo umetia ndani kweli zote ambazo Yesu alizisema na ambazo wanafunzi wake waliandika. Waeneza-evanjeli wa kweli leo wanashikamana kwa uaminifu na kichwa hicho kimoja.
Ni Nani Ambaye Anadhamini Uenezaji-Evanjeli wa Kweli?
Waeneza-Evanjeli wa kweli wanaabudu Yehova akiwa Mungu. Yeye ndiye Mweneza-Evanjeli Mkuu; yeye ndiye Mdhamini wa kule kuhubiri habari njema. (Wagalatia 3:8; Ufunuo 10:7) Na yeye anatamani watu wote kila mahali wasikie na kutii ujumbe wake. “Hakika natambua ya kuwa Mungu hana upendeleo,” akatangaza mtume Petro kwa kutano dogo katika bandari ya Kaisaria katika Bahari ya Kati. “Bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki [uadilifu, NW] hukubaliwa na yeye. Neno lile alilowapelekea wana wa Israeli, akihubiri habari njema ya amani kwa Yesu Kristo (ndiye Bwana wa wote).”—Matendo 10:34-36.
Soma katika makala inayofuata baadhi ya mambo yaliyoonwa ambayo Mashahidi wa Yehova wanapata wanapotangaza zile habari njema kuzunguka dunia. Chunguza kumbukumbu lao la kuhubiri katika kurasa 12 mpaka 15 za gazeti hili. Ndipo sema pamoja na Mashahidi wa Yehova wakati wao watakapokutembelea mlangoni pako na uone kama wewe hukubali kwamba wao ndio waeneza-evanjeli wa kweli leo.
[Maelezo ya Chini]
a Kitenzi cha Kigiriki kinachosema “Leta habari njema,” au “eneza evanjeli,” (eu·ag·ge·liʹzo·mai) kilikuja kusimamia neno la Kiebrania linalofasiriwa ‘leta habari njema’ (bis·sarʹ) katika Isaya 52:7. Kile kitenzi bis·sarʹ hapa kinamaanisha “kupeleka ujumbe wa kushinda ulimwengu ambako enzi kuu ya ulimwengu wote mzima ya Yahweh imepata na wa utawala wake wa kifalme” na pambazuko la kipindi kipya, inasema The New International Dictionary of New Testament Theology.—Linganisha Nahumu 1:15, New World Translation of the Holy Scriptures with References, maelezo ya chini.