Maarifa Sahihi ya Kujua Mungu na Mwana Wake Yanaongoza Kwenye Uhai
“Hii ndiyo maana ya uhai wa milele, kutwaa ndani maarifa ya kukujua wewe, Mungu wa kweli mmoja tu, na ya yeye uliyemtuma, Yesu Kristo.”—YOHANA 17:3, NW.
1. Kwa sababu gani maarifa sahihi ya kujua Mungu na Yesu Kristo ni ya maana sana?
MAARIFA sahihi ya kujua Mungu na Mwana wake, Yesu Kristo, ni ya muhimu kwa wale wanaotaka uhai wa milele. “Penzi la [Mungu] ni kwamba binadamu wa aina yote wapaswa kuokolewa na waje kwenye maarifa sahihi ya kujua ukweli.” (1 Timotheo 2:4, NW) Maarifa hayo kutoka kwa Neno la Mungu lililovuviwa, Biblia, yatatuandaa tujue Mungu ni nani na wajibu wetu ni nini kuelekea yeye. (2Timotheo3:16,17; lYohana2:17) Pia yatatuwezesha kwa kufaa kutambua Yesu Kristo na uhusiano wetu pamoja naye.—Zaburi 2:12; Wafilipi 2:5-11.
2. Ni jambo gani huenda likatokea kwa kukosa maarifa sahihi ya kujua?
2 Pasipo maarifa sahihi, ya kujua huenda tukanaswa na mafundisho ya bandia yanayoendelezwa na mpingaji wa Mungu, Shetani Ibilisi, ambaye “ni mwongo, na baba wa huo.” (Yohana 8:44) Kwa hiyo, ikiwa fundisho la kidini linapinga Neno la Mungu, ikiwa ni la uwongo, basi kuliitikadi na kulifundisha kunapunguzia Yehova sifa na kutuleta katika upinzani naye. Kwa hiyo tunahitaji kuchunguza Maandiko kwa umakini ili kupambanua kweli kutokana na uwongo. (Matendo 17:11) Hatutaki kuwa kama wale ambao “sikuzote wanajifunza na bado hawawezi kamwe kuja kwenye maarifa sahihi ya kujua ukweli.”—2 Timotheo 3:1, 7, NW.
3. Ni nini fundisho la Biblia lililo wazi kuhusu Mungu, Yesu Kristo, na roho takatifu?
3 Kama tulivyoona katika makala iliyotangulia, fundisho la kidini la Utatu si fundisho la Biblia. Katika Neno la Mungu mwenyewe, yeye anatuambia waziwazi kwamba yeye ndiye Muumba wa vitu vyote na kwamba kiumbe chake cha kwanza mbinguni kilikuwa Mwana wake. (Ufunuo 4:11; Wakolosai 1:15, 16) Mungu alimpeleka Mwana wake duniani akiwa Mwanadamu ili aandae dhabihu ya ukombozi iliyotumika kuwa msingi wa msamaha wa dhambi za aina ya binadamu, na kuelimisha watu wenye moyo mnyofu zaidi juu ya Mungu na makusudi yake. (Mathayo 20:28; Yohana 6:38) Hata hivyo, lile fundisho rahisi lililo wazi kwamba Mungu na Kristo ni watu wawili mbalimbali, na kwamba roho takatifu si mtu bali ni kani ya utendaji ya Mungu, limepotoshwa karne zote. Badala yake, fundisho la Utatu limekuwa fundisho lenye msingi wa kidini la Jumuiya ya Wakristo.
“Mimi na Baba tu Umoja”
4. Kwa sababu gani dai ambalo makanisa yanafanya kuhusu Yohana 10:30 si la kweli?
4 Mara nyingi makanisa yanataja Yohana 10:30 ili kujaribu kuunga mkono Utatu, ijapokuwa mtu wa tatu hatajwi kamwe katika mstari huo. Yesu alisema hivi hapo: “Mimi na Baba tu umoja.” Lakini je! Yesu alimaanisha kwamba yeye mwenyewe alikuwa Mungu Mweza Yote, katika umbo tofauti tu? La, haingeweza kuwa hivyo kwa kuwa sikuzote Yesu alisema kwamba yeye alikuwa Mwana wa Mungu, mdogo Kwake na alitiishwa chini Yake. Basi, Yesu alimaanisha nini katika Yohana 10:30?
5, 6. (a) Ni katika maana gani Yesu alimaanisha kwamba yeye na Baba yake ni umoja? (b) Hili linatolewa kielezi jinsi gani kuhusiana na wanafunzi wa Yesu?
5 Yesu alimaanisha kwamba alikuwa na wazo na kusudi moja pamoja na Baba yake. Jambo hilo linaweza kuonwa katika Yohana 17:21, 22, NW ambapo Yesu alisali kwa Mungu ili wanafunzi wake “wote na wawe mmoja, kama vile wewe, Baba, umo katika umoja pamoja nami na mimi nimo katika umoja pamoja nawe, ili kwamba wao pia waweze kuwa katika umoja pamoja na sisi. . . ili wao wawe mmoja kama vile sisi tulivyo mmoja.” Je! Yesu alikuwa akisali kwamba wanafunzi wake wote wawe mtu mmoja? La, yeye alikuwa akisali kwamba wao wawe katika umoja wa nia na kusudi moja, kama vile Yesu na Mungu walivyokuwa.
6 Wazo lile lile linaonyeshwa katika 1 Wakorintho 1:10, NW, ambapo Paulo anataarifu kwamba Wakristo ‘wapaswa wote waseme kwa mwafaka, na kwamba imepasa kusiwe migawanyiko miongoni mwao, bali kwamba wao wapate kuunganika kwa kufaa katika akili moja na katika mstari mmoja wa fikira.’ Kwa hiyo Yesu aliposema kwamba yeye na Baba yake walikuwa mmoja, yeye hakumaanisha kwamba wao walikuwa mtu yule yule, kama vile alivyosema kwamba wanafunzi wake wapaswa wawe mmoja yeye hakumaanisha kwamba walikuwa mtu yule yule.
“Neno” Alikuwa Nani?
7. (a) Jumuiya ya Wakristo inadai nini kuhusu Yohana 1:1? (b) Ni nini kilicho katika Yohana 1:1 ambacho kinaonyesha mara moja kwamba Utatu hauzungumziwi?
7 Hata hivyo, namna gani Yohana 1:1, ambayo inasema hivi katika King James Version: “Katika mwanzo kulikuwako Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu”? Yohana 1:14 inatuambia kwamba “Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu.” Jumuiya ya Wakristo inadai kwamba huyu “Neno” (Kigiriki, lo’gos) aliyekuja duniani akiwa Yesu Kristo yeye mwenyewe alikuwa Mungu Mweza Yote. Hata hivyo, angalia kwamba hata katika King James Version Yohana 1:1 inasema “Neno alikuwa pamoja na Mungu.” Mtu fulani aliye pamoja na mtu mwingine si sawa na mtu yule mwingine. Kwa hiyo hata kutoka tafsiri hii, watu wawili wenye nyutu mbalimbali wanaonyeshwa. Pia, hakuna mtu wa tatu wa Utatu wo wote anayetajwa kamwe.
8. Tafsiri fulani zinafasiri sehemu ya mwisho ya Yohana 1:1 jinsi gani?
8 Kwa habari ya usemi wa King James Version kusema katika sehemu inayofuata ya Yohana 1:1 kwamba “Neno alikuwa Mungu,’ tafsiri nyingine zinasema jambo tofauti. Nyingine zinasema yafuatayo:
1808: “na neno alikuwa kamungu.” The New Testament, in an Improved Version, Upon the Basis of Archbishop Newcome’s New Translation: With a Corrected Text, London.
1864: “na kamungu alikuwa Neno.” The Emphatic Diaglott, na Benjamin Wilson, New York na London.
1935: “na Neno alikuwa wa kimungu.” The Bible—An American Translation, na J. M. P. Smith na E. J. Goodspeed, Chicago.
1935: “yule Logosi alikuwa wa kimungu.” A New Translation of the Bible, na James Moffatt, New York.
1975: “na kamungu (au, wa aina ya kimungu) alikuwa yule Neno.” Das Evangelium nach Johannes, by Siegfried Schulz, Göttingen, Ujeremani.
1978: “na Logosi alikuwa wa aina ya kimungu.” Das Evangelium nach Johannes, na Johannes Schneider, Berlin.
1979: “na kamungu alikuwa Logosi.” Das Evangelium nach Johannes, by Jurgen Becker, Würzburg, Ujeremani.
Pia katika 1950 New World Translation of the Christian Greek Scriptures, iliyotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society ya New York, Inc., ilifasiri maneno hayo, “na yule Neno alikuwa kamungu.”
9. Katika maandishiasilia ya Kigiriki, ni nini kinachotangulia tukio la nomino the-os’ (kamungu) kwenye Yohana 1:1 ambacho kinaonyesha kwamba rejezo ni kwa Mungu mweza yote?
9 Je! fasiri hizo zinapatana na utungo kisarufi wa Yohana 1:1 katika lugha ya Kigiriki? Ndiyo, zinapatana. Kwenye Yohana 1:1 kuna matukio mawili ya nomino ya Kigiriki the-os’ (kamungu). Tukio la kwanza linarejeza kwa Mungu mweza yote, ambaye Neno alikuwa naye—“na Neno [Lo’gos] alikuwa pamoja na Mungu [namna fulani ya the-os’].” The-os’ ya kwanza inatangulizwa na namna fulani ya nukta dhihirisho ho (the) ya Kigiriki nomino The-os’ ikiwa na nukta dhihirisho ho mbele yalo inaelekeza kwenye mfano ulio tofauti, katika kisa hiki Mungu mweza yote—“na Neno alikuwa pamoja na [the (yule)] Mungu.”
10. Kuhusiana na tukio la pili la the-os’ kwenye Yohana 1:1, kukosekana kwa nukta dhihirisho ho kunaonyesha nini?
10 Lakini katika sehemu ya mwisho mwisho ya Yohana 1:1, tafsiri kama zile ambazo zimeorodheshwa katika fungu 8 zinafasiri the-os’ ya pili (nomino kiarifu kama “kimungu” au “kamungu” badala ya “Mungu.” Kwa sababu gani? Kwa sababu the-os’ ya pili ni nomino kiarifu ya umoja inayoonekana baada ya kitenzi na bila nukta dhihirisho ho katika Kigiriki. Katika mstari huu, utungo huu wa sentensi unaelekeza kwenye tabia au sifa ya kiima hicho. Inakazia asili ya Neno, kwamba yeye alikuwa wa “kimungu,” “kamungu,” lakini si Mungu mweza yote. Hii inapatana na maandiko mengi yanayoonyesha kwamba “Neno” alikuwa mnenaji wa Mungu, aliyepelekwa duniani na Mungu. Kama Yohana 1:18, NW inavyotaarifu: “Hakuna mtu ambaye amemwona Mungu wakati wo wote; kamungu mzaliwa wa pekee [Mwana aliyeumbwa katika mbingu na Mungu mweza yote] aliye mahali pa kifua pamoja na Baba ndiye ambaye [amekuja dunia akiwa mwanadamu Yesu na] amemweleza [Mungu mweza yote].”
11. Kuna kielelezo gani cha Biblia kinachoonyesha kwamba aliongeza mtafsiri kuongeza nukta isiyo dhahiri mahali ambapo haimo katika Kigiriki na kwa sababu gani jambo hilo linafanywa?
11 Kuna mistari mingine mingi ya Biblia ambamo wale ambao wanatafsiri kutoka Kigiriki kuingia lugha nyingine wanaingiza nukta “a” kabla ya nomino kiarifu ingawa hakuna nukta katika maandishiasilia ya Kigiriki. Kuingizwa huku kwa nukta hiyo katika tafsiri kunatokeza tabia au sifa ya nomino ile. Mathalani, kwenye Marko 6:49, wanafunzi walipomwana Yesu akitembea juu ya maji, King James Version inasema, “wao walidhani ilikuwa imekuwa roho” (Kigiriki, phan’ta-sma). New World Translation inafasiri fungu hili la maneno kwa usahihi kabisa, “Wao walidhani: ‘ni mzuka!’ “Katika njia ile ile, tafsiri sahihi ya Yohana 1:1 inaonyesha kwamba Neno hakuwa “Mungu,” bali “kamungu.”
12. Ni matumizi gani kama hayo ya nukta isiyo dhahiri “a” hupatikana kwenye Yohana 8:44?
12 Vielelezi viwili vinavyofanana kidogo na hicho vinapatikana katika Yohana sura ya 8 mstari 44. Hapa Yesu, akizungumza juu ya Ibilisi, anasema: “Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo . . . Yeye ni mwongo na baba wa huo.” Sawa na Yohana 1:1, katika Kigiriki cha asili ile nomino kiarifu katika maneno haya yote (“muuaji,” “mwongo”) inatangulia kitenzi na haina nukta-dhihirisho. Katika kila kisa, sifa moja au tabia ya Ibilisi inaelezwa na katika tafsiri nyingi za lugha ya ki-siku-hizi, ni jambo la lazima kabisa kutia ndani nukta isiyo dhahiri (“a”) ili lieleweke. Hivyo, King James Version inafasiri maneno haya hivi, “Yeye alikuwa muuaji . . . yeye ni mwongo na baba wa huo.”—Ona pia Marko 11:32; Yohana4:19; 6:70; 9:17; 10:1, 13, 21; 12:6.
“Bwana Wangu na Mungu Wangu”
13, 14. Kwa sababu gani Tomaso angeweza kumwita Yesu “Mungu wangu” bila kumaanisha kwamba Yesu alikuwa Yehova?
13 Wanautatu pia wanataja Yohana 20:28 ili kuunga mkono madai yao. Hapo Tomaso alimwambia Yesu: “Bwana wangu na Mungu wangu!” Kama inavyoonyeshwa juu, hakuna kinza kwa rejezo la Tomaso kwa Yesu kuwa kamungu. Hiyo ingepatana na uhakika wa kwamba Yesu, akiwa katika kuwapo kwake kabla ya kuwa mwanadamu, hakika alikuwa kamungu, yaani, mtu wa kimungu mwenye nguvu. Naye kwa hakika amekuwa hivyo tangu kifo na ufufuo wake kwenye uhai wa kimbingu. Yesu hata alinukuu kutoka Zaburi ili kuonyesha kwamba wanadamu wenye nguvu walisemwa kuwa “miungu.” (Zaburi 82:1-6; Yohana 10:34, 35) Mtume Paulo aliandika kwamba kuna “miungu wengi na mabwana wengi.” (1 Wakorintho 8:5) Hata Shetani anaitwa “kamungu ka mfumo huu wa mambo.”—2 Wakorintho 4:4, NW.
14 Kristo ana cheo kilicho juu zaidi kuliko wanadamu wasiokamilika, au Shetani. Kama hao wanaweza kurejezelewa kuwa “miungu,” hakika Yesu anaweza kurejezewa kuwa kamungu. Kwa sababu ya cheo chake kisicho na kifani kuhusiana na Yehova, Yesu ni “kamungu ka pekee” (1 Yohana 1:18, NW), “Mungu mwenye uweza” (Isaya 9:6, NW), na “mungu” (Yohana 1:1). Hivyo hakukuwa na jambo lo lote lisilofaa kuhusu rejezo hilo la Tomaso kwa Yesu. Tomaso alikuwa akisema kwamba Yesu alikuwa kamungu kwake, wa kimungu, mwenye uweza. Lakini hakuwa akisema kwamba Yesu alikuwa Yehova, ndiyo sababu Tomaso alisema Mungu “wangu” na si ndiye yule Mungu.
15. Mstari wa 31 wa Yohana sura ya 20 unatambulisha Yesu waziwazi kuwa nani?
15 Mistari mitatu tu baadaye, katika Yohana 20:31, Biblia inataarifu: “Lakini hizi zimeandikwa; ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu.” Mashaka yote kuhusu kile ambacho huenda Tomaso alimaanisha yanaondolewa hapa. Mwandikaji wa Biblia Yohana anasema wazi wazi kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, si Mungu mweza yote.
Hakuwa Sawa na Mungu
16. Wayahudi walifanya dai gani, na Yesu alilikanusha jinsi gani?
16 Andiko lingine ambalo makanisa yanatumia ni Yohana 5:18. Linasema kwamba Wayahudi walitaka kumuua Yesu kwa sababu “alimwita Mungu Baba yake, akijifanya sawa na Mungu.” Ni nani aliyekuwa akisema kwamba Yesu alijifanya sawa na Mungu? Si Yesu. Yeye anaondolea mashaka jambo hili katika mstari unaofuata (19) kwa kutaarifu: “Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda.” Hivyo Yesu hakudai kwamba yeye alikuwa Mungu mweza yote au alikuwa sawa Naye. Yeye alikuwa akiwaonyesha Wayahudi kwamba wao walikuwa wamekosea, kwamba yeye hakuwa Mungu, bali alikuwa Mwana wa Mungu, na akiwa mnenaji wa Mungu, hangeweza kutenda neno mwenyewe. Je! tunaweza kuwazia Mungu mweza yote akisema kwamba hawezi kutenda neno mwenyewe? Kwa hiyo Wayahudi walitoa shtaka, naye Yesu alilikanusha.
17. (a) Ni ushuhuda gani ulio wazi kutoka kwa Neno la Mungu mwenyewe lililovuviwa kuhusu utambulishi wa Yehova, Yesu Kristo, na roho takatifu? (b) Ni jambo gani ambalo linapaswa lifanywe na andiko lo lote ambalo huenda Wanautatu wakaonyesha katika jitihada ya kujaribu kuthibitisha itikadi zao?
17 Hivyo, kutokana na ushuhuda wa Mungu katika Neno lake mwenyewe lililovuviwa, kutokana na ushuhuda wa Yesu, na kutokana na ushuhuda wa wanafunzi wa Yesu, ithibati yenye kufunikiza kabisa inaonyesha waziwazi kwamba Mungu mweza yote na Yesu Kristo ni watu wawili wenye nyutu mbalimbali, Baba na Mwana. Pia ithibati hiyo inaonyesha wazi-wazi kwamba roho takatifu si mtu wa tatu katika Utatu wo wote bali ni kani ya utendaji ya Mungu. Ni jambo lisilofaa kuchukua maandiko kutoka mistari inayoyazunguka au kujaribu kuyapotosha ili kuunga mkono Utatu. Maandiko yo yote kama haya lazima yapatanishwe na ushuhuda mwingine wa Biblia ulio wazi.
Kwa Sababu Gani Utatu Ulikua?
18. Fundisho la kidini la Utatu lilitoka wapi?
18 Ukitazama ukurasa 18, “Ukuzi wa Kihistoria wa Fundisho la Kidini la Utatu,” utaona kwamba chanzo cha Utatu ni cha kipagani. Si fundisho la Biblia, bali liliingizwa na Jumuiya ya Wakristo katika karne ya nne. Hata hivyo, muda mrefu kabla ya hapo, kulikuwa na utatu-utatu katika Babuloni ya kale, Misri, na sehemu nyingine. Hivyo Jumuiya ya Wakristo ilitia wazo la kipagani katika mafundisho yalo. Jambo hili lilianzishwa na maliki Mroma Konstantino, ambaye hakupendezwa na ukweli kuhusu jambo hili, lakini alitaka kufanya imara milki yake iliyofanyizwa na wapagani na Wakristo wenye kuasi imani. Mbali na kuwa ukuzi wa fundisho la Kikristo, Utatu ulikuwa ithibati ya kwamba Jumuiya ya Wakristo ilikuwa imeasi imani kutoka kwa mafundisho ya Kristo na badala yake ilikuwa imeingizwa mafundisho ya kipagani.
19. Kwa sababu gani fundisho la kidini la Utatu lilikua?
19 Kwa sababu gani fundisho hilo la kidini lilikua? Hakika, masilahi ya Mungu hayatumikiwi kwa kuvuruga na kufanya Yeye, Mwana wake, na roho Yake takatifu iwe fumbo. Na kuvurugwa hakutumikii masilahi ya watu. Badala yake, kadiri watu walio wengi wanavyovurugwa juu ya Mungu na makusudi yake ndivyo inavyopendeza Shetani Ibilisi, mpinzani wa Mungu, “mungu wa dunia hii” anayefanya kazi ili ‘apofushe fikira za wasioamini.’ (2 Wakorintho 4:4) Kwa kuwa fundisho hilo la kidini linafanya ionekane kwamba wanatheolojia tu ndio wanaoweza kuelewa mafundisho ya Biblia, hilo linawapendeza pia viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo. Jambo hili linawasaidia waendelee kuwabamba watu wa kawaida.
20. (a) Ni ukweli gani ulio rahisi juu ya Utatu? (b) Kutwaa ndani maarifa sahihi ya kujua kweli zenye kukomboa kutamaanisha nini kwetu sisi?
20 Hata hivyo, ukweli kuhusu habari hii ni rahisi sana hivi kwamba mtoto anaweza kuuelewa. Kijana mdogo anajua kwamba yeye si sawa na baba yake bali wao ni watu wawili walio mbalimbali. Vivyo hivyo, Biblia inaposema kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu, hivyo ndivyo inavyomaanisha. Huo ndio ukweli rahisi, huku fundisho la kidini la Utatu si rahisi. Ni uwongo. Kwa hiyo ni lazima mbuni wao awe yule “aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote.” (Ufunuo 12:9) Lakini ukweli rahisi wenye kuburudisha juu ya Mungu, Mwana wake, Yesu Kristo, na roho takatifu ya Mungu yenye nguvu inawaweka watu huru kutoka mafundisho ya bandia ambayo mizizi yayo ni ya kipagani na yanayobuniwa na Shetani. Kama alivyosema Yesu kwa watafutaji ukweli wenye weupe wa moyo: “Tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.” (Yohana 8:32) Kutwaa ndani maarifa sahihi ya kujua kweli zenye kukomboa, vilevile kuzitenda, ‘kunamaanisha uhai wa milele.’—Yohana 17:3, NW.
Wewe Ungejibu Jinsi Gani?
◻ Kwa sababu gani maarifa sahihi ya kujua Mungu na Mwana wake ni ya maana sana?
◻ Yesu alimaanisha nini aliposema, “Mimi na Baba tu umoja”?
◻ Ni jinsi gani Yohana 1:1 inapambanua kati ya Neno na Mungu?
◻ Kwa sababu gani Tomaso angeweza kwa kufaa kumwita Yesu “Mungu wangu”?
◻ Fundisho la kidini la Utatu lilitokea jinsi gani na ni nani aliyelitunga?
[Sanduku katika ukurasa wa 18]
Ukuzi wa Kihistoria wa Fundisho la Kidini la Utatu
The New Encyclopædia Britannica, ya 1985, Micropædia, Buku la pili, ukurasa 928, inasema hivi chini ya kichwa cha Utatu: “Wala neno Utatu wala fundisho hilo la kidini lililo dhahiri halionekani katika Agano Jipya, wala Yesu na wafuasi wake hawakukusudia kupinga ile Shema katika Agano la Kale: ‘Sikiza, Ee Israeli: Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja.’ (Kum. 6:4)” Ensaiklopedia hii inasema hivi pia: “Fundisho hilo la kidini lilitokea polepole katika muda wa karne nyingi na kupitia ubishi mwingi. . . . Baraza la Nicaea katika 325 lilitaja ile kanuni yenye maana kwamba kwa kukiri kwa fundisho hilo la kidini la kwamba Mwana ni ‘wa asili ile ile . . . kama Baba,’ hata ijapokuwa lilisema machache sana kuhusu Roho Takatifu. . . . Kufikia mwisho wa karne ya 4 . . . fundisho la kidini la utatu lilichukua kwa nguvu umbo lile lile lililodumisha tangu mwanzo.”
New Catholic Encyclopedia, ya 1967, Buku 14, ukurasa 299, inakubali hivi: “Ile kanuni ‘Mungu mmoja katika Watu watatu’ haikuimarishwa, hakika haikutumiwa kikamili katika maisha ya Kikristo na ungamo layo la imani, mwanzoni mwa karne ya 4. . . . Miongoni mwa Mababa wa Kimitume, hakukuwa na jambo dogo lililokaribia tabia au kimo hicho.”
Hivyo, fundisho la kidini la Utatu si la Kimaandiko bali liliingizwa rasmi na Baraza la Nicaea katika mwaka 325 W.K. Fundisho hili la kidini lilitia ndani wazo la kipagani ambalo lilianza muda mrefu kabla katika Babuloni na Misri wa kale na lilikuwa likitumiwa katika mabara mengine pia. Mwanahistoria Will Durant alionelea hivi katika The Story of Civilization: Sehemu Ya 3, ukurasa 595: “Ukristo haukuharibu upagani; uliutia ndani— Kutoka Misri yakaja yale mawazo ya utatu wa kimungu.”
Katika An Encyclopedia of Religion, kilichohaririwa na Vergilius Ferm, 1964, katika kurasa 793 na 794, chini ya neno “utatu,” utatu-utatu wa Wababulonia, Wabuddha, Wahindu, Wanose, Wataoisti, na dini nyingine pamoja na zile za Jumuiya ya Wakristo umeorodheshwa. Kama kielezi, kinaeleza kwamba katika India, “Utatu mkubwa unatia ndani Brahma, Muumba, Vishnu, Mhifadhi na Shiva, Mharabu. Huo unawakilisha marudio wa kuwapo, kama vile utatu wa Kibabuloni wa Anu, Enlil na Ea unavyowakilisha asili ya kuwapo, hewa, maji, dunia.”
Jumba la Kuhifadhi Vitu la Uingereza lina vitu vilivyotengenezwa na wanadamu ambavyo vinaonyesha utatu-utatu wa kale, kama ule wa Isis wa Misri, Harpokrates, na Nephthys. Kichapo kimoja cha Idara ya Kikale ya jumba hilo ya kuhifadhi vitu na Matukio ya Nyakati za Baadaye kinaeleza yafuatayo yaliyokuwa yameandikwa katika vito vya kale: “[Upande] wa juu, miungu ya Misri Horus-Bait (mwenye kichwa cha kengewa), Buto-Akori (nyoka), na Hathor (mwenye kichwa cha chura). [Upande] wa chini, mstari wa Kigiriki ‘Bait mmoja, Hathor mmoja, Akori mmoja; nguvu zao ni moja. Msalimu, baba wa ulimwengu, msalimu, mungu mwenye maumbo matatu!’ Hivyo miungu hao wanatambulishwa kuwa vidhihirisho vitatu vya nguvu moja, labda mungu-jua.”
Historia inathibitisha kwamba Utatu uliazimwa kutoka kwa wapagani na ulikuwapo karne nyingi kabla Yesu hajaja duniani. Muda mrefu baada ya kifo chake, uliendelezwa na wale waliokuwa wameshawishwa na falsafa za kipagani na ambao walikuwa wameasi imani kutoka katika ibada ya kweli ya Mungu kama ilivyofundishwa na Yesu na mitume wake.
[Picha katika ukurasa wa 16]
Yesu alisali kwa ajili ya wanafunzi wake wawe katika wazo na kusudi moja kama yeye na Baba yake walivyokuwa katika umoja