Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 6/15 kur. 3-6
  • Utawala wa Ulimwengu Unabadilika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utawala wa Ulimwengu Unabadilika
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hangaikio la Mungu Juu ya Serikali
  • Mtu Fulani Aliye Kama Mwana wa Binadamu
  • Serikali Kubwa ya Ulimwengu Iliyo ya Mwisho ya Kibinadamu
  • Ile Serikali ya Ufalme
  • Watawala-Washirika
  • Badiliko la Utawala Karibuni!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Ufalme wa Mungu Ni Bora Katika Njia Zote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Serikali Kubwa za Ulimwengu za Historia ya Biblia Zapiga Miguu Kwenda Kwenye Mwisho Wazo!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 6/15 kur. 3-6

Utawala wa Ulimwengu Unabadilika

KAMA wewe ungekuwa unaweza kuchagua, ni serikali ya aina gani ambayo wewe ungetaka kuishi chini yayo? Inaelekea kwamba walio wengi kati yetu tungechagua serikali thabiti yenye kutoa kiasi fulani kinachofaa cha uhuru wa kibinafsi. Sisi tungependa serikali ambayo ingeweza huzuia uhalifu, kuendeleza amani, kukuza haki ya hukumu katika jamii, na kusitawisha ufanisi wa vitu vya kimwili. kwa uhakika, sisi tungeona ni afadhali kuwa na serikali isiyo ya uonevu wala ufisadi.

Jambo lenye kuhuzunisha ni kwamba, serikali zilizo nyingi zimekuwa si za namna hiyo. Wakati sisi tunapofikiria ulimwengu kama ulivyo katika hii nusu ya mwisho-mwisho ya karne ya 20, tunaona nini? Umaskini, ufisadi, kutotimizwa vizuri kwa mambo yapasayo, uonevu, ukosefu wa haki ya hukumu katika jamii, uhalifu, na ukosefu wa masikilizano ya kimataifa. Hili ndilo tokeo la mwisho la maelfu ya miaka ya kuwako kwa serikali ya kibinadamu.

Bila shaka, ni kweli kwamba watawala fulani mmoja mmoja wamekuwa na akili ya kutoonea na wenye uwezo wa kutimiza wajibu wao. na mifumo fulani ya kiserikali imekuwa thabiti kwa kadiri fulani na yenye matokeo mazuri kwa wakati fulani. Lakini kushindwa kwa serikali ya kibinadamu kwa ujumla kufanya yale ambayo sisi tunahisi kisilika kwamba inapaswa kuyafanya kwa ajili ya aina ya binadamu kunathibitisha ukweli wa taarifa hii ya Biblia: “Njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.” (Yeremia 10:23) Ndiyo kusema, mwanadamu hakufanywa ajiongoze mwenyewe bila msaada wa nje.

Hiyo ndiyo sababu ni vizuri kujua kwamba utawala wa ulimwengu unabadilika. Tunamaanisha nini kwa msemo huu? Tunamaanisha kwamba karibuni uongozi wa kila siku wa maisha za aina ya kibinadamu utaingia mikononi mwa namna mpya kabisa ya serikali ambayo itafanikiwa kikamili. Badiliko hilo kubwa sana la serikali lilitabiriwa na Mungu. Kweli kweli, hicho ndicho kichwa chenyewe cha Biblia.

Hangaikio la Mungu Juu ya Serikali

Sikuzote Mungu amehangaikia kuongozwa kwa aina ya binadamu. Yeye huchungulia kwa ukaribu ili aone ni kwa kipimo gani serikali za kibinadamu zinatimiza daraka lazo, na nyakati nyingine yeye huziitisha hesabu ya matendo yazo. Kweli kweli, historia za baadhi ya mifumo ya kiserikali iliyo ya kutokeza ya miaka 2,500 iliyopita ya historia zilitabiriwa katika Biblia. Katika kitabu cha Danieli, kilichoandikwa zaidi ya miaka 500 kabla ya kuzaliwa kwa Kristo, katika kumbukumbu yaliandikwa manabii yaliyotabiri anguko kamili la Babuloni wa kale, na vilevile inuko na anguko la Umedi-Uajemi, Ugiriki, na Roma. Manabii hayo hata yalitabiri ule usitawi wa Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza-Amerika ya siku yetu wenyewe. Mfikirio mfupi wa baadhi ya manabii haya utatusaidia tuelewe linalomaanishwa na taarifa ya kwamba utawala wa ulimwengu unabadilika.

Wa kwanza wa manabii haya ya kustaajabisha ulikuwa ndoto yenye kuvuviwa, ambamo serikali kubwa za kisiasa za ulimwengu kutoka siku ya Danieli kuteremka mpaka kufikia wakati wetu ziliwakilishwa na mfano mkubwa sana. Ndipo, jiwe ambalo lilikatwa si kwa mikono, likapiga na kuponda-ponda mfano huu. Jiwe hilo lilisaga-saga hizi serikali kubwa za ulimwengu zikawa mavumbi, “kama makapi kutoka sakafu ya upuraji wa kiangazi, na upepo ukazichukulia mbali hivi kwamba hakuna kidalili hata kidogo kilichopatikana cha hizo.”​—Danieli 2:31-43, NW.

Sura hiyo hiyo ya Danieli inaeleza ni nini iliyokuwa maana ya jambo hilo. Inaonyesha kwamba serikali za kibinadamu zenye kushindwa kutimiza wajibu zingeondolewa na mahali pazo pachukuliwe na kitu fulani kinachozipita kwa ubora usio na mipaka. Inatuambia hivi: “Katika siku za wafalme hao Mungu wa mbingu atasimamisha ufalme ambao hautaletwa kwenye angamizo. Na ufalme wenyewe hautapitishwa kwa watu wengineo wote. Utaponda-ponda na kuweka mwisho kwenye falme zote [za kibinadamu] hizi, na huo wenyewe utasimama hadi nyakati zisizo dhahiri. . . . Na ndoto ile ni ya kutegemeka, na fasiri ile yayo ni ya kustahili itibari.”​—Danieli 2:44, 45, NW.

Lakini huo haukuwa ndio mwisho wa jambo hilo. Katika njozi ya pili, zile serikali kubwa za ulimwengu zenye kufuatana-fuatana ziliwakilishwa na hayawani wakubwa sana wenye vitabia vya serikali iliyowakilisha. Ndipo Danieli aliporuhusiwa kuiona njia yote ile ya kupanda juu mpaka kwenye kiti-ufalme cha kimbingu chenye kuvuvia hofu nyingi, cha “yule Mkale wa Siku,” na akaonyeshwa jambo fulani ambalo lingetukia, si katika siku yake bali wakati wa utawala wa ile Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza-Amerika ya wakati wetu. Yeye aliona Mahakama ya Yehova ya kimbingu iliyo na adhama ikiketi kutoa hukumu juu ya hizi serikali kubwa za ulimwengu. (Danieli 7:2-12) Kama mistari inayofuata inavyoonyesha, uamuzi wenye amri ya kimungu ulitolewa ili kuwe na badiliko katika utawala. Utawala huu ungepewa kwa nani?

Mtu Fulani Aliye Kama Mwana wa Binadamu

Danieli anatoa lile jibu la kusisimua:

“Mimi nikaendelea kutazama katika njozi za usiku, na, ona kule! pamoja na mawingu ya zile mbingu mtu fulani kama mwana wa binadamu akawa anakuja; na kwa yule Mkale wa Siku yeye akapata ruhusa ya kukaribia, nao wakamleta juu karibu, hata mbele za Mmoja huyo. Na kwake yeye ukapewa utawala na hadhi na ufalme, kwamba jamii za watu, vikundi vya kitaifa na lugha-lugha vipaswe vyote kumtumikia hata huyo. Utawala wake ni utawala wa kudumu kwa wakati usio dhahiri ambao hautapitilia mbali, na ufalme wake ni mmoja ambao hautaletwa kwenye uangamivu.”​—Danieli 7:13, 14, NW.

Hivyo Danieli alitumiwa kutabiri kwamba “yule Mkale wa Siku,” Yehova Mungu mwenyewe, ataondolea mbali utawala mbaya wa serikali za kibinadamu zenye uonevu. Yeye ataweka mahali pao serikali nzuri sana kuliko vile ambavyo aina ya kibinadamu ingeweza kuwazia—Ufalme usioonekana wenye kuzoea kutumia nguvu na mamlaka kutoka mbinguni. Lakini ni nani huyu “mtu fulani kama mwana wa binadamu” ambaye atapokea Ufalme ule?

Sisi hatuachwi tukiwa katika shaka. Yesu alijitambulisha mwenyewe kuwa “Mwana wa binadamu.” Yeye alieleza kuwapo kwake kuwa ndio wakati ambapo “Mwana wa binadamu afika katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye.” (Mathayo 25:31, NW) Wakati kuhani mkuu Myahudi alipodai kwamba Yesu aambie mahakama kama yeye alikuwa “ndiye Kristo Mwana wa Mungu,” Yesu alijibu hivi: “Wewe mwenyewe ulisema hivyo. Hata hivyo mimi nasema kwa ninyi wanaume, Kutoka sasa na kuendelea ninyi mtaona Mwana wa binadamu akiketi kwenye mkono wa kuume wa nguvu na akija juu ya mawingu ya mbinguni “a—Mathayo 26:63, 64, NW.

Serikali Kubwa ya Ulimwengu Iliyo ya Mwisho ya Kibinadamu

Yapata miaka 600 baada ya wakati wa Danieli, (mtume Yohana aliandika kitabu cha Biblia cha Ufunuo chini ya uvuvio wa kimungu. Kitabu hicho kinarejeza kwenye hizi serikali kubwa za ulimwengu kuwa “wafalme” wenye uwezo, kikisema: “Na kuna wafalme saba: watano wameanguka, mmoja yupo, yule mwingine hajawasili bado, lakini wakati yeye atakapofanya kuwasili ni lazima yeye abaki kwa kitambo kifupi.”​—Ufunuo 17:10, NW.

Wale watano waliokuwa tayari wameanguka wakati Yohana alipoandika hivi walikuwa Misri, Ashuru, Babuloni, Umedi-Uajemi, na Ugiriki. Milki ya Kiroma ilikuwa ingali ‘ipo.’ Kwa uwazi, yule wa saba, Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza-Amerika ya wakati wetu, ilikuwa haijawasili bado. Kulingana na Ufunuo, hakuna serikali kubwa ya ulimwengu inayotokea baada ya ile ya saba—ile moja iliyopo leo. Hii ndiyo ya mwisho. Hakutakuwa na nyingine.

Hata hivyo, hilo halipasi kuwa wazo la kuogopesha—ni la kusisimua! Linamaanisha kwamba utawala wa kibinadamu usiofuata haki ya hukumu, wenye kufanya vita, uko karibu na mwisho wao. Manabii yanaungana katika kusimulia juu ya badiliko lenye umaana mkubwa katika njia ambayo dunia inatawalwa—badiliko la kutoka kwenye serikali ya kibinadamu yenye ubinafsi, kuja kwenye moja ya kimbingu iliyo na uadilifu, Ufalme wa Mungu.

Ile Serikali ya Ufalme

Lakini Ufalme huo ni nini? Ni zaidi sana kuliko uvutano wa kutokeza mema tu katika mioyo na maisha za watu. Pia ni zaidi sana kuliko maisha ya lile linaloitwa kanisa la Kikristo eti. Ufalme wa Mungu ni serikali halisi. Huo una mfalme, watawala-washirika, eneo la utawala, na raia. Nao utatokeza zile baraka nzuri ajabu zilizotajwa mapema.

Yesu anatambulishwa kuwa Mfalme wa Ufalme huo. Yeye alijifananisha mwenyewe na mwanamume mmoja wa uzaliwa msharifu ambaye “alisafiri kwenye bara la mbali akajisalimishie mwenyewe nguvu ya kifalme na kurudi.” Kuhusu wakati huo ujao, yeye alisema: “Wakati Mwana wa binadamu atakapowasili katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo yeye atakapoketi juu ya kiti cha ufalme chake chenye utukufu.”​—Luka 19:12; Mathayo 25:31, NW.

Ni wakati gani “Mwana wa binadamu” angewasili? Si lazima sisi tukisie jibu. Maneno ya Yesu hapa ni sehemu ya jibu lake kwa swali hili: “Ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” (Mathayo 24:3, 30, NW) Kama vile ambavyo imeonyeshwa mara nyingi katika safu za gazeti hili, “kuwapo” huko kulianza katika mbingu bila kuonekana, mwishoni mwa “zile nyakati zilizowekwa rasmi za mataifa” katika 1914.b—Luka 21:24, NW.

Kama vile Ufunuo sura ya 12 ulivyosema ingetukia, hapo ndipo Yesu alipochukua nguvu yake na akavurumisha Shetani kutoka mbinguni aje chini kwenye ujirani wa dunia. Sauti moja katika mbingu ilitangaza hivi: “Sasa umekuja kupita wokovu na nguvu na ufalme wa Mungu wetu na mamlaka ya Kristo wake, kwa sababu mshitaki wa ndugu zetu amevurumishwa chini.” Hiyo inaeleza sababu inayofanya hali za ulimwengu zizidi kuwa mbaya tangu wakati huo. Hivyo, ile sauti ya kimbingu iliendelea kusema: “Ole kwa dunia na kwa bahari, kwa sababu Ibilisi amekuja chini kwenu ninyi, akiwa na kasirani kuu, akijua yeye ana kipindi kifupi cha wakati.”​—Ufunuo 12:9-12, NW.

Wakati huo mfupi utamalizika karibuni. Sura chache baadaye, Yesu mtukuzwa anaonwa akiwa juu ya farasi mweupe. Yeye anaitwa “Lile Neno la Mungu,” na yeye ‘atadhurubu mataifa’ na ‘kuyachunga kwa ufito wa chuma’​—sawa na vile Danieli alivyokuwa ameonyesha kwamba mataifa yangepondwa-pondwa na Ufalme wa Mungu ulio kama jiwe ambalo lingekua lijaze dunia nzima.​—Ufunuo 19:11-16; Danieli 2:34, 35, 44, 45.

Serikali za kibinadamu za kisiasa zilizo kama hayawani hazitaonea tena kamwe aina ya binadamu!

Watawala-Washirika

Lakini kuna zaidi. Danieli alivuviwa na Mungu kusema kwamba Ufalme huo ungepewa, si kwa “mtu fulani kama mwana wa binadamu” peke yake, bali pia “kwa watu ambao ndio watakatifu wa yule Mmoja Aliye Mkubwa Zaidi ya Wote.”​—Danieli 7:27, NW.

Hawa ni akina nani? Ufunuo unasema hivi juu ya Mwana-Kondoo, Kristo Yesu: “Wewe ulinunua watu kwa ajili ya Mungu kutoka kila kabila na ulimi na jamii ya watu na taifa, na wewe ulifanya hao wawe ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, na wao ni wa kutawala wakiwa wafalme juu ya dunia.” Unazidi kusema kwamba wao watakuwa “makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala wakiwa wafalme pamoja naye kwa ile miaka elfu.” Hesabu yao inapewa kuwa 144,000.​—Ufunuo 5:9, 10–14:1; 20:6, NW.

Hawa ndio wale ambao Mungu Aliye Juu Zaidi anachagua washiriki katika serikali ya ulimwengu pamoja na Mwanaye, Yesu Kristo. Je! wakati ujao wetu ungeweza kuwa salama zaidi katika mikono mingine iliyo tofauti na ya hawa ambao Mungu anachagua? Hapana, Ufalme huu utakuwa ndiyo serikali bora inayowezekana—bora kwa mbali kuliko cho chote ambacho mwanadamu amepata kujua. Chini ya utawala wayo dunia yote itageuzwa iwe Paradiso iliyokusudiwa na Mungu hapo awali.

Soma makala inayofuata na uone kama hii ndiyo aina ya serikali ambayo wewe ungechagua kuishi chini yayo.

[Maelezo ya Chini]

a Kuhusu njozi ya Danieli, New Catholic Encyclopedia inasema: “Hakuwezi kuwa na shaka kubwa kwamba hapa Danieli ananena juu ya tukio lililo la umaana wa milele kwenye mwisho wa wakati.” Inaongezea hivi: “Taarifa ya kujitetea kwa Yesu mbele ya Sanhedrini inatupa sisi ithibati isiyoweza kubishaniwa ya utambulisho Wake wa kuwa ndiye Mwana wa Binadamu na rejezeo la wazi juu ya kuja Kwake katika nguvu ya mamlaka.”

b Ona matoleo ya Mnara wa Mlinzi ya Oktoba 1, 1982 na Oktoba 1, 1984.

[Sanduku katika ukurasa wa 4]

“Kichwa Kikuu cha Fundisho la Yesu”

“Kichwa cha ufalme wa Mungu kinachukua mahali pakuu katika kuhubiri kwa Yesu.”​—New Catholic Encyclopedia.

“[Ufalme wa Mungu] unafikiriwa kwa ujumla kuwa ndio kichwa kikuu cha fundisho la Yesu.”​— Encyclopædia Britannica.

Lakini ni lini uliokuwa wakati wako wa mwisho kusikia hicho “kichwa kikuu cha fundisho la Yesu” kikizungumzwa katika kanisa?

[Sanduku katika ukurasa wa 5]

Mvurugo Juu ya Ufalme wa Mungu

Watu fulani wamewaza kwamba “kanisa lililo duniani” ndilo Ufalme wa Mungu, hali wengine wameitikadi kwamba ulimwengu uliopo “utasitawi ukiwa chini ya uvutano wa Kikristo mpaka uwe ndio ule Ufalme.” Na bado wengine wanasema kwamba Ufalme wa Mungu ni “utawala wa Mungu katika moyo na maisha ya mtu akiwa peke yake.”

Lakini je! mambo haya tu ndiyo yanayohusika katika Ufalme wa Mungu​—mfumo wa kidini, badiliko la kisiasa lenye kuja pole kwa pole, au hali fulani ya kiroho katika mioyo ya watu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki