Serikali Kubwa za Ulimwengu za Historia ya Biblia Zapiga Miguu Kwenda Kwenye Mwisho Wazo!
JE! WEWE unaweza kuwazia historia ikiandikwa mapema kabla ya kutukia? ‘Haiwezekani,’ wewe unasema? Hata hivyo, kuna kitabu ambacho kwa kweli kinaeleza historia mapema kabla haijatukia—mamia, nyakati fulani hata maelfu ya miaka kabla ya matukio yale kutukia! Kitabu hicho ndicho Biblia.
Biblia haikuripoti matukio ya kale kwa usahihi tu bali hata ilitabiri kwa njia ya kustaajabisha sana ule mfuatano wa mambo makubwa-makubwa ya historia ya ulimwengu kulingana na vile yangeathiri watu wa Mungu, kutoka ule wakati wa Babuloni ya kale, miaka zaidi ya 2,500 iliyopita, kuteremka mpaka na hata kupita siku yetu iliyopo.
Danieli, nabii ambaye aliishi katika karne ya sita kabla ya Wakati wa Kawaida wetu, alipewa mafunuo manne mbalimbali ambayo yalihusu wakati ujao wa historia ya ulimwengu. Yeye alipata wapi habari zake? Akasema Danieli: “Kuna Mungu katika mbingu ambaye ni Mfunuaji wa siri.” (Danieli 2:28, NW) Walipofukua mabaki yaliyoachwa nyuma na serikali kubwa za ulimwengu za kale, wachimbuzi wa vitu vya kale wamepata uthibitisho wa kushangaza sana juu ya ukweli wa ile historia na pia ule unabii unaopatikana katika Biblia.
Mbili za zile serikali kubwa za ulimwengu za historia ya Kibiblia, Misri na Ashuru, zilikuwako muda mrefu kabla ya wakati wa Danieli. Babuloni ilikuwa ikitawala katika siku ya Danieli, na majina ya serikali kubwa mbili za ulimwengu zilizofuata hizo yalifunuliwa kwa nabii yule. (Danieli 2:47, 48; 8:20, 21) Nyingine mbili zingefuata hizo, zikitupandisha kutuleta kwenye wakati uliopo.
Ngapi?
Kulingana na Biblia, kungekuwa na ngapi za serikali kubwa hizo za ulimwengu? Jibu lilipewa kwa Yohana yule mtume aliyezeeka na linaonyesha sisi tuko wapi katika ule mtiririko wa wakati. Malaika mmoja aliambia Yohana: “Kuna wafalme saba: watano wameanguka, mmoja yupo, yule mwingine hajawasili bado.”—Ufunuo 17:10, NW.
Ni serikali tano gani kubwa za ulimwengu ambazo zilikuwa tayari zilikuja na kwenda ilipofika siku ya Yohana? Misri, Ashuru, Babuloni, Umedi-Uajemi, na Ugiriki. Ni ipi moja ilikuwako bado? Roma. Na ni serikali ipi ilikuwa ‘haijawasili bado’? Ni ile Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza-Amerika ya siku yetu. Hizo ndizo serikali kubwa za ulimwengu ambazo watu wa Mungu, wa kale na wa ki-siku-hizi, wamekuwa wakijihangaisha kujua habari zazo.
Uhakika ulio wa maana kubwa hasa ni huu: Kungekuwa na mfuatano-mfuatano wa saba tu za serikali kubwa hizo! Serikali kubwa ya nane iliyo ya rika moja na sehemu ya mfuatano huo, ambayo ingetia ndani mabaki wa zile saba, ilitabiriwa kuwako kwa wakati mfupi katika zile siku za ile ya saba. (Ufunuo 17:10, 11) Hiyo inamaanisha kwamba sisi tunaishi katika ule wakati wa ile ya mwisho ya zile serikali kubwa za ulimwengu zenye kutawalwa na wanadamu. Hakutakuwa na zaidi!
Karibuni sasa, zile serikali kubwa za ulimwengu zitakuwa zimeishiwa na siku yazo. Danieli alitoa unabii kwamba mifumo hiyo ya kibinadamu itapondwa-pondwa na ‘kuchukuliwa mbali na upepo.’ (Danieli 2:35, NW) Ni nini ambacho kitachukua mahali pazo? Kitu fulani kizuri zaidi! Danieli anaripoti: “Katika siku za wafalme hao Mungu wa mbingu atasimamisha ufalme ambao hautaletwa kwenye angamizo. . . . Utaponda-ponda na kuweka mwisho kwenye falme zote hizi, na huo wenyewe utasimama hadi nyakati zisizo dhahiri,” milele. (Danieli 2:44, NW) Kwa hiyo hakuna kitu cho chote kinachopungua ule Ufalme wa Mungu ambacho kitachukua mahali pa hizo serikali kubwa za ulimwengu zilizo za kibinadamu. Hayo ni maendeleo maadhimu kama nini katika utawala wa ulimwengu!
Bila shaka wewe unajua jambo fulani juu ya zile serikali kubwa za ulimwengu. Lakini je! maarifa zaidi ya kujua desturi zazo, dini yazo, na uhusiano wazo pamoja na watu wa Mungu na unabii wa Biblia yangekusaidia wewe ufahamu mengi zaidi juu ya historia ya aina ya wanadamu kwa msaada wa Maandiko?
Ndivyo, kweli kweli. Kwa hiyo sisi tunafurahi kuchapisha, kuanza na toleo hili, mfufulizo wa makala nane zinazohusu zile serikali kubwa za ulimwengu. Makala hizo zinapasa kusaidia kukusadikisha wewe kwamba ile historia ambayo inasimuliwa katika Biblia ni yenye kutegemeka na inayostahili itibari. Hizo zinapasa pia kuimarisha imani yako wewe katika ule uhakika wa kwamba maunabii ya Biblia ni ya uaminifu na kweli!