Watangazaji wa Ufalme Waripoti
Udumifu Katika Utume Wao wa Kimungu
MASHAHIDI WA YEHOVA wanachukua kwa uzito sana utume wao wa kimungu kuhubiri zile habari njema za Ufalme wa Mungu. (1 Wakorintho 9:16; Matendo 20:26, 27) Mume na mke katika Ufaransa walihisi ile kani ya utume huo wa kufikia kila mmoja wakiwa na zile habari njema. Katika eneo lao palikuwa na hosteli moja ambayo ilikuwa makao ya wakimbizi wa kisiasa na wafanya kazi vijana wa nchi za kigeni. Mume na mke hao wanaeleza hivi: “Sisi tulishangaa tukijiuliza ni jinsi gani tungeweza kupata kuingia ndani tusipoalikwa ndani na mtu fulani ambaye alishi humo. Kwa hiyo sisi tukaamua kupashana habari na watu pale pale nje na labda ingewezekana kupata mwaliko wa kuwatembelea mle ndani. Mwanamume mmoja kijana alikubali magazeti kwa hamu nyingi na akaomba afanyiwe ziara.
“Sisi tulizuru mwanamume kijana huyo, na funzo lilianzwa mara hiyo. Kila wakati rafiki mmoja yake alikuwako, lakini rafiki huyo hakusema kamwe hata neno moja. Wakati, mwishoni mwa funzo la pili, sisi tulipouliza kama yeye pia angependa kujifunza mengi zaidi juu ya Neno la Mungu, yeye alijibu: ‘Sababu gani nisijifunze?’ Hivyo funzo la pili lilianzwa. Sisi tulialika wao kwenye mikutano kutoka pale mwanzoni, na wao hawajakosa hata mkutano mmoja tangu wakati huo. Maendeleo yao yalikuwa dhahiri sana, hasa kwenye hosteli ile, ambako wao walianza mara hiyo kuongea juu ya mambo ambayo walikuwa wakijifunza, na hiyo ikatokeza kuanzishwa kwa funzo la tatu pamoja na mume na mke fulani. Siku moja kikundi chote kile kilikuwa pale penye mwingilio, kikiwa tayari kuondoka kwa ajili ya mkutano, wakati rafiki mwingine alipoamua kuja pamoja nao pia. Msichana huyo alikuwa mwenye idili nyingi na alitaka rafiki-mvulana wake ajifunze kuhusu yote hayo. Wote wawili walianza kujifunza.
“Kufikia hapo mafunzo matano yalikuwa yakiongozwa. Kila moja lilikuwa kama mkutano! Kila mmoja alihudhuria funzo la kila mmoja mwingine, na wapya walijiunga ndani pia. Wao wote waliongea juu ya ukweli, na tokeo likawa kwamba, funzo la sita lilianzwa pamoja na mwanamume mwingine, ambaye yeye pia alianza kuhudhuria mikutano na kumtolea ushuhuda rafiki-msichana wake.
“Bila shaka, wote huo ulikuwa ushuhuda mzuri ajabu katika hosteli ile. Halikuwa jambo rahisi kwa vijana hao kuvaa ule utu mpya. Iliwalazimu kushinda kuvuta tumbako, uzoelevu wa matumizi ya vileo, jeuri, maadili malegevu, na ushirika mbaya. Shetani alihakikisha kwamba waliokuwa marafiki walijaribu kukwaza maendeleo yao, wakishawishi hao kuvuta sigareti au kufanya karamu za makelele-makelele. Mmoja wa wanaume wale wengine alikuwa amefanya uchumba na msichana mmoja ambaye alikuwa wa kidhehebu fulani. Msichana huyo alijaribu kumgeuzia mbali na ukweli. Hata hivyo, mwishowe msichana huyo alianza kujifunza na tangu wakati huo amefanya maendeleo mazuri.
“Kulingana na habari za karibuni zaidi,” wanaripoti mume na mke hao, “mmoja wa wanaume vijana wale alipelekwa gerezani kwa ajili ya msimamo wake juu ya kutokuwamo. Katika muda unaopungua mwaka mmoja, sita wengine walibatizwa, na watano kati yao wakaingia mara hiyo utumishi wa painia msaidizi. Katika kikundi chote kile, sasa sita ni mapainia wa kawaida, mradi wao ukiwa ni upainia wa pekee.”
Mume na mke hao walithawabishwa kama nini kwa udumifu wao katika kuufikiliza utume wao wa kimungu kutafuta wenye mfano wa kondoo! Kwa uhakika Yehova alibariki jitihada zao za uaminifu. Ingawa huenda sisi tusiwe na maono hayo ya kutokeza, sikuzote sisi tunataka kufikiliza utume wetu wa kimungu kwa uaminifu kuhubiri zile habari njema za UfaIme.—Mathayo 24:14.
[Picha katika ukurasa wa 21]
Mume na mke hao katika Ufaransa wakiwa pamoja na wale mapainia wa kawaida sita