Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 8/1 uku. 21
  • Habari Njema Kutoka Norowei

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Habari Njema Kutoka Norowei
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Kondoo wa Yesu Husikiliza Sauti Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • “Mwenye Furaha Ni Yule Mtu Ambaye Amepata Hekima”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • “Mungu Hana Upendeleo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Upendo Wafanya Jamaa Ziwe na Umoja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 8/1 uku. 21

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

Habari Njema Kutoka Norowei

MAMBO mengi mazuri yaonwa na wapiga mbiu ya Ufalme zaidi ya 9,500 wa habari njema katika Norowei. Wenye mioyo ya kufuata haki hutambua ujumbe wa Biblia ambao wapigwa mbiu na Mashahidi wa Yehova kuwa ndio ukweli na jibu kwa sala zao, kama ionyeshwavyo katika maono yafuatayo.

◻ Mume na mke vijana walisali kwa Mungu awasaidie kupata kusudi maishani. Juma moja baadaye Mashahidi wa Yehova waliwatembelea, na mke akawakaribisha waingie ndani. Mume alikuwa ameonywa dhidi ya Mashahidi, kwa hiyo akaenda nje ya nyumba akaoshe gari lake. Mke alizaliwa katika Lebanoni na alikuwa na tatizo la lugha, kwa hiyo Mashahidi wakamwonyesha jina la Yehova katika Biblia yake ya Kiarabu. Majuma mawili baadaye Mashahidi walirudi, na mume akaenda nje tena akaoshe gari lake. Mashahidi walimwuliza mke huyo alionaje kama mume wake angeweza kuwapo wakati ule mwingine wajapo ili yeye aweze kufasiri, naye akaahidi kumwuliza mume wake.

Katika ziara ya tatu, gari lilikuwa safi sana hivi kwamba mwanamume huyo hakuhisi angeweza kulitumia kama udhuru wa kuondoka, kwa hiyo alikaa akauliza maswali kadhaa ili aone tofauti kati ya Mashahidi na kanisa la Serikali. Ziara hiyo iliendelea kwa saa tatu, na mume na mke hao wakaachiwa broshua. Mashahidi walipoondoka, mke alienda kulala lakini mume akaanza kuisoma broshua, akifungua maandiko yote. Usiku katikati akamwamsha mke wake na kusema: “Ni lazima usome hiki.” Mke aliamka, nao wakasoma pamoja mpaka saa kumi na moja ya asubuhi. Kwa kung’amua kwamba walikuwa wameupata ukweli, walilia machozi ya shangwe na kusali kwa Yehova, wakitumia jina lake. Funzo la Biblia lenye ukawaida lilianzwa pamoja nao, nao wakaanza kuhudhuria mikutano. Mume aliacha kazi yake ya kijeshi, nao wakajiuzulu kanisani na kuacha kuvuta sigareti. Sasa wao wamebatizwa na wanatumikia Yehova kwa furaha pamoja na ndugu na dada zao wa kotekote ulimwenguni.

◻ Dada wawili wakiwa katika huduma yao ya nyumba kwa nyumba katika Norowei walikuta mwanamke aliyeonyesha kupendezwa. Aliwaalika warudi na kuwauliza kama angeweza kualika wanawake wengine. Katika ziara iliyofuata, wanawake wengine wanne walikuwapo. Mmoja wao alikuwa mtendaji sana kanisani. Alitaarifu kwamba tangu alipokuwa kijana, alikuwa ametaka kutii amri ya Yesu kufanya wanafunzi. Hiyo ilikuwa imemwongoza kwenda Afrika pamoja na mume wake katika mradi wa kusaidia nchi za kigeni. Wanawake wote walikuwa na maswali mengi, na ikapangwa kwamba dada hao wangewazuru kila majuma mawili. Majirani wapya walialikwa, na baadhi yao waliendelea kuja hali wengine waliacha kuhudhuria, lakini yule mshiriki mtendaji wa kanisa alithamini kwamba alikuwa akijifunza ukweli. Siku moja, mhudumu wa kanisa lake alipotaarifu kwamba yeye angeunga vita mkono na kwamba aliliamini fundisho la Utatu, mwanamke huyo alijiondoa kanisani. Alianza kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova na muda si muda akaanza kushiriki katika kazi ya kuhubiri. Muda mfupi baada ya yeye kubatizwa, na sasa, baada ya miaka 30, yeye bado hufurahia kuitii kikweli amri ya Yesu ya kufanya wanafunzi.—Mathayo 28:19.

Yehova anabariki akina ndugu katika Norowei katika utumishi mtakatifu wao na pia wale wanaosikiliza habari njema!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki