Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 4/1 uku. 31
  • Upendo Wafanya Jamaa Ziwe na Umoja

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Upendo Wafanya Jamaa Ziwe na Umoja
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hong Kong
  • Uingereza
  • Pasifiki ya Kusini
  • Mke Anayependwa Sana
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • “Mungu Hana Upendeleo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Nufaika na Mwongozo wa Yehova Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 4/1 uku. 31

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

Upendo Wafanya Jamaa Ziwe na Umoja

UMOJA wa jamaa unaweza kupatikana wakati tu ndoa inapokuwa juu ya msingi wa upendo unaoongozwa na ukosefu wa ubinafsi. Upendo huo hutoka kwa Yehova, Mungu wa upendo, kwa hiyo ni tunda la roho ya Mungu. (Wagalatia 5:22, 23; 1 Yohana 4:8) Maono yanayofuata yanatoa kielezi juu ya jinsi upendo ambao msingi wao ni maarifa ya Biblia umefanya jamaa zikawa na umoja.

Hong Kong

◻ Katika Hong Kong painia mmoja alianzisha funzo la nyumbani la Biblia pamoja na mke wa kinyumbani na binti zake wawili. Mume alitaja hangaiko lake la kwamba huenda mke wake akawa anahusika na kikundi cha kidini chenye kutaka mapinduzi. Painia huyo akadokezea mke huyo kwamba aalike mume wake kuketi katika funzo na kujiamulia mwenyewe, na ndivyo mume huyo alivyofanya. Kwa wakati huo, mke alianza kuhudhuria mikutano, lakini alikuwa na tatizo la kuzoeza watoto wake. Alikuwa akimgombeza-gombeza yule mkubwa na kumwendekeza yule mchanga. Kisha ikajulikana kwamba yeye na mume wake walikuwa na matatizo. Mara nyingi magomvi yao yalifoka yakawa jeuri, na mara kadhaa ikawa lazima polisi waitwe. Painia huyo alitumia Neno la Mungu lenye nguvu nyingi kuwafundisha jinsi ya kudhihirisha upendo wa kimungu katika ndoa yao. Karibuni njia na tabia zao za zamani zikaanza kubadilika. Wote wawili wakawa wahudhuriaji wa kawaida wa mikutano, na hali yenye furaha zaidi ikawa nyumbani. Mume aliacha kuvuta sigareti na sasa amejiunga na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Sasa mke ni mhubiri aliyebatizwa.

Umoja wa jamaa ulipatikana kwa kuonyesha upendo, tunda la roho ya Mungu.

Uingereza

◻ Ono moja kutoka Uingereza linatoa kielezi juu ya jinsi Yehova hubariki mume anayeonyesha upendo, saburi, na uvumilivu katika kushughulika na mke wake. Mume alipokuwa akiingia katika ukweli miaka 12 iliyopita, upinzani mchungu wa mke wake ulimwongoza mke huyo kupata talaka ya kisheria. Hata hivyo, mume aliendelea kumwonyesha fadhili, akihakikisha kumtunza kifedha, kumfanyia kazi ndogo-ndogo kwa ukawaida. Baada ya miaka minne na ijapokuwa alikuwa amepingwa na mke huyo hapo kwanza, mume akaamua kumtajia ukweli tena. Alipodokeza kwamba dada mmoja ajifunze Biblia pamoja naye, mke huyo alikubali, mume akashangaa sana. Hatimaye alichukua msimamo wake upande wa ukweli na kubatizwa. Mume alikuwa hajapoteza kamwe upendo wake kwake, na alipothibitisha kwamba alikuwa ameufanya ukweli uwe wake mwenyewe, alimwomba aolewe naye tena. Mke alisisimuka, kwa kuwa hakutarajia kamwe kwamba mume angefanya hivyo kwa sababu yeye mke alikuwa na mwelekeo mbaya hapo kwanza. Sasa wamekuwa katika hali ya kufunga ndoa upya kwa karibu miaka minane, na wote wawili wafanya maendeleo katika ukweli.

Pasifiki ya Kusini

◻ Zaidi ya miaka 20 iliyopita, mwanamume kijana katika kisiwa kimoja cha Tuvalu katika Pasifiki ya Kusini aliandikia Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi akiomba fasihi. Wakati huo hakukuwa na Mashahidi katika kisiwa hicho. Hata hivyo, yeye alisoma fasihi hizo mwenyewe na kuzitambua kuwa ndio ukweli. Ingawa hivyo, mke wake alipinga vikali imani yake mpya, kwa hiyo mwanamume huyo akaiacha.

Hivi majuzi, wakati fasihi zilipopatikana katika lugha ya Kituvalu, mke huyo alipata kuwa na baadhi ya vichapo na akaweza kujisomea mwenyewe. Sasa aliutambua ukweli na kumlalamikia mume wake hivi: “Miaka yote hii wewe umekuwa na nuru, lakini hukuiinua juu sana. Mbona angalau hukunieleza ni kwa sababu gani uliitikadi kwamba Mashahidi ndio walio sawa?” Sasa wakiwa wameungamana katika ukweli wa Biblia, wenzi hawa wa ndoa walianza kushiriki pamoja na Mashahidi.

Wakati binti zao wawili, waliokuwa wakienda shuleni katika Fiji, waliporudi nyumbani, wazazi waliwaarifu juu ya uamuzi wao kuwa Mashahidi wa Yehova. Wakawatia moyo wasichana hao wajiunge nao katika funzo la Biblia, lakini wakashangaa kupata kwamba tayari wasichana hao walikuwa wakihudhuria mikutano katika Fiji. Jamaa hiyo iliukubali ukweli kwa furaha ikiwa pamoja, na baba, mama, na mmoja wa binti hao wamekuwa wahubiri wa Ufalme.

Ni shangwe kama nini kuona jinsi ukweli wa Biblia na upendo unavyoziungamanisha jamaa kote kote ulimwenguni.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki