Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 10/1 uku. 31
  • “Mwenye Furaha Ni Yule Mtu Ambaye Amepata Hekima”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mwenye Furaha Ni Yule Mtu Ambaye Amepata Hekima”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jemadari Aliyestaafu Ajifunza Kweli
  • Kutoka Mshuko wa Moyo Hadi Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • “Mungu Hana Upendeleo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Mwishowe Mbegu Ilichipuka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kondoo wa Yesu Husikiliza Sauti Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 10/1 uku. 31

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

“Mwenye Furaha Ni Yule Mtu Ambaye Amepata Hekima”

MITHALI hiyo imethibitika kuwa kweli katika Korea, ambako sasa kuna Mashahidi wa Yehova wenye furaha zaidi ya 71,000. (Mithali 3:13, NW) Na ebu wazia, asilimia 42 ya wahudumu hao wamo katika utumishi wa wakati wote! Maono yafuatayo yataonyesha kwamba furaha ndiyo fungu la wale wanaotafuta hekima ya kweli.

Mwanamke mmoja katika Pusan alikuwa amehudhuria mojawapo makanisa ya Jumuiya ya Wakristo kwa miaka 16. Alikuwa ameona mazoea mengi yasiyo ya kimaandiko hivi kwamba alianza kufikiri kwamba Mungu asingeweza kuwako. Kwa upande ule mwingine, hangeweza kukanusha kuwako kwa Mungu, kwa hiyo alimwomba Mungu kwa moyo mweupe kwamba aweze kupata kanisa la kweli kama kuna jambo kama hilo. Ndipo kwa ghafula akawafikiria Mashahidi wa Yehova, akakumbuka kwamba kanisa lake lilikuwa limewadharau na kuwaonya wahudhuria-kanisa dhidi yao kwa sababu Mashahidi hawakutia imani katika Utatu, moto wa helo, na mafundisho mengine ya Jumuiya ya Wakristo. Labda wao ndio waliokuwa kanisa la kweli? Kwa msaada wa jirani, alipata mahali pa Jumba la Ufalme. Siku iliyofuata tu, alihudhuria mkutano.

Alistaajabu juu ya utaratibu wa mkutano. Hakukuwa kupaaza sauti kwa ushupavu au kuimba kwa kihisiamoyo kama ilivyokuwa katika kanisa lake. Alijulishwa kwa Shahidi mmoja aliyekuwa tayari kujifunza Biblia naye, na funzo la kwanza lilidumu muda wa saa kadhaa kwa sababu ya maswali yake mengi. Kwenye funzo la pili, alijulisha kwamba angejiuzulu kutoka katika kanisa lake na kuwa Shahidi. Alimwambia yule dada kwamba hangehitaji kujifunza naye tena, kwani angeweza tu kuihudhuria mikutano. Hata hivyo, alionyeshwa thamani ya kuwa na funzo la Biblia la kibinafsi pamoja na kuhudhuria mikutano. Alikubali dokezo hilo, akajitahidi katika mafunzo yake, akabatizwa hatimaye.

Sasa yeye amefurahi sana kwamba amepata hekima ya Mungu wa kweli, Yehova, na ana tumaini la kuishi milele katika ulimwengu mpya wa Mungu.

Jemadari Aliyestaafu Ajifunza Kweli

Mke wa jemadari mmoja wa jeshi alibatizwa katika 1962. Mume wake alimpinga mwanzoni, lakini baadaye aliacha kumpinga, na kwa miaka 28 iliyofuata, ndugu mbalimbali walijifunza naye pindi kwa pindi, wakijaribu kumpendeza na kweli. Alihudhuria mikutano na mikusanyiko kadhaa, lakini alikuwa mmoja wa wale waliosita kuichukua kweli kwa uzito. Katika 1990 yeye na mke wake walienda Japani, walikohudhuria mkusanyiko mmoja wa wilaya. Kwenye pindi hiyo alisikiliza hotuba kwa makini—jambo ambalo hakuwa amefanya kabla ya hapo. Alishtushwa na zile hotuba zenye ujasiri zilizofunua dini bandia, lakini kwa hakika hizo zilifungua macho yake yaone unafiki wa Jumuiya ya Wakristo. Alivutiwa na utaratibu na furaha ya watu wa Mungu katika Japani, uliokuwa sawa na ule aliokuwa ameona katika Korea. Aliporudi Korea, alianza funzo la Biblia lenye uzito akabatizwa hatimaye.

Kwa hiyo baada ya ubatizo wake angepaswa kufanya nini? Alijiuzulu cheo chake akiwa msimamizi wa hoteli moja maarufu ya watalii akajiunga na mke wake katika huduma ya painia ya wakati wote. Yeye ahisi kwamba kuwa painia wa kawaida ndiyo njia bora zaidi kulipia ile miaka 28 aliyopoteza alipokuwa akisita kuchukua hatua.

Sasa ang’amua kwamba ile mithali “mwenye furaha ni yule mtu ambaye amepata hekima” yamhusu yeye pia!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki