Mwishowe Mbegu Ilichipuka
KARIBU na Tokyo, Japan, zilipatikana mbegu tatu za yungiyungi ambazo wataalamu walionyesha zilikuwa zimefunikizwa katika mtumbwi chini ya ziwa la mimea iliyooza kwa miaka 2,000. Mtaalamu wa mimea ya yungiyungi alizitayarisha mbegu hizi na kuziweka majina. Mbili kati ya zile mbegu za kale zilichipuka nazo zikasitawi kuwa maua yaliyochanua kabisa na ya kupendeza ya yungiyungi. Zijapokuwa zilikuwa zimekuwa zilizokufa kwa karibu miaka 2,000 zikiwa katika hali za kufaa, mbegu zile zingali ziliweza kuchipuka na kusitawi.—The Plants, ukurasa wa 94.
Katika mfano wake wa namna mbalimbali za udongo, Yesu alizungumza juu ya namna nyingine ya mbegu, akisema: “Mbegu ni neno la Mungu.” (Luka 8:11) Namna hii ya mbegu yaweza vile vile kukaa imekufa kwa muda fulani na mwishowe kuchipuka hali zinapokuwa zifaazo. Hii yaonyeshwa vizuri katika maono ya majuzi katika sehemu ya kusini ya United States. Ni juu ya kijana mwanamke aliyekutana na kweli ya Neno la Mungu kwa mara ya kwanza miaka fulani.
Alipokuwa mwenye umri wa miaka kumi na mitatu kijana huyu wa kike alikuwa amependezwa sana na siasa. Siku moja kijana huyu wa kike alimwuliza mjakazi wa jamaa yeye angechagua nani katika uchaguzi. Kwa kuwa alikuwa mmoja wa mashahidi wa Yehova, mjakazi huyu alimwambia kijana yule wa kike kwamba yeye hachagui katika uchaguzi wa kisiasa kwa sababu ya isemavyo Biblia juu ya hali ya Wakristo ulimwenguni. (Yohana 17:16) Kijana wa kike hakuwa amesikia kitu kama hicho hapo kwanza. Kwa hiyo siku na majuma yaliyofuata, akawa anamfuata-fuata mjakazi yule nyumbani pote akiuliza maulizo mengi juu ya Biblia. Hata hivyo, wazazi wa kijana yule wa kike walilikataa jambo hili nao wakamfukuza mjakazi yule. Lakini mbegu za kweli zilikuwa zimekwisha pandwa.
Hakukuwako kundi lo lote la mashahidi wa Yehova katika mji ambamo jamaa iliishi, na kwa hiyo miaka mitano iliyofuata mbegu hivi za kweli zilikaa zimekufa. Hata hivyo kijana huyu wa kike alijiwekea nadhiri kwamba wakati ukifika wa kuondoka kwake nyumbani na kwenda kwenye chuo kikuu, angekutana tena na mashahidi wa Yehova. Anasema hivi: “Mimi sikuweza kuyaondoa mambo niliyojifunza kwa mjakazi akilini mwangu.”
Wakati ambapo mwishowe aliondoka akahudhurie chuo kikuu, aliona nakala ya The Watchtower yenye makala “Ni Kipi Kinachotangulia—Kanisa Lako au Mungu Wako?” Hii ilimsukuma ayaandikie makao makuu ya Watchtower Society. Mmojawapo wa mashahidi wa Yehova karibuni akaelekezwa kwake. Upesi akaanza kuhudhuria mikutano yao ya Kikristo. Aliyashiriki mambo aliyokuwa akijifunza pamoja na mwenzake aliyekaa naye chumba kimoja naye vile vile akaanza kuihudhuria mikutano. Wote wawili waliendelea vizuri katika funzo lao la Neno la Mungu.
Wakati wa likizo yake ya wakati wa hari kijana huyu wa kike alirudia nyumbani. Akayashiriki mambo mengine aliyokuwa akijifunza kutoka kwa Biblia na wazazi wake. Wazazi wake waliudhika sana na hata hawakutaka aandikiane barua na Mashahidi. Ajapokuwa aliwapenda na kuwaheshimu wazazi wake, alijua kwamba haikumpasa kuzing’oa mbegu za kweli ya Biblia ambazo zilikuwa zimekwisha pandwa moyoni mwake na ambazo zilikuwa zikikua sasa. Hivyo aliporudia shuleni wakati wa mvua alishirikiana tena na mashahidi wa Kikristo naye akaendelea kushiriki pamoja na mwenzake aliyekaa naye chumba kimoja na vijana wengine wa kike katika jumba la kulala mambo aliyokuwa akijifunza. Vile vile kijana huyu wa kike alianza kufanya mageuzi katika utendaji wake, kwa maana yeye alikuwa mkuu wa tengenezo la wanawake la Kibaptist, mwalimu wa “Sunday School,” mkuu wa jumba lake la kulala na afisa katika maongozi ya wanafunzi penye chuo kikuu. Aliona kutokana na Biblia kwamba ilimpasa kuchukua hatua za kukomesha kuwamo kwake katika utendaji huo, naye alifanya hivyo.
Vile vile, alifahamu alipaswa kufanya mageuzi mengine; alipaswa kuukomesha ushirika wake katika lililokuwa kanisa lake. Kiongozi wa kanisa la mahali pake ambaye kijana huyu alizungumza naye alisema yeye aliamini kwamba habari za Mwanzo za uumbaji na sehemu nyingine za Biblia zisingeweza kuchukuliwa kwa njia halisi. Zaidi ya hayo, yeye (kiongozi wa dini) alikubali kwamba mambo mengi yaliyofundishwa makanisani yalikuwa na chanzo cha kipagani. Alipokwisha kujitahidi mara kwa mara, kijana yule wa kike mwishowe aliondolewa kanisani.
Kwa kuzidi kufanya maendeleo katika funzo lake na matumizi ya Neno la Mungu, alibatizwa kama shahidi wa Kikristo wa Yehova. Alipokuwa nyumbani tena katika likizo aliwaambia wazazi wake kwamba alikuwa mwenye furaha kuwa pamoja na jamaa lakini kwamba dhamiri yake isingeweza kumruhusu ashiriki katika utendaji wao wa kidini kanisani. Wazazi wake wakamweleza wazi kwamba ilikuwa lazima achague kati ya dini yake na wao (wazazi wake). Je! kweli ilikuwa imetia mizizi moyoni mwake hata aweze kuvumilia?
Alipangwa awe na sehemu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika kundi la mashahidi wa Yehova alikuwa ametoka katika mji wa chuo kikuu. Mama yake alionyesha kwamba binti yake akienda kutoa hotuba hiyo, asingeweza kuchukua cho chote ila mavazi aliyokuwa ameyavaa. Alipokwisha kufika katika mji wa chuo kikuu na kufanya sehemu yake kundini, aliwapigia wazazi wake simu kuwajulisha aliwasili salama. Mama yake akamwambia asijisumbue kuja nyumbani.
Mkristo yule anaendelea kufanya maendeleo anapomtumikia Yehova Mungu kwa kawaida. Katika kusanyiko la majuzi la mashahidi wa Yehova alikutana na Shahidi aliyekuwa amekuwa mjakazi wa jamaa miaka saba mapema. Ulikuwa wakati wa kusisimua kwa wote wawili, lakini zaidi kwa Shahidi ambaye hapo kwanza alikuwa amezipanda mbegu za kweli. Alimwambia kijana yule wa kike: “Mimi niliona tangu mwanzoni kwamba wewe ungesimama upande wa Yehova, kwa maana ulionyesha upendo kwa Neno la Mungu upesi.”