Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 10/1 kur. 451-453
  • Jina la Mungu Lina Muhimu Gani Kwako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jina la Mungu Lina Muhimu Gani Kwako?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MUHIMU ULIOKUWA NA JINA LA MUNGU KWA YESU
  • JE! KWELI KUFUNDISHA KWAKO KUNALIHESHIMU JINA LA MUNGU?
  • KULIWEKA JINA LA MUNGU KUWA TAKATIFU KWA HABARI YA KAZI
  • KULIPENDA JINA LA MUNGU KWA KUHUDUMIA WENGINE
  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Jina la Mungu na Lako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Jina la Mungu
    Amkeni!—2017
  • Jina Lililo Kuu Kupita Majina Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 10/1 kur. 451-453

Jina la Mungu Lina Muhimu Gani Kwako?

KWA kuhubiri kwa mashahidi wa Yehova, mamilioni ya watu wamekuja kulijua jina la Mungu, Yehova. Pengine hata wewe umelisoma jina hili katika Biblia yako, kama vile katika Zaburi 83:18.

Mungu analiheshimu jina lake sana. Hii yaonyeshwa kwa namna ambavyo linapatikana mara nyingi katika Neno lake, Biblia. “Yehova” lapatikana mara 6,973 katika “Agano la Kale” peke yake au sehemu ya Maandiko ya Kiebrania ya New World Translation of the Holy Scriptures. Waweza kulipata mara 237 katika “Agano Jipya” au Maandiko ya Kigiriki ya tafsiri hiyo. Hiyo ni jumla ya mara 7,210!

MUHIMU ULIOKUWA NA JINA LA MUNGU KWA YESU

“Jina” la Mungu ni muhimu kwa Yesu Kristo vile vile. Muda mfupi tu mbele ya kifo chake yeye alisali hivi: “Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu . . . kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa . . . Nami naliwajulisha jina lake, tena nitawajulisha hilo.”​—Yohana 17:6, 11, 26.

Haitupasa kudhani kwamba Yesu aliposema, ‘‘Naliwajulisha jina lako” au “nimewadhihirishia,” alimaanisha matamshi tu ya jina la kimungu. Wasikilizaji wake walikuwa Wayahudi ambao, kulingana na habari hawakujua matamshi ya zile herufi nne za Kiebrania zilizofanyiza jina lake, isipokuwa kuhani mkuu. Kwa hiyo basi, Yesu ‘alijulishaje jina la Mungu kwa mitume zaidi ya kulitamka jina sawasawa? Angalia jibu lililotolewa na mfafanuzi mmoja wa Biblia:

“Neno jina [katika Yohana 17] latia ndani na sifa, au wema wa Mungu. Yesu alikuwa amejulisha wema wake, sheria yake, mapenzi yake, mpango wake wa rehema. Au kwa njia nyingine, alikuwa amewafunulia Mungu alivyo. Neno jina mara nyingi latumiwa kumaanisha mtu mwenyewe.”​—Notes, Explanatory and Practical, on the Gospels kilichoandikwa na Albert Barnes (1846).

Kwa hiyo, kwa maana Yesu ‘alimsimulia Baba’ kwa mwendo wake wote wa maisha ulio mkamilifu duniani, kwa kweli alikuwa ‘akilijulisha jina la Mungu.’ Yeye alionyesha kwamba alizungumza kwa msaada kamili wa Mungu na mamlaka. Kwa hiyo Yesu angeweza kusema: “Aliyeniona mimi amemwona Baba.” “Jina” la Mungu kwa njia hiyo lilipata muhimu zaidi kwa wafuasi wake wa kwanza. Kwa hiyo, kuona ubora wake na Mtu liliyesimamia vyapaswa vionyeshwe katika kila upande wa maisha ya Mkristo,​—Yohana 14:9; 1:18; 5:19, 30; Mt. 11:27.

JE! KWELI KUFUNDISHA KWAKO KUNALIHESHIMU JINA LA MUNGU?

Kwa mfano, mtume wa Kikristo Paulo anaonyesha kwamba upendo mwingi sana kwa Yehova mwenyewe, Mtu anayewakilishwa na jina la kimungu, ungevuta Mkristo ‘kumpa Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake.​—Ebr. 13:15.

Je! wewe waitangaza imani yako waziwazi katika jina la Mungu? Paulo anataja “tunda la midomo,” lakini kwa wazi anamaanisha mengi zaidi kuliko kutangaza tu kwa kijuujuu. “Dhabihu ya sifa” itokayo kinywani mwa mtu lazima iwe ya moyoni, ya kweli. Kwa hiyo, kuliweka jina la Mungu kuwa takatifu kwa kuhubiri na kufundisha kwatia ndani mengi zaidi kuliko maneno tu yanayosikika yenye kuvuta. Angalia namna ambavyo hili linavyoonyeshwa katika Warumi 2:21-24:

“Basi wewe umfundishaye mwingine, je! hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe? Wewe usemaye kwamba mtu asizini, wazini mwenyewe? Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu? Wewe ujisifuye katika torati, wamvunjia Mungu heshima kwa kuiasi torati? Kwa maana jina la Mungu latukanwa katika Mataifa kwa ajili yenu,”

Kufundisha katika jina la Mungu kwamhitaji mwalimu aishi maisha yanayopatana na ‘ungamo’ lake la waziwazi. Tuseme baba anamfundisha mwanawe “Usiibe.” Lakini, basi, namna gani iwapo baba mwenyewe anatenda tofauti yake, asilipe kodi za mapato au kumwibia jirani yake? Kufundisha kwa kinywa kwa mwanamume yule hakuelekei kwamba kutamsadikisha mtoto wake. La muhimu zaidi, mwanamume yule anatoa sababu ya ‘kutukanwa’ kwa “jina la Mungu.” Kwa hiyo, upendo wa kweli kwa jina la Mungu na vile vile kufundisha kwenye matokeo vyaamrisha kwamba Mkristo ‘afanyo yale anayoyahubiri. Je! wewe unafanya hivyo?

KULIWEKA JINA LA MUNGU KUWA TAKATIFU KWA HABARI YA KAZI

Zaidi ya hayo, je! ulijua kwamba matendo yako kazini pako yanaliletea jina la Mungu sifa fulani? Paulo anaonyesha hili katika 1 Timotheo 6:1:

“Wo wote walio chini ya kongwa, hali ya utumwa, na wawahesabie bwana zao kuwa wamestahili heshima yote, jina la Mungu lisitukanwe wala mafundisho yetu.”

Katika karne ya kwanza watumwa wa Kikristo walipaswa kumpa bwana ye yote “heshima kamili” au “heshima iliyo kuu zaidi.” (An American Translation) Kufanya vingine kungemaanisha kwamba kweli ya Mungu haikuwa imefanya mageuzi yo yote katika mtumwa. Kufundisha kwa Kikristo kungeweza kuelekea kuwa kusiko na uwezo wa kugeuza maisha. Jina la Mungu, ndiyo, Mungu mwenyewe, ‘angetukanwa.​—Linganisha 1 Petro 2:18.

Watu wachache leo wanaishi utumwani hasa. Lakini kanuni zinazoongoza tajiri na mfanya kazi ni sawa na zile za mtumwa na bwana. Kama Mkristo, je! tabia zako za kazi zinaleta sababu kwa ye yote ‘kulitukana jina la Mungu’? Kwa mfano, je! mara kwa mara wewe unafika kazini umechelewa? Je! wewe unampa tajiri wako “heshima kamili,” hata usipokuwa karibu naye? Je! unafanya hivi ajapokuwa aweza kuwa ni tajiri mwenye kudai sana? Iwapo tajiri wako ni “mwamini,” Mkristo mwenzako, je! unakosa kufanya mengi sana ati kwa sababu yeye ni mwenye fadhili? Iwapo jina la Yehova ni takatifu kwako kweli kweli, hata na ujamaa wako wa biashara utaonyesha hivyo.

KULIPENDA JINA LA MUNGU KWA KUHUDUMIA WENGINE

Vile vile mtu anaonyesha upendo kwa jina la Mungu kwa namna anavyoshughulika na Wakristo wenzake. Angalia hili katika Waebrania 6:10: “Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu.”

Paulo alipoyaandika maneno hayo, “kazi” njema bila shaka zilitia ndani na kutoa msaada wa mambo ya kimwili kwa Wakristo wenzao waliokuwa na uhitaji au waliokuwa wakiteswa. (Ebr. 10:32-34) Je! wewe unazoea ukarimu wa Kikristo?

Kutokana na tuliyoyazungumza ni wazi kwamba ulizo, “Jina la Mungu lina muhimu gani kwako,” latia ndani mengi zaidi kuliko kujua namna ya kutamka tu jina la kipekee la Mungu. Lamsimamia Mungu mwenyewe. Kwa hiyo, sifa zake zipendezazo zapaswa kuonekana wazi katika matendo yote ya Mkristo.

Je! wewe ni mtu ambaye hajajifahamisha na Yehova bado? Mashahidi Wake watafurahia kukufundisha juu yake. Waweza kuonana nao kwa kuwaandikia wachapaji wa gazeti hili. Jifunze namna ambavyo maisha yake yanavyoweza kuwa sifa kweli kweli kwa ‘jina la Mungu.’

[Picha katika ukurasa wa 452]

Ikiwa baba anatumia Biblia kumfundisha mwanawe asiibe lakini yeye mwenyewe anadanganya juu ya kodi, mwanamume huyo analeta suto juu ya jina la Mungu

Mkristo afikaye kazini amechelewa mara kwa mara huenda akafanya jina la Mungu ‘litukanwe’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki