Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 9/1 uku. 15
  • Kutoka Mshuko wa Moyo Hadi Furaha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoka Mshuko wa Moyo Hadi Furaha
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Kutatua Matatizo ya Vijana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Mwishowe Mbegu Ilichipuka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • “Mwenye Furaha Ni Yule Mtu Ambaye Amepata Hekima”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Anawafariji Wengine Licha ya Matatizo Yake ya Afya
    Masimulizi ya Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 9/1 uku. 15

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

Kutoka Mshuko wa Moyo Hadi Furaha

YEHOVA ni Mungu mwenye furaha. (1 Timotheo 1:11) Ataka wale wanaomtumikia wawe na furaha pia. Kwa sababu hiyo, ikiwa mmoja wa watumishi wake ameshuka moyo, Yehova atamsaidia avumilie maumivu na nyakati fulani hata apate tena roho yenye furaha. Ono lifuatalo la kutoka Uruguay ni kielezi cha jambo hilo.

Dada mmoja alikuwa akingoja katika kliniki katika Montevideo ili apate matokeo ya uchunguzi wa Eksirei. Bibi mmoja mwenye kuketi karibu naye aliogopa sana juu ya jambo awezalo kuambiwa na daktari kutokana na uchunguzi aliokuwa amefanyiwa. Dada huyo akamwambia kwamba tangu awe Shahidi kwa ajili ya Yehova, alikuwa hajaogopa jambo lolote. Hata hivyo, bibi huyo alisema kwamba hakuwapenda Mashahidi kwa sababu walitarajia kiwango cha juu mno kutoka kwa watu.

Ndipo dada alipomwambia bibi huyo jinsi maarifa juu ya ukweli wa Biblia yalivyokuwa yamemsaidia. Alikuwa amepoteza binti yake wa miaka 18 katika kifo na kuingia katika hali ya kina kirefu ya mshuko wa moyo kwa miaka minane. Matabibu wa akili wala dawa za gharama kubwa hazikumsaidia kushinda huo mshuko wa moyo. Bibi huyo alisema alilazwa hospitali mara kadhaa, lakini hakukuwa na nafuu yoyote. Watu wa nyumba yake walitunzwa na watumishi kwa sababu yeye mwenyewe hakuweza kutunza chochote. Alijaribu kujiua kwa sababu alikuwa amepoteza upendezi katika maisha. Hakuna lolote lililoonekana likisaidia.

Halafu, dada akamwambia bibi huyo kwamba, siku moja Mashahidi wa Yehova walimtembelea wakamwachia fasihi fulani za Biblia. Hiyo iliwasha cheche ya upendezi wake katika Neno la Mungu, naye akaanza kuisoma Biblia yote. Jambo fulani lilianza kubadilika ndani yake. Alianza kuamka asubuhi na kuonyesha upendezi katika watu wa nyumba yake. Mwishowe akaamua kutunza nyumba yeye mwenyewe na kukuta kwamba angeweza kufanya hivyo. Ilikuwa kana kwamba hakupata kamwe kuwa mgonjwa! Hiyo ilimfanya ahisi kuwa mwenye furaha sana.

Hakurudi kwa yule tabibu wa akili. Nia yake ya kuishi ilichochewa na maarifa yake juu ya Neno la Mungu, na hiyo ikathibitika kuwa ndiyo dawa iliyo bora kabisa. Aliwatafuta Mashahidi wa Yehova, nao wakaanzisha naye funzo la ukawaida. Pia alianza kuhudhuria mikutano, na upesi sana akabatizwa. Kwa kutosumbuliwa tena na mshuko wa moyo, sasa yeye hupata shangwe katika kumtumikia Yehova.

Bibi aliyekuwa katika chumba cha ungojezi alisikiliza kwa uangalifu. Halafu akamwambia dada hivi: “Kwa muda fulani, nimekuwa nikionana-onana na Mashahidi wa Yehova; lakini ikiwa kwa kweli nitakuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova wakati fulani ujao, itakuwa ni kwa sababu ya yale ambayo umeniambia sasa hivi. Kukusikiliza wewe ni kama kuanza kuona nuru katika mahali penye giza.”

Watu wengi kotekote ulimwenguni wanaona ubatili wa kujaribu kutatua matatizo ya maisha kwa kujitegemea wenyewe, na wanamgeukia Yehova Mungu. Wao ni wenye furaha kama nini kujifunza juu ya ulimwengu mpya wa Mungu unaokuja ambapo kila mmoja atakuwa mwenye furaha, na mshuko wa moyo utakuwa jambo la zamani!—Mithali 16:20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki