Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 7/15 kur. 7-8
  • “Kristo, Mwana wa Mungu Aliye Hai”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kristo, Mwana wa Mungu Aliye Hai”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Alikubali Yesu —Je! Wewe Unamkubali?
  • Je, Kweli Yesu Alikuwa Mwana wa Mungu?
    Amkeni!—2006
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mtu wa Kwanza Kutiwa Mafuta Kwa Roho Takatifu na Nguvu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 7/15 kur. 7-8

“Kristo, Mwana wa Mungu Aliye Hai”

BAADA ya wanafunzi wake Yesu kuripoti watu wanasema yeye ni nani, Yesu aliuliza: “Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”​—Mathayo 16:15, 16.

Je! Petro alifikia mkataa huu akiwa peke yake? Hata kidogo! Angalia ni nani pia Walioufikia, na uone msingi wao wa kutambua hivyo.

WATEGEMEZAJI WA MAPEMA: Yohana Mbatizaji, wanafunzi Nathanaeli na Martha, na Saulo wa Tarso, miongoni mwa wengine wengi, wote walimwita Yesu Mwana wa Mungu. (Mathayo 14:33; Yohana 1:33, 34, 49; 11:27; Matendo 9:20) Usadikisho wao uliimarishwa walipoona jinsi manabii yaliyoandikwa ili kutambua Mesiya aliyeahidiwa yalivyotimizwa katika Yesu.

WAPINZANI WA MAPEMA: Wayahudi waliotaka kumwua Yesu walirejeza kwake kuwa Mwana wa Mungu, sawa na walivyofanya askari waliokuwapo alipouawa. (Mathayo 27:54; Yohana 19:7) Ijapokuwa jambo hilo kwa lazima halionyeshi itikadi kwa upande wa wapinzani hao, angalau linaonyesha kwamba walifahamiana na yale ambayo wengine walikuwa wakidai juu ya Yesu, matukio yapitayo uwezo wa kibinadamu yaliyozunguka kuuawa kwake kwa wazi yalisababisha wengine wao kufikiria tena swali la utambulishi wake.

MALAIKA: Wakati wa kutangaza uzawa wa Yesu, malaika Gabrieli alimwita Mwana wa Mungu. (Luka 1:32, 35) Hata watu waliopagawa na mashetani wakiwa chini ya uvutano wa malaika waovu walipaaza sauti: “Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu?” (Mathayo 8:28-32) Kwa sababu ya kuwapo kwa Yesu mbinguni kabla ya kuwa mwanadamu, ni wazi kwamba malaika wabaya na wazuri wote wangejua yeye alikuwa nani.

YESU MWENYEWE: Yesu hakujisifu kamwe kuwa Mwana wa Mungu kwa kujaribu kupata upendeleo wa wengine au kujifurahia sifa ambayo uhusiano huo ulitoa. Kinyume na hilo, katika visa vingi yeye alirejezea kwa unyenyekevu kuwa “Mwana wa mtu.” (Mathayo 12:40; Luka 9:58, NW) Lakini katika pindi mbali mbali yeye alikiri kuwa Mwana wa Mungu.​—Yohana 5:24, 25; 10:36; 11:4.

YEHOVA MUNGU: Ni nani ambaye angeweza kutambua Yesu Kristo kwa uwezo mkubwa kuliko Yehova Mungu mwenyewe? Mara mbili Yehova alishuhudia kutoka mbinguni. “Huyu ndiye Mwanangu, mpendwa, ambaye mimi nimekubali.”​—Mathayo 3:17; 17:5, NW.

Mungu Alikubali Yesu —Je! Wewe Unamkubali?

Katika karne ya kwanza, maelfu ya watu walimkubali Yesu kama alivyokuwa: Mesiya aliyeahidiwa, au Kristo, aliyepelekwa duniani ili kutetea enzi kuu ya Yehova na kutoa uhai wake uwe dhabihu kwa aina ya wanadamu. (Mathayo 20:28; Luka 2:25-32; Yohana 17:25 26; 18:37) Wakati wa upinzani mkali, watu hawangechochewa kamwe kuwa wafuasi wa Yesu ikiwa walikuwa hawana uhakika wa utambulishi wake. Kwa bidii na kwa ushujaa walikubali kazi aliyowapa, “kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.”​—Mathayo 28:19, NW.

Leo, mamilioni ya wanafunzi Wakristo wanajua kwamba Yesu si mtu wa hadithi tu. Wao wanamkubali yeye kuwa Mfalme aliyemilikishwa katika Ufalme wa Mungu uliosimamishwa, ambaye sasa anachukua uongozi wa dunia na shughuli zayo hatua kwa hatua. Ufalme huo wa kimungu unaokuja ni habari zenye kukaribishwa kwa sababu unaahidi kitulizo kutoka kwa matatizo ya ulimwengu. Wakristo hao wa kweli wanaonyesha utegemezo wao wa moyo wote kwa Mtawala mchaguliwa wa Mungu kwa kuwatangazia wengine “habari njema hizi za ufalme.”​—Mathayo 24:14, NW.

Wale wanaotegemeza mpango wa Ufalme kupitia “Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai” watafurahia baraka za milele. Baraka hizi zinaweza kuwa zako pia!

[Blabu katika ukurasa wa 8]

Mamilioni ambao wakati mmoja hawakuwa na uhakika wa utambulishi wa Yesu sasa wameungana kwa kumtegemeza yeye akiwa Mtawala wa Ufalme wa Mungu

[Picha katika ukurasa wa 7]

Petro alimtambulisha Yesu kuwa “Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”Ndivyo wanavyofanya mashahidi wa Yehova zaidi ya 3,000,000 leo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki