Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 8/1 kur. 23-26
  • ‘Kamba Zimeniangukia Mahali Pema’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kamba Zimeniangukia Mahali Pema’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Malezi ya Kiroho
  • Taharuki Wakati wa Marufuku
  • Jinsi Mimi Nilivyopata Kuwa Mfungwa-Gereza
  • Uhuru—Lakini Mapigano Zaidi
  • Maisha Katika Bara Jipya
  • Pamoja na Mwenzi wa Ndoa
  • “Mahali Pema”
  • Maamuzi Mazuri Yalileta Baraka za Kudumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Yehova Ni Ngome na Nguvu Yangu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • ‘Fadhili-Upendo Zako ni Njema Kuliko Uhai’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Yehova Alinifundisha Kufanya Mapenzi Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 8/1 kur. 23-26

‘Kamba Zimeniangukia Mahali Pema’

Kama ilivyosimuliwa na D. H. MacLean

MIMI nikaketi hapo, saa nenda saa rudi, huku mmoja wa Kikosi cha Polisi-Farasi wa Kanada akiwa kando yangu. Mimi nilikuwa mfungwa-gereza wake. Sisi tulikuwa tukielekea kwenye kambi ya gereza kule Mto Chalk, Ontario, Kanada, na ilionekana kama kwamba ile safari ya kilometa 2,400 kwa gari-moshi haingemalizika kamwe.

Ilikuwa katika 1944, na Vita ya Ulimwengu 2 ilikuwa kwenye upeo. Lakini kwa nini nilikuwa hapa nikielekea gerezani? Basi, ilikuwa sana-sana ni kwa sababu ya mambo ambayo Baba alikuwa amenifundisha tangu utotoni na kuendelea. Kwa kawaida yeye angekomesha zungumzio lolote zito pamoja nami kwa kutumia kuhusu maisha yake mwenyewe maneno ya mtunga zaburi: “Kamba zangu zimeniangukia mahali pema.” Ndipo yeye angenihimiza nijitahidi kupatwa na jambo lile lile.​—Zaburi 16:6.

Malezi ya Kiroho

Mambo ambayo Baba alikuwa ameona alipokuwa akitumikia kwa muda wa miaka minne akiwa sajini wakati wa Vita ya Ulimwengu 1, hasa mambo aliyokuwa ameona juu ya mwenendo wa kinafiki wa viongozi wa kidini, yalimzindua. Kwa hiyo, katika 1920, wakati Mwanafunzi wa Biblia mwenye idili alipoeleza utatuzi wa Mungu kwa matatizo ya ulimwengu, kweli za Biblia ziligusa mshipa wenye itikio zuri katika moyo wa Baba. Mama pia alipendezwa na akawa mtumishi wa Yehova mwenye bidii ya kujitoa. Kwa sababu hiyo, dada yangu Kay na mimi tulikuwa na faida ya kupata malezi ya kiroho.

Baada ya muda, Baba aliuza biashara yake, na yeye na Mama wakaanza kusafiri kutoka mji kwa mji katika kazi ya kuhubiri wakati wote. Hivyo, wakati wa mwaka wa kwenda shuleni katika 1928, nilipokuwa na miaka sita na Kay miaka minane, tuliandikishwa katika shule nane tofauti-tofauti! Tuliendelea na mtindo-maisha huu wa kusafiri-safiri kwa muda wa miezi 18 iliyofuata. Lakini ilipozidi kuwa vigumu kutunza vizuri elimu yetu, wazazi wangu walinunua kituo cha petroli na banda la kutengenezea magari lililoungana na kiduka cha kuuzia tamutamu. Hata hivyo, miezi 18 hiyo ya kupainia ilitia mawazo ya daima katika akili ya dada yangu na mimi.

Maskani yetu karibu na Halifax, Nova Scotia, ilikuwa sikuzote nyumba-wazi kwa mapainia na waangalizi wenye kusafiri. Baba alikuwa mkarimu na mwenye msaada kwa wale wenye kuhitaji matengenezo ya magari au speapati, huku Mama akitunza mahitaji ya kinyumbani ya wageni wetu wengi wenye kuzuru. Mimi nina kumbukumbu zilizo dhahiri sana juu ya mambo yaliyoonwa, yenye kuimarisha imani, yaliyosimuliwa na wafanya-kazi hao wa wakati wote. Naweza kukumbuka pia wakati ule ambapo nilikuwa na umri wa miaka 18 na mmoja wa wale ndugu wenye kusafiri akanialika niandamane naye kwa majuma matatu huku akizuru makundi ya karibu. Pendeleo hilo lisilotarajiwa limebaki likiwa limetiwa nakshi akilini mwangu.

Taharuki Wakati wa Marufuku

Katika 1940, nilipokuwa na miaka 17 tu, wenye mamlaka katika Kanada walitangaza rasmi “Tengenezo la Mashahidi wa Yehova” kuwa haramu, na kazi ya Mashahidi ya kueneza evanjeli ikapigwa marufuku. Mnara wa Mlinzi ulichapwa kwa siri katika nyumba yetu, na kutoka hapo ulizungushwa katika sehemu zote za mkoa wa Nova Scotia. Mimi nakumbuka taharuki iliyokuwapo wakati ambapo tarishi angewasili katikati ya usiku akiwa na stenseli na vifurushi vya karatasi na wino.

Wakati wa sehemu ya mapema ya marufuku, sisi tulishiriki tukiwa jamaa wakati wa usiku wa manane katika kugawa kotekote taifani kijitabu cha pekee chenye kichwa End of Nazism (Mwisho wa Utawala wa Nazi). Lakini lazima mimi niungame kwamba moyo wangu ulikuwa unadunda-dunda nilipotoka ndani ya gari katika giza la usiku huo wenye hewa ya theluji-theluji. Baba alitoa mielekezo ya haraka-haraka, iliyo wazi. Ndipo sisi tulipotengana na kila mtu akashika njia tofauti.

Unaweza kuwazia hangaiko letu wakati Kay alipokosa kurudi kwenye gari wakati ule tuliokuwa tumeafikiana. Baada ya kungoja kwa zaidi ya muda wa saa moja, hatukuwa na la kufanya isipokuwa kwenda nyumbani. Tulipata kitulizo kikubwa kwa yeye kuwa huko, akitungojea kwa hamu nyingi. Yeye alikuwa amechukuliwa na polisi lakini si kwa sababu ya kugawa vitabu haramu. Polisi mmoja alikuwa ametupa jicho akamwona na kushangaa ni kwa nini msichana-tineja wa kuvutia alikuwa anatembea peke yake kwenye barabara za Halifax katika saa za mapema-mapema za asubuhi yenye baridi ya kipupwe. Kwa hiyo wakati yeye alipojitolea kumpeleka kwa gari kwenye maskani yetu, Kay alikubali​—ingawaje vijitabu vyake vyote vilikuwa vimegawanywa. Kampeni hiyo ilifanikiwa sana na ikapata mvumisho kati ya watu wa sehemu zote za Kanada.

Jinsi Mimi Nilivyopata Kuwa Mfungwa-Gereza

Baada ya kumaliza shule ya sekondari katika 1941, nilifanya kazi kimwili kwa karibu miaka miwili. Ndipo mimi nilipohudhuria mkusanyiko wa wilaya katika United States, ambako nilikutana na Milton Bartlett, painia mwenye bidii wa umri wangu mwenyewe. Uchangamfu wake tele kwa ajili ya ukweli na shangwe yake yenye kuonekana wazi katika kupainia ni mambo yaliyoshiriki sana katika uamuzi wangu wa kuacha kazi ya kuajiriwa kimwili na kuingia huduma ya wakati wote katika Machi 1943.

Kwa kuwa bado marufuku ilikuwapo, kuhubiri Biblia nyumba kwa nyumba kulikuwa sana kama mchezo wa panya kufukuzana na paka kwa kuhusiana na polisi. Kwenye mgawo mpya katika Charlottetown, Kisiwa cha Prince Edward, mimi nilikuwa na hamu sana ya kwenda nje katika huduma nikaone jibizo la watu mpaka nikasahau kuandika anwani ya mahali nilipokuwa nikilala.

Nilikuwa nimezuru maskani chache wakati niliposhikwa na polisi, wakapekua-pekua mkoba wangu na kunikamata. Kwa kuwa singeweza kueleza nilikuwa nikikaa wapi, mwisho ulikuwa ni kupelekwa jela, nami nikashikwa huko nikiwa mfungwa asiyepaswa kuwasiliana na mtu yeyote kwa muda wa siku nne. Kwa nasibu, binti mmoja wa Shahidi katika kutano letu alisikia kwa mhali mkuu wa polisi akinena habari za Shahidi kijana ambaye wao walikuwa wameshika, na hiyo ikaongoza kufanya akina ndugu wanitoe humo kwa dhamana.

Kesi ya kujaribiwa kwangu iliahirishwa kwa miezi kadhaa, na kwa hiyo mimi niliendelea na huduma ya mlango kwa mlango. Ndipo mimi nilipopewa mgawo mwingine, kwenda Hori ya Glace, Nova Scotia. Miezi michache baadaye, nilipokea agizo la kurudi mbele ya mahakama katika Charlottetown. Mimi nilijitayarishia kesi yangu kwa bidii-endelevu, nikitumainia kutokeza uthibitisho imara wa huduma yangu.

Hakimu aliridhika kwamba nilitimiza sifa zote za mhudumu wa dini. Hata hivyo, yeye aliongezea kwamba ilikuwa desturi kupeleka Mashahidi wa Yehova kwenye kambi za gereza kwa kupatana na sheria za kurekebi-rekebi utumishi wa kitaifa. Hivyo ndivyo mimi nilivyokuja kuwa katika lile gari-moshi la kwenda kwenye kambi ya gereza kule Mto Chalk, Ontario. Wakati wa miaka miwili iliyofuata, mimi nilipelekwa kwenye kambi tatu tofauti-tofauti.

Uhuru—Lakini Mapigano Zaidi

Mimi nilifunguliwa katika 1946 na nikarudia kupainia kwenye Hori ya Glace. Marufuku juu ya Mashahidi wa Yehova ilipoinuliwa, sisi tulikuwa huru tena kufanya kazi yetu katika Kanada tukiwa na himaya ya kisheria. Mahali pamoja ambapo hatukupaswa kufanya kazi palikuwa mkoa wa Kikatoliki wa Kwibeki wenye kunena Kifaransa, ambako mnyanyaso wa kidini ulikuwa mkubwa. Hivyo ndivyo lilivyoanza lile lililokuja kuitwa Pigano la Kwibeki.

Siku ya Jumapili, Novemba 3, 1946, mkutano wa pekee ulipangwa katika Montreal, ukihudhuriwa na msimamizi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi na wengine kutoka kwenye makao makuu ya Brooklyn. Ile trakti yenye maneno-moto Quebec’s Burning Hate for God and Christ and Freedom Is the Shame of All Canada iliachiliwa wazi, na programu ya ugawaji wa kotekote taifani ikaorodheshwa. Mapainia walialikwa wajaze ombi la kuwa katika darasa lifuatalo la Gileadi ili kupokea mazoezi ya kuwapa mafaa ya kufuatia ile kampeni ya pekee katika Kwibeki. Mimi nilijaza ombi hilo na katika muda wa miezi michache nikapokea mwaliko wa kwenda kwenye darasa la tisa la Gileadi.

Maisha Katika Bara Jipya

Kwa kuwa mimi nilihisi nimetayarishwa kwa ajili ya Kwibeki, nilishangaa kabisa wakati, baada ya kuhitimu, niligawiwa kuwa mwangalizi wa mzunguko katika Ontario, Kanada, kuzuru makundi yenye kunena Kiingereza huko. Hata hivyo hiyo haikuwa kitu ikilinganishwa na mshtuko uliokuja miezi sita baadaye wakati nilipopewa barua kutoka kwa Sosaiti ikiwa na mgawo wa kwenda Australia.

Huko katika bara jipya hilo, mgawo wangu wa kwanza ulikuwa kutumikia mzunguko mmoja wenye kuchukua mkoa mzima wa Australia ya Magharibi, hilo likiwa ni eneo kubwa sana la kilometa za mraba 2,528,000! Mzunguko mwingine wa mapema ambao mimi nilitumikia katika sehemu ya kati ya Australia ulitia ndani kituo cha mbali nje-nje kilichoitwa William Creek. Shahidi mmoja tu wa huko ndiye aliyeendesha duka moja tu lililokuwa huko kwenye kituo cha gari-moshi. Siku moja mimi nilistaajabu kuona msafara wa ngamia wenye kuendeshwa na Waaborijini Waaustralia ukija karibu na duka lile. Walikuwa wamekuja kununua vifaa. Maongezi yaliyotokea yalikuwa haya:

Mnunuzi: Taka mabuti.

Mwenye-duka: Makubwa au madogo?

Mnunuzi: Makubwa.

Na hapo ununuzi na uuzaji ukamalizika, na mnunuzi akatoka ndani ya duka hilo akapakie mabuti yake mapya juu ya ngamia wake. Mwingine akaingia.

Mnunuzi: Nataka vazi kwa ajili ya lubra (neno la Kiaborijini kwa mke).

Mwenye-duka: Mnene au kimbaombao?

Mnunuzi: Kimbaombao.”

Vazi likatolewa, likalipiwa, likatumbukizwa ndani ya mfuko ili likapakiwe juu ya ngamia mwenye kungoja.

Pamoja na Mwenzi wa Ndoa

Miaka mitatu baada ya kuwasili katika Australia, mimi nilioa msichana mrembo kutoka Brisbane jina lake June Dobson. Baada ya ndoa yetu, tulipainia kwa mwaka mmoja kabla ya kualikwa turudi ndani ya kazi ya kusafiri, kwanza katika kazi ya mzunguko na baadaye katika kazi ya wilaya.

Wakati mimi nilipokuwa mseja, nilitumikia maeneo mengi ya kule mbali nje-nje nikiendesha pikipiki. Hata hivyo, sasa mke wangu na mimi tulisafiri kwa gari. Barabara ya kuvuka ule Uwanda Nullarbor ulio kombokombo, ambako hali za joto kwa kawaida zinainuka juu ya digrii 46 Selsio, ilikuwa haijatandazwa vizuri kwa kilometa kama 1,200 na ilikuwa na mavumbi-mavumbi mepesi. Mavumbi hayo yalikuwa yakinyunyizika, hivi kwamba gari lilishabihiana na mashua-kasi yenye kupita ikikata maji pande zote. Sisi tulifunga milango na madirisha yote kwa uangalifu kwa kutumia kisetiri ili kuzuia vichangarawe vyenye kunyunyizika vyenye madhara ya polepole. Hiyo ilisababisha joto la ndani ya gari liongezeke sana, lakini angalau ilituokoa tusifunikwe na utando wa vichangarawe na vumbi.

Wakati wa miaka yetu katika kazi ya wilaya, tulivuka-vuka upande huu na ule mwingine wa kontinenti ya Australia mara kwa mara, tukizuru makorija ya miji na majiji na kutumikia makusanyiko ya mizunguko katika mandhari ya kila namna iliyowezekana. Tulipoanza katika kazi ya wilaya katika 1953, wilaya ilikuwa moja tu katika Australia. Sasa kuna tano.

Katika 1960 mwaliko usiotarajiwa ulitujia​—kutumikia kwenye Betheli ya Sydney katika Strathfield. Utofautiano na ile kazi ya kuzunguka ulikuwa mkubwa, lakini mwishowe mimi nilizoea kazi ya dawatini. Hata hivyo, baada ya muda mfupi tulipata mshangazo mwingine bado. Baada ya kutumikia kwenye Betheli kwa miezi 18, June na mimi tulipokea mwaliko wa kuhudhuria mtaala mpya wa miezi 10 wa Shule ya Gileadi.

Katika utofautiano na kisomo changu kilichotangulia cha shule ya Gileadi kule South Lansing, New York, wakati huu tulikuwa mle mle katika Brooklyn, kwenye makao makuu ya ulimwengu ya Mashahidi wa Yehova. Tulipohitimu, tuligawiwa kurudi Australia, mara nyingine kwenye kazi ya kusafiri. Tulitumikia katika nafasi hiyo mpaka 1981, wakati tulipoalikwa turudi kwenye Betheli ya Sydney. Huko tuliweza kushiriki katika jukumu kubwa la kuhamisha afisi ya tawi nzima, kiwanda, na jamaa ya Betheli kutoka Strathfield kwenda kwenye sehemu mpya zilizojengwa kule Ingleburn, karibu kilometa 48 kutoka kitovu cha Sydney.

“Mahali Pema”

Hapa kazi yangu katika dawati ya utumishi ni upendezo wa kila siku. Kwa kuwajua kibinafsi ndugu na dada wengi sana kutoka sehemu zote za kontinenti hii kwa sababu ya miaka ya kuwa katika kazi ya wilaya, mimi napata hisia ya kuwa huko pamoja na waangalizi wa mizunguko wakati ripoti zao zinapoingia kila juma. Ripoti za waangalizi wa wilaya zinanisafirisha moja kwa moja ndani ya majumba makubwa ya mikutano na Majumba ya Mikusanyiko yakiwa pamoja na ile hewa ya hali za kusanyiko la mzunguko. Kukiwa na jamaa ya Betheli yenye watu zaidi ya 110, iliyo katika eneo la nusu-mashambani ambayo iko mbali vya kutosha na kelele na uchafuzi wa jiji, mke wangu na mimi tunahisi kwamba maisha Betheli ndiyo upeo wa “mahali pema.”

Siku moja ya mwisho-mwisho wa majira ya vuli katika Mei 1984, mratibu wa Halmashauri ya Tawi, H. V. Mouritz, aliniambia mimi kwa unyamavu kwamba nilikuwa nimepokea mweko-rasmi kutoka Baraza Linaloongoza nitumikie nikiwa mshiriki wa Halmashauri ya Tawi la Australia. Hisia yangu alasiri hiyo ilikuwa kama ile ile katika 1947 wakati niliposoma ile barua yenye kunigawia nitumikie katika bara hili la huku chini lenye kujaa upendezo.

Kupitia kuangalia miaka yangu 63 ya maisha katika tengenezo la Yehova ni kuhisi utimizo wa kibinafsi wa Zaburi 16:6. Kweli kweli, “kamba” zimeniangukia “mahali pema.” Kama mimi ningelazimika kupanga upya ramani ya maisha yangu, pasipo kusitasita ningechagua mwendo ule ule kabisa ambao nimechukua. Kungekuwa hakuwezi kuwa na tokeo lenye kufurahisha kuliko hilo​—kungekuwa hakuna jambo lililoonwa lenye kuthawabisha kuliko hilo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki