Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 8/1 uku. 30
  • Jina la Mungu na Watafsiri wa Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jina la Mungu na Watafsiri wa Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Jina la Mungu na “Agano Jipya”
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Magumu ya Kujua Maana ya Jina la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 8/1 uku. 30

Jina la Mungu na Watafsiri wa Biblia

KATIKA 1952, The Bible Translator kilitangaza zungumzo la “tatizo” la kuwakilisha jina la Mungu katika tafsiri za Biblia zilizokusudiwa kutumiwa katika nyanja za misheni za Jumuiya ya Wakristo. Wachangaji walitambua umaana wa jina hilo katika Biblia​—jina ambalo linaonekana katika Maandiko ya Kiebrania karibu mara 7,000. Lakini wao hawakuweza kuafikiana juu ya jinsi linavyopasa kufasiriwa katika lugha za ki-siku-hizi. Watu fulani walipendelea neno kama vile “Aliye wa Milele.” Wengine walichagua mtajo wa cheo “Bwana.” Hakuna wowote waliopendekeza fasiri ya “Yehova” au “Yahweh.” Kwa nini sivyo?

Sababu mbili zilitajwa na mchangaji H. Rosin. Kwanza, yeye aliitikadi kwamba wakati Biblia ya Kiebrania ilipotafsiriwa hapo awali kuingizwa katika Kigiriki (ile Septuagint Version ya kabla ya wakati wa Kikristo) watafsiri walifasiri jina la Mungu kwa neno la Kigiriki la kusema “Bwana.” Pili, yeye alihofu kwamba kuingiza jina Yehova ndani ya tafsiri “huenda pia kukagawanya-gawanya kanisa.” Kwa maana je, yeye akaongezea, ‘“Mashahidi wa Yehova’ si wapinga utatu?”

Kuhusu jambo la kwanza la Rosin, magunduzi ya uchimbuzi wa vitu vya kale yamemthibitisha kuwa mwenye makosa. Kwa uhakika, watafsiri wa Septuagint hawakuwakilisha jina la kimungu kwa kutumia neno la Kigiriki la kusema “Bwana.” Bali, wao waliliandika lote katika herufi za awali za Kiebrania moja kwa moja kuliingiza katika andishi-awali la Kigiriki, hivi kwamba nakala za tafsiri ya Septuagint zilizotumiwa na Wakristo wa mapema zilikuwa na lile jina la kimungu.

Kwa kupendeza, wakati Wakristo wa mapema waliponukuu kutokana na Septuagint, haielekei kwamba wao waliondoa jina hilo kwenye nukuu lao. Hivyo, inaelekea sana sana kwamba hati za awali zilizonakiliwa kwa mkono za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo (lile “Agano Jipya”) zilikuwa na jina la Mungu. Profesa George Howard, katika makala moja yenye kuonekana katika Biblical Archaeology Review, Machi 1978, alitoa hoja imara za kukata shauri hivyo. Mathalani, yeye anataja “kifungu kimoja cha kirabbi kilicho maarufu (Talmud Shabbat 13.5)” ambacho “kinazungumzia tatizo la kuharibu maandishi-awali ya uzushi (labda vikiwa ni kutia sana na vitabu vya Wakristo wa Kiyahudi) “Tatizo lilikuwa nini? “Hayo maandishi-awali ya uzushi yana jina la kimungu, na kuyaharibu yote kabisa kwa ujumla kungetia ndani kuliharibu jina la kimungu.”

Lakini namna gani juu ya lile katao la pili la Rosin? Je! utumizi wa jina la Mungu ungesababisha matatizo kwa Jumuiya ya Wakristo? Basi, fikiria jambo lililotukia wakati jina hilo lilipoondolewa. Baada ya karne ya kwanza wanakili “wa Kikristo” waliweka mahali pa jina la Mungu maneno kama “Mungu” na “Bwana” katika Septuagint na pia Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kulingana na Profesa Howard, inaelekea kwamba hii ilichangia machafuko yaliyopata Jumuiya ya Wakristo katika miaka ya baadaye: “Huenda ikawa kwamba kuondolewa kwa Tetragramatoni [jina la Mungu katika Kiebrania] kulichangia sana ile mijadala ya baadaye kati ya fundisho la Kristo na Utatu, ambayo ilikumba kanisa la karne za mapema za Kikristo.”

Kwa uhakika, kuondolewa kwa jina la Mungu katika Biblia kulifanya iwe rahisi zaidi Jumuiya ya Wakristo kuchagua kufuata fundisho la Utatu. Kwa sababu hiyo, kama Jumuiya ya Wakristo hiyo ingerudisha jina hilo katika Biblia kamili na katika ibada, hiyo ingesababisha magumu. Yehova, kama vile anavyofunuliwa katika Maandiko ya Kiebrania na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, kwa uwazi yuko katika hali ya kutengeka kutoka kwenye Yesu Kristo na yeye si sehemu ya Utatu fulani.

Profesa Howard alisema hivi kwa kuongezea: “Kuondolewa kwa Tetragramatoni labda kulifanyiza mazingira ya kitheolojia yaliyo tofauti na yale yaliyokuwako wakati wa kipindi cha Agano Jipya cha karne ya kwanza Mungu wa Kiyahudi ambaye sikuzote alikuwa kwa uangalifu amepambanuliwa na wengine wote kupitia utumizi wa jina lake la Kiebrania, alipoteza kadiri fulani ya upambanufu wake wakati Tetragramatoni ilipopita.” Mashahidi wa Yehova wamerudisha jina la Mungu si katika Biblia kamili tu, bali pia katika ibada yao ya kila siku. Hivyo, wao wanaona ‘upambanufu wa uangalifu’ kati ya yule Mungu wa kweli na tule tumiungu twa bandia twa ulimwengu huu. Kwa njia hii wao wamewezeshwa kurudisha “mazingira ya kitheolojia” yaliyokuwako katika lile kanisa la Kikristo la karne ya kwanza.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki