Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 8/15 kur. 4-7
  • Kufanikiwa kwa Gharama Yoyote?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufanikiwa kwa Gharama Yoyote?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kupotezwa Njia—Jinsi Gani?
  • Yale Maumivu ya “Mafanikio”
  • Aina Bora ya Mafanikio
  • Fulizeni Kutafuta Mafanikio ya Kiroho
  • Jinsi Unavyoweza Kupata Mafanikio ya Kweli Maishani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Jinsi ya Kupata Mafanikio ya Kweli
    Amkeni!—2014
  • Je, Ni Lazima Wakristo Wawe Maskini?
    Amkeni!—2003
  • Baraka ya Yehova Inatajirisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 8/15 kur. 4-7

Kufanikiwa kwa Gharama Yoyote?

KULE kupiga moyo konde ili kupata mafanikio kunaonyesha kwamba mmoja ana mradi wa wazi kabisa. Mradi wako wewe ni nini maishani? Wewe unajitayarisha kufanya nini ili uufikie? Kweli kweli, je! ni nini kinachopasa kuwa ufuatiaji wako ulio wa kwanza kabisa ili utosheke kweli kweli na kuwa mwenye furaha?

Katika mabara mengi ya Ulimwengu wa Tatu, kiwango cha ujumla cha maisha kinapungukiwa na mambo mengi. Kwa sababu ya matatizo yanayokabiliwa huko, kufikiria mashauri yanayofaa kutokana na Neno la Mungu kutatusaidia kukadiri vizuri zaidi ubora wa miradi yetu wenyewe na mafanikio, hata tuwe tunaishi wapi.

Kwa kuwa umaskini ni tele, watu wengi wamefuatia mafanikio ya kipesa kwa kusahaulia mbali kila kitu kinginecho. Watu fulani wanageukia kutofuata haki ili watimize jambo hilo. Ingawa hivyo, wanapokuwa Wakristo wa kweli, inawapasa wawe wamekwisha kuuacha nyuma daima mwelekeo huu ili kujipatanisha na viwango vyenye uadilifu vya Biblia.

Hata hivyo, hata Wakristo fulani wananasika tena katika kulenga shabaha kwenye miradi ya kilimwengu. Huenda wao wakaanguka ndani ya mwenendo usio wa Kikristo ili wafikie mafanikio. Wazazi wanaachilia jamaa zao bila kuzijali. Watu mmoja mmoja wanakosa kujali utumishi wao kwa Mungu. Je! wewe unafikiri tokeo lingekuwa nini kuhusiana na kupata utoshelevu na furaha maishani?

Ikitutia chonjo juu ya tokeo lenyewe, Biblia inaonya hivi: “Wale ambao wamepiga moyo konde wawe matajiri wanaanguka katika kishawishi na kitanzi na tamaa nyingi zisizo za akili na zenye kujaa maumizo . . . Kwa maana upendo wa pesa ni mzizi wa namna zote za mambo yenye kudhuru, na kwa kujitahidi kufikia upendo huo watu fulani wamepotezwa njia kutoka kwenye imani na wamejichoma-choma wenyewe mwili wote kwa maumivu mengi.”​—1 Timotheo 6:9, 10, NW.

“Namna zote za mambo yenye kudhuru.” ‘Kuchomwa-chomwa mwili wote kwa maumivu mengi.’ Kwa uhakika huo hausikiki kama usimulizi wa utoshelevu na furaha, au unasikika? Hata hivyo, mambo ambayo mamilioni ya watu wamejionea wenyewe muda wote wa karne zilizopita, hata mpaka leo hii, yanathibitisha jinsi taarifa hiyo ya Biblia ilivyo ya kweli. Basi, je! hiyo inapendekeza nini kwa habari ya miradi na mwendo wa maisha ya Mkristo?

Kupotezwa Njia—Jinsi Gani?

Ni kwa njia gani mbalimbali Wakristo wanaweza kupotezwa njia kutoka kwenye imani? Wengine wamefikia hatua ya kukataa kabisa maadili na itikadi zilizo za kuogopa Mungu. Katika visa vingine watu mmoja mmoja wamegeuziwa kando kutoka kwenye mwendo wa bidii ya kujitolea Mungu, hata wakatumia bidii hiyo kama njia ya kupata uvutano juu ya wengine. Kwa hiyo Biblia inanena juu ya ‘watu waliofisidika katika akili na kutekewa ule ukweli, wakifikiri kwamba bidii ya kujitolea Mungu ni njia ya kupata pato.’ (1 Timotheo 6:5, NW) Ingawa hawaachi Ukristo kabisa, huenda wao wakajikuta wanavunja kanuni za Biblia ambazo ni sehemu zinazohitajiwa sana za imani ya Kikristo.

Yesu aliambia wafuasi wake wasiwe kama watu wa ulimwengu wanaopiga ubwana juu ya wengine. Yeye alisema: “Hivyo sivyo ilivyo miongoni mwa ninyi; lakini ye yote yule anayetaka kuwa mkuu miongoni mwa ninyi lazima awe mhudumu wenu.” Katika kuwashutumu viongozi wa kidini Wayahudi, Yesu alisonga mbele kidogo. Yeye alionyesha kwamba upendo mwingi wa fahari ya kilimwengu unachumia mtu kukosa kibali cha Mungu. (Mathayo 20:26; 23:6-9, 33, NW) Hivyo, Wakristo wanapaswa watafute kutumikiana badala ya kushindana na kutawala wengine. Mpenda pesa anayetafuta mafanikio kwa gharama yo yote anaweza kupotezwa njia kwa urahisi atoke katika mwendo huu.

Wewe uko namna gani unapojilinganisha na jambo hilo? Je! wewe unajikuta ukipima mafanikio yako kulingana na kadiri ambayo unatokeza mamlaka juu ya wengine? Je! wewe unaelekeza-elekeza kanuni na mafundisho ya Kikristo kwa akili nyingi au kuzipinda-pinda ili ujidaie au ujipatie mamlaka? Je! wewe unahisi kwamba ni lazima ufikie mambo mengi zaidi ya marika yako hata kama bei ya kufanya hivyo ni nini? Je! wewe unafurahia sana kuongea juu ya utajiri wako au mambo uliyoweza kupata katika kazi-maisha? Ikiwa ndivyo, basi unahitaji kuchanganua kama wewe unapotezwa njia kutoka kwenye ile imani.

Yale Maumivu ya “Mafanikio”

Yesu alisema hivi pia: “Msijiwekee hazina duniani . . . kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako . . . Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.” (Mathayo 6:19-24) Je! wazazi wanaoelekeza watoto wao hasa kwenye miradi ya vitu vya kimwili na kazi-maisha za kilimwengu wanafuata shauri hili? Je! mkazo unaotiwa juu ya mafanikio ya kilimwengu unaistahiki ile gharama ikiwa watoto wanaacha ukweli na kuanza kufuata mitindo-maisha isiyo ya Kikristo? Je! kuna ustahiki wa kudhabihu au, angalau, kuhatirisha maisha zao za kiroho kwa ajili ya “hazina juu ya dunia”? Mara nyingi wazazi wanaofanya hivyo wanapata kwamba hata wao ‘wanachomwa-chomwa mwili wote kwa maumivu mengi’ kwa sababu ya kuhangaikia watoto wao na kuwa na majuto ya kuwapoteza kiroho, na nyakati nyingine kimwili.

Upendo wa mali ni bwana-mkubwa mwenye kudai-dai. Huo unawatoza watu wakati, imara, na uwezo mbalimbali; na unakaba roho ya bidii ya kujitolea Mungu na kuitoa. Kwa kawaida unashawishi-shawishi watu watafute utajiri ulio mkubwa hata zaidi na fahari ya kilimwengu, hivyo ukiwavuta hata zaidi kutoka kwenye ile imani. Biblia inasema hivi kwa kufaa: “Mpendaji tu wa fedha hatatosheka na fedha, wala mpendaji ye yote wa utajiri atosheke na mapato.”​—Mhubiri 5:10, NW.

Hata baada ya kuwa Mkristo, upendo wa mafanikio ya kipesa wa mwanamume mmoja Mwafrika aliye mfanya biashara uliendelea kuchukua mahali pa kwanza maishani mwake. Yeye alikosa kujali utendaji wake wa Kikristo kwa kupendelea ziara za starehe za kirafiki pamoja na washirika walimwengu wa kikazi. Yeye hakufanya maendeleo yo yote kiroho, wazee wa kundi lake wajapofanya jitihada za kumsaidia. Hivyo yeye alijipata akiwa katika mfadhaiko wa kiroho​—akiwa mkosa-upande, ambapo alikuwa si Mkristo wa sawasawa na bado alitaka kutambuliwa kuwa mmoja. Sisi sote tunaweza kuthamini kwamba hali hii haikuwa yenye kuleta utoshelevu wenye kina kirefu maishani au furaha ya kudumu.

Watu kama hao watakabiliana na maumivu ya kiroho, hata iweje. Biashara na uhusiano wa starehe za kijamii pamoja na watu wasioingiwa sana na mashaka wanapokosa kufuata haki au maadili ya ngono ni mambo yanayotia mtu katika uwezekano wa kupatwa na mavutano yasiyofaa. Wakristo wanaotiwa katika uwezekano huo wanalazimika kupiga vita dhidi ya mavutano hayo na kwa kawaida wanakuwa na pambano pamoja na dhamiri yao. Baadhi yao baadaye huwa kama washirika wao na wanapotezwa njia kabisa kutoka kwenye ile imani. (1 Wakorintho 15:33) Mafanikio ya kipesa ambayo yanaongoza kwenye ushinde huo wa kiroho na kiadili yana mafaa gani? Kama vile Yesu alivyosema: “Itakuwa manufaa gani kwa mtu ikiwa yeye anapata ulimwengu mzima lakini apate hasara ya nafsi yake?”​—Mathayo 16:26, NW.

Aina Bora ya Mafanikio

Mambo yaliyoonwa yamehakikisha kwamba ni jambo la hekima kutii shauri hili la Biblia: “Mwache kufanyizwa kulingana na mtindo wa huu mfumo wa mambo, bali . . . mpate kujithibitishia wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.” “Msiwe mkipenda wala ulimwengu wala vitu katika ulimwengu. Ikiwa mtu ye yote anapenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo katika yeye.” Ndiyo, sisi ni wenye hekima ikiwa hatunakili ulimwengu au kutamani sana matoleo yao. Hangaikio letu kuu linapasa kuwa kupata kibali cha Mungu, ambacho hakiwezi kupatwa kwa kufuatia vitu vya ulimwengu.​—Warumi 12:2; 1 Yohana 2:15, 16, NW.

Yesu alitoa kielezi cha jambo hili kuhusiana na mkulima aliyeitibari katika utajiri wake lakini Mungu akamwambia: “Ewe usiyefikiria mambo vizuri, usiku huu wao wanadai nafsi yako kutoka kwa wewe. Basi, ni nani atakuwa mwenye vitu ambavyo wewe umerundika akibani?” Akitoa muhtasari wa kielezi chake, Yesu alisema: “Hivyo ndivyo inavyoenda kwa mtu ambaye anajiwekea mwenyewe hazina lakini si tajiri kuelekea Mungu.” Yesu alikuwa anaonyesha kwamba “hata wakati mtu anapokuwa ana utele uhai wake hautokani na vitu ambavyo yeye anavyo.”​—Luka 12:15-21, NW.

Yesu alitumia kielelezo kilicho hai cha mtawala mmoja kijana tajiri kuonyesha jambo hilo hilo. Mwanamume huyu alikuwa mwenye mafanikio kwa maana ya kilimwengu, na kwa uwazi yeye alitaka kuwa mnyoofu kiadili. Hata hivyo, Yesu hakumtokeza wazi mbele ya watu kuwa kifananishi chema cha mafanikio. Bali, Yesu alisema ingekuwa vigumu kwa watu hao “kufaulu kuingia ndani ya ufalme wa Mungu.” Watu walio wengi walio katika hali hiyo hawako tayari kudhabihu masilahi ya vitu vya kimwili na kutafuta Ufalme wa Mungu ukiwa ndio mradi mkuu katika maisha zao.​—Luka 18:18-30, NW.

Akikazia zaidi utangulizo wa masilahi ya kiroho, Yesu alisema: “Msiwe na wasiwasi na kusema, ‘Sisi tutakula nini?’ au, ‘Sisi tutakunywa nini?’ au, ‘Sisi tutavaa nini?’ Kwa maana hivi vyote ndivyo vitu ambavyo mataifa yanafuatia kwa hamu nyingi. Kwa maana Baba yenu wa kimbingu anajua ninyi mnahitaji vitu vyote hivi. Basi, fulizeni kutafuta kwanza ule ufalme na uadilifu wake, na vitu vyote hivi vingine ninyi mtaongezewa.” Kwa hiyo, hata kuhusiana na vitu vinavyohitajiwa kabisa, ni lazima sisi tupange vizuri mambo tunayopaswa kutanguliza. Ili sisi tuwe wenye mafanikio kikweli​—tufikie furaha na kupata utoshelevu halisi​—ni lazima mambo ya kiroho yaje mbele ya mambo ya kimwili.​—Mathayo 6:31-33, NW.

Fulizeni Kutafuta Mafanikio ya Kiroho

Kwa hiyo kwa uwazi mwendo ulio wa hekima ni kutafuta mafanikio kwa kufuatia Ufalme wa Mungu na uadilifu wake. Hiyo inahusisha ndani kujifunza Biblia ili “kujithibitishia wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.” Mapenzi yake yanahusisha ndani kuweka utumishi wake kwanza katika maisha yako, kuwa kwako na ushiriki kamili katika huduma ya Kikristo, kutokosa kwako kujali mikutano ya Kikristo; na kuendesha kwako maisha manyoofu ya kiadili kwa kupatana na uadilifu wa Mungu. Mambo hayo hayapasi kuwekwa kando kwa ajili ya masilahi ya vitu vya kimwili, wala hayapasi kufunikwa nayo. Hilo ndilo jambo lililomaanishwa na shauri la Yesu kwa yule mtawala kijana tajiri: “Uza vitu vyote ambavyo wewe unavyo na ugawanyie watu maskini, na wewe utakuwa na hazina katika mbingu; na uje uwe mfuasi wangu.”​—Warumi 12:2; Luka 18:22, NW.

Katika kufanya jambo hili, utakuwa unajenga hali ya kiroho yako mwenyewe na ile ya jamaa yako. Badala ya kuwa na akili ya kutaka makubwa au kuweka tumaini lako juu ya mali zisizo na uhakika, wewe utakuwa miongoni mwa wale ambao ni ‘matajiri katika kazi zilizo nzuri sana, wenye kujihazinia kwa usalama msingi mzuri sana kwa ajili ya wakati ujao, ili kwamba wao wapate kuwa na mshiko thabiti juu ya uhai ulio halisi.’ Ndiyo, mradi wako unaweza kuwa uhai wa milele katika Paradiso ya kidunia ambayo itarudishwa kwa sababu “ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hubaki milele.” Hakuna mafanikio ambayo wewe ungeweza kufikia yaliyo makubwa kuliko hayo.​—1 Timotheo 6:17-19; 1 Yohana 2:17, NW.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Je! pesa ndizo ufunguo?

[Picha katika ukurasa wa 7]

Je! wazazi wataacha watoto wao waende zao wakafuatie mafanikio kupitia elimu ya juu zaidi?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki