Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 9/15 kur. 3-4
  • Je! Watu Wema Wote Huenda Mbinguni?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Watu Wema Wote Huenda Mbinguni?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Mbinguni Kukoje?’
  • Ukweli Kuhusu Mbingu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Mbinguni
    Amkeni!—2016
  • Ni Nani Wanaoenda Mbinguni, na kwa Sababu Gani?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Wapendwa Wetu Walio Wafu Wako Wapi Sasa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 9/15 kur. 3-4

Je! Watu Wema Wote Huenda Mbinguni?

Maziko yalikuwa yamemalizika lakini si ule mshtuko wenye kugandisha mwili kama barafu. . . . Lilikuwa kama jambo lisiloaminika kwamba majuma machache tu mapema kivulana wangu alikuwa amekuwa akipiga hatua zake za kwanza, huku uso wake mdogo ukiwa umenawiri kwa kicheko cha shangwe tupu. Lakini sasa Andrew alikuwa amekufa!. ..

“Mimi nilifuliza kusimama kwenye dirisha, nikitazama nje ndani ya usiku ule, nikizipekua mbingu. ‘Yuko wapi jamaa huyo mdogo sasa?’ mimi nikataka kujua. ‘Je! yuko mahali fulani kule juu mbinguni akiwa miongoni mwa nyota?’”

LABDA kifo cha mtoto aliye kipenzi ndilo tukio lenye kushtua sana hisia-moyo kuliko matukio yote yanayoweza kupata wazazi. ‘Sasa mtoto wetu yuko wapi?’ wao wanataka kujua. ‘Yuko mbinguni au mahali pengine?’ Dini zilizo nyingi hufundisha kwamba watoto wachanga wanaokufa huenda mbinguni. Katika Johannesburg, Afrika Kusini, maneno ya kumkumbuka mfu katika jiwe la kaburi moja yanasema hivi: “Mungu alitaka ua lenye kufunguka, malaika wake alichukua ua moja kati ya yale yetu.” Lakini huenda mmoja akataka kujua hivi: ‘Kwa nini Mungu atake “ua lenye kufunguka” na hali, kulingana na itikadi ya watu wengi, tayari yeye ana maua mengi sana?’ Na watu wasio na hesabu wanataka kujua hivi . . .

‘Mbinguni Kukoje?’

Watu walio wengi wana kiwazo cha juujuu tu juu ya mbinguni. Baadhi yao wanakuwa na mioyo iliyochangamka wanaponena juu ya kuingia katika raha mustarehe kule angani baada ya kufa. Lakini Biblia inasema nini? Ule ule mstari wayo wa kwanza unasema: “Katika mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.” (Mwanzo 1:1, ZSB) Hiyo inarejeza kwenye mbingu za vitu vya kimwili, ule mpangilio mtukufu wa nyota na magalaksi ya nyota. (Kumbukumbu 4:19) Lakini kuna mbingu za kiroho pia. Hivyo, Biblia inanena juu ya ‘makao ya utukufu na fahari’ ya Yehova.​—Isaya 63:15.

Ni nani aliyekuwa wa kwanza kupaa kwenda kwenye haya “makao ya utukufu” ya Baba yetu wa kimbingu? Alikuwa Mwana wake mpendwa, Yesu Kristo. Yeye alisema: “Hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu.” (Yohana 3:13) Hiyo inaonyesha wazi kwamba hakuna viumbe wowote wa kibinadamu waliokuwa wameenda mbinguni. Lakini Yesu aliahidi kwamba wanadamu fulani wangeenda huko. Muda mfupi tu kabla ya yeye kupaa mbinguni, alisema hivi kwa wanafunzi wake waaminifu: “Naenda kuwaandalia mahali. . . . Nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.”​—Yohana 14:2, 3.

Basi, kwa uwazi watu fulani walio wema huenda mbinguni. Lakini je! watu wote walio wema huenda mbinguni? Namna gani juu ya maskani ya mwanadamu​—dunia? Je! hiyo itaharibiwa na vita ya nyukilia iwe kaa lililochomeka lenye kuelea-elea katika anga? Hasha. Biblia inasema: “Kizazi huenda, kizazi huja; nayo dunia hudumu daima.” (Mhubiri 1:4) Na mbona Muumba aharibu dunia hii yenye sura nzuri, hata ingawa sehemu fulani zayo zimechafuzwa na watu wenye ubinafsi? Neno la Mungu linaahidi hivi: “Wenye haki watairithi nchi [dunia, NW], nao watakaa humo milele.”​—Zaburi 37:29.

Basi, inaonekana wazi kwamba dunia ina wakati ujao wenye kupendeza. Katika Mahubiri ya Mlimani yake ambayo yanajulikana sana, Yesu alitabiri hivi: “Wenye furaha ni wale wapole, kwa kuwa wao watairithi dunia.” (Mathayo 5:5, NW) Waaidha, kitabu cha mwisho cha Biblia, Ufunuo, kinaonyesha kwamba dunia itakuwa paradiso. Kinasema hivi kuhusu aina ya wanadamu watiifu: “Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, atakuwa Mungu wao. Naye atapangusa kila chozi katika macho yao; wala mauti haitakuwa tena; wala maombolezo, wala kilio, wala uchungu hautakuwa tena.”​—Ufunuo 21:3, 4, ZSB.

Kutokana na yaliyotangulia, inaweza kuonwa kwamba watu fulani walio wema huenda mbinguni, hali wengine watafurahia maisha duniani. Hiyo inamaanisha kwamba kuna vikundi viwili vya watu vyenye kutofautiana kabisa ambavyo vinahusishwa ndani. Hiyo inawezekana jinsi gani? Waaidha, kama vile mama ya Andrew, wengi wanafanya wasiwasi juu ya jambo linalopata watoto wao wachanga wanaokufa bila kubatizwa. Wakatoliki wa Kiroma wanafundishwa kwamba hao huenda mahali panapoitwa Limbo. Je! kuna mahali kama hapo? Je! watoto wachanga huenda huko? Majibu yenye kuridhisha na kufariji yanaandaliwa katika makala inayofuata.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki