Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 11/1 uku. 7
  • Udumifu wa Mume Waungamanisha Jamaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Udumifu wa Mume Waungamanisha Jamaa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Upendo Wafanya Jamaa Ziwe na Umoja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kuazimia Kumtumikia Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Je, Mashahidi wa Yehova Wanavunja Ndoa za Watu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 11/1 uku. 7

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

Udumifu wa Mume Waungamanisha Jamaa

WEWE ungefanya nini kama ungeukubali ukweli halafu mwenzi wako wa ndoa akupinge vikali na kufanya kila jambo lililo katika nguvu zake ili avunje ukamilifu wako? Je! wewe ungeimarishwa na maneno ya Paulo katika 2 Timotheo 3:12, NW, ambapo yeye anasema: “Wale wote wanaotamani kuishi kwa kujitolea Mungu katika ushirika na Kristo Yesu watateswa pia”? Je! wewe ungevumilia au ungekubali kushindwa? Mwanamume mmoja Mkristo katika Italia alikabili usoni mwito huo wa ushindani. Yeye hakukubali kushindwa, na Yehova alimbariki kwa sababu hiyo.

Hapo kwanza mwanamume huyo alifuata Ukomunisti kwa bidii nyingi, lakini pia alikuwa Mkatoliki mwenye juhudi. Yeye aliitikadi katika usawa wa watu wote, na alihisi kwamba makundi yote hayo mawili yalihubiri wazo hilo bora Mmoja wa wafanya kazi wenzake alinena kwake juu ya Ufalme wa Mungu na mara hiyo yeye akatambua kwamba, kwa kweli, hii ilikuwa ndiyo njia pekee ambayo usawa ungeweza kufikiwa. Yeye alianza kufuata ukweli kwa joto lile lile alilokuwa ameonyesha kwa Ukomunisti na Ukatoliki na akabatizwa katika 1972. Namna gani juu ya mke wake? Mke huyo alimpinga vikali. Mke huyo anasimulia hivi:

“Ilikuwa katika 1970 kwamba mume wangu akaonana kwa mara ya kwanza na Mashahidi wa Yehova kwenye mahali pake pa kazi. Pole kwa pole, kadiri yeye alivyojifunza Biblia, mimi nilikuja kung’amua kwamba hiyo ilikuwa dini mpya na ilikuwa na mambo ambayo mimi sikuafikiana nayo. Mnyanyaso ulianza mara hiyo kutoka kwa mimi na washiriki wengine wa jamaa.”

Yeye anaendelea kusema: “Wazazi wa mume wangu walimsumbua-sumbua, wakitumia kila njia iliyowezekana ili wamkomeshe. Mume wangu alipofanya maendeleo katika maarifa ya Biblia aliona uhitaji wa kuondolea mbali sanamu zitoke katika maskani yetu. Mimi nilimwambia kama angefanya hivyo jambo fulani lililo baya sana lingetukia. Yeye aliharibu picha moja ya kidini nami nikaanza kumshambulia kwa maneno na kimwili na kurarua hesabu fulani ya magazeti yake. Nilipopiga makelele mengi, wazazi-wakwe wangu walikuja mbio na kujitupa kwake pia, lakini yeye hakulipa kisasi.

“Hali hizo za kutoafikiana ziliendelea mpaka nikamwacha, wakati alipopinga binti yetu asihudhurie darasa la katekisimu kanisani. Mume wangu aliniambia kwamba kama mimi nisingerudi kwenye maskani yetu angenifanyia shtaka la kuacha kuishi nikiwa chini ya himaya ya ndoa. Baada ya juma moja niliamua kurudi.

“Katika jaribio zaidi la kumkomesha, mimi nilienda kwa mtu aliye chombo cha mawasiliano ya ulimwengu wa roho na kuomba kwamba anaswe kwa dawa za ulozi. Chombo huyo akaanza kuniuliza-uliza maswali nami nikaeleza hali ilivyokuwa. Alipojua ilivyokuwa, yeye akaniambia kwamba hakuna aina yoyote ya dawa ya unasaji iliyo na athari yoyote juu ya mmoja wa Mashahidi wa Yehova

“Sisi tukafikiria kutafuta ushauri wa padri wa mtaa wetu Padri alitushauri twende kwa mwanasheria. Mimi nikashangaa wakati mwanasheria huyo aliponitia moyo nihudhurie mikutano ya Mashahidi wa Yehova pamoja na mume wangu. Baba-mkwe wangu aliyekuwa pamoja nami alikinza jambo hilo akisema kwamba jamaa yake ilikuwa imejitoa kwa bidii nyingi kufuata San Rocco, ‘Yute Mpa-Himaya’ wa mji wetu. Hata hivyo, mwanasheria huyo alieleza kwamba ‘mtakatifu’ huyo, kama sanamu nyinginezo zote, alikuwa wa bandia. Halafu yeye akajitambulisha kuwa ndiye mwenyekiti wa Aksio Katoliki, na kutuambia kwamba yeye hakushiriki hata kidogo katika zile sikukuu za miadhimisho ya kidini kwa sababu, akiwa amekwisha kusoma Biblia, aliona kwamba zote zilikuwa za bandia. Kwa kumalizia, yeye akasema: ‘Nenda pamoja na mume wako na uwe na amani. Msikilize yeye, nawe pia uanze kujifunza Biblia.’

“Kwa kupata kitia-moyo hicho mimi nilifikiria mwenendo, mabadiliko, na udumifu wa mume wangu; kwa hiyo nikaanza kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova pamoja naye. Kwa kuvutiwa na upendo ulioonyeshwa huko, nilijifunza, nikajiandikisha katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, na kuanza katika utumishi wa shambani. Hatimaye, nilionyesha wakfu wangu katika 1977 na nina furaha sasa kuwa katika ukweli, asante kwa Yehova aliyesaidia mume wangu kuwa na udumifu na kuungamanisha jamaa nzima katika ibada Yake.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki