Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 12/1 kur. 4-7
  • Mapokeo ya Kidini na Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mapokeo ya Kidini na Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wawekwa Huru Kutoka Mapokeo Yenye Madhara
  • Mapokeo ya Kidini Je! Ni Kuabudu Mungu Katika Ukweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Pokeo Lipinganapo na Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Je, Ni Lazima Pokeo Lipingane na Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Ni Ibada ya Nani Anayoikubali Mungu?
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 12/1 kur. 4-7

Mapokeo ya Kidini na Biblia

‘NYINYI mnafanya neno la Mungu litanguke kwa pokeo lenu.” Hayo hayakuwa maneno ya mwingine ila Yesu Kristo. (Marko 7:13, NW) Kama vile walivyo watu wengi leo, Wayahudi katika siku ya Yesu walifuatilia kwa uaminifu kigezo kilichotatanika cha miongozo ya kiadili na desturi. Na kama vile walivyo wengi wa makasisi wa leo, viongozi wao wa kidini walikuwa na rai ya kwamba mapokeo hayo yalikuwa ya maana kuliko Biblia.

Kutoa kielezi: Neno la Mungu liliamuru waziwazi kwamba watoto waheshimu wazazi wao. (Kutoka 20:12) Kwa uwazi hiyo ilitia ndani kusaidia wazazi waliotumbukia katika shida kubwa za kipesa. Hata hivyo, pokeo moja la Kiyahudi lilisitawi ambalo liliandaa njia nzuri ya kuepa wajibu huo wa Kibiblia. Mtu mbinafsi alipaswa tu kutoa ahadi rasmi kwamba mali yake ya kibinafsi ingetolewa baadaye iwe upaji kwa hekalu, akiweka kando mali hiyo kwa kuitangaza kuwa “korbani.” Neno hilo lilimaanisha “zawadi iliyowekwa wakfu kwa Mungu.” Ingawa kuna ithibati ya kwamba mwabudu huyo Myahudi alikuwa huru kuendelea kutumia korbani hiyo ili kujifaidi binafsi, yeye angeweza kunyima wazazi wake kitu hicho kwa njia ya utawa.​—Marko 7:9-12, NW.

Ingawa hivyo, Yesu alishindana na pokeo hilo na ‘mapokeo matakatifu’ mengine ya Kiyahudi, akisema: “Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema, Watu hawa huniheshimu kwa midomo; ila mioyo yao iko mbali nami. Nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.”​—Mathayo 15:3-9.

Kulingana na aliyoyasema Yesu, je! kweli Mkristo anaweza kuchukua ya kwamba pokeo lolote la kidini linapatana na Biblia? Hasha. Hata uwe ni msisimuko au hisiamoyo ya kadiri gani inayohusianishwa na desturi fulani, hangaikio la Mkristo ni kuona kama inapatana na Neno la Mungu au haipatani. Kuonyesha kisa kimoja, fikiria vitendo fulani vya mapokeo ya kidini vilivyoelezwa katika kitabu cha Kikatoliki Liturgy​—An Elementary Course, kilichotungwa na Maria A. Lombillo Clark, T.D. Mapokeo hayo yanalingana jinsi gani na mambo ambayo Biblia inasema hasa?

[Sanduku]

LITURJIA NENO LA MUNGU

(Kawaida Rasmi ya ibada)

“Sisi tunadhihirisha ibada yetu “Watoto wadogo, jilindeni nafsi kwa Mungu kupitia vitendo vya zenu na sanamu.”—1 Yohana 5:21.​kidini.”

“Mungu ni Roho, nao wamwabuduo imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”​—Yohana 4:24.

“Twaenenda kwa imani, si kwa kuona.”—2 Wakorintho 5:7.

“Mimi ni BWANA [Yehova, NWJ; ndilo jina mfalme huwa ameheshimiwa wakati langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, heshima inapopewa kwa mawaziri wala sitawapa sanamu sifa zangu.”—Isaya 42:8.

“Sisi tunapaswa kufanya vitendo “Usijifanyie sanamu ya

vya kidini kwa Mariamu Bikira kuchonga, wala mfano wa kitu

Mtakatifu Sana, kwa malaika, na cho chote kilicho juu mbinguni,

kwa watakatifu. Lakini vitendo wala kilicho chini duniani. . . [hivyo] vya kidini vya staha Usivisujudie wala kuvitumikia.”

nyingi mno . . . huja kwa Mungu​ ​—Kutoka 20:4, 5.

mwishowe, kwa njia ile ile

ambayo mfalme hua ameheshimiwa “Nami Yohana . . . nalianguka,

wakati heshima inapopewa kwa ili nisujudu mbele ya miguu

mawaziri wake.”​ ya malaika yule . . . Naye

akaniambia, Angalia, usifanye

hivi; . . . sujudie [abudu, NW]

Mungu.”​—Ufunuo 22:8, 8.

“Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu.”​—1 Timotheo 2:5.

“Msalaba hauwezi kukosa kutumiwa “Mungu aliyeufanya ulimwengu

madhabahu; bila huo Misa Takatifu na vitu vyote juu yavilivyomo,

haiwezi kuadhimishwa. Nguo tatu yeye, kwa kuwa ni Bwana wa

za madhabahuni, vitegemeza mbingu na nchi, hakai katika -mishumaa viwili, na tableti za hekalu zilizojengwa kwa kisakramenti vinahitajiwa kabisa mikono.”​—Matendo 17:24. “Sisi pia.”

Sisi tunaweka macho yetu, si juu ya vitu vyenye kuonwa, bali juu ya vitu visivyoonwa.”​—2 Wakorintho 4:18, NW,

“Novemba 1 . . . mwadhimisho wa “Sio wafu wamsifuo BWANA

Siku ya Watakatifu Wote. Hiyo [Yah, NW], wala wo wote

ndiyo Siku Takatifu ya nafsi washukao wote kwenye kimya.” zote zinazoishi kwa furaha ​—Zaburi 115:17.

mbinguni, na ambayo siku moja

itakuwa yetu.” “Wafu hawajui neno lo lote.”

​—Mhubiri 9:5.

“Kila nafsi ambayo haitasikia mnabii huyo itaharibiwa.”​—Matendo 3:23, Douay Version.

“Kwa kusaidia nafsi hizo [Kanisa “Wala kazi, wala kusababu

lili-] anzisha ‘Ukumbuko wa mambo, wala hekima,

waaminifu waliokufa’ uwe siku wala maarifa, havitakuwa katika

ya Novemba 2.  Siku hiyo helo [kuzimu, UV; kaburi, ZSB],

mapadri huadhimisha Misa mara ambako wewe unaharakisha

tatu ili kupunguza mateso ya​ kwenda.”—Mhubiri 9:10, Douay

pargatori ya nafsi hizo zenye Version.

baraka na kuharakisha kuingia

kwazo mbinguni.” “Usitie itibari yako katika

[binadamu;] . . . yeye atarudi “Mambo yanapochanganuliwa ndani ya dunia yake: katika

kabisa, ni wazi kwamba msingi siku hiyo fikira zao zote wa

fundisho la Kikatoliki juu ya zitapotelea mbali.” —Zaburi pargatori ni pokeo, si Andiko 145:2-4, Douay Version. Takatifu.”​—New Catholic

Encyclopedia, Buku 11,

ukurasa 1034.

Wawekwa Huru Kutoka Mapokeo Yenye Madhara

Kwa hiyo mapokeo mengi ya kidini yaliyo maarufu hayafurahishi Mungu na hivyo ni yenye madhara. Ingawa hivyo, kwa kupendeza mtume Paulo aliandika hivi: “Basi nawasifu, kwa sababu . . . katika mambo yote . . . mmeyashika yale mapokeo vile vile kama nilivyowatolea.” (1 Wakorintho 11:2) Hata hivyo, mapokeo hayo yalikuwa ya hali njema, yenye manufaa, yakiwa yametegemezwa juu ya msingi wa Neno la Mungu​—si desturi tupu za kidini, zilizofanyizwa na binadamu. Hayo yalichukua mahali pa ile “namna ya mwenendo usio na matunda uliopokewa kwa njia ya pokeo” ambayo wengi katika karne ya kwanza waliizoea kabla ya kuwa Wakristo.​—1 Petro 1:18, NW.

Vivyo hivyo leo, ni lazima mtu mcha Mungu achunguze sana na kukataa pokeo lolote linalothibitika kuwa lisilo la Kimaandiko. Kwa uhakika, uhusiano wa mtu pamoja na Mungu ni wa thamani kubwa sana kuliko namna zozote za ibada zilizofanyizwa na binadamu! Bila shaka, si rahisi hata kidogo kukataa mapokeo yasiyo ya Kimaandiko. Mara nyingi hiyo inataka kurekebisha violezo vya mwenendo ambavyo vimeimarika kwa muda mrefu. Mathalani, mwanamume mmoja kijana katika Kolombia alikuwa amekolea sana katika pokeo la kidini. Kuanzia utotoni yeye alikuwa amekuwa akiwaka tamaa ya kuwa padri Mkatoliki. Mara nyingi angeigiza-igiza ‘usemaji wa Misa’ akiwa pamoja na dada zake, hata kupokea “maungamo” kutoka kwao. Miaka kadhaa baadaye aliweza kuingia shule ya utangulizi wa seminari, mwishowe akijiandikisha katika chuo kikuu cha Kikatoliki. Akiwa huko, mapokeo ya kidini yakatia mizizi maishani mwake kwa kina kirefu hata zaidi.

Siku moja, mmoja wa Mashahidi wa Yehova alizuru maskani yake. Ingawa ilikuwa vigumu sana wazazi wake kuruhusu Shahidi huyo ajieleze, machache yaliyosemwa yalivutia kijana huyo mwenye fikira za kidini. Baadaye yeye alipanga kujifunza Biblia kwa siri pamoja na Shahidi huyo. “Tamaa yangu halisi,” yeye anakumbuka, “ilikuwa kupata kujua Biblia kwa rai ya upande tofauti bila kubadili dini yangu. Mimi nilikuwa na tamaa kubwa sana ya kutumikia Mungu nikiwa padri, kujaribu kufanyiza mabadiliko katika mioyo ya watu. Baada ya kujifunza Biblia kwa mwezi mmoja, hitilafiano lilitokea ndani yangu, kwa kuwa mapokeo na desturi za ibada za dini yangu zilipigana na viwango vyenye kutakata vya Maandiko.”

Jamaa yake ilimbana aache kujifunza Biblia, na mwishowe akalazimishwa kuondoka kwenye maskani yao. Hata hivyo, yeye anasema hivi: “Baada ya miezi miwili ya kujifunza Biblia, mimi nilisadiki kwamba nilikuwa katika ukosaji mkubwa, nami nikaacha chuo kikuu na kazi yangu ya mwalimu katika koleji ya kidini na kujitoa kwa bidii nihubiri nyumba kwa nyumba. Sasa maisha yangu yamebadilika na pia desturi zangu. Nilihisi furaha ya pekee siku ile isiyosahaulika nilipoonyesha wakfu wangu kwa Yehova kwa kubatizwa.” Mwanamume huyu kijana sasa anatumikia wakati wote katika kusaidia wengine wajiondoe katika mapokeo yenye kuvunjia Mungu heshima.

Ikiwa wewe unafuata pokeo la kidini kwa bidii nyingi sana, huenda wewe pia ukapata kwamba unahitajiwa kabisa kufanya mabadiliko fulani. Kumbuka tena yale ambayo wakati mmoja Yesu alisema kwa mwanamke Msamaria kisimani. Mwanamke huyo na watu wake walikuwa na ile desturi iliyokuwa imekuwako muda mrefu ya kuabudu Mungu katika Mlima Gerizimu. Hata hivyo, Yesu alimwonyesha kwamba hilo lilikuwa pokeo la bure tu, akisema hivi: “Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu. . . . Waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.”​—Yohana 4:19-23.

Je! wewe ni mmoja ambaye ‘Baba anatafuta’? Je! wewe una tamaa inayowaka ya kutaka kuabudu Mungu katika ukweli? Basi onyo la mtume Paulo kwenye Wakolosai 2:8 linafaa sana: “Jihadharini msiache mtu yeyote awahadae nyinyi kwa mafunzo yake ya kifalsafa, kwa misisimuko mitupu iliyochotwa kutokana na pokeo la kibinadamu.” (The Holy Bible, Ronald A. Knox) Badala ya hivyo, wewe fuata mafundisho ya Ukristo wa kweli, yanayoweza kukuongoza kwenye uhai wa milele!—Yohana 17:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki