Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti
Yehova Abariki Udumifu
MASHAHIDI WA YEHOVA wanahisi upendo wenye kina kirefu kwa Yehova Mungu na daraka kwa mwanadamu mwenzao, hiyo ikiwasukuma wajaribu kumpa kila mmoja fursa ya kusikia habari njema za Ufalme wa Mungu. (Mathayo 24:14) Hiyo ndiyo sababu dada mmoja alipiga moyo konde kuhubiria askari na jamaa zao kwenye uwanja wa kijeshi katika eneo lake.
Kila mara alipojaribu, kapteni mwenye kuchunga mahali hapo alimnyima ruhusa ya kuingia. Dada anasimulia hivi: “Kwa hiyo nikaamua kumwona ofisa mwenye amri, ambaye ni kanali. Nilipopigia simu mwandishi wake, mwanamume huyo alikataa kupitisha simu hiyo kwa kanali yule. Mimi nikapanga kuzuru kanali huyo kwenye maskani yake, kwa maana aliishi mbali na makao hayo ya askari. Nilipofanya hivyo, yeye aliniuliza mimi nilikuwa mtu wa kutoka wapi. Kwa nasibu, mimi nilizaliwa katika kisiwa kidogo kilicho kikuu zaidi katika Fiji. Kwa kunistahi alisikiliza ombi langu na akasema alikuwa amekwisha kusikia juu ya Mashahidi wa Yehova lakini hakuwa ameelezwa juu ya kazi yetu. Hiyo ilinipa fursa nzuri ajabu ya kumtolea ushuhuda, naye akakubali kutoka kwangu misaada mitatu ya kujifunzia Biblia. Aliniambia niwe kwenye ofisi yake kwenye makao ya askari saa 3:00 asubuhi. Dada mwingine na mimi tulipowasili huko, walinzi walikuwa wamekwisha kuelezwa juu ya ziara yetu na wakatuambia kwamba sisi tulipewa ruhusa ya kuhubiri katika uwanja huo. Amiri wa walinzi akasema: ‘Sasa mimi ninaarifu maofisa wote ya kwamba nyinyi mwe mkifunguliwa wazi milango yote siku ya Ijumaa, na hata ingawa sisi sote tuna dini tofauti-tofauti, yenu ingeweza kuwa ndiyo ile moja ya kuvumisha onyo la Ufalme wa mbinguni na mwisho wa ulimwengu.’
“Tulipowasili siku ya Ijumaa,” dada huyo anaendelea kusema, “gari la kijeshi la uvumishaji habari likapita katika kambi hiyo likitangaza hivi: ‘Wanawake wawili wa umri mkubwa watakuwa kambini wakiwavumishia nyinyi onyo, kwa hiyo tafadhali fungueni milango yenu na kuwasikiliza. Jiepusheni na kubishana nao au kufanyiza uhasama.’ Sisi tulifanya kazi katika kambi hiyo kuanzia saa 2:30 asubuhi hadi saa 11:00 jioni, tukiangusha vitabu 100 na magazeti 200. Na tokeo likawa nini? Ziara nyingi za kurudia zimefanywa na mafunzo mengi ya Biblia yakaanzwa.”
Ono la kupendeza linatoka kwenye kisiwa kingine katika Pasifiki ya Kusini ambacho hivi majuzi kiliifungulia kazi ya kuhubiri yenye kufanywa na mapainia wa pekee. Hao mapainia wa pekee wanapingwa na viongozi wa Kanisa United. Wakati wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko, wao walipata ugumu wa kufanya ziara ya kurudia, kwa kuwa chifu wa kijiji, kwa kutolewa uvutano na viongozi wa kanisa hilo, alikataa kuruhusu Mashahidi wa Yehova kuingia kijijini. Walipowasili, chifu huyo hakuwako, kwa hiyo mtu yule mwenye kupendezwa akatembelewa, na ushuhuda bora ukatolewa. Walipokuwa wakiondoka, mtumbwi mkubwa ulionwa ukikaribia, na ni wazi ulikuwa na matatizo ya enjini, kwa kuwa watu walikuwa wakipiga makasia. Ndiyo, alikuwa ni yule chifu wa kijiji akiwasili kwa kuchelewa mno asiweze kuzuia hiyo ziara ya kurudia. Waliporudi kwenye maskani yao, mapainia walimwambia mwangalizi wa mzunguko kwa lugha ya kuvunja: “Mimi iko pikiri malaika navunja injin ya mtu hiyo.”
Kwa hiyo Yehova alibariki udumifu wa ndugu hao katika kutii amri ya kuhubiri “habari njema hizi za ufalme.”