Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 2/1 kur. 10-15
  • Maagano Yanayohusisha Kusudi la Milele la Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maagano Yanayohusisha Kusudi la Milele la Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Agano la Kiabrahamu​—Msingi wa Baraka za Milele
  • Mbegu ya Kiroho ya Abrahamu
  • Agano la Sheria Laongezewa kwa Muda Tu
  • Agano la Ufalme wa Kidaudi
  • Wewe Utanufaika na Maagano ya Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Baraka Kubwa Zaidi Kupitia Agano Jipya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Yehova ni Mungu wa Maagano
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Agano la Mungu Pamoja na “Rafiki” Yake Tayari Lafaidi Mamilioni
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 2/1 kur. 10-15

Maagano Yanayohusisha Kusudi la Milele la Mungu

“Yehova . . . amekumbuka agano lake hata kwa wakati usio dhahiri, neno lile ambalo yeye aliamuru, mpaka vizazi elfu moja.”​—ZABURI 105:7, 8, NW.

1, 2. Kwa nini tunaweza kusema kwamba walio wengi kati yetu wameathiriwa na agano fulani?

INAELEKEA sana kwamba agano fulani limekuathiri wewe​—wakati wako uliopita, wakati wako uliopo, na wakati wako ujao. ‘Agano gani?’ huenda wewe ukataka kujua. Katika kisa hiki, ni ndoa, kwa maana walio wengi kati yetu ni wazao wa ndoa fulani na wengi wetu tumefunga ndoa sisi wenyewe. Hata wale ambao hawajafunga ndoa huenda wakati ujao wakafikiria baraka za kuwa na ndoa yenye furaha.

2 Karne kadhaa zilizopita mnabii Mwebrania Malaki aliandika juu ya “mke wa ujana wako,” “mwenzako, na mke wa agano lako.” (Malaki 2:14-16) Yeye angeweza kuita ndoa agano, kwa maana huo ni mkataba au afikiano rasmi, mpango ulio kati ya huyu na huyu ili kufanya jambo kwa uungano. Patano la ndoa ni agano kati ya watu wawili ambamo wao wanaafikiana kuwa mume na mke, wakikubali kuwa na wajibu mbalimbali kwa mmoja na mwenzake na kutazamia manufaa za kudumu.

3. Kwa nini huenda maagano mengine yakatuathiri kwa kadiri kubwa kuliko ndoa?

3 Huenda ndoa ikaonekana kana kwamba ndilo agano lenye umaana mkubwa zaidi wa kibinafsi juu yetu, na hata hivyo Biblia inazungumzia maagano ya umaana mpana zaidi. Kwa kutofautisha maagano ya Kibiblia pamoja na yale ya dini zisizo za Kibiblia, ensaiklopedia moja inasema kwamba ni katika Biblia tu kwamba “mpango huu wa uhusiano kati ya Mungu na watu wake unakuwa mfumo wenye mambo mengi ambao hatimaye utahusisha ndani watu wote.” Ndiyo, maagano hayo yanahusisha ndani kusudi la milele la Muumba wetu mwenye upendo. Kama utakavyoona, kupokea kwako baraka zisizoelezeka kuna ufungamano na maagano hayo. ‘Lakini jinsi gani hivyo?’ huenda wewe ukawa na sababu ya kuuliza.

4. Ni agano gani la kwanza-kwanza linaloelekeza kwenye kusudi la milele la Mungu?

4 Wewe una habari sana juu ya msiba uliotokea wakati Adamu na Hawa walipokataa mamlaka ya Mungu. Sisi tulirithi kutokamilika kutoka kwao, na uhakika huo ndio unaoleta magonjwa ambayo yametutesa, yanayoongoza kwenye kifo. (Mwanzo 3:1-6, 14-19) Hata hivyo, tunaweza kushukuru kwamba dhambi yao haingeweza kuondosha kando kusudi la Mungu la kujaza dunia waabudu wa kweli wenye shangwe ya kuwa na afya na furaha ya kudumu. Kuhusiana na hilo, Yehova alifanyiza agano lile lililoandikwa kwenye Mwanzo 3:15, NW; “Na mimi nitaweka uadui kati yako na mwanamke na kati ya mbegu [uzao, UV] yako na mbegu yake. Yeye atachubua wewe kichwani na wewe utachubua yeye kisiginoni.” Hata hivyo, ufupi na usemi wa mfano wa taarifa hiyo uliacha maswali mengi bila kujibiwa. Yehova angetimizaje ahadi hiyo ya agano?

5, 6. (a) Mungu aliamua kutumia njia gani katika kufanyiza hatua-hatua za kutimiza kusudi lake? (b) Kwa nini inatupasa tupendezwe kujua njia ya Mungu ya kufanya hivyo?

5 Mungu alizidi na kupangia mfululizo hususa wa maagano ya kimungu, ambayo, yakiwa pamoja na lile agano la Kiedeni, yanajumlika kuwa saba. Kila mmoja wetu anayetumainia kuona shangwe ya baraka za milele anapaswa kuelewa maagano hayo. Hiyo ni kutia ndani kujua ni wakati gani na jinsi gani yalifanyizwa, ni nani waliohusika, malengo au masharti yayo yalikuwa nini, na ni jinsi gani maagano hayo yanavyohusiana yenyewe kwa yenyewe katika kusudi la Mungu la kubariki aina ya binadamu yenye utii kwa kuipa uhai wa milele. Huu ni wakati unaofaa kuyapitia maagano hayo, kwa maana siku ya Machi 22, 1989, makundi ya Wakristo yatakutanika kukumbuka Mlo wa Jioni wa Bwana, unaohusisha ndani maagano hayo moja kwa moja.

6 Bila shaka, kwa watu fulani huenda wazo la maagano likasikika kuwa lisilo na ladha, kuwa ni mambo ya kisheria tu, yasiyo na upendezi wa kibinadamu. Ingawa hivyo, fikiria vile Theological Dictionary of the Old Testament inavyosema: “Maneno ya kusema ‘agano’ katika Mashariki ya Karibu wakati wa kale na pia katika ulimwengu wa Kigiriki na wa Kiroma . . . hufanyiwa matumizi mbalimbali kulingana na maana mbili: kwa upande mmoja kiapo na kujikabidhi katika wajibu, kwa upande mwingine upendo na urafiki.” Sisi tunaweza kuona pande zote mbili​—kiapo na urafiki—​kuwa ndio msingi hasa wa maagano ya Yehova.

Agano la Kiabrahamu​—Msingi wa Baraka za Milele

7, 8. Ni agano la namna gani ambalo Yehova alifanya pamoja na Abrahamu? (1 Mambo ya Nyakati 16:15, 16)

7 Abrahamu mzee wa ukoo, “baba ya wote walio na imani,” alikuwa “rafiki ya Yehova.” (Warumi 4:11; Yakobo 2:21-23, NW) Mungu alimwapia kwa apizo zito, akiweka wazi agano lililo msingi wa kupokea kwetu baraka za milele.​—Waebrania 6:13-18.

8 Abrahamu alipokuwa katika Uru, Yehova alimwambia ahamie bara jingine, nalo likawa ni Kanaani. Wakati huo Yehova alimwahidi hivi Abrahamu: “Mimi nitafanyiza taifa kubwa kutoka kwa wewe na nitakubariki wewe na nitafanya jina lako kuwa kuu; . . . na jamaa zote za nchi kwa uhakika zitajibarikia zenyewe kupitia wewe.”a (Mwanzo 12:1-3, NW) Baada ya hapo, pole kwa pole Mungu aliongeza mambo mengine mengi kwenye lile ambalo kwa kufaa tunalinena kuwa agano la Kiabrahamu: mbegu ya Abrahamu, au mrithi, ingerithi lile Bara Lililoahidiwa; mbegu yake ingeongoza kwenye wazao wasiohesabika; Abrahamu na Sara wangekuwa ndicho chanzo cha wafalme.​—Mwanzo 13:14-17; 15:4-6; 17:1-8, 16, NW; Zaburi 105:8-10.

9. Tunajuaje kwamba sisi tunaweza kuhusika katika agano la Kiabrahamu?

9 Mungu aliliita “agano langu kati ya mimi na wewe [Abrahamu].” (Mwanzo 17:2) Lakini kwa uhakika sisi tunapaswa kuhisi kwamba maisha zetu zinahusika ndani, kwa maana baadaye Mungu alipanua habari za agano hilo, akitaarifu hivi: “Kwa uhakika mimi nitakubariki wewe na kwa uhakika nitazidisha mbegu [uzao, UV] yako kama nyota za mbingu na kama punje za mchanga zilizo juu ya ufuo wa bahari; na mbegu yako itamiliki lango la adui zake. Na kupitia mbegu yako mataifa yote ya dunia kwa uhakika yatajibarikia yenyewe.” (Mwanzo 22:17, 18, NW) Sisi ni sehemu ya mataifa hayo; tunaweza kupata baraka fulani iliyo akibani.

10. Ni nini miono-ndani ambayo tunapata kutokana na agano lililofanywa pamoja na Abrahamu?

10 Acheni tutue kidogo tufikirie tunayoweza kujifunza kutokana na agano la Kiabrahamu. Kama lile agano la Kiedeni lililokuwa kabla, hili linaelekeza kwenye kuja kwa “mbegu” fulani, hivyo likidokeza kwamba mbegu hiyo ingekuwa na ukoo wa kibinadamu. (Mwanzo 3:15, NW) Ukoo huo ungekuwa katika mstari wa Shemu, kuteremka mpaka kwa Abrahamu, na kupitia Isaka mwana wake. Mstari huo ungehusisha ndani umaliki, na kwa njia fulani ungewezesha kuwe na baraka si kwa jamaa moja tu bali wanadamu wa mabara yote. Agano hilo lilitimizwaje?

11. Utimizo halisi wa agano la Kiabrahamu ulitukiaje?

11 Watu wa ukoo wa Abrahamu kupitia Yakobo, au Israeli, walizidika wakawa taifa kubwa. Wakiwa ni mbegu halisi ya Abrahamu isiyo na hesabu, wao walikuwa wakfu kwa ibada yenye kutakata ya Mungu wa Abrahamu, Isaka, na Yakobo. (Mwanzo 28:13; Kutoka 3:6, 15; 6:3; Matendo 3:13) Mara nyingi Waisraeli waligeuka kutoka kwenye ibada yenye kutakata, hata hivyo “Yehova aliwaonyesha upendeleo na akawa na rehema juu yao . . . kwa ajili ya agano lake pamoja na Abrahamu, Isaka na Yakobo; naye hakutaka kuwaleta kwenye angamizo.” (2 Wafalme 13:23; Kutoka 2:24; Walawi 26:42-45) Hata baada ya Mungu kukubali kundi la Kikristo liwe watu wake, kwa muda fulani yeye aliendelea kuonyesha upendeleo wa pekee kwa Waisraeli wakiwa kikundi cha watu waliokuwa mbegu halisi ya Abrahamu.​—Danieli 9:27.

Mbegu ya Kiroho ya Abrahamu

12, 13. Yesu alithibitikaje kuwa sehemu ya kwanza ya ile mbegu katika utimizo wa kiroho wa agano la Kiabrahamu?

12 Agano la Kiabrahamu lilikuwa na utimizo mwingine, wa kiroho. Ni wazi kwamba utimizo huo mkubwa zaidi usingalikuwa wa kabla ya wakati wa Yesu, lakini sisi tunaweza kufurahi kwamba unaeleweka wazi katika wakati wetu. Sisi tuna maelezo juu ya utimizo huo katika Neno la Mungu. Paulo anaandika hivi: “Lakini kwa Abrahamu ahadi zilisemwa, na kwa uzao [mbegu, NW] wake. Hasemi wazao kama wengi, ila kama mumoja, muzao wake ndiye Kristo.”​—Wagalatia 3:16, ZSB.

13 Ndiyo, mbegu huyo angekuja kupitia mstari mmoja tu, au jamaa, na ndivyo ilivyokuwa kuhusu Yesu, aliyezaliwa akiwa Myahudi wa kiasili, mtu wa ukoo halisi wa Abrahamu. (Mathayo 1:1-16; Luka 3:23-34) Kwa kuongezea, yeye alikuwa sehemu ya jamaa ya Abrahamu Mkubwa Zaidi mbinguni. Kumbuka kwamba Abrahamu mzee wa ukoo alikuwa amekuwa na nia ya kudhabihu Isaka mwana wake akiwa na imani ya kina kirefu ikiwa Mungu alitaka hivyo. (Mwanzo 22:1-18; Waebrania 11:17-19) Vivyo hivyo, Yehova alituma Mwana wake mzaliwa wa pekee aje duniani kuwa dhabihu ya ukombozi kwa aina ya binadamu yenye kuitikadi. (Warumi 5:8; 8:32) Hivyo inaeleweka ni kwa nini Paulo alitambulisha Yesu Kristo kuwa sehemu iliyo kuu ya mbegu ya Abrahamu kulingana na agano hilo.

14. Sehemu ya pili ya mbegu ya Abrahamu ni nini, na hiyo inaongoza kwenye zungumzo gani zaidi?

14 Paulo aliendelea kuonyesha kwamba Mungu ‘angezidisha mbegu ya Abrahamu’ katika utimizo wa kiroho. Aliandika hivi: “Ikiwa nyinyi ni wa Kristo, kweli kweli nyinyi ni mbegu ya Abrahamu, warithi kuhusiana na ahadi.” (Mwanzo 22:17; Wagalatia 3:29, NW) Hao ni wale Wakristo wapakwa-mafuta 144,000 wanaofanyika sehemu ya pili ya mbegu ya Abrahamu. Wao hawamo katika upinzani kwa ile sehemu ya kwanza ya mbegu hiyo bali “ni wa Kristo.” (1 Wakorintho 1:2; 15:23) Tunajua kwamba wengi wao hawawezi kufuatisha ukoo wao kwa kuurudisha nyuma mpaka kwa Abrahamu, kwa maana wao ni wa kutoka mataifa yasiyo ya Kiyahudi. Ingawa hivyo, lililo la maana zaidi katika utimizo wa kiroho ni kwamba wao si sehemu ya kiasili ya jamaa ya Abrahamu Mkubwa Zaidi, Yehova; bali, wao wametoka kwenye jamaa isiyokamilika ya Adamu mtenda dhambi. Kwa hiyo tutahitaji kuona kutokana na maagano ya baadaye jinsi wao wanavyostahili kuwa sehemu ya “mbegu ya Abrahamu.”

Agano la Sheria Laongezewa kwa Muda Tu

15-17. (a) Kwa nini agano la Sheria liliongezwa kwenye agano la Kiabrahamu? (b) Sheria ilitimizaje malengo hayo?

15 Baada ya Mungu kufanyiza agano la Kiabrahamu likiwa hatua ya msingi kuelekea kutimiza kusudi lake, mstari wa kutokea kwa yule aliye Mbegu ungepewaje himaya usichafuliwe au kukomeshwa kabisa mpaka ufike wakati wa kutokea kwa huyo? Mbegu huyo alipowasili, waabudu wa kweli wangeweza kumtambuaje? Paulo anajibu maswali hayo kwa kuonyesha wazi hekima ya Mungu katika kuongezea agano la Sheria (Torati) kwa muda tu. Mtume anaandika hivi:

16 “Torati ni [ya] nini basi? Iliingizwa kwa sababu ya makosa, hata aje huyo mzao [mbegu, NW] aliyepewa ile ahadi; iliamriwa kwa utumishi wa malaika kwa mkono wa mjumbe [mpatanishi, NW]. . . . Torati imekuwa kiongozi [mwalimu-mwelekezaji, AW] kutuleta kwa Kristo, ili tuhesabiwe haki [uadilifu, NW] kwa imani.”​—Wagalatia 3:19, 24.

17 Kwenye Mlima Sinai, Yehova alifanyiza agano la kitaifa lisilo na kifani kati yake mwenyewe na Israeli​—agano la Sheria (Torati), Musa akiwa ndiye mpatanishi walo.b (Wagalatia 4:24, 25) Watu waliafikiana kuwa katika agano hilo, nalo likahalalishwa kwa damu ya mafahali na mbuzi. (Kutoka 24:3-8; Waebrania 9:19, 20) Liliwapa Israeli sheria za kitheokrasi na mpangilio wa kuwa na serikali ya uadilifu. Agano hilo lilikataza kufunga ndoa pamoja na wapagani au kushiriki katika mazoea ya ukosefu wa adili na ya dini bandia. Hivyo lililinda Waisraeli na lilikuwa kani ya kuudumisha bila kuchafuliwa mstari wa yule mbegu. (Kutoka 20:4-6; 34:12-16) Lakini kwa kuwa hakuna Mwisraeli yeyote asiyekamilika angeweza kushika Sheria hiyo kwa ukamili, ilifanya dhambi zidhihirike. (Wagalatia 3:19) Pia ilionyesha uhitaji wa kuhani mkamilifu aliye wa kudumu, na wa kuwa na dhabihu ambayo haingehitaji kurudiwa kila mwaka. Sheria hiyo ilikuwa kama mwalimu-mwelekezaji aliyeongoza mtoto kwa mkufunzi aliyehitajiwa, ambaye angekuwa ndiye Mesiya, au Kristo. (Waebrania 7:26-28; 9:9, 16-22; 10:1-4, 11) Agano la Sheria lingekoma likiisha kutimiza kusudi lalo.​—Wagalatia 3:24, 25; Warumi 7:6; ona “Maswali Kutoka kwa Wasomaji,” ukurasa 31.

18. Ni tazamio gani zaidi lililohusiana na agano la Sheria, lakini kwa nini ilikuwa vigumu kuelewa jambo hilo?

18 Alipokuwa akifanyiza agano hilo la muda tu, Mungu alitaja pia lengo hili la kusisimua: “Ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu [mali ya pekee, NW] kwangu . . . nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.” (Kutoka 19:5, 6) Lo, ni tazamio lililoje! Taifa la wafalme-makuhani. Lakini, ingewezaje kuwa hivyo? Kama vile Sheria ilivyosema wazi baadaye, kabila lenye kutawala (Yuda) na kabila la kikuhani (Lawi) yalipewa madaraka tofauti-tofauti. (Mwanzo 49:10; Kutoka 28:43; Hesabu 3:5-13) Hakuna mtu ambaye angeweza kuwa mtawala wa kiraia na kuwa kuhani pia. Hata hivyo, maneno ya Mungu kwenye Kutoka 19:5, 6 yalitoa sababu ya kuitikadi kwamba kwa njia fulani isiyofunuliwa wazi, wale walio katika agano la Sheria wangekuwa na fursa ya kuandaa washiriki wa “ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.”

Agano la Ufalme wa Kidaudi

19. Ilionyeshwaje katika maagano hayo kwamba kungekuwa na umaliki?

19 Baada ya muda Yehova aliongezea agano jingine lililozidi kuelewesha wazi jinsi yeye angetimiza kusudi lake, kwa baraka yetu ya milele. Tumeona kwamba agano la Kiabrahamu lilielekeza mbele kwenye umaliki miongoni mwa mbegu halisi ya Abrahamu. (Mwanzo 17:6) Agano la Sheria pia lilitazamia wafalme miongoni mwa watu wa Mungu, kwa maana Musa aliambia Israeli hivi: “Utakapokwisha kuingia katika [Bara Lililoahidiwa], nawe utakaposema, Nitaweka mfalme juu yangu, mfano wa mataifa yote yaliyo kandokando yangu; usiache kumweka yule atakayechaguliwa na BWANA [Yehova, NW], Mungu wako, awe mfalme juu yako; . . . usimtawaze mgeni juu yako.” (Kumbukumbu 17:14, 15) Mungu angepangiaje umaliki huo, nao ungehusuje agano la Kiabrahamu?

20. Daudi na mstari wake walikujaje kuhusika ndani?

20 Ingawa mfalme wa kwanza wa Israeli alikuwa Sauli wa kabila la Benyamini, yeye alifuatwa na Daudi wa Yuda aliye shujaa na mshikamanifu. (1 Samweli 8:5; 9:1, 2; 10:1; 16:1, 13) Baada ya muda kusonga sana katika utawala wa Daudi, Yehova alichagua kufanya agano pamoja na Daudi. Kwanza Yeye alisema: “Nitainua mzao [mbegu, AW] wako nyuma yako, atakayetoka viunoni mwako, nami nitaufanya imara ufalme wake. Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa jina langu, nacho kiti cha enzi cha ufalme wake nitakifanya imara milele [mpaka wakati usio dhahiri, NW]” (2 Samweli 7:12, 13) Kama ilivyoonyeshwa hapo, Sulemani mwana wa Daudi akawa mfalme aliyefuata, naye alitumiwa kumjengea Mungu nyumba, au hekalu, katika Yerusalemu. Hata hivyo, kulikuwa na mengi zaidi ya hilo.

21. Agano la Ufalme wa Kidaudi lilifanya uandalizi kwa jambo gani?

21 Yehova aliendelea kufanya agano hili pamoja na Daudi: “Nyumba yako, na ufalme wako, vitathibitishwa milele [mpaka wakati usio dhahiri, NW] mbele yako. Nacho kiti chako kitafanywa imara milele [mpaka wakati usio dhahiri, NW].” (2 Samweli 7:16) Ni wazi kwamba kwa njia hiyo Mungu alikuwa akisimamishia Israeli nasaba ya kifalme katika jamaa ya Daudi. Haingekuwa mfuatanofuatano wa daima tu wa wafalme wa Kidaudi. Mwishowe, mtu fulani katika mstari wa Daudi angekuja kutawala “mpaka wakati usiojulikana, na kiti cha ufalme wake [kingekuwa] kama jua mbele za [Mungu].”​—Zaburi 89:20, 29, 34-36; Isaya 55:3, 4, NW.

22. Agano lililofanywa pamoja na Daudi lilihusianaje na mstari wa yule Mbegu, na tokeo likiwa nini?

22 Basi, ithibati inaonyesha kwamba agano la Kidaudi lilifanya mstari wa kutokea kwa yule Mbegu uzidi kuwa mwembamba. Hata Wayahudi wa karne ya kwanza waling’amua kwamba Mesiya angepaswa kuwa mtu wa ukoo wa Daudi. (Yohana 7:41, 42) Yesu Kristo, sehemu ile ya kwanza ya mbegu ya agano la Kiabrahamu, alistahili kuwa Mrithi wa kudumu wa Ufalme huu wa Kidaudi, kama vile malaika mmoja alivyoshuhudiza. (Luka 1:31-33) Hivyo Yesu alipata haki ya kutawala juu ya Bara Lililoahidiwa, ile milki ya kidunia ambayo Daudi alikuwa ametawala. Jambo hilo linapasa kuongeza uhakika wetu katika Yesu; yeye anatawala, si kwa unyakuzi ambao ni haramu kisheria, bali kupitia mpango uliosimamishwa kisheria, agano la kimungu.

23. Ni maswali na mambo gani yanayobakia kutafutiwa jibu?

23 Tumefikiria manne tu ya maagano ya kimungu yanayohusu jinsi Mungu alivyopanga kutimiza kusudi lake la kuletea aina ya binadamu baraka za milele. Inaelekea kwamba wewe unaweza kuona kwamba picha yenyewe haijakamilika. Maswali yanabaki: Kwa sababu wanadamu waliendelea kuwa wasiokamilika, ni kuhani au dhabihu gani ambayo ingeweza kubadili daima jambo hilo? Wanadamu wangestahilije kuwa sehemu ya mbegu ya Abrahamu? Je! kuna sababu ya kuitikadi kwamba haki ya kutawala ingepanuka itie ndani eneo ambalo ni zaidi ya lile la kidunia tu? Ni jinsi gani mbegu ya Abrahamu, ile ya kwanza na ile ya pili pia, ingeweza kuleta baraka kwa “Mataifa yote ya dunia,” kutia na kila mmoja wetu? Acheni tuone.

[Maelezo ya Chini]

a Hili ni agano lenye kuhusisha upande mmoja tu, kwa kuwa ni mtu mmoja tu (Mungu) aliyejikabidhi wajibu wa kutekeleza masharti yalo.

b “Wazo la kufanya maagano lilikuwa sehemu maalumu ya dini ya Israeli, ikiwa ndiyo dini ya pekee iliyodai ushikamanifu kwa kitu kimoja tu na kuzuia uwezekano wa kuonyesha ushikamanifu kwa vitu viwili au vingi kama ule ulioruhusiwa katika dini nyinginezo.”​—Theological Dictionary of the Old Testament, Buku 2, ukurasa 278.

Jibu lako Ni Nini

◻ Agano la Kiabrahamu liliwekaje msingi wa kupokea kwetu baraka za milele?

◻ Mbegu halisi, ya kimnofu, ya Abrahamu ilikuwa nini? Na mbegu ya mfano?

◻ Kwa nini agano la Sheria liliongezwa kwenye agano la Kiabrahamu?

◻ Ni jinsi gani agano la Ufalme wa Kidaudi lilivyosogeza mbele kusudi la Mungu?

[Mchoro katika ukurasa wa 13]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Agano la Kiedeni Mwanzo 3:15

Agano la Kiabrahamu

Mbegu ya Kwanza

Mbegu va Pili

Baraka za Milele

[Mchoro katika ukurasa wa 14]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Agano la Kiedeni Mwanzo 3:15

Agano la Kiabrahamu

Agano la Sheria

Agano la Ufalme wa Kidaudl

Mbegu ya Kwanza

Mbegu ya Pili

Baraka za Milele

[Picha katika ukurasa 10]

Ili afanyize hatua-hatua za kutimiza kusudi lake kwa ajili ya aina ya binadamu, Mungu alifanya agano pamoja na Abrahamu mwaminifu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki