Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 4/1 kur. 7-9
  • Babuloni—Kitovu cha Ibada Bandia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Babuloni—Kitovu cha Ibada Bandia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Babuloni​—Adui Mfidhuli wa Ibada ya Kweli
  • Babuloni Alaumiwa Wazi na Kuaibishwa
  • Babuloni Mkubwa—Kaanguka na Kuhukumiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Jiji Kubwa Lateketezwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Babiloni Mkubwa Ni Nani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • “Yule Kahaba Mkuu” Akaribia Kuuawa Kwake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 4/1 kur. 7-9

Babuloni​—Kitovu cha Ibada Bandia

“AMEANGUKA! Babuloni ameanguka, na mifano yote ya kuchongwa ya miungu yake yeye ameivunja mpaka kwenye ardhi!” Babuloni ambao Isaya aliusema kwa unabii ulikuwa jiji la aina gani? Hicho ni kidokezi muhimu ili sisi tuelewe umaana wa Babuloni Mkubwa wa ki-siku-hizi.​—Isaya 21:9, NW.

Babuloni ya kale ilijulikana kwa ibada yayo ya miungu na miungu-wake wa kipagani. Katika kitabu chake Babylonian and Assyrian Religion, Profesa S. H. Hooke anataarifu hivi: “Babuloni ndilo jiji ambako Marduki alikuwa na cheo kikuu miongoni mwa miungu mingine iliyoabudiwa huko. . . . Katika Babuloni wakati wa Nebukadreza 2 kulikuwa na mahekalu yasiyopungua hamsini na manane [58] ya miungu iliyotajwa wazi, licha ya mahekalu mengine mengi asiyogawiwa mungu yeyote. Kwa sababu hiyo inaweza kuonwa kwamba ni lazima jamii ya makuhani iwe ilihusika sana katika maisha ya jiji kubwa hivyo.” Inasemwa kwamba hekalu la Marduki katika Babuloni lilikuwa na vihekalu 55 vya kandokando. Hiyo inakumbusha kama nini juu ya mahekalu, makanisa, na makathedro mengi ya leo yaliyo na vikanisa vya kandokando kwa ajili ya miungu midogo zaidi, watakatifu, na sanamu Madonna (Bikira Maria) zilizo za cheo kidogo!

Babuloni kilikuwa kitovu cha sanamu katika ibada ya miungu. Usimulizi mmoja unataarifu kwamba makuhani na waaminifu “walikuwa wakielekeza fikira nyingi juu ya mifano yao mitakatifu, wakiziona sanamu hizo kuwa vipitio vya kuwasiliana na miungu. Sanamu hizo zilifunikwa kwa mavazi ya bei kubwa, zikapambwa kwa mikufu, vikuku, na pete; zilipumzika juu ya vitanda vya gharama kubwa na zilipelekwa nje kwa kuinuliwa juu na andamano la watu walioenda wakikanyaga ardhi na maji kwa miguu, zikiwa katika magari ya kuzibebea na mashua za matumizi ya kibinafsi.”a Hiyo inafanana kama nini na ibada inayopewa kwa miungu, watakatifu, na Madonna katika Uhindu wa ki-siku-hizi, Ubuddha, na Ukatoliki, ambamo wanapitisha mifano yao jinsi hiyo hiyo katika mabarabara na katika mito na bahari!

Kwa kutoa kielelezo zaidi cha ulinganifu kati ya Babuloni ya kale na dini ya ki-siku-hizi, fikiria elezo lifuatalo lililotolewa katika ensaiklopedia iyo hiyo: “Waitikadi wake waaminifu humwita majina mazuri kweli kweli: Si kwamba tu yeye ni mungu-mke na bibi mheshimiwa tu bali pia ni mama mwenye rehema, yeye ambaye husikiliza sala, yeye ambaye huombea watu . . . yeye ambaye ameupa uhai ulimwengu wote mzima na wanadamu.” Linganisha hilo na sala ifuatayo kutoka El Santo Rosario (Tasbihi Takatifu): “Tunakupa shukrani, Binti-Mfalme Mwenyezi, kwa mapendeleo tunayopokea kila siku kutoka mkono wako wenye hisani; uwe mwenye fadhili sana, Bibi Mheshimiwa, hata utupokee sasa na milele chini ya ulinzi na kinga yako.”

Elezo na sala hiyo ni kuhusu nani? Wengi watakata shauri mara hiyo kwamba ni “Bikira Maria.” Hilo ni jibu sawa lakini si kabisa. Sala yenyewe hutolewa kwa Maria. Hata hivyo, kama tunavyojulishwa na Las Grandes Religiones Ilustradas, maneno yaliyonukuliwa kwanza yanaeleza juu ya Ishtari, yule “Bibi wa Upendo,” mungu-mke Mbabuloni wa nguvu za uzazi, upendo, na vita. Nyakati fulani yeye huwakilishwa katika mifano akiwa “kama mama anayenyonyesha mtoto wake mvulana.”b Hicho tena ni kielelezo kingine cha jinsi dini ya ki-siku-hizi isivyotofautiana sana na Babuloni ya kale!

Tungeweza pia kulinganisha Babuloni ya kale pamoja na mawazo yayo ya nafsi ya kibinadamu na utatu mbalimbali wa miungu na yale mawazo yaliyo kama hayo leo ya nafsi isiyokufa na utatu mbalimbali wa dini ya ki-siku-hizi. Ushuhuda unautilia nguvu uelewevu wetu wa kwamba “Babuloni Mkubwa” anafaa kufananisha milki ya ulimwengu wa Shetani ya dini bandia.

Babuloni​—Adui Mfidhuli wa Ibada ya Kweli

Babuloni ilikuwa pia adui mfidhuli wa watu wa kale wa Yehova, Israeli, na mwenye kudharau ibada yao ya kweli. Babuloni iliharibu hekalu katika Yerusalemu katika 607 K.W.K., ikachukua vyombo vyote vya thamani kubwa vya ibada ya Yehova, na kudharau utakatifu wa vyombo hivyo kwenye karamu ya Belshaza.​—Danieli 5:3, 4.

Vilevile, katika nyakati za ki-siku-hizi Babuloni Mkubwa ameendelea kuwa mpinzani wa ibada ya kweli. Katika visa vingi ambapo Mashahidi wa Yehova wamenyanyaswa, makasisi ndio wameendeleza jambo hilo, mara nyingi kwa kutumia mapatano yao na watawala wa kisiasa.

Kielelezo kimoja kilicho wazi cha upinzani wenye kuchochewa na makasisi ni cha kule nyuma 1917, na kiolezo hicho kimerudiwa tena na tena. Katika mwaka huo Wanafunzi wa Biblia wa Kimataifa, kama vile Mashahidi walivyojulikana wakati huo, walitangaza kwa chapa kitabu The Finished Mystery, Makasisi Wakanada na wa United States, ambao nchi zao zilihusika sana katika Vita ya Ulimwengu 1, walinenea kurasa chache za kitabu hicho kuwa na mambo ya kutaka kupindua serikali. Walifanya haraka kujulisha hawara zao wa kisiasa juu ya kichapo hicho. Tokeo likawa nini? Kulingana na Profesa Martin Marty, katika kitabu chake Modern American Religion—The Irony of It All: “Makasisi waligeuka dhidi ya Warusseli [Mashahidi] na kushangilia waliposikia kwamba hukumu za kufungwa miaka ishirini [kwa kusemekana kuwa wenye kufitini serikali] zingefikilizwa juu ya viongozi walioshtakiwa wa Mashahidi wa Yehova.”

Lakini makasisi walitendaje miezi michache baadaye wakati viongozi hao walipoondolewa mashtaka? “Washiriki wa makanisa yale makubwa-makubwa hawakushangilia.” Mashahidi walisimama peke yao upande wa kanuni za Biblia “kufikia hatua ya kwamba walifanya serikali kuu iwe na uhasama juu ya dini yao.” Mashahidi hawakuwa na hawajawa kamwe na nia ya kujipendekeza mno ili wawe wenzi wenye kuoana na watawala wa kisiasa, hata chini ya utawala wa Nazi katika Ujeremani au chini ya utawala wa Kifashisti katika Italia, Hispania, na Ureno.

Babuloni Alaumiwa Wazi na Kuaibishwa

Basi, inafaa kama nini wakati Ufunuo unapotaarifu kwamba Babuloni Mkubwa “amelewa damu ya watakatifu na damu ya mashahidi wa Yesu” na “katika yeye ilipatikana damu ya wanabii na ya watakatifu na ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.” Hatia ya damu ambayo dini ya ulimwengu inayo kwa kushiriki vita kwa utendaji au kwa kuviachilia bila kufanya lolote na kunyanyasa Wakristo wa kweli inaweza kuonwa kuwa ni ya tangu karne zilizopita.​—Ufunuo 17:6; 18:24, NW.

Babuloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini bandia, ameona shangwe kwa kuwa na anasa na mamlaka muda wote wa historia. Lakini malaika alionya Yohana kwamba siku ya huyo kahaba mkubwa ingekuja. Usimulizi unatuambia hivi: “Na yeye akalia kwa sauti yenye nguvu, kusema: ‘Yeye ameanguka! Babuloni Mkubwa ameanguka, na yeye amekuwa mahali pa kukaa roho waovu na mahali pa kujibanza kila pumzi isiyo safi na mahali pa kujibanza kila ndege asiye safi na mwenye kuchukiwa!’”​—Ufunuo 18:2, NW.

Babuloni ataanguka lini? Au amekwisha kuanguka? Yeye anaangukaje? Na hiyo inakuathirije wewe? Maswali hayo na mengine yanayohusiana nayo yatajibiwa katika toleo letu linalokuja la Mnara wa Mlinzi.

[Maelezo ya Chini]

a Las Grandes Religiones Ilustradas (Zile Dini Kubwa Zafanyiwa Kielezi): Asirio-Babildnica, Buku 20, Mateu-Rizzoli, Barcelona, Hispania, 1963, ukurasa 53.

b Buku 19, kurasa 19, 20.

[Picha katika ukurasa wa 8, 9]

Babuloni Mkubwa ana mizizi yake katika dini ya kale ya Kibabuloni

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki