Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 4/15 kur. 4-9
  • Kahaba Mwenye Sifa Mbaya Sana—Anguko Lake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kahaba Mwenye Sifa Mbaya Sana—Anguko Lake
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Milki ya Kidini ya Duniani Pote
  • Siku ya Hukumu ya Yehova
  • “TOKENI KATIKATIYAKE, O WATU WANGU”!
  • “Kugaa-gaa Matopeni”
  • Babuloni Mkubwa—Kaanguka na Kuhukumiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Jiji Kubwa Lateketezwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • “Yule Kahaba Mkuu” Akaribia Kuuawa Kwake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • “Babeli” Usio na Usalama Wahukumiwa Kuangamizwa
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 4/15 kur. 4-9

Kahaba Mwenye Sifa Mbaya Sana​—⁠Anguko Lake

“Ameanguka! Babuloni Mkubwa ameanguka, yeye ambaye alifanya mataifa yote wanywe ya divai ya kasirani ya uasherati wake!”​—⁠UFUNUO 14:8 NW.

Makala hii na ile inayofuata zilikuwa hotuba ya kumalizia ya mazungumzo-mfululizo yenye kichwa “Wakati Uliowekwa U Karibu,” iliyotolewa wakati wa 1988 kwenye Haki ya Kimungu Mikusanyiko ya Wilaya ya Mashahidi wa Yehova

1. Ni nani “kahaba” mwenye sifa mbaya sana, na kwa nini tunahitaji kujua habari zake?

“KAHABA” mwenye sifa mbaya sana 14​—⁠yeye ni nani? Kwa nini tunahitaji kuongea juu yake? Kwani riwaya za kusisimua, sinema, televisheni, na vidio hazina machukizo ya kutosha kuhusu ukosefu wa adili? Ni kweli! Lakini huyu si bibi-mtembea-jioni wa kikawaida. Kwa uhakika yeye ndiye malaya aliye mshawishi mkubwa, mwenye sifa mbaya na muuaji zaidi katika historia yote. Naye amekuwa akiuza mapenzi yake kwa zaidi ya miaka 4,000! Tunahitaji kujua habari zake kwa ulinzi wetu. Kwenye Ufunuo 14:​8, malaika wa kimbingu anamwita huyu mwanamke mwenye sifa mbovu “Babuloni Mkubwa” na kueleza kwamba ni mtongozaji wa mataifa. Kwa kuwa yeye ni hatari hivyo, tunapaswa kufurahi kwamba “wakati [wa Yehova] uliowekwa u karibu” ili kufikiliza hukumu juu yake.​—⁠Ufunuo 1:​3, NW.

2. Kahaba huyu anapata wapi jina lake, na milki ya ulimwengu ya dini bandia ilianzaje?

2 Kahaba huyu anachukua jina lake kutoka Babuloni la kale, jiji lenye kiburi lililosimamishwa imara katika Mesopotamia zaidi ya miaka 4,000 iliyopita na Nimrodi, “mwindaji hodari katika upinzani kwa Yehova.” Wababuloni walipoanza kujenga mnara wa dini ya kipagani, Yehova alivuruga lugha yao na kuwatawanya kwenye miisho ya dunia. Walienda na dini yao, na hivyo ndivyo milki ya ulimwengu ya dini ya Kibabuloni ilivyoanza. Nayo ni Babuloni MKUBWA kweli kweli. (Mwanzo 10:​8-10; 11:​1-9) Kuteremka kufikia wakati wetu, mafumbo ya Babuloni ya kale yanaonyeshwa katika itikadi na mazoea ya dini za ulimwengu. (Ufunuo 17:7) Jina la Kiebrania kwa jiji hilo, Babeli, linamaanisha “Mvurugo,” nacho ni kibandiko kinachoufaa mchanganyiko ovyo wa dini bandia leo!

3. (a) Ni kwa muda gani Babuloni alishika watu wa Mungu wakiwa mateka, akiwaweka katika ukaribiano mkubwa na kitu gani? (b) Ni wakati gani Babuloni alipopata anguko lenye msiba, na kwa nini mwisho wake haukuja wakati huo?

3 Babuloni wa kale alipona kipingamizi hicho cha kwanza na kuwa serikali kubwa ya tatu ulimwenguni katika historia ya Biblia, wakati Ashuru ilipopinduliwa katika 632 K.W.K. Utukufu wake akiwa hivyo ulikuwa wa muda mfupi​—⁠chini ya miaka mia moja ​—⁠lakini kwa karibu 70 ya miaka hiyo, aliwashika mateka watu wa Mungu. Hiyo ikawaweka katika ukaribiano mkubwa na mahekalu na vihekalu elfu moja vya Babuloni, utatu-utatu wa miungu yake na utatu-utatu wa maibilisi, ibada yake kwa mama na mwana, na unajimu wake wenye kuabudu miungu iliyosemwa haiwezi kufa. Hivyo, Waisraeli watekwa walikuwa hapo penye kitovu cha ulimwengu cha dini bandia wakati jiji la Babuloni lilipopata anguko lenye msiba, katika 539 K.W.K. Lakini mwisho wake ulikuwa bado! Wenye kumshinda waliendelea kumtumia akiwa kitovu cha kidini chenye fahari nyingi.

Milki ya Kidini ya Duniani Pote

4. (a) Wanabii wa Yehova walijulisha nini wazi kuhusu Babuloni, na ni jambo gani lililopata Babuloni? (b) Ni Babuloni gani mwingine anayeendelea kuishi, kwa madhara ya watu wa dunia?

4 Wanabii wa Yehova walikuwa wamejulisha wazi hukumu yake kwamba ni lazima Babuloni ifagiliwe mbali “kwa ufagio wa uharibifu”​—⁠“kama Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza.” Je! manabii hayo yalitimizwa baadaye? Ndiyo, yalitimizwa kila chembe! Baadaye, Babuloni ya kale ikawa rundo la mabomoko​—⁠bila wa kuikaa isipokuwa watambaazi na hayawani-mwitu​—⁠sawasawa na ilivyotabiriwa! (Isaya 13:​9, 19-22; 14:23; Yeremia 50:​35, 38-40) Hata hivyo, Babuloni yule mwingine, Babuloni Mkubwa wa ki-siku-hizi, anaendelea kuishi. Akiwa ndiyo milki ya ulimwengu ya dini bandia, yeye anaendeleza daima mafundisho na roho ya kutakabari ya Babuloni wa awali. Yeye ndiye chombo kikuu cha Shetani cha kupofusha watu wasione makusudi ya Ufalme wa Yehova.​—⁠2 Wakorintho 4:​3, 4.

5. (a) Ni dini gani zilizositawi wakati Babuloni alipokuwa katika upeo wa utukufu wake, lakini kwa nini Shetani hakufaulu kutopeza-topeza ulimwengu mzima kwa dini bandia? (b) Shetani alitumiaje dini bandia baada ya kuanzishwa kwa Ukristo?

5 Karibu karne ya sita kabla ya Kristo, hiyo serikali kubwa ulimwenguni ya Babuloni ilipokuwa katika upeo wayo wa utukufu, dini za Uhindu, Ubuddha, Ukonfyushasi, na Ushinto zilitokeza mbele pia. Lakini je! Shetani alifaulu kutopeza-topeza ulimwengu mzima kwa dini bandia? Sivyo, kwa maana mabaki ya mashahidi wa kale wa Yehova walirudi Yerusalemu kutoka Babuloni ili kusimamisha upya ibada ya Yehova. Hivyo, karne sita baadaye Wayahudi waaminifu walikuwa huko ili kumkaribisha Mesiya na kuwa washiriki wa kwanza wa kundi la Kikristo. Dini bandia ilitokeza kuuliwa imani kwa Mwana wa Mungu mwenyewe na ikawa chombo cha Shetani cha kupinga Ukristo wa kweli, sawa na vile Yesu na mitume wake walivyokuwa wameonya.​—⁠Mathayo 7:15; Matendo 20:​29, 30; 2 Petro 2:1.

6. (a) Shetani alifisidije mafundisho ya Kikristo, na yakasitawi mafundisho gani yenye kuvunjia Mungu heshima? (b) Maelfu waliopendelea ukweli wa Biblia badala ya fundisho la Kibabuloni lenye kushikiliwa sana walipatwa na nini?

6 Baada ya uharibifu wa pili wa Yerusalemu katika 70 W.K., ndipo hasa Shetani alipotumia mitume bandia kufisidi mafundisho ya Kikristo, akiyachanganya na mafumbo ya Kibabuloni na falsafa ya kilimwengu ya Ugiriki. Hivyo, ‘utatu wa kimungu,’ ule Utatu, uliwekwa mahali pa “Yehova mmoja” wa Biblia. (Kumbukumbu 6:4; Marko 12:29; 1 Wakorintho 8:​5, 6, NW) Na fundisho la kutokufa kwa nafsi ya kibinadamu, kama lilivyofundishwa na Plato mwanafalsafa mpagani, likaingizwa ili kukanusha yale mafundisho ya Biblia yaliyo na thamani kubwa kuhusu ukombozi wa Kristo na ufufuo. Hiyo ilifungua njia ya kuitikadi katika moto wa mateso na purgatori yenye moto mchache zaidi. (Zaburi 89:48; Ezekieli 18:​4, 20) Mafundisho hayo yenye kuvunjia Mungu heshima yanayoogopesha watu ili watende mambo wanayotakiwa kufanya yalisaidia kujaza masanduku ya sadaka za makanisa. Zaidi ya hilo, katika siku za lile Baraza la Kuhukumu Wazushi wa Kidini na za Mgeuzo Mkubwa wa Kidini, makasisi walishindwa kungojea ili moto wenyewe uje kujifanyia utesi-tesi. Maelfu waliopendelea ukweli wa Biblia badala ya mafundisho ya Kibabuloni yenye kushikiliwa sana walichomwa na Wakatoliki na Waprotestanti wakiwa hai mtini. Lakini kama tutakavyoona, ukahaba wa Babuloni Mkubwa ni zaidi ya kuendeleza ubandia tu.

Siku ya Hukumu ya Yehova

7. (a) Ni wakati gani na jinsi gani Yehova alianza kurudisha kweli za msingi za Biblia na kufichua mafundisho bandia ya Kibabuloni? (b) Ni kweli gani za msingi ambazo Wanafunzi wa Biblia walirudisha?

7 Siku ya hukumu ya Yehova juu ya kahaba huyu ilikuwa lazima ije! (Waebrania 10:30) Kulikuwa na kipindi cha matayarisho, kuanzia miaka ya 1870, wakati Yehova alipotuma “mjumbe” wake​—⁠kikundi chenye moyo mweupe cha wanafunzi wa Biblia​—⁠akarudishe kweli za msingi za Biblia na kufichua mafundisho bandia ya Kibabuloni. (Malaki 3:la) Kikundi hiki cha “mjumbe” kilikubaliana na maneno ya kiunabii ya Ufunuo 4:​11, NW: Wewe wastahiki, Yehova, hata Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu wewe uliumba vitu vyote, na kwa sababu ya penzi lako hivyo vilikuwako na vikaumbwa.” “Mjumbe” huyo akawa pia mtetezi wa kutoboa wazi mambo kuhusu dhabihu ya ukombozi ya Yesu, uandalizi wa Mungu wa kukomboa aina ya binadamu. Aina ya binadamu wakombolewa ingetia ndani, kwanza, “kundi dogo” ambalo litatawala pamoja na Yesu katika Ufalme wake wa kimbingu na, baadaye, mamia ya mamilioni ambao wataishi milele katika dunia-Paradiso​—⁠wengi wao wafufuliwe kwa wafu. (Luka 12:32; 1 Yohana 2:2; Matendo 24:15) Ndiyo, hao Wanafunzi wa Biblia walirudisha kweli hizi za msingi, na kwa njia ya kitamathali, wao hata ‘walielekeza mrija wa maji juu ya moto wa mateso na kuuzima moto huo’ wa fundisho la Kibabuloni lenye kushikiliwa sana kuhusu mateso ya milele!a

8. (a) Makasisi wa Jumuiya ya Wakristo walitumiaje Vita ya Ulimwengu 1 kujaribu kuwaharibu Wanafunzi wa Biblia? (b) Ikawaje kwa hakimu aliyewaweka gerezani maofisa wanane wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi kwa kukataa kuwapa dhamana?

8 Kwa miaka ipatayo 40 Wanafunzi wa Biblia walipiga mbiu kijasiri kwamba mwaka 1914 ungetia alama mwisho wa Nyakati za Watu Wasio Wayahudi. Kama ilivyotarajiwa, mwaka huo ukaleta matukio yenye kutikisa ulimwengu, moja la yaliyo makubwa zaidi likiwa ni vita ya ulimwengu ya kwanza. Wee, acha makasisi wa Jumuiya ya Wakristo​—⁠sehemu iliyo mashuhuri zaidi ya Babuloni Mkubwa​—⁠wajaribu kutumia mgogoro huo wa ulimwengu kuwaharibu wale Wanafunzi wa Biblia wenye kusema wazi! Mwishowe, katika 1918, walifanya maofisa wanane wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi wasafirishwe kwa gari-moshi wakaingizwe gerezani kwa kutungiwa mashtaka ya kufitini serikali. Lakini maofisa hao walifunguliwa baada ya miezi tisa na baadaye wakaondolewa mashtaka hayo. Hakimu wa serikali ya United States, Martin T. Manton, aliyekuwa amewaweka hawa Wanafunzi wa Biblia gerezani kwa kukataa kuwapa dhamana, baadaye alipambwa medali na Papa Pius 11, akifanywa kuwa “Mheshimiwa wa daraja la St. Gregory Mkubwa.” Hata hivyo, utukufu wake ukawa wa muda mfupi, kwa maana katika 1939 alihukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani na faini nzito. Kwa nini? Kwa sababu alipatikana na hatia ya kuuza maamuzi sita ya mahakama kwa dola 186,000 za mahongo!

9. Unabii wa Malaki ulielezaje lililokuwa likipata watu wa Yehova, na kwa hiyo hukumu ilianza na nani?

9 Kama vile tumeona sasa tu, watu wa Yehova waliingia kipindi cha kutahiniwa vikali katika 1918. Maneno zaidi ya mnabii kwenye Malaki 3:​1-3, NW, yanaeleza lililokuwa linatukia: “Na kwa ghafula kutakuja kwenye hekalu Lake yule Bwana wa kweli [Yehova], ambaye nyinyi watu mnamtafuta, na yule mjumbe wa agano [la Kiabrahamu]”​—⁠Yesu. Ndiyo, Yehova alikuja pamoja na Kristo wake kwa ajili ya hukumu. Ndipo Yehova anapouliza hivi: “Ni nani atakayekuwa akichukuliana na ile siku ya kuja kwake, na ni nani atakuwa mwenye kusimama wakati ambapo yeye anatokea? Kwa maana yeye atakuwa kama moto wa mtakasataka na kama lai ya wafuaji.” Kulingana na 1 Petro 4:​17, hukumu ingeanza na wale wanaodai kuwa wa “nyumba ya Mungu.” Hivyo, Wakristo wa kweli walitakaswa taka na kusafishwa sana kwa ajili ya utumishi wa Yehova.

“TOKENI KATIKATIYAKE, O WATU WANGU”!

10. Ni hukumu gani ya kimungu iliyokuja juu ya Jumuiya ya Wakristo na juu ya dini bandia yote kufikia 1919, ikitokeza nini kwa Babuloni Mkubwa?

10 Wakiwa sehemu isiyotubu ya Babuloni Mkubwa, makasisi wa Jumuiya ya Wakristo hawangeweza kuvumilia hukumu ya Yehova. Wao walikuwa wameyatia mavazi yao madoa mabaya sana wakiwa washiriki katika kule kufyeka-fyeka watu kwa vita ya ulimwengu na wakiwa wanyanyasi wa Wakristo wa kweli. (Yeremia 2:34) Badala ya kushangilia Ufalme wa kimbingu wa Kristo unaokuja, waliendeleza Ushirika wa Mataifa uliofanyizwa na binadamu, wakaja kuueleza kuwa ndio “wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani.” Kufikia 1919 ilionekana wazi kwamba Yehova alikuwa amekata hukumu juu ya Jumuiya ya Wakristo​—⁠na kwa kweli juu ya dini bandia yote. Babuloni Mkubwa akawa ameanguka, akashutumiwa kufa! Wakati ulikuwa umefika ili wote walio wapendaji ukweli na uadilifu wafanye kitendo kulingana na amri ya kiunabii iliyo kwenye Yeremia 51:​45, NW: “Tokeni katikati yake, 0 watu wangu, na kila mmoja aandalie nafsi yake mponyoko kutoka kwenye kasirani inayowaka moto ya Yehova.”

11, 12. (a) Malaika anasema nini kwenye Ufunuo 17:​1, 2 kuhusu hukumu ya Babuloni Mkubwa? (b) Ni nini yale “maji mengi” ambayo kahaba mkubwa anayakalia, naye amefanyaje wakaaji wa dunia ‘walewe divai ya uasherati wake’?

11 Babuloni Mkubwa ameanguka! Lakini hajaharibiwa bado. Akiwa milki ya ulimwengu ya dini bandia, yeye atakuwapo kwa muda mrefu kidogo akiwa mnenaji stadi wa udanganyifu wa Shetani. Ni nini hukumu ya Mungu ya mwisho juu yake? Hatuachwi na shaka! Acheni tufungue Biblia zetu kwenye Ufunuo 17:​1, 2, NW. Hapa malaika anasema kwa Yohana na, kupitia kwake, anasema kwa wanafunzi wa unabii leo, akiwaambia: “Njoo, mimi nitaonyesha wewe hukumu juu ya kahaba mkubwa ambaye huketi juu ya maji mengi, ambaye wafalme wa dunia walifanya uasherati na yeye, huku wale ambao huikaa dunia walifanywa kulewa divai ya uasherati wake.” Mtajo “maji mengi” unahusu matungamo yenye msukosuko ya aina ya binadamu, ambao wameonewa kwa muda mrefu sana na yule kahaba mkubwa. Na unabii unataarifu kwamba “wale ambao huikaa dunia” wanaleweshwa divai yake. Wanakunywa mafundisho bandia na njia za kilimwengu za ukosefu wa adili wa Babuloni Mkubwa na kupepesuka, kana kwamba wamelevywa divai-haramu ya bei rahisi.

12 Kwenye Yakobo 4:​4, NW, tunasoma hivi: “Wazinzi wa kike, je! nyinyi hamjui kwamba urafiki pamoja na ulimwengu ni uadui pamoja na Mungu?” Dini ya karne ya 20 ina utayari mwingi mno wa kujitafutia upendeleo wa ulimwengu, na hasa Jumuiya ya Wakristo. Si kwamba makasisi wayo wanashindwa tu kupiga mbiu ya habari njema za Ufalme wa Yehova unaokuja bali wanapunguza pia uzito wa mafundisho ya adili za Biblia, wakiachilia uendekevu wa kilimwengu miongoni mwa wanakanisa. Hata makasisi hawakosi sana hatia ya uasherati wa kimnofu, ulioshutumiwa kabisa kabisa na mtume Paulo aliposema hivi: “Msiongozwe vibaya. Wala waasherati, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wanaume wanaotunzwa kwa makusudi yasiyo ya asili, wala wanaume wanaolala pamoja na wanaume . . . hawatarithi ufalme wa Mungu. Na hata hivyo ndivyo baadhi ya nyinyi mlivyokuwa. Lakini nyinyi mmeoshwa kuwa safi.” ​—⁠ 1 Wakorintho 6:​9-11, NW.

“Kugaa-gaa Matopeni”

13, 14. (a) Ni vielelezo gani vinavyoonyesha kwamba makasisi wa ki-siku-hizi ‘hawakuoshwa kuwa safi’? (b) Mkutano wa baraza la Kanisa la Uingereza ulichukua mwelekeo gani juu ya vitendo vya kutumia viungo vya uzazi katika ugoni-jinsia-moja, na mwandikaji wa habari alidokeza kwamba kanisa hilo liitwe upya jina gani? (c) Makasisi waasi-imani wanafaana sana na maneno gani ya mtume Petro?

13 Je! makasisi wa ki-siku-hizi ‘wameoshwa kuwa safi’? Basi, kama kielelezo, angalia hali katika Uingereza, ambayo wakati mmoja ilikuwa ngome ya Uprotestanti. Katika Novemba 1987, wakati waziri mkuu wa Uingereza alipokuwa akiwatolea makasisi wito wa kuandaa uongozi wa kiadili, rekta wa kanisa la Kianglikana alikuwa akisema hivi: “Wagoni-jinsia-moja wana haki ile ile ya wonyesho wa kingono sawa na kila mtu mwingineye; inatupasa sisi tutafute mema yaliyomo katika jambo hilo na kutia moyo uaminifu [miongoni mwa wagoni-jinsia-moja].” Nyusipepa moja ya London iliripoti hivi: “Mazoea ya ugoni-jinsia-moja yalikuja kuenea sana katika koleji moja ya theolojia ya Kianglikana hata ikawa lazima kukataza wanafunzi kutoka koleji nyingine na wafanya kazi wa hapo wasizuru koleji hiyo.” Uchunguzi mmoja ulifanya hesabu ikaonwa kwamba “katika wilaya moja ya London, idadi ya makasisi wenye miegemeo ya ugoni-jinsia-moja huenda ikawa ni zaidi ya nusu ya jumla yao.” Na kwenye mkutano mmoja wa baraza la kanisa, asilimia 95 ya makasisi wa Kanisa la Uingereza waliunga mkono dokezo lililosema kwamba uasherati na uzinzi ni madhambi, lakini vitendo vya kutumia viungo vya uzazi katika ugoni-jinsia-moja si dhambi; vitendo hivyo vya ugoni-jinsia-moja vilisemwa kuwa vilipungukiwa kidogo kuwa jambo lile lililo la halisi hasa. Akieleza juu ya haya yote, mwandikaji mmoja wa habari alidokeza kwamba hata ingefaa Kanisa la Uingereza liitwe upya Sodoma na Gomora. Nyusipepa nyingine ya London ilijulisha wazi hivi: “Watu wa Uingereza wamejawa na mfadhaiko wanapoyafikiria matokeo ya kizazi cha uendekevu.”

14 Muda wa miaka yote hii makasisi waasi-imani wamefaana sana na maneno ya mtume Petro: “Imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni”!​—⁠2 Petro 2:22.

15. (a) Ni mvunjiko gani umetukia katika maadili kote kote katika Jumuiya ya Wakristo? (b) Ni lazima nani ashiriki daraka la mavuno haya yenye ole?

15 Kote kote katika Jumuiya ya Wakristo, na kweli kweli katika ulimwengu mzima, mna mvunjiko wa kuogofya katika maadili. Katika jamii fulani-fulani, ndoa sasa inaonwa kuwa isiyohitajiwa kabisa, na wale waliofunga ndoa wanafikiri kwamba kulingana na mtindo wa kisasa haifai kuwa na uaminifu katika ndoa. Ni watu wachache zaidi wanaohalalisha miungano yao, na talaka inapanda miongoni mwa wale wanaohalalisha. Katika United States, talaka zimeongezeka zaidi ya mara tatu katika muda wa miaka 25 iliyopita zikawa zaidi ya milioni moja kila mwaka. Wakati wa kile kipindi cha miaka 20 kuanzia 1965, talaka katika Uingereza ziliongezeka mara nne, kuanzia 41,000 kufikia 175,000. Waseja wanapendelea zaidi kuishi kinyumba pamoja na waseja wa jinsia tofauti, na wengi wanahama-hama kutoka kwa mwenzi mmoja hadi kwa mwingine. Wao wanaomboleza juu ya yale magonjwa yanayoambukizwa kingono, zaidi sana UKIMWI, ambayo yanaambukiza sana kama tokeo la mtindo-maisha wao wa kukosa adili lakini wanaendelea kusisitiza juu ya kufuata mazoea yao ya ngono zinazoshusha tabia. Makasisi wa Jumuiya ya Wakristo hawakuwatia nidhamu wanakanisa wenye kukosa. Ni lazima wao washiriki daraka la mavuno haya yenye ole, kwa kadiri ambavyo wao wameuachilia ukosefu wa adili.​—⁠Yeremia 5:​29-31.

16. (a) Ni nini kinachokazia uhakika wa kwamba Babuloni Mkubwa ameanguka, na ni mlio gani unaofaa uliopaazwa na malaika kwenye Ufunuo 18:2? (b) Ni lazima wote wanaotaka kuokoka mwisho wa ulimwengu wafanye nini?

16 Hali ya kusikitisha kiadili iliyo katika milki ya ulimwengu ya dini bandia inakazia pia uhakika wa kwamba Babuloni Mkubwa ameanguka. Mungu amemhukumu na kumtia alama kuwa ni wa kuharibiwa. Basi, unafaa kama nini ule mlio uliopaazwa na malaika kwa sauti imara, kwenye Ufunuo 18:​2, NW: “Ameanguka! Babuloni Mkubwa ameanguka, na yeye amekuwa mahali pa kukaa roho waovu na mahali pa kujibanza kila pumzi isiyo safi na mahali pa kujibanza kila ndege asiye safi na mwenye kuchukiwa!” Tena ni jambo la maana kama nini kwamba wote wanaotaka kuokoka mwisho wa ulimwengu wafanye kitendo sasa kwa kujibu wito ulio katika mstari wa 4: “Ondokeni katika yeye, watu wangu, ikiwa nyinyi hamtaki kushiriki pamoja na yeye katika madhambi yake, na ikiwa nyinyi hamtaki kupokea sehemu ya tauni zake”! Kuondoka katika dini bandia ni hatua muhimu kuelekea kuiokoka “dhiki kubwa” iliyo hapa mbele tu. (Ufunuo 7:​14, NW) Lakini mengi zaidi yanatakwa, kama tutakavyoona!

[Maelezo ya Chini]

a Siku ya Novemba 1, 1903, baada ya lile la mwisho la mfululizo wa majadiliano yaliyofanywa Carnegie Hall, Pittsburgh, Pennsylvania, U.S.A., kati ya Charles T. Russell na Dakt. E. L. Eaton, mmoja wa makasisi wenye kuhudhuria alikiri ushindi wa Ndugu Russell, akisema: “Mimi naterema kuona wewe ukigeuza mrija wa maji juu ya moto wa mateso na kuuzima moto huo.”

[Sanduku katika ukurasa wa 8]

Maadili ya Makasisi

“Mamia ya watoto ambao wameshikwa-shikwa uchi na mapadri Wakatoliki katika United States wakati wa miaka mitano iliyopita wamekuwa wakishtuka sana hisia-moyo wanapokumbuka tukio hilo, wanasema wazazi, wasaikolojia, maofisa wa polisi na mawakili wa sheria waliohusika katika kesi hizo.”​—⁠Akron Beacon Journal, Januari 3, 1988.

“Kanisa Katoliki la Kiroma katika United States limelazimishwa kulipa mamilioni ya dola za madhara kwa jamaa ambazo zinashikilia kwamba watoto wao wametumiwa vibaya kingono na mapadri. Ijapokuwa hivyo, tatizo lenyewe limeongezeka likawa kali sana hivi kwamba wanasheria na majeruhi wengi wanasema kanisa linapuuza na kuficha kesi hizo.”​—⁠The Miami Herald, January 3, 1988.

[Picha katika ukurasa wa 6]

Mifano ya miungu ya utatu​—⁠kutoka Misri ya Kale na kutoka Jumuiya ya Wakristo

[Hisani]

Mkusanyo wa Jumba la Makumbusho la Saint-Remi, Reims, picha imepigwa na J. Terrisse

Jumba la Makumbusho la Louvre, Paris

[Picha katika ukurasa wa 9]

Biblia inafananisha viongozi wa kidini wasio na adili na nguruwe aliyeoshwa anayerudi kugaa-gaa matopeni

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki