Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 5/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • “Uwaambie Neno Hili”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • “Siwezi Kunyamaza Kimya”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • “Nimeyatia Maneno Yangu Katika Kinywa Chako”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • “Nitaishibisha Nafsi Iliyochoka”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 5/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

■ Je! Yehova hutumia viini-macho au udanganyifu kuhusiana na watu, kutia na watumishi wake, kama vile Yeremia 4:10 na 20:7 yanavyoelekea kudokeza?

Sivyo, Muumba si mdanganyifu, mtunga hila, wala mjanja katika shughuli zake. Ingawa hivyo, yeye anaweza kutimiza na hutimiza penzi lake adilifu wanadamu wajapotarajia jambo lolote lile.

Tunaona upande mmoja wa jambo hilo kutokana na Yeremia 4:​10, ambapo mnabii alisema hivi: “Aa, Bwana MUNGU [Yehova, NW]! hakika umewadanganya sana watu hawa na Yerusalemu, ukisema, Mtakuwa na amani; lakini upanga umeingia katika nafsi za watu.”

Yehova alitumia Yeremia kutabiri afa lenye kujia taifa hilo asi lililojidhania lilikuwa likimtumikia Yeye. (Yeremia 1:​10, 15-19; 4:​5-8; 5:​20-30) Hata hivyo, walikuwako wengine wenye kudai kuwa ni wanabii. (Yeremia 4:9) Watu walisikia nini kwa hao wenye kuitwa wanabii eti? Mungu aliainisha jambo hilo hivi: “Manabii wanatabiri uongo . . . na watu wangu wanapenda mambo yawe hivyo.”​—Yeremia 5:31; 20:6.

Ingawa Yehova hakuwatuma hao wanabii bandia, wala hakuwazuia wasieneze jumbe, kama vile: “Mtakuwa na amani” na, “Hamtapatwa na ubaya wo wote.” (Yeremia 23:​16, 17, 25-28, 32) llikuwa lazima watu hao wachague​—⁠wakubali yale manabii makali lakini yaliyo ya kweli ambayo yalitolewa na Yeremia au wajiache waongozwe vibaya na wanabii bandia wa kujifanyiza wenyewe, kama Hanania na Shemaya. (Yeremia 28:​1-4, 11;29:​30-32) Kwa kuwa Mungu hakuwazuilia wanabii hao wenye kuongoza watu vibaya, ingeweza kusemwa hivi juu yake: “Hakika umewadanganya sana watu hawa na Yerusalemu, ukisema, Mtakuwa na amani.”

Katika maana tofauti, Yeremia alipumbazwa. “Ee Bwana [Yehova, NW], umenihadaa, nami nimehadaika; wewe una nguvu kuliko mimi, ukashinda; nimekuwa kitu cha kuchekesha, mchana kutwa; kila mtu hunidhihaki.”​—⁠Yeremia 20:7.

Pashuri, kuhani mashuhuri, alimshambulia Yeremia peupe na kumtia katika mkatale. Kwa maoni ya kibinadamu, Yeremia angaliweza kuhisi kwamba alikuwa amefikia kikomo cha uvumilivu wake, kwamba hakuwa tena na imara ya kusonga mbele kwa kukabili ubaridi, kukataliwa, dhihaka, na jeuri ya kimwili. Lakini sivyo. Yehova alitumia imara Yake ili iwe dhidi ya mwelekeo wa kibinadamu wa Yeremia, au iwe kinyume chao. Mungu alimpumbaza Yeremia katika jambo la kwamba Yeye alimtumia mwanadamu huyo asiyekamilika ili atimize mambo ambayo mnabii huyo asingaliweza kufanya kwa imara yake mwenyewe. Ingawa huenda ikawa Yeremia alipumbazwa au akashangazwa sana na jambo hilo, lilikuwa na kusudi jema: Wenye kumnyanyasa waliaibishwa, na ujumbe wa Mungu ukatolewa.​—⁠Yeremia 20:11.

Basi, yanapoeleweka kulingana na habari zinazozunguka, Yeremia 4:10 na 20:7 yanapatana na shauri lililokatwa na Elihu: “Mungu hatatenda mabaya, wala Mwenyezi hatapotosha hukumu.”​—Ayubu 34:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki