Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 6/1 kur. 30-32
  • Mtafute Yehova na Umtumikie kwa Moyo Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mtafute Yehova na Umtumikie kwa Moyo Wote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Siku ya Yehova I Karibu
  • Wokovu Wawezekana
  • Watu Waliorudishwa
  • Masomo Kutokana na Maandiko: Hagai 1:1–2:23
  • Tanguliza Kazi ya Yehova
  • Utumishi wa Moyo Wote Watakwa
  • Kitabu Cha Biblia Namba 37—Hagai
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • “Fulizeni Kunitarajia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Kitabu Cha Biblia Namba 36—Sefania
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • “Mikono Yako Isilegee”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 6/1 kur. 30-32

Masomo Kutokana na Maandiko: Sefania 1:1–3:20

Mtafute Yehova na Umtumikie kwa Moyo Wote

MIAKA 50 hivi kabla ya Wababuloni kukumba Yuda yenye kuasi imani, Yehova alijulisha wazi hivi kupitia mnabii wake Sefania: “Nitavikomesha kabisa vitu vyote, visionekane juu ya uso wa nchi.” (1:1, 2) Lakini pia Mungu alionyesha watu wake njia ya kupata usalama. (2:3; 3:9) Kwa habari hii, kitabu cha Sefania kina masomo yenye thamani kwa wote wanaoelekeana sasa na “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.”​—Ufunuo 16:14.

Siku ya Yehova I Karibu

Siku ya Yehova ikiwa karibu sana, yawapasa wowote ambao wamejiondoa kwa Mungu wamrudie upesi. Miongoni mwa wale ambao Mungu ‘atakomesha kabisa’ ni ‘wale wanaorudi nyuma na kuacha kumfuata Yehova.’ Wamegeukia kando na wao hawajishughulishi tena na mapenzi ya Mungu. Ni hali yenye hatari kama nini! Yapasa isahihishwe mara moja.​—Sefania 1:3-11.

Utajiri wa vitu vya kimwili hauwezie kuandaa usalama katika siku ya Yehova. Baadhi ya wale wanaodai kumtumikia Yehova huhangaikia kufuatia vitu vya kimwili, wakijiweka katika hali yenye raha. Lakini huko ni kujidanganya kulikoje! Vitu vyao vya kimwili havitatoa usalama katika “siku ile.”​—Sefania 1:12-18.

Wokovu Wawezekana

lli kufichwa katika siku ya Yehova, mengi zaidi ya maarifa ya kijuu-juu ya Maandiko yahitajiwa. “Wanyenyekevu” ambao wamezitenda hukumu zake’ wanaonywa kwa upole ‘wamtafute Yehova, watafute haki, watafute unyenyekevu.’ Wale tu ambao ‘wamevumilia mpaka mwisho’ ndio wataokolewa.​—Sefania 2:1-3; Mathayo 24:13.

Mataifa ambayo huonea watu wa Yehova leo yatapatwa na uharibifu. Yatapatwa na jambo kama lile lile lililopata Moabu, Amoni, Ashuru, na mataifa mengine kuzunguka Yuda. Pia uharibifu wamngojea Babuloni Mkubwa. (Ufunuo 18:4-8) Lo! jinsi hilo linavyotutia moyo tuendelee kusonga mbele katika kujulisha wazi hukumu za Yehova!​—Sefania 2:4-15.

Watu Waliorudishwa

Sasa Yehova anatayarisha watu wake kwa ajili ya wokovu. Je! wewe umeacha mawazo ya Kibabuloni na kuanza kunena “lugha iliyo safi” ya ukweli wa Biblia wenye thamani? Je! wewe ‘umeliitia jina la Yehova’ kwa kujiweka wakfu kwake? Je! wewe ‘unaleta zawadi,’ yaani, “tunda la midomo iliungamayo jina lake”? Ili kuokoka, lazima utumikie “kwa nia moja” pamoja na watu wa Yehova walio wakfu.​—Sefania 3:1-10; Warumi 10: 13-15; Waebrania 13:15.

Ili tuokolewe, lazima tumtafute Yehova na kuliheshimu jina lake takatifu. Kiburi, utovu wa adili, na uwongo havina nafasi miongoni mwa watu wake. (Waefeso 4:25-32) ‘Walioonewa [wanyenyekevu, NW ] na maskini’ tu ndio watakaookolewa atakasapo jina lake.​—Sefania 3:11-20.

Masomo Kutokana na Maandiko: Hagai 1:1–2:23

KITABU cha Hagai hutuleta kwenye mwaka 520 K.W.K., miaka 17 baada ya mabaki ya Kiyahudi kurudi Yerusalemu ili wajenge upya hekalu la Yehova. (Hagai 1:1) Huo ulikuwa wakati wa kila mmoja kuweka moyo wake kwenye kazi ya Mungu. Hata hivyo, Yehova aliona kuwa inahitajiwa kabisa kupeleka mnabii Hagai kukumbusha watu Wake juu ya wajibu wao. Je! kuna masomo yoyote kwa ajili yetu katika jambo hili?

Tanguliza Kazi ya Yehova

Usitangulize kamwe masilahi ya kimwili mbele ya wajibu wa kiroho. Wayahudi waliorudi kwenye bara la kwao walikuwa na sababu ya kuhangaikia mashaka ya kiuchumi, majirani wenye uhasama, na kadhalika. Lakini hivyo havikuwa ndivyo visababishi vya upuuzaji wao, kwa kufikiria hali zao za kuishi kwa anasa. Ilikuwa baada tu ya kuamshwa na Hagai wakaanza kujenga hekalu. Vivyo hivyo leo, tunahitaji ‘kutafakari’ juu ya njia zetu na kuhakikisha kwamba sisi tunaunga mkono kazi ya Mungu kwa kadiri kubwa iwezekanavyo.​—Hagai 1:2-15.

Yehova hubariki jitihada za wale ambao hufanya kazi yake kwa moyo wote. Mungu angebariki kazi ya Zerubabeli na Wayahudi wengine katika kumaliza hekalu, na utukufu walo ungepita ule wa nyumba ya kwanza. “Mkutano mkubwa” ukiwa unaitikia ujumbe wa Ufalme leo, “vitu vinavyotamanika vya mataifa yote” vinakuja kwenye hekalu la kiroho la Yehova, naye ‘anajaza nyumba yake utukufu.’​—Hagai 2:1-9, NW; Ufunuo 7:9.

Utumishi wa Moyo Wote Watakwa

Ibada yetu ina thamani ikiwa tu sisi ni safi, makusudio yetu ni yenye kutakata, nasi tunatumikia Yehova kwa moyo kamili. Kupuuza nyumba ya Yehova kuliwafanya Wayahudi wawe najisi, lakini yeye angewabariki mara tu kazi ya hekalu ianzapo tena. Kwa hiyo, ikiwa tutafurahia baraka ya Yehova, lazima tusahihishe jambo lolote linalohitaji kuangaliwa na kuweka moyo wetu katika kazi yake. (Linganisha Hesabu 19:11-13.) Tunapongojea Mungu atikise mbingu na dunia, akipindua falme, acheni sisi tufuate Yesu Kristo, aliyefananishwa na Zerubabeli, na kushiriki kwa moyo wote katika kazi ya Yehova.​—Hagai 2:10-23.

[Sanduku katika ukurasa wa 30]

MAANDIKO YA BIBLIA YACHUNGUZWA

○ Sefania 1:5​—Malkamu, yawezekana ndiye yule yule Milkomu, Moleki, au Moloki, alikuwa ndiye mungu mkuu bandia wa Waamoni. (1 Wafalme 11:5, 7) Ibada ya Moleki ilitia ndani kudhabihu watoto kwenye kuchukiza nako kulishutumiwa vikali na Sheria.​—Walawi 20:2-5; Matendo 7:42, 43.

○ Sefania 2:14​—Kama ilivyotabiriwa, nguzo zilizoangushwa za Ninawi lililoachwa ukiwa zikawa mahali pa kukaa ndege na hayawani-mwitu. Ndege na yaelekea upepo uliimba’ kwenye madirisha yaliyoachwa. Viingilio na hata sehemu za ndani za jumba la kifalme vilikumbwa.

○ Sefania 3:9​— Lugha ya kibinadamu yenye kusemwa na wote haihakikishi umoja, kama inavyoonyeshwa na vita vinavyopigwa kati ya watu wa lugha ile ile moja. “Lugha iliyo safi” ni ukweli wa Kimaandiko, “kigezo cha maneno yenye afya.” (2 Tim. 1:13, NW) Inaruka mipaka ya kiburi, inamtukuza Mungu, na kuunganisha pamoja wote wanaoisema.

○ Hagai 1:6​—Kwa kuwa Wayahudi walikuwa wakipuuza hekalu la Yehova, hawakuwa na baraka yake. Kwa sababu hiyo, walipanda kwa wingi lakini wakakusanya mazao machache na wakakosa chakula na kinywaji cha kutosha kutimiza mahitaji yao. Mavazi yao yalikuwa ya kiasi kisichotosha au ya ubora usiotosha kuwapasha moto, na ilionekana kama kwamba wachuma mshahara nao waliweka pesa zao katika mfuko uliojaa matundu. Tofauti na Wayahudi hao, sisi na tusipuuze kamwe masilahi ya kimungu.​—Mithali 10:22; Nehemia 10:39.

○ Hagai 2:9​—Ingawa lile hekalu ‘la kwanza,’ lililojengwa na Sulemani, lilisimama kwa miaka 420, ile ‘nyumba ya mwisho’ ilitumiwa kwa miaka 584 (515 K.W.K.-70 W.K.). Kwa hiyo hekalu la pili lilidumu kwa muda mrefu zaidi. Waabudu zaidi waliliendea makundi makundi, kama wakati wa Pentekoste 33 W.K., Wayahudi na waongofu walipokusanyika humo wakiwa wamekuja kutoka nje ya Yudea. Zaidi ya hilo, Mesiya, Yesu Kristo, alifundisha katika ‘nyumba ya mwisho.’ Mambo hayo ya hakika yaliipa utukufu mkubwa zaidi wa kidini.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki