Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 10/1 uku. 21
  • Walipata Sababu ya Kubadilika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Walipata Sababu ya Kubadilika
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • “Nilikuwa Nikijichimbia Kaburi”
    Biblia Inabadili Maisha
  • Mambo Tupaswayo Kujua Kuhusu Magenge
    Amkeni!—1998
  • Toa Magazeti Katika Huduma
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 10/1 uku. 21

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

Walipata Sababu ya Kubadilika

JE! WAHALIFU na hata viongozi wa magenge waweza kubadili mwenendo wao? Ni nini kingeweza kuwasaidia wafanye hivyo? Mabadiliko makubwa ya kutazamisha katika mwenendo yawezekana kama ionwavyo katika kisa cha Sauli wa Tarso, aliyebadilika akaacha kunyanyasa Wakristo na kuwa Mkristo yeye mwenyewe. Baada ya hapo alijulikana kuwa mtume Paulo. (Wagalatia 1:13, 14; 1 Timotheo 1:13) Mabadiliko ya kutazamisha jinsi iyo hiyo yaripotiwa kutoka Kenya.

◻ Kijana mmoja wa kiume alikuwa mshirika wa genge moja katika eneo la Nairobi na alitumwa magharibi mwa Kenya akapeleleze mawezekano ya kufanya manyakuzi katika benki za huko. Alitafuta mahali pa kulala kwa mwanamume mmoja mzee-mzee na kupata fungu la magazeti ya zamani ya Amkeni! katika nyumba yake. Kijana huyo wa kiume alijihusisha sana katika kusoma magazeti haya hata akasahau kabisa mipango yake iliyohusu kufanya manyakuzi katika benki. Alipokuwa amesoma kila kitu, aliomba zaidi, na mwanamume yule mzee-mzee akamwambia kwamba kungekuwa na moja lenye kuja kila majuma mawili kwa njia ya posta. Tangu wakati huo kijana huyo wa kiume alimsihi sana mkaribishaji wake aende kwenye ofisi ya posta kila siku kutafuta magazeti zaidi. Kwa sasa, yeye alifanya uamuzi wa kuacha kabisa njia zake mbaya, afuate mambo aliyokuwa amejifunza kutokana na magazeti, na kuwa Shahidi wa Yehova. Hata alianza kuambia majirani kwamba yeye ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Baadaye, painia wa pekee alifanya kazi katika eneo lile akagutuka kumpata kijana huyu wa kiume akidai kuwa ni Shahidi. Funzo la Biblia lilianzwa pamoja naye, akapata ukomavu, na leo yeye ni painia wa kawaida. Maarifa sahihi ya Biblia yalimpa sababu ya kubadili maisha yake.

◻ Mwingine aliyekuwa mhalifu hapo kwanza alikuwa amekuwa kiongozi wa genge na alionwa kuwa hatari sana hivi kwamba polisi wakatoa maagizo ya kwamba apigwe risasi akionekana. Polisi mmoja aliwapasha habari hizo watu wa ukoo wa mhalifu huyo, lakini mwanamume huyo alipoambiwa, yeye alitikisa mabega kwa kupuuza na kucheka tu. Hata hivyo, muda mfupi baada ya hapo paramio moja lililofanywa na genge lao halikwenda kama lilivyopangwa, na mwanamume yule akajipata akiwa peke yake akiwa amezungukwa na umati wenye kasirani. Polisi walikuja kumponyosha na kumtia gerezani ajaribiwe mahakamani. Mwana-sheria wake alimshauri atamke kuwa hana hatia, lakini mwanamume huyo alipokuwa katika kijumba chake cha gereza, alikumbuka ziara alizofanyiwa na painia wa pekee miaka kadhaa mapema. Painia huyo alikuwa amemwambia kuhusu ukweli wa Biblia. Mhalifu huyo aliyeingizwa jela alianza kujuta juu ya njia zake mbovu na kupelekea Mungu sala ili apate msaada, hata akatumia jina la Mungu, Yehova.

Kwenye jaribio lake alikiri hatia yake, hakimu akashangaa sana. Hivyo, hakimu alimpa kifungo kipole kikilinganishwa na hatia yake; badala ya kuhukumiwa kifo, alihukumiwa kufungwa miaka kumi katika gereza la ulinzi mkali. Huko, kwa bidii ya uendelevu alisoma kichapo kimoja cha Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi na kuanza kuwahubiria wafungwa wenzake mambo aliyojifunza. Pia alipeleka-peleka sala kwa Yehova na kuonyesha toba yake, akiomba kwamba, ikiwa yawezekana, wakati wake wa kukaa gerezani upunguzwe ili aweze kutumikia Yehova kwa uhuru. Bila kutarajia, sala yake ilijibiwa alipoambiwa kwamba hukumu yake imepunguzwa ikawa miaka mitano. Baada ya miaka mitano hiyo, alifunguliwa na mara hiyo akaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi. Muda mfupi baada ya hapo, alibatizwa. Leo, yeye ni painia wa kawaida mwenye bidii sana!

Maarifa sahihi ya Biblia yaliwapa wanaume hawa sababu ya kubadili njia yao ya maisha, na yaweza kusaidia mtu yeyote mwenye kutamani maisha yenye umaana zaidi sasa na tumaini la uhai wa milele katika ulimwengu mpya wa Mungu ulio na furaha. —Yohana 17:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki