Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 10/15 kur. 4-7
  • Ufufuo—Kwa Ajili ya Nani na Wakati Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufufuo—Kwa Ajili ya Nani na Wakati Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Watu Walazimike Kufa?
  • Ni Nini Hali ya Wafu?
  • Ufufuo wa Kidunia
  • Ufufuo—Chanzo cha Faraja
  • Ufufuo—Wakati Gani?
  • Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Suluhisho Pekee la Kifo!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Tumaini Hakika
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
  • Kutakuwa na Ufufuo!
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 10/15 kur. 4-7

Ufufuo—Kwa Ajili ya Nani na Wakati Gani?

ILITUKIA katika mwaka 32 W.K. kule Bethania, ambako Lazaro aliishi pamoja na dada zake wawili, Martha na Mariamu. Dada hao walikuwa wamempelekea Yesu ujumbe kwamba Lazaro ni mgonjwa. Yesu alipenda Lazaro na dada zake, kwa hiyo Yeye alianza safari kwenda Bethania. Akiwa barabarani, Yesu alijulisha wanafunzi wake hivi: “Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.” Wanafunzi walifikiri kwamba Yesu alimaanisha usingizi halisi. Kwa hiyo Yesu akataarifu wazi hivi: “Lazaro amekufa.”—Yohana 11:1-15.

Wageni hao wenye kuzuru waliwasili siku nne baada ya kifo cha Lazaro. Yesu alipoona Mariamu na wengine wakilia machozi, yeye “aliachilia machozi yamtoke,” akionyesha upendo na huruma yake ya kina kirefu. (Yohana 11:17, 35, AW) Mwili mfu wa Lazaro ulikuwa umetiwa katika kaburi-pango. Yesu alielekeza kwamba jiwe lile lenye kufunika mwingilio wa kaburi liondolewe. Alimpelekea Baba yake sala halafu akapaaza sauti hivi: “Lazaro, njoo huku nje.” Lazaro alikuja nje. Lo, lazima hiyo iwe iliwaletea dada zake shangwe iliyoje!—Yohana 11:38-45.

Tukio hili laandaa tumaini halisi la ufufuo. Hata hivyo, kwa ujumla, kifo ni adui mbaya sana ambaye huchukua wapendwa wetu bila taraja la kwamba Yesu atawafufua mara iyo hiyo. Kama tujuavyo sana, wengi wa wapenzi hawa ni wema na wenye fadhili sana. Kwa sababu hiyo, swali la uwazi latokea . . .

Kwa Nini Watu Walazimike Kufa?

Ikiwa twataka jibu sahihi, lenye kutegemeka, ni lazima tutazame nyuma kwenye mwanzo wa aina ya binadamu katika bustani ya Edeni. Akitahini utii wa Adamu, Mungu alimwamuru humo asile tunda la mti fulani. Kama yeye na Hawa wangekula tunda hilo, Mungu alisema, ‘wangekufa hakika.’ (Mwanzo 2:17) Waliposhawishwa na Shetani, walikosa utii kwa Mungu wakashindwa mtihani huo wa maana sana. Tokeo likawa ni kifo.

Kwa nini kuwe na adhabu hiyo kwa uhalifu ulioonekana kuwa mdogo? Kitendo chao kilikuwa kidogo, lakini uhalifu wenyewe ulikuwa mzito sana, tena sana—uasi wa watu wakamilifu, Adamu na Hawa, dhidi ya Muumba wao. Wao hawakuwa tena wakamilifu, na Mungu alipitisha hukumu ya kifo. Hata hivyo, Mungu amepanga kwamba hukumu hiyo ya haki ipinduliwe kwa ajili ya wazao wa Adamu. Jinsi gani? Paulo aliandika kwamba “Kristo Yesu . . . alijitoa mwenyewe awe ukombozi unaolingana kwa ajili ya wote.”—1 Timotheo 2:5, 6, NW; Warumi 5:17, UV.

Ni Nini Hali ya Wafu?

Lazaro alikuwa mfu kwa siku nne. Kama wewe ungalikuwa umekufa lakini kwa kweli uwe uko hai katika makao ya kiroho kwa siku nne halafu ufufuliwe, je! hungetaka kuambia wengine kuhusu jambo hilo? Lakini Lazaro hakusema lolote kwamba alikuwa amekuwa hai katika makao fulani mengine. Biblia yasema: “Lakini wafu hawajui neno lo lote.”—Mhubiri 9:5; Zaburi 146:3, 4.

Fikiria mimaanisho ya jambo hilo. Mamilioni ya watu huamini kuna purgatori, ingawa neno hilo halionekani katika Biblia. Wengine zaidi huamini kwamba kuna helo yenye moto. Hata hivyo, wewe hungechoma hata adui milele katika moto. Ikiwa wewe ungekataa kutenda ukatili wa jinsi hiyo, je! Muumba wetu mwenye upendo angefanya hivyo kwa kutesa watu mmoja mmoja katika moto wa helo? Lakini tafadhali ufikirie uhakikisho wenye faraja ya Kibiblia ambao umetajwa juu—wafu “hawajui neno lo lote.”

Kulingana na Maandiko, hesabu ya watakaotawala pamoja na Kristo mbinguni ni ndogo. Yesu aliwaeleza kuwa “kundi dogo.” (Luka 12:32) Mtume Yohana aliona “Mwana-Kondoo [Yesu Kristo] amesimama juu ya mlima Sayuni [wa kimbingu], na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, . . . walionunuliwa katika nchi [dunia, NW].” (Ufunuo 14:1-3) Basi, hiyo yamaanisha kwamba hapo kwanza watu hao walikuwa wanadamu, wakafa, na baadaye wakafufuliwa wakaishi mbinguni pamoja na Kristo.

Kama vile uwezavyo kuwazia, watu wamesaidiwa kwa kuelewa kweli hizi za Biblia —kwamba hakuna purgatori wala helo inayowaka moto na kwamba kuna tumaini la kwamba wafu waweza kufufuliwa waende mbinguni. Hata hivyo, ikiwa wale wenye kufufuliwa waende mbinguni ni wachache sana, kuna tumaini gani kwa ajili ya wengine?

Ufufuo wa Kidunia

Yesu Kristo ndiye aliyefungua, au akazindua, njia ya kufufuliwa kwenye uhai mbinguni. (Waebrania 9:24; 10:19, 20) Hivyo, Yohana Mbatizaji hatashiriki katika ufufuo huo wa kimbingu kwa sababu aliuawa kabla Yesu hajafa na kufungua njia ya kwenda kwenye uhai wa kimbingu. Yesu alisema: “Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.” (Mathayo 11:11) Ni thawabu gani ambayo Mungu amtolea mwanamume huyu mwaminifu na wengine kama yeye ambao wamekufa?

Fungua Biblia yako kwenye Luka 23 na usome mistari 39 hadi 43, NW. Mmoja wa watenda maovu aliyetundikwa kando ya Yesu alisema hivi: “Yesu, nikumbuke mimi uingiapo katika ufalme wako.” Yesu alimhakikishia kwamba yeye angekuwa katika Paradiso. Hiyo si mbinguni, bali ni paradiso ya kidunia, kama ilivyokuwa ile Paradiso ya kwanza.

Ufufuo—Chanzo cha Faraja

Sisi tungekuwa na sababu ya kutarajia kwamba tazamio hilo halali la Kibiblia lapasa kufariji sana. Kwa nini? Kwa sababu Yehova ni upendo. (1 Yohana 4:8) Aliporuhusu Mwana wake afe kifo chenye aibu, kwa kweli Mungu alikuwa akidhihirisha sifa yake ya upendo iliyo nzuri ajabu. Wakati fulani kabla ya hapo, Yesu alikuwa amesema hivi: “Mungu aliupenda ulimwengu [aina ya binadamu], hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”—Yohana 3:16.

Yesu pia alionyesha upendo usio wa kikawaida kwa kutoa uhai wake uwe ukombozi kwa ajili ya aina ya binadamu yenye kuamini. Yeye mwenyewe alisema hivi: “Mwana wa binadamu alikuja, si ahudumiwe, bali kuhudumia na kutoa nafsi yake ukombozi badala ya wengi.”—Mathayo 20:28, NW.

Carolann, aliyetajwa katika makala ya kwanza kuwa alipoteza hesabu fulani ya wapendwa wake katika aksidenti mbaya sana, aliduwaa baadaye kwa kulemewa na hisia. Lakini alifarijika kwa kujua kwamba wapendwa hao walio wafu hawateseki. Ni nini zaidi kilichomsaidia akabili hali hiyo? Upendo na pole za kikweli alizoonyeshwa na ndugu zake wa kiroho, Mashahidi wa Yehova, zilithibitika kuwa zenye msaada sana.—Zaburi 34:18.

Sala kwa Yehova ilisaidia sana pia. Yeye alikuwa akiamka nyakati nyingi za usiku na kufikiri kwamba ilikuwa ndoto mbaya tu, lakini ndipo angegutuka kwa kuuona uhalisi wenyewe. Dua ya kumsihi sana Yehova ilikuwa ikimtuliza, naye akathamini kwa kina kirefu zaidi yale ambayo Paulo aliandika: “Msihangaikie chochote, bali katika kila jambo kwa sala na dua ya kusihi pamoja na shukrani, Mungu na ajulishwe maombi yenu. Na amani ya Mungu inayoshinda mawazo yote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kupitia Kristo Yesu.”—Wafilipi 4:6, 7, NW.

Shirley aandaa kielelezo kingine juu ya jinsi tumaini la ufufuo hufariji sana. Riccardo mwana wake mchanga alikufa papo hapo wakati kipande cha saruji kilipomwangukia kifuani, kikapasua moyo wake mdogo. Baada ya tanzia hii, katika Januari 1986, Shirley aliambia marafiki hivi: “Lilikuwa kama jinamizi la usiku.” Katika Kanisa Katoliki yeye alisikia maneno haya: “Mungu atahukumu walio hai na wafu.” Shirley akaanza kufikiri hivi, ‘Ikiwa Mungu atahukumu walio hai na wafu, basi mtu aweza kujuaje mahali ambako watu huenda baada ya kufa? Na ikiwa wa0 wako mbinguni, kwa nini awafufue baadaye kuwahukumu? Zaidi ya hilo, wao waweza kufufuliwaje ikiwa wako hai mbinguni?’ Hakuna mahali popote ambapo Biblia hutaja ufufuo wa walio hai bali wa wafu tu.

Shirley aliuliza mume wake kuhusu tatizo hili, kwa kuwa alijua mambo machache ya Biblia. Mara alipoelewa baadhi ya mambo ambayo Maandiko yasema kuhusu habari hiyo, Shirley hakurudi tena kanisani. Mtu mmoja wa ukoo aliye mmoja wa Mashahidi wa Yehova alianza kujifunza Biblia na Shirley na mume wake katika Machi 1986, na muda si muda wakabatizwa. Sasa Shirley akata shauri hivi: “Ni vizuri ajabu kuujua ukweli, kujua kuhusu ufufuo, na kujua jinsi Yehova alivyo mtu mzuri ajabu.”

Ufufuo—Wakati Gani?

Katika njozi, mtume Yohana aliona “umati mkubwa ambao hakuna binadamu aliyeweza kuhesabu kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na ndimi, wakisimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo.” (Ufunuo 7:9, NW) Jambo la kwamba umati mkubwa huo ‘umesimama mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu’ lapatana na uhakika wa kwamba wao watazamia kuishi duniani. (Isaya 66:1) Ikiwa baadhi yao watakufa sasa, watafufuliwa wakati gani? Biblia haitoi tarehe, lakini itakuwa baada ya vita ile inayokaribia ambamo Mungu atawaondoa kabisa duniani wote wale wasio na nia ya kuishi kwa kufuata viwango vyake vya uadilifu. (2 Wathesalonike 1:6-9) Hiyo itafungua njia ya kuwako kwa Siku ya Hukumu na ufufuo wa wale ambao Mungu awaona kuwa wamo katika mstari wa kustahili ufufuo wa kidunia. (Yohana 5:28, 29, NW; Matendo 24:15, UV) Utimizo wa unabii wa Biblia wathibitisha kwamba matukio haya yenye kusisimua yaliyo ya ajabu yatatukia karibuni! —Ufunuo 16:14-16.

Wakati mmoja wanafunzi wa Yesu walimuuliza hivi: “Ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” Katika kujibu Yesu alitaja vita, upungufu wa vyakula, matetemeko ya dunia, magonjwa ya kipuku, na kuhubiriwa duniani pote kwa habari njema za Ufalme.—Mathayo 24:3-14; Luka 21:7-11, NW.

Unabii huu wa kutazamisha umekuwa ukitimizwa tangu 1914, wakati Vita ya Ulimwengu 1 ilipoanza. Iliua mamilioni na kutokeza njaa kubwa na upungufu wa vyakula katika nchi nyingi. Hali ya ulimwengu wakati wa Vita ya Ulimwengu 2 na baadaye ilikuwa mbaya zaidi.

Kwa habari ya magonjwa ya kipuku, watu wengi wahisi kwamba kielelezo kilicho kibaya zaidi ni UKIMWI. “Kipuku hicho kimeenea kwa mapana sana na kinaua sana hivi kwamba wastadi wanakilinganisha na kile Kifo Cheusi kilichoua robo moja ya idadi ya wakaaji wa Ulaya katika karne ya kumi na nne.”—Reader’s Digest, Juni 1987.

Kwa sababu ya maogofyo hayo ya wakati uliopo, lo, ufufuo utakuwa tukio zuri kama nini! Utakuwa wakati wa shangwe isiyoweza kukandamizwa wakati jamaa zilizotenganishwa na kifo, kama zile za Carolann na Shirley, zitakapoungana! Kwa uwazi, mwendo wa kiakili kwa kila mmoja wetu ni kupanga maisha zetu sasa zipatane na penzi la Mungu na hivyo tustahili kuwapo wakati ufufuo utakapotukia.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Wafu wale ambao Mungu anawakumbuka, Biblia yasema wanaweza kuinuka vile mti hukatwa na bado ukachipuka.—Ayubu 14:7-9, 14, 15

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki