Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 5/1 uku. 15
  • Ni Nini ‘Chenye Kuhitajiwa’?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nini ‘Chenye Kuhitajiwa’?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Kodeksi ya Vatikani—Kwa Nini Ni Yenye Thamani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Funzo Namba 6—Maandishi-awali ya Kigiriki ya Kikristo ya Maandiko Matakatifu
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kodeksi Bezae Hatimkono Isiyo na Kifani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • “Nimeamini”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 5/1 uku. 15

Ni Nini ‘Chenye Kuhitajiwa’?

HII Kodeksi W ya zile Gospeli imeshiriki sehemu fulani katika kutafsiriwa kwa elezo moja ambalo Yesu alimtolea Martha, dada ya Lazaro rafiki yake wa karibu. Yesu alipozuru jamaa ile, Martha aliwaza ni jambo la maana kabisa kutayarishia Yesu mlo mzuri, lakini Yesu akadokeza kwa fadhili kwamba yeye afuate kielelezo cha Mariamu dada yake, aliyeketi kwenye miguu yake kumsikiliza. Alisema hivi: “Ingawa hivyo, mambo machache yahitajiwa, au moja tu. Kwa upande wake, Mariamu alichagua aria njema, na haitaondolewa kutoka kwake.”—Luka 10:42, NW.

Maneno haya hutafsiri maandishi ya Kigiriki ya 1881 yaliyotayarishwa na Westcott na Hort, ambayo ndiyo msingi wa New World Translation. Maelezo ya chini kwenye Chapa Marejezo ya 1984 ya Biblia hiyo huonyesha kwamba msomeko huu ulitokana na hati-mkono za Sinaitic (א) na Vatican (B), zote mbili zikiwakilisha namna ile ile moja ya maandishi. Lakini hati-mkono ya Alexandrine (A) husomeka hivi: “Ingawa hivyo, jambo moja lahitajiwa kabisa. Kwa upande wake . . . ” Kama vile maelezo ya chini yaonyeshavyo wazi, Kodeksi W, na pia funjo la Chester Beatty (P45) na funjo la Bodmer (P75), yote mawili yakiwa ni ya karne ya tatu W.K., hukubaliana na fasiri hii ya mwisho. Lakini hati-mkono zote hizi ziligunduliwa muda mrefu baada ya Westcott na Hort kuchapisha maandishi yao katika mwaka 1881, hivi kwamba wao hawakuwa na fursa ya kufikiria fasiri hii ya namna nyingine. Ingawa hivyo, hata iwe ni tafsiri ipi ya andiko hilo ambayo tutachagua kutambua leo, Yesu atuambia wazi tuweke mambo ya kiroho kwanza katika maisha zetu—ushauri ambao ingefaa tuufuate.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki