Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 9/15 kur. 5-7
  • Upate Ukweli Wote!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Upate Ukweli Wote!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Ni Nani?
  • Cheo cha Yesu Ni Nini?
  • Ni Nini Litakalopata Dunia Mwishowe?
  • Kwa Nini Kuupata Ukweli Wote?
  • Utafute Ukweli Wote
  • Wakristo Huabudu kwa Roho na Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kwa Kweli ni Nani Walio na Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 9/15 kur. 5-7

Upate Ukweli Wote!

“NILIKUWA sijaona kamwe jina hilo katika Biblia yangu,” akasema Francisco. Jina Yehova lilikuwa ndipo tu limetokea katika mazungumzo pamoja na mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Kweli, yeye hangaliweza kuliona jina la Mungu katika Biblia yake, chapa ya 1969 ya fasiri yake ya Kireno Almeida. Lile jina Yehova halionekani humo. Akiwa Mkatoliki Mbrazili, Francisco huhudhuria Misa kwa ukawaida siku za Jumapili na huona shangwe kusoma Biblia nyumbani mwake. Lakini lile jina Yehova lilimchochea sana.

Mungu Ni Nani?

Juma lililofuata, Shahidi huyo alimletea chapa nyingine ya fasiri ya Almeida. Wakalinganisha chapa hizo mbili kwenye Zaburi 83:18. Nao wakapata nini? Katika chapa hiyo ya 1966, andiko hilo husomeka hivi: “Wewe, ambaye peke yako ndiwe mwenye kumiliki jina YEHOVA, ndiwe Aliye Juu Zaidi juu ya dunia”! Hata hivyo, katika chapa ya 1969, badala ya “YEHOVA” mtajo “BWANA” umetumiwa. “Waona, walibadili kitu fulani hapa,” akasema Shahidi huyo, halafu akauliza: “‘Bwana’ kwa uhakika si jina, au vipi?” “La,” akasema Francisco. Kwa kughadhibika kidogo, akaongezea hivi: “Wangewezaje kufanya hivyo?”

Hiyo ilifungua njia ya utafiti kidogo juu ya jina la Mungu. Mathalani, Francisco alijifunza kwamba kulingana na The Catholic Encyclopedia (1910), Yehova “ndilo jina lifaalo la Mungu katika Agano la Kale.” Pia alijifunza kwamba katika lugha ya Kiebrania, ambayo kwayo sehemu kubwa ya “Agano la Kale” iliandikwa, jina hilo huonekana mara karibu 7,000. Hakuna mtafsiri aliye na haki ya kubadili jina hususa la Yehova kwa mtajo wa cheo cha Bwana ambao si dhahiri. Francisco alitaka ukweli juu ya jina Yehova, naye akaupata kutokana na Biblia yenyewe na kupitia utafiti wenye mwongozo ufaao.

Cheo cha Yesu Ni Nini?

Kama ilivyosemwa katika makala iliyotangulia, dini za kilimwengu zimechafua kweli nyingi. Basi, katika huduma ya nyumba kwa nyumba, Mashahidi wa Yehova huwa na fursa ya kujua watu wanaamini nini. Bila shaka, huenda hiyo ikatofautiana mahali na mahali, lakini mawazo fulani huwa ya kikawaida. Mathalani, wenye nyumba waulizwapo, ‘Mungu ni nani?’ baadhi yao husema, ‘Yesu.’ Kwa kusema hivyo wao humaanisha kwamba Yesu ni Mungu Mweza Yote. Lakini je! wazo hilo huwakilisha ukweli?

Fikiria mambo yanayofuata. Yesu alisali hivi kwa Baba yake: “Hii ndiyo maana ya uhai wa milele, wapate maarifa ya kukujua wewe, Mungu wa kweli mmoja tu, na ya yeye uliyemtuma, Yesu Kristo.” (Yohana 17:3, NW) Je! uliona kwamba Yesu alirejezea, si yeye mwenyewe bali, Baba yake wa kimbingu kuwa ndiye “Mungu wa kweli mmoja tu”? Kwa hiyo, wanafunzi wa mapema wa Yesu walisema ifaavyo walipomwambia: “Hakika wewe u Mwana wa Mungu.” Yesu mwenyewe alisema: “Mimi ni Mwana wa Mungu.” Kwa hiyo, ukweli ni kwamba Yesu si Mungu Mweza Yote, bali yeye ni Mwana wa Yehova Mungu.—Mathayo 14:33; Yohana 10:36.

Ni Nini Litakalopata Dunia Mwishowe?

Namna gani jambo litakalopata kizazi hiki na dunia mwishowe? John F. Kennedy, aliyekuwa rais wa United States hapo zamani, alisema hivi katika hotuba kwa Kusanyiko Kuu la UM: “Sisi tuna nguvu ya kukifanya hiki kiwe ndicho kizazi bora kabisa cha ainabinadamu katika historia ya ulimwengu—au kukifanya kiwe ndicho cha mwisho.” Yaonekana viongozi wa ulimwengu wakati wa sasa wahisi ivyo hivyo. Jambo ambalo Mashahidi wa Yehova husikia mara nyingi katika huduma yao ni kwamba kwenye mwisho wa ulimwengu, Dunia sayari itaharibiwa kwa moto au kwa vita ya nyukilia. Kwa kuunga mkono imani hiyo, watu fulani huelekeza kwenye Ufunuo 21:1, NW, ambao husema: “Nikaona mbingu mpya na dunia mpya; kwa maana mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza zilikuwa zimepitilia mbali, na bahari haipo tena.”

Mara nyingi Biblia hutumia mtajo “dunia” katika maana ya kitamathali, ikirejezea ainabinadamu. Kielelezo kimoja chapatikana kwenye Mwanzo 11:1 (The Old Testament in Swahili [Mombasa], 1949), ambao wasema: “Dunia ilikuwa ya lugha moja na ya maneno mamoja.” (Ona pia 1 Wafalme 2:1, 2; Zaburi 96:1.) Kwenye Ufunuo 21:1, NW, “dunia ya kwanza” yarejezea, si sayari hii bali, jamii mbovu ya kibinadamu itakayoharibiwa. Hiyo itafungulia njia kurudishwa kwa Paradiso duniani. (Luka 23:43, ZSB; 2 Wathesalonike 1:6-9; Ufunuo 21:4) Na hilo laafikiana na sehemu nyingine yote ya Biblia, ambayo yaonyesha kwamba dunia halisi haitaharibiwa kamwe. Mathalani, Zaburi 104:5, NW, yataarifu kwamba Mungu “ameweka msingi wa dunia juu ya mahali payo palipoimarika; haitafanywa iyumbeyumbe kwa wakati usio dhahiri, wala milele.” (Linganisha Mhubiri 1:4.) Kwa kweli, Yehova ‘aliiumba dunia ili ikaliwe’ milele.—Isaya 45:18.

Kwa Nini Kuupata Ukweli Wote?

Vilivyotangulia ni vielelezo tu vya mawazo yenye makosa yaliyo ya kawaida sana leo. Hata hivyo, mwenye nyumba awapo na nia ya kusababu mambo, kama kilivyokuwa kisa cha Francisco, Mashahidi wa Yehova hupendezwa na jambo la kwamba njia iko wazi kwa mazungumzo yenye kutoa nuru ya kweli za Kimaandiko.

Kutopata ukweli wote huenda kukaongoza kwenye matokeo yenye majuto. Kutoa kielezi: Yesu alipokuwa duniani, wengi walishawishwa waamini kwamba yeye alikuwa mwana mwingine tu wa Mariamu na Yusufu, mtu ambaye hapo zamani alikuwa seremala tu wa kutoka Nazareti. Kwa sababu hiyo, hawakutoa uangalifu mwingi kuelekea yeye. Kwa kadiri fulani, walikuwa na maoni yafaayo. Yesu alikuwa mwana wa Mariamu, aliyechukuliwa mimba kwa roho takatifu. Alikuwa mwana mlelewa wa Yusufu, na kwa kweli alikuwa amefanya kazi akiwa seremala. (Marko 6:3) Hata hivyo, je! huo tu ulikuwa ndio ukweli wote juu yake? Sivyo! Yeye alikuwa Mesiya kamili akitazamiwa kuwa “Mfalme wa Wafalme”! (Ufunuo 17:14; Luka 1:32-35; Matendo 2:36) Kutopata ukweli wote juu ya Yesu kuliongoza watu wengi wakose pendeleo ambalo halitarudiwa kamwe—kupata shangwe ya ushirika wa kibinafsi pamoja na Yesu duniani.

Utafute Ukweli Wote

Jiji la Beroya (ambalo sasa laitwa Véroia) katika Makedonia ya kale lajulikana vizuri na wasomaji wa Biblia kwa sababu ya mtazamo wenye kupongezeka wa wakaaji walo wa karne ya kwanza. Ulikuwa mtazamo gani? Maandishi yasema: “Walilipokea lile neno [lililohubiriwa na mtume Paulo] kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku [kwa uangalifu, NW], waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.” Tokeo likawa nini? “Watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa Kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache.”—Matendo 17:11, 12.

Wala mtazamo wa manabii wa zamani wa Mungu haukukosa ustahili wa sifa kwa kadiri iyo hiyo. “Walitafuta-tafuta na kuchunguza-chunguza [kwa uangalifu, NW]” kuhusu wokovu ambao ungekuja kupitia Mesiya. (1 Petro 1:10) Mungu alibariki jitihada zao. Basi, kwa wazi, hakuna njia ya mkato. Kutafuta kwa udumifu na kuchunguza mafundisho kwa uangalifu—hiyo ndiyo njia ya kupata ukweli wote kutokana na Biblia!

Huenda wewe ukashangaa hivi, ‘Nianzie wapi?’ Baada ya kusoma vichapo fulani vya Kikristo, mwanamke mmoja mwenye kuishi katika Brazili aliandika hivi: “Muda si muda sisi [yeye na mume wake] tuling’amua kwamba tulihitaji kadiri nyingi zaidi ya maarifa ya aina hiyo, kupata majibu kwa maswali mengi tuliyokuwa nayo . . . Tafadhali, naweza kupataje Biblia na vitabu vingine ambavyo vitanisaidia nijue mengi zaidi juu ya Baba yetu wa kimbingu?” Mwanamke huyo alikuwa akifuata njia ifaayo: kusoma Biblia pamoja na fasihi za ukweli zenye msingi wa Biblia. Ikiwa wewe pia wataka ukweli wote, mfungulie Yehova Mungu moyo wako na uombe msaada wake. Na tafadhali angalia maneno haya yenye kutia moyo: “Mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa. Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote.”—Yakobo 1:5, 6.

Mamilioni ya watu wanazungumza juu ya Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, hivyo wakifanya maulizio yenye bidii ya uendelevu na kuutafuta ukweli kwa uangalifu. Kutwaa na kutumia hayo maarifa sahihi ya Mungu wa kweli na ya Yesu Kristo humaanisha uhai wa milele. (Yohana 17:3) Hiyo yaweza kuwa baraka yako kubwa ukiutafuta na kuupata ukweli wote kwa bidii ya uendelevu.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Ukweli wote juu ya Yesu ulikuwa kwamba yeye alikuwa ndiye Mesiya, wala si seremala tu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki