Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 9/15 kur. 8-9
  • Sala ya Kumalizia Katika Chumba cha Juu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sala ya Kumalizia Katika Chumba cha Juu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Sala ya Mwisho ya Yesu Katika Chumba cha Juu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Kuwatayarisha Mitume kwa Ajili ya Kuondoka Kwake
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Tenda Kupatana Na Sala Ya Yesu Ya Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • “Nifuateni, Nami Nitawafanya Kuwa Wavuvi Watu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 9/15 kur. 8-9

Maisha na Huduma ya Yesu

Sala ya Kumalizia Katika Chumba cha Juu

KWA kusukumwa na upendo wa kina kirefu kwa mitume wake, Yesu amekuwa akiwatayarisha kwa ajili ya mwondoko wake ulio karibu. Sasa, baada ya kuwaonya kwa upole na kuwafariji kirefu, ainua macho yake mbinguni na kumwomba Baba yake kwa bidii hivi: “Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe; kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.”

Lo, Yesu afanya utangulizi wa kichwa chenye kuchochea kama nini—uhai wa milele! Akiisha kupewa “mamlaka juu ya wote wenye mwili,” Yesu aweza kuipa ainabinadamu yote yenye kufa manufaa za dhabihu yake ya ukombozi. Hata hivyo yeye huwapa “uzima wa milele” wale tu ambao Baba awakubali. Akikuza kichwa hiki cha uhai wa milele, Yesu aendelea na sala yake hivi:

“Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.” Ndiyo, wokovu wategemea kutwaa kwetu maarifa juu ya wote wawili, Mungu na Mwana wake. Lakini mengi zaidi yahitajiwa kuliko maarifa ya kichwani tu.

Ni lazima mtu apate kuwajua kindani, akisitawisha urafiki wenye uelewano pamoja nao. Ni lazima mtu ahisi kama vile wao huhisi juu ya mambo na ayaone kupitia macho yao. Na juu ya yote, ni lazima mtu ajitahidi kuiga sifa zao zisizo na kifani katika kushughulika na wengine.

Halafu Yesu asali hivi: “Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.” Akiwa ametimiza mgawo wake hivyo kufikia hapo na kuwa mwenye uhakika juu ya mafanikio yake ya wakati ujao, aomba kwa bidii hivi: “Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.” Naam, sasa aomba kwamba kwa njia ya ufufuo arudishwe kwenye utukufu wa kimbingu aliokuwa nao hapo kwanza.

Akitoa muhtasari wa kazi yake kuu duniani, Yesu asema hivi: “Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika.” Yesu alitumia jina la Mungu, Yehova, katika huduma yake na akaonyesha tamko lalo sahihi, lakini alifanya mengi zaidi ya kudhihirisha jina la Mungu kwa mitume. Pia alipanua maarifa na uthamini wao juu ya Yehova, juu ya utu wake, na juu ya kusudi lake.

Akimpa Yehova sifa ya kuwa Mkuu kuliko yeye, Mmoja ambaye yeye hutumika chini yake, Yesu akiri kwa unyenyekevu hivi: “Maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”

Akifanya upambanufu kati ya wafuasi wake na wale wengine wa ainabinadamu, Yesu asali hivi halafu: “Siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa . . . Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda . . . , nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu,” yaani, Yuda Iskariote. Wakati huo huo, Yuda yuko kwenye safari yake ya kudharaulika ili amsaliti Yesu. Hivyo, bila kujua Yuda anatimiza Maandiko.

“Ulimwengu umewachukia,” Yesu aendelea kusali. “Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu. Wao si wa ulimwengu [si sehemu ya ulimwengu, NW], kama mimi nisivyo wa ulimwengu.” Wafuasi wa Yesu wamo katika ulimwengu, jamii hii ya kibinadamu iliyopangwa kitengenezo yenye kutawalwa na Shetani, lakini wao wametengeka na ni lazima wabaki sikuzote wakiwa wametengeka kutoka kwao na uovu wao.

“Uwatakase kwa ile kweli,” Yesu aendelea, “neno lako ndiyo kweli.” Hapa Yesu ayaita “kweli” Maandiko ya Kiebrania, ambayo alinukuu kutokana nayo kwa uendelevu. Lakini yale aliyowafundisha wanafunzi wake na yale waliyoyaandika baadaye chini ya uvuvio yakiwa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ni “kweli” vilevile. Ukweli huu waweza kutakasa mtu, ubadili maisha yake kabisa, na kumfanya mtu aliyetengeka kutoka kwenye ulimwengu.

Sasa Yesu ‘haombei hao tu; lakini na wale watakaomwamini kwa sababu ya neno lao.’ Kwa hiyo Yesu asali kwa ajili ya wale watakaokuwa wafuasi wake wapakwa-mafuta na wanafunzi wengine wa wakati ujao ambao bado watakusanywa ndani ya “kundi moja.” Yeye aomba nini kwa ajili ya wote hao? “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu [ulivyo katika mwungano pamoja nami, NW], nami ndani yako . . . ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.”

Yesu na Baba yake si mtu mmoja kihalisi, bali wana mwafaka juu ya mambo yote. Yesu asali kwamba wafuasi wake wapate shangwe ya umoja uo huo ili “ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.”

Kwa ajili ya wale ambao wangekuwa wafuasi wake wapakwa-mafuta, Yesu aomba kwamba: “Wawe pamoja nami po pote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi [wa] ulimwengu,” wakati Adamu na Hawa walipotunga mimba ya wazao wao wa kwanza. Muda mrefu kabla ya hapo, Mungu alipenda Mwana wake mzaliwa pekee, ambaye akawa Yesu Kristo.

Akimalizia sala yake, Yesu akazia tena hivi: “Naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; [ili] pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao [katika mwungano pamoja nao, NW].” Kwa mitume, kujifunza jina la Mungu kumehusisha kupata kuujua kibinafsi upendo wa Mungu. Yohana 17:1-26; 10:16; Mithali 8:22, 30.

◼ Ni katika maana gani Yesu amepewa “mamlaka juu ya wote wenye mwili”?

◼ Yamaanisha nini kutwaa maarifa juu ya Mungu na Mwana wake?

◼ Ni katika njia zipi Yesu alidhihirisha jina la Mungu?

◼ “Kweli” ni nini, nayo ‘yatakasaje’ Mkristo?

◼ Ni jinsi gani Mungu, Mwana wake, na waabudu wote wa kweli walivyo mmoja?

◼ ‘Kuwekwa msingi wa ulimwengu’ kulikuwa lini?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki