Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 9/15 kur. 26-27
  • “Endeleeni Kutahini Kama Nyinyi Mmo Katika Imani”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Endeleeni Kutahini Kama Nyinyi Mmo Katika Imani”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hudumia Mungu wa Faraja
  • Kamilisha Utakatifu na Uwe Mkarimu
  • Paulo—Mtume Mwenye Kujali
  • Endelea Kutahini!
  • Kitabu Cha Biblia Namba 47—2 Wakorintho
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kupata Kuwajua Wakristo wa Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • 2 Wakorintho—Yaliyomo
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Kitabu Cha Biblia Namba 46—1 Wakorintho
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 9/15 kur. 26-27

“Endeleeni Kutahini Kama Nyinyi Mmo Katika Imani”

Mambo Makuu Kutoka Wakorintho ya Pili

MTUME Paulo aliwahangaikia Wakristo katika Korintho. Wao wangelionaje shauri lililotolewa katika barua yake ya kwanza kwao? Yeye alikuwa katika Makedonia wakati Tito alipowasili akiwa na ripoti yenye kupendeleka kwamba barua hiyo ilikuwa imewahuzunisha Wakorintho wakatubu. Lo, hiyo ilifanya Paulo ashangilieje!—2 Wakorintho 7:8-13.

Paulo aliandika Wakorintho ya Pili akiwa Makedonia, labda baada ya mwaka kufika katikati katika 55 W.K. Katika barua hii, yeye alizungumza juu ya hatua zilizopasa kuchukuliwa kuweka kundi likiwa safi, kusitawisha tamaa ya kuwachangia wahitaji katika Yudea, na kutetea utume wake. Mengi ya aliyosema Paulo yaweza kutusaidia ‘tuendelee kutahini kama sisi tumo katika imani.’ (13:5, NW) Hivyo basi, twaweza kujipatia nini kutokana na barua hii?

Hudumia Mungu wa Faraja

Mtume alionyesha kwamba kama vile Mungu hutufariji sisi katika dhiki zetu zote, twapaswa kuwafariji wengine na kusali kwa ajili yao. (1:1–2:11) Ingawa Paulo na washirika wake walikuwa chini ya mkazo wa kupita kiasi, Mungu aliwaokoa. Hata hivyo, Wakorintho wangeweza kusaidia kwa sala zenye kutolewa kwa ajili yao, kama vile sisi twapaswa kusali kwa ajili ya wengine wenye kufuata imani ya kweli kwa moyo. Lakini namna gani juu ya mwanamume mkosa adili aliyetajwa katika 1 Wakorintho sura ya 5? Yaonekana alikuwa ametengwa na ushirika lakini akawa ametubu. Ni lazima awe alifarijiwa kama nini wakati Wakorintho walipomsamehe na kumrudisha kwa upendo katikati yao.

Maneno ya Paulo yaweza kuongeza uthamini wetu kwa huduma ya Kikristo, yakiimarisha msimamo wetu kwa ajili ya imani ya kweli. (2:12–6:10, NW) Kwani, wahudumu wa agano jipya wamependelewa kuwa katika “andamano lenye shangwe ya ushindi” Mungu akiwa ndiye aongoza! Paulo na wafanya kazi wenzake walikuwa na huduma iliyo hazina kubwa kwa sababu ya rehema waliyoonyeshwa. Kama wao, wapakwa-mafuta wa siku hizi wana huduma ya upatanisho. Hata hivyo, Mashahidi wote wa Yehova hutajirisha wengine kupitia huduma yao.

Kamilisha Utakatifu na Uwe Mkarimu

Paulo atuonyesha kwamba ni lazima wahudumu Wakristo wakamilishe utakatifu katika hofu ya Yehova. (6:11–7:16) Ikiwa sisi tutasimama imara katika imani, ni lazima tuepuke kufungwa nira pamoja na wasioamini, nasi twahitaji kusafishwa uchafu wa kimnofu na wa kiroho. Wakorintho walifanya kitendo cha kusafisha kwa kumtenga na ushirika mtenda kosa aliyekuwa mkosefu wa adili, na Paulo alishangilia kwamba barua yake ya kwanza ilikuwa imewahuzunisha wawe na toba yenye kuleta wokovu.

Sisi pia twajifunza kwamba wahudumu wenye kuhofu Mungu huthawabishwa kwa ukarimu wao. (8:1–9:15) Kuhusu michango kwa ajili ya “watakatifu” wenye uhitaji, Paulo alitaja kielelezo kizuri cha Wamakedonia. Walikuwa wamekuwa wakarimu kupita uwezo wao, naye alitumainia kuona ukarimu wa aina iyo hiyo kwa upande wa Wakorintho. Kutoa kwao—na kwetu—kwapasa kutoke moyoni, kwa maana “Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu” na hutajirisha watu wake kwa ajili ya kila namna ya ukarimu.

Paulo—Mtume Mwenye Kujali

Wakati sisi tufanyapo jambo lolote katika utumishi wa Yehova tukiwa wahudumu, acheni tujisifu katika yeye, wala si katika sisi wenyewe. (10:1–12:13) Ingawaje, ni kwa kuwa na silaha za kiroho ‘zenye uwezo kwa Mungu’ tu kwamba twaweza kupindua mawazo yenye kusababiwa kwa ubandia. Wale “mitume walio wakuu” waliokuwa miongoni mwa Wakorintho hawangeweza kamwe kulingana na rekodi ya Paulo ya uvumilivu akiwa mhudumu wa Kristo. Hata hivyo, ili yeye asije akakwezwa kupita kiasi, Mungu hakuondoa ‘mwiba wake katika mwili’—labda kutokuona vizuri au mitume hao bandia. Paulo aliona afadhali tu ajisifie manyonge yake ili “uweza wa Kristo” uweze kubaki juu yake kama hema. Akiwa mwanamume aliyesimama imara katika imani, yeye hakuwa amethibitika kuwa wa hali ya chini kuliko hao mitume walio wakuu. Wakorintho walikuwa wameiona vithibitisho vya utume ambavyo Paulo alikuwa ametokeza miongoni mwao “katika saburi yote, kwa ishara na maajabu na miujiza.”

Akiwa mhudumu na akiwa mtume, Paulo alizingatia moyoni masilahi ya kiroho ya waamini wenzake, kama vile sisi pia tupaswavyo kufanya. (12:14–13:14) Yeye ‘angetapanywa kwa furaha nyingi kwa ajili ya roho [nafsi, NW] zao.’ Lakini Paulo alihofu kwamba akiisha kuwasili katika Korintho, angepata watu fulani ambao wasiokuwa wametubu juu ya kazi za mnofu. Kwa sababu hiyo, aliwashauri wote waendelee kutahini kama wamo katika imani na wasali ili ‘wasifanye lolote lililo baya.’ Kwa umalizio, aliwahimiza washangilie, warekebishwe upya na kufarijiwa, wafikiri kwa kuafikiana, na waishi kiamani. Lo, shauri zuri kama nini kwa sisi pia!

Endelea Kutahini!

Hivyo barua ya pili ya Paulo kwa Wakristo Wakorintho yadokeza njia mbalimbali za kuendelea kutahini kama tumo katika imani. Kwa uhakika maneno yake yapasa kutusukuma tufariji wengine, kama vile Mungu hutufariji sisi katika dhiki yetu yote. Mambo aliyosema mtume juu ya huduma ya Kikristo yapasa yatuchochee tuitimilize kwa uaminifu huku tukikamilisha utakatifu katika hofu ya Yehova.

Kutumia shauri la Paulo kungeweza kutufanya wakarimu na wenye kusaidia zaidi. Hata hivyo, maneno yake yapasa yatusukume kujisifu katika Yehova, si katika sisi wenyewe. Yapaswa kuongeza kimo cha hangaiko letu lenye upendo kwa waamini wenzetu. Na kwa uhakika mambo haya na mengine katika Wakorintho ya Pili yaweza kutusaidia ‘tuendelee kutahini kama sisi tumo katika imani.’

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 26]

FANYA MRUDISHO WA UTUKUFU WA YEHOVA: Musa aliposhuka kutoka Mlima Sinai akiwa na mabamba ya Ushuhuda, uso wake ulitoa mionzi kwa sababu Mungu alikuwa amesema naye. (Kutoka 34:29, 30) Paulo alitaja hilo na kusema hivi: “Sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana [Yehova, NW], kama vile katika kioo, tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho.” (2 Wakorintho 3:7-18) Vioo vya kale vya utumizi wa mkononi vilifanywa kwa metali kama shaba nyeusi au shaba nyekundu na kung’arishwa sana ili viwe na nyuso zenye kurudisha nuru. Kama vioo, wapakwa-mafuta hurudisha utukufu wa Mungu ambao huwaangazia wao kutoka kwa Yesu Kristo, kidato kwa kidato ‘wakibadilishwa umbo wafanane na mfano’ wenye kutokezwa na Mwana wa Yehova mwenye kurudisha nuru ya utukufu Wake. (2 Wakorintho 4:6; Waefeso 5:1) Kupitia roho takatifu na Maandiko, Mungu huumba ndani yao “utu mpya,” mrudisho-nuru wa sifa zake mwenyewe. (Waefeso 4:24; Wakolosai 3:10) Kama tumaini letu ni la kimbingu au la kidunia, acheni tuonyeshe utu huo na kulithamini sana pendeleo la kurudisha nuru ya utukufu wa Mungu katika huduma yetu.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 27]

“SILAHA ZA HAKI [UADILIFU, NW]”: Njia moja ambayo Paulo na washirika wake walijipendekeza kuwa wahudumu wa Mungu ilikuwa “kwa silaha za haki [uadilifu, NW] za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto.” (2 Wakorintho 6:3-7) Mkono wa kuume ulitumiwa kupunga upanga, na wa kushoto kushika ngao. Ingawa walishambuliwa kutoka pande zote, Paulo na wafanya kazi wenzake walizatitiwa kufanya vita ya kiroho. Ilifanywa dhidi ya walimu bandia na “mitume walio wakuu” ili kundi la Korintho lisiongozwe mbali kutoka kwenye ujitoaji kwa Kristo. Paulo hakugeukia silaha za mnofu wenye dhambi—ujanja, udanganyifu, wala kufanya hila. (2 Wakorintho 10:8-10; 11:3, 12-14; 12:11, 16) Bali, “silaha” zilizotumiwa zilikuwa njia za uadilifu, au za haki, za kusogeza mbele lengo la ibada ya kweli dhidi ya mashambulio yote. Sasa Mashahidi wa Yehova hutumia hizo ‘silaha za uadilifu’ kwa kusudi ilo hilo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki