Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 10/1 uku. 3
  • Je! Wewe Una Hamu Sana Kuuona Wakati Ambapo . . .

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Una Hamu Sana Kuuona Wakati Ambapo . . .
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Ugaidi Utakoma Karibuni!
    Amkeni!—2001
  • Yaliyomo
    Amkeni!—2005
  • Ni Nini Husababisha Ukosefu wa Makao?
    Amkeni!—2005
  • Je, Ugaidi Utakwisha?
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 10/1 uku. 3

Je! Wewe Una Hamu Sana Kuuona Wakati Ambapo . . .

◻ wewe waweza kuhisi salama salimini katika nyumba yako—hata uwe ni wakati gani wa siku?

◻ hakutakuwa na uhitaji wa kufuli, makomeo, ving’ora, vitundu vya kuchungulia mlangoni, nyua za kuzungukia nyumba, walinzi, mbwa walinzi, na vilinda-usalama vinginevyo?

◻ waweza kutembea barabarani ukiwa peke yako katika usalama kamili, hata usiku?

◻ dawa za kulevya zenye kudhuru na matatizo yote yenye kuhusiana nazo yatakuwa kumbukumbu la zamani za kale?

◻ vita vyote vitakuwa vimekoma, na silaha zisifanyizwe wala zisirundikwe?

◻ hutalazimika tena kuwa na wasiwasi juu ya chakula, hewa na maji yaliyochafuzwa?

◻ ugaidi, kutekwa kwa watu nyara, na vitisho vya makombora vitaondolewa kabisa?

◻ mali za asili za dunia zitalindwa, zidumishwe, na kutumiwa kwa hekima kwa manufaa ya wote?

◻ pupa na ubinafsi hazitakuwa tena kani zenye kusukuma ainabinadamu?

◻ watoto watakapodumisha hali yao isiyo na hatia na kuwa wastahifu kwa wengine na mali zao?

◻ wanawake hawataonewa na kuchukuliwa kama wahanga wa kutendwa yasiyofaa?

◻ sheria na virekebi vitakapokuwa vya haki na kutekelezwa kwa haki kwa manufaa ya wote?

◻ serikali itakafanya maamuzi kwa msingi wa mahitaji halisi wala si kwa msingi wa siasa?

◻ uhuru na usawa hautakuwa ukihubiriwa tu bali pia ukizoewa?

◻ umaskini hautakuwako tena, bali wote watakuwa na vyote vyenye kuhitajiwa kwa afya, hali njema, na furaha yao?

◻ watoto watatakiwa na kutunzwa na wasitumiwe tena vibaya wala kuachwa peke yao?

◻ magonjwa na kifo vitakuwa vimewezwa kabisa, na kusiwe na tauni za kutisha?

◻ kila mtu ukutanaye naye atakuwa mwenye fadhili, mwenye kusaidia, na mwenye kutumainika?

◻ uhai wa kila mtu utathaminiwa kikweli, na wote waweze kupata furaha ya kudumu?

◻ dini haitakuwa tena kani ya migawanyiko, yenye kuongoza kwenye ushupavu, chuki, na vita?

◻ wote watakuwa na makao ya kutosha yenye kupendeza, na ukosefu wa nyumba uwe jambo la zamani?

Ikiwa waweza kusema ndiyo kwa lolote la hayo yaliyo juu, utapendezwa kusoma makala zifuatazo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki