Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 12/1 uku. 30
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Kushindana na Mshiko wa Dhambi Juu ya Mwili Wenye Dhambi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Wekeni Akili Juu ya Roho Mkaishi!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Tembea Kupatana na Roho ili Upate Uzima na Amani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Tunahitaji Sifa ya Kujizuia
    Mwimbieni Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 12/1 uku. 30

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Kwenye Warumi 8:27, New World Translation inafasiri neno la Kigiriki phroʹne·ma kuwa “kumaanisha” (“maana”), lakini katika mistari 6 na 7, fasiri ni “kuweka akili.” Kwa sababu gani neno lile lile moja la Kigiriki limetafsiriwa tofauti?

Habari zinazozunguka zinapendekeza fasiri mbili hizo zilizochaguliwa.

Dibaji ya New World Translation of the Christian Scriptures (1950) ilisema hivi: “Kwa kila neno kuu tumegawia maana moja na kushikilia maana hiyo kwa kadiri ambavyo habari zinazozunguka ziliruhusu.” Watu fulani hawangechukua kwamba phroʹne·ma ni neno kuu, kwa kuwa hutukia mara nne tu. Ingawa hivyo, linahusiana na maneno yanayotumiwa mara nyingi zaidi. Moja ni phro·neʹo, linalomaanisha “kufikiri, kuweka akili katika njia fulani.” (Mathayo 16:23; Marko 8:33; Warumi 8:5; 12:3; 15:5) Maneno mengine ya Kigiriki yanayohusiana yanatoa wazo la kutumia hekima yenye kutumika, akili nzuri, au utambuzi.—Luka 1:17; 12:42; 16:8; Warumi 11:25; Waefeso 1:8.

The Kingdom Interlinear Translation of the Greek Scriptures inaonyesha kwamba phroʹne·ma linatukia mara nne kwenye Warumi 8:6, 7, 27 na kwamba maana yake halisi inakuwa “kuweka akili.” Wanachuo Wagiriki Bauer, Arndt, na Gingrich wanaeleza phroʹne·ma hivi: ‘njia ya kufikiri, (kuweka) akili, lengo, tamanio kuu, kujitahidi.’—A Greek-English Lexicon of the New Testament and Other Early Christian Literature.

Katika Warumi sura ya 8, mtume Paulo alishauri Wakristo wasitembee kulingana na mwili usiokamilika wa kibinadamu. Ili kufanikiwa katika jambo hili, wanapaswa kujikinga na maelekeo au misisimuko ya mwili, na pia njia za kusababu za moyo usiokamilika. ‘Kuweka akili zao’ juu ya mambo yanayopatana na roho takatifu ya Mungu kutasaidia katika jambo hili.—Warumi 8:1-5, NW.

Paulo alitoa utofauti huu: “Kuweka akili juu ya mnofu kwamaanisha kifo, lakini kuweka akili juu ya roho kwamaanisha uhai na amani; kwa sababu kuweka akili juu ya mnofu kwamaanisha uadui pamoja na Mungu, kwa maana huo hauko chini ya ujitiisho kwa sheria ya Mungu.” (Warumi 8:6, 7, NW) Wanadamu ndio wanaotajwa katika mistari hii miwili. Wanadamu, hasa Wakristo, hawapaswi ‘kuweka akili’ yao juu ya mambo ya mwili wenye dhambi. Bali, wanapaswa kuwa ‘wakiweka akili’ zao juu ya mambo yanayopatana na roho na yenye kuchochewa nayo.

Kwa utofauti, mstari wa 27 unashughulika na Mungu mwenyewe. Tunasoma hivi: “Hata hivyo yeye [Yehova] ambaye hupekua mioyo ajua ni nini maana ya roho, kwa sababu inasihi kupatana na Mungu kwa ajili ya watakatifu.” Ndiyo, “yeye” hapa ni Yehova, yule Msikiaji wa sala.

Neno phroʹne·ma lingaliweza kutafsiriwa katika mstari wa 27 kuwa “kuweka akili.” Lakini roho takatifu si mtu ambaye kwa kweli anafikiri au mwenye kufikiri kwake mwenyewe. Roho ni nguvu ya utendaji ya Mungu, ambaye anajua jinsi roho takatifu yake inafanya kazi katika kutimiza mapenzi yake. Zaidi ya hilo, maana ya mstari huu ni tofauti ni ile ya Warumi 8:6, 7. Mistari hiyo ya mapema kidogo ilikazia uhitaji ambao wanadamu wanao kudhibiti kufikiri na vitendo vyao. Lakini Yehova halazimiki kujitahidi, au kung’ang’ana, ili ajidhibiti (ajiongoze vizuri) mwenyewe. Yeye anajua yaliyoandikwa katika Biblia chini ya uvuvio, kama vile semi za Kibiblia zinazoonyesha mapenzi yake kwa watumishi wake wa kidunia. Dakt. Heinrich Meyer anaeleza hivi juu ya Warumi 8:27: “Mungu angejua kusudi la Roho katika kila kisa.”

Kwa hiyo, kule kufasiri “kumaanisha” kunapatana na habari zinazozunguka au uzito wa Warumi 8:27, na kunaruhusiwa na Kigiriki chenyewe. The Translator’s New Testament inaufasiri hivi: “Yeye ambaye hupekua mioyo ajua kile ambacho Roho humaanisha.”

◼ Kwa nini nyakati fulani New World Translation inafasiri neno la Kigiriki pi·steuʹo kuwa ”amini”(kama tafsiri zilizo nyingi) na nyakati nyingine kuwa ”jizoeze [au tia] imani katika”?

Hili linafanywa ili kuonyesha tofautitofauti za maana ambazo zinatolewa na neno la Kigiriki pi·steuʹo.

Kwa mfano, A Grammar of New Testament Greek, cha James Moulton, kinasema kwamba Wakristo wa mapema walitambua wazi “umaana wa tofauti iliyopo kati ya imani tu . . . na amana ya kibinafsi.” Mawazo yote haya mawili yanaweza kuelezwa kwa kutumia lile neno la Kigiriki pi·steuʹo.

Mara nyingi, tofautitofauti za maana ya pi·steuʹo ni lazima zitambuliwe kutokana na habari zinazozunguka. Ingawa hivyo, nyakati fulani miundo tofauti ya kisarufi inatusaidia tuone jambo ambalo mwandikaji alikuwa nalo akilini. Kwa mfano, ikiwa pi·steuʹo linafuatwa na nomino (jina) ya mhusika asiye wa moja kwa moja katika kitendo, kwa kawaida New World Translation inalifasiri “amini”—isipokuwa kama habari zinazozunguka zinaonyesha jambo tofauti. (Mathayo 21:25, 32; lakini ona Warumi 4:3.) Ikiwa pi·steuʹo linafuatwa na neno e·piʹ, “juu ya,” kwa ujumla linafasiriwa “amini juu ya.” (Mathayo 27:42; Matendo 16:31) Ikiwa linafuatwa na eis, “kwa,” kwa kawaida linatafsiriwa “jizoeze imani katika.”—Yohana 12:36; 14:1.

Fasiri hii ya mwisho (inayotukumbusha kwamba pi·steuʹo limetolewa katika neno la Kigiriki pi·stosʹ, “imani”) inapatana na elezo moja katika An Introductory Grammar of New Testament Greek, cha Paul Kaufman. Kichapo hiki kinasema hivi: “Muundo mwingine ulio wa kawaida katika Agano Jipya (hasa katika Gospeli ya Yohana) ni πιστεύω [pi·steuʹo] pamoja na εἰς [eis] na hali ya kitendewa . . . Muundo mzima wa εἰς kuongezea hali ya kutendewa ni lazima utafsiriwe badala ya kujaribu kutafsiri kiambishi-kionyeshi εἰς kikiwa neno lililo peke yalo. Imani inafikiriwa kuwa utendaji, kuwa jambo fulani ambalo wanadamu wanafanya, yaani, kutia imani ndani ya mtu fulani.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki