Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 4/1 kur. 16-19
  • Jitihada Ya Ainabinadamu Kutafuta-tafuta Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jitihada Ya Ainabinadamu Kutafuta-tafuta Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Chombo Chenye Kutumika
  • Msingi wa Kuwa na Mafunzo ya Biblia
  • Kutoa Ushahidi kwa Watu wa Lugha na Dini Zote
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Kwa Nini Kupendezwa na Dini Nyingine?
    Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
  • Uhitaji wa Ainabinadamu wa Kutafuta-Tafuta Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Jinsi Unavyoweza Kujibu Vizuia-Mazungumzo Vikitokea
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 4/1 kur. 16-19

Jitihada Ya Ainabinadamu Kutafuta-tafuta Mungu

KWA nini sisi, tulio Mashahidi wa Yehova, tumepewa “lugha iliyo safi”? Hakika, si ili tujiwekee sisi wenyewe tu. Na si ili tuweze kuonea shangwe mtindo-maisha ulio kama mwendo wa Jumuiya ya Wakristo wa kujilegeza na kuridhiana. Bali, ni ili kwamba ‘wote wapate kuliitia jina la Yehova, ili wamtumikie bega kwa bega.’ (Sefania 3:9, NW) Ndiyo, lugha iliyo safi yahusisha utendaji wa bega kwa bega pamoja na mamilioni ya ndugu na dada zetu Wakristo—kutoka rangi zote, mataifa, na lugha—ambao wanahubiri kwa uaminifu zile habari njema kabla ya mwisho kuja.—Marko 13:10; Warumi 13:11; Ufunuo 14:6, 7.

Kuhubiri kwetu leo nyakati fulani hutokeza miito ya ushindani isiyo ya kawaida. Kwa nini? Katika karne ya 20 hii, kumekuwa na mihamo ya watu kutokana na vita, uonevu, misongo ya kiuchumi, na kwa sababu nyinginezo. Tokeo ni kwamba, watu wa lugha na dini nyingi wamehamia ndani ya tamaduni zisizo zao wenyewe. Hivyo, jumuiya kubwa-kubwa za Wahindu, Wabuddha, na Waislamu zimehamia ndani ya ulimwengu wa Magharibi. Tushirikipo lugha iliyo safi kutoka nyumba kwa nyumba, twawakuta watu hawa. Nyakati fulani sisi hutatanika kwa sababu twajua kidogo sana juu ya malezi yao ya kidini. Twaweza kufanya nini juu ya hilo?—Linganisha Matendo 2:5-11.

Tushirikije ukweli pamoja na Mwislamu au Myahudi? Wao watofautianaje? Mhindu huamini nini kwa kweli? Kwa nini Wasiki (Wakalasinga) huvaa vilemba? Ni nini kitabu chao kitakatifu? Mbuddha atofautianaje na Mhindu? Washinto Wajapani huamini nini? Je! Watao Wachina au Wakonfyushasi huamini katika Mungu?a Myahudi Mworthodoksi atofautianaje na Myahudi Mmarekebisho au Myahudi Asiye Mmarekebisho? Ili kufikia unamna-namna mkubwa huu wa watu, ni lazima kwanza kabisa tuelewe maoni yao na ndipo tujue jinsi ya kuwaelekeza kwa njia fulani ya fadhili na busara kwenye Mungu wa kweli, Yehova.—Matendo 17:22, 23; 1 Wakorintho 9:19-23; Wakolosai 4:6.

Kutusaidia tuwe na uelewevu wa wazi zaidi juu ya dini nyinginezo, mafundisho yazo, na malezi yazo ya kihistoria, Watch Tower Society ilitoa kotekote ulimwenguni wakati wa Mikusanyiko “Lugha Iliyo Safi” ya 1990 kichapo kipya chenye kichwa Mankind’s Search for God. Tukiwa na chombo hiki, tutaweza vizuri zaidi kuhubiria watu wa ulimwengu usio wa Kikristo na pia wale wa Jumuiya ya Wakristo.

Chombo Chenye Kutumika

Kitabu hiki cha kurasa 384 kina sura 16 ambazo zasimulia historia ya kumtafuta-tafuta Mungu kwa ainabinadamu muda wa miaka elfu sita iliyopita. Chajibu mamia ya maswali juu ya dini za ulimwengu. Huu ni mfano wa baadhi yayo: Kwa kawaida ni mambo gani ambayo huamua dini ya mtu itakuwa gani? Kwa nini si kosa kuchunguza imani nyinginezo? Kuna mafanano gani kati ya Ukatoliki wa Kiroma na Ubuddha? Hadithi za kutungwa hushiriki sehemu gani katika dini nyingi? Kwa nini watu wengi huamini katika mazingaombwe, uwasiliano na roho waovu, na unajimu? Kwa nini Wahindu wana miungu mingi na miungu-wake wengi sana? Wasiki (Wakalasi-nga) watofautianaje na Wahindu? Buddha alikuwa nani, naye alifundisha nini? Kwa nini Ushinto ni dini ya Kijapani hasa? Kwa nini Wayahudi wana sheria ya kupokezwa kwa mdomo na pia iliyoandikwa? Twajuaje kwamba Kristo si hadithi ya kutungwa? Korani yatofautianaje na Biblia? Kwa nini Wakatoliki husema kwamba Petro ndiye aliyekuwa papa wa kwanza? Kwa nini Lutheri padri Mkatoliki alivunja uhusiano kutoka kwenye Kanisa Katoliki la Kiroma?

Maswali ni kama yasiyokwisha, na kichapo hiki kimejaa majibu ili sisi tuweze kuwahubiria kwa matokeo zaidi watu wenye malezi mbalimbali ya kidini. Kitabu hiki chatambua kwamba watu wengi wana dini yao wenyewe na kwamba dini ni kitu cha kibinafsi sana. Hata hivyo, katika ukurasa wa 8, chasema hivi: “Kuanzia uzaliwa hasa mawazo ya kidini au ya kiadabu hupandwa katika akili yetu na wazazi wetu na watu wa ukoo. Tokeo ni kwamba, kwa kawaida sisi hufuata mawazo ya kidini ya wazazi wetu na wazazi wakuu.” Hiyo yamaanisha kwamba “katika visa vingi wengine ndio wametuchagulia dini yetu. Imekuwa hivyo kwa sababu tu ya mahali tulipozaliwa na wakati tulipozaliwa.”—Linganisha Wafilipi 3:4-6.

Ndipo kitabu hiki chatokeza lile swali la ufikiri mzuri. “Je! ni jambo la akili kuchukua kwamba dini iliyowekwa juu ya mtu wakati wa kuzaliwa ndiyo kwa lazima iliyo ukweli mzima?” Hivyo, kila mtu atiwa moyo kuchunguza dini nyinginezo kwa akili iliyofunguka. Kama vile isemwavyo katika ukurasa wa 10: “Kuelewana maoni mtu na mwenzake kwaweza kuongoza kwenye uwasiliano na maongezi yenye maana zaidi kati ya watu wa imani tofauti-tofauti.” Chaendelea hivi: “Ni kweli, huenda watu wakakosa kukubaliana juu ya imani zao za kidini, lakini hakuna msingi wa kuchukia mtu kwa sababu tu yeye ana maoni tofauti.”—Mathayo 5:43, 44.

Swali moja la msingi ambalo hutokea kotekote katika kitabu ni, Je! binadamu ana nafsi isiyoweza kufa ambayo huendelea kuwa hai na kusonga mbele kwenye uhai wa baada ya kifo? Katika namna moja au nyingine, karibu kila dini hufundisha dhanio hilo. Kama vile kisemavyo Mankind’s Search for God (ukurasa wa 52): “Katika kumtafuta-tafuta Mungu, binadamu ametegemea vitegemeo ba-ndia, kwa kukosa kuelewa lile wazo la kutokufa. . . . Imani katika nafsi isiyokufa au namna zayo mbalimbali ni urithi ambao umetufikia sisi kwa kupokezwa muda wa zile mileani.” Maswali mengine ni haya: Je! kuna mahali kama moto wa helo ambako nafsi huteswa-teswa? Ni nini tumaini la kweli kwa ajili ya watu? Je! kuna Mungu mmoja, au kuna miungu mingi?—Mwanzo 2:7; Ezekieli 18:4.

Msingi wa Kuwa na Mafunzo ya Biblia

Kwa utaratibu ulio kama orodha ya matukio kulingana na jinsi yalivyotokea katika tamasha ya ulimwengu, kitabu chazungumza juu ya ukuzi wa zile dini kubwa-kubwa za ainabinadamu—Uhindu, Ubuddha, Utao, Ukonfyushasi, Ushinto, Uyuda, Ukristo, Jumuiya ya Wakristo, na Uislamu. Katika kila sura vile vitabu vitakatifu vya dini hizo vyanukuliwa ili mwamini yeyote mwenye moyo mweupe aweze kuchunguza manukuu hayo yeye mwenyewe. Kwa ajili ya sura ihusuyo Uislamu, tafsiri tofauti tatu za Kiingereza za Korani zimetumiwa. Tafsiri iliyo ya karibuni zaidi ya Jewish Publication Society ya Tanakh—A New Translation of the Holy Scriptures imenukuliwa katika ile sura juu ya Uyuda.—Linganisha Matendo 17:28; Tito 1:12.

Kuna nini kwa ajili ya asiyeamini kuna Mungu na aaminiye kwamba ya Mungu hayajulikani? Sura ya 14 yashughulika na kutoamini kwa siku hizi katika Mungu na kwa nini Mashahidi wa Yehova wajua kwamba Mungu yuko. Katika kila sura, msomaji aelekezwa kwenye Biblia. Hivyo, kwa kutumia kichapo hiki, Mankind’s Search for God, tumeandaliwa vizuri zaidi kuanzisha mafunzo ya Biblia pamoja na watu wa kila imani au pamoja na wale wadaio kutokuwa na imani yoyote. Hicho chaitendea kila dini kwa staha na kwa busara, lakini chatokeza maswali yawezayo kuongoza mtu kwa Yehova na kwenye ukweli. Kwa ajili ya wale wanaomtafuta-tafuta Mungu kwa bidii ya moyoni, kitabu hiki kitakuwa baraka kweli kweli.—Zaburi 83:18; Yohana 8:31, 32; 2 Timotheo 3:16, 17.

Masanduku ya kufunza yenye maagizo yametiwa katika kila sura. Kwa kielelezo, katika kurasa 226 na 227, kuna sanduku juu ya “Uyuda—Dini Yenye Sauti Nyingi” ambalo laeleza migawanyiko mikubwa ipatikanayo katika ima-ni ya Kiyahudi. Chini ya “Uhindu—Kutafuta-tafuta Ukombozi,” kuna sanduku katika kurasa 116 na 117, “Uhindu—Miungu Fulani na Miungu-Wake.” Hili latoa orodha ya michache tu ya ile miungu zaidi ya milioni 330 iabudiwayo na Wahindu. Je! Wabuddha huamini katika Mungu kwa jinsi ulimwengu wa Magharibi ulielewavyo neno hilo? Sanduku “Ubuddha na Mungu” katika ukurasa wa 145 lajibu swali hilo. Pia kitabu hicho kina faharisi yenye kutumika kwa marejezo ya haraka kwenye vichwa vikuu. Orodha ya vyanzo vikuu vya madondoo vilivyotumiwa katika utafiti ni msingi pia wa usomaji zaidi ikiwa mtu ataka habari zaidi.

Kitabu hiki kina picha na vielezi zaidi ya 200, lakini hazimo humo kwa mapambo tu. Kila kielezi kina jambo la kufunza ambalo huelewesha zaidi dini yenye kuzungumzwa. Kwa mfano, katika ukurasa wa 238 kuna mfululizo wa picha zionyeshazo mingine ya mifano ya maneno ambayo Yesu alifundisha. Mahali pengine, pana mfululizo wa picha tano ambazo pia zaonyesha pande tofauti za huduma ya Kristo—miujiza yake, mgeuko wake wa sura, kifo chake cha dhabihu, na kutuma wanafunzi wake wakahubiri katika ulimwengu wote.

Katika ukurasa 289 kuna mfuatano wa foto ambazo zitapendeza Waislamu. Champeleka mtazamaji ndani ya Meka, ndani ya lile hekalu kubwa ambamo Kaaba imo halafu kwenye lile jiwe halisi jeusi ambalo Waislamu huheshimu mno. Ibada ya Ubuddha iliyo ya namna mbalimbali imeonyeshwa kwa picha katika ukurasa wa 157. Wahindu watapendezwa kuona picha za miungu yao maarufu Ganesa na Krishna katika kurasa 96 na 117.

Wahudumu Wakristo wenye kustahili kotekote ulimwenguni waliombwa ushauri ili kupata mfikio maalumu kuhusu kila dini kubwa. Kwa mfano, habari zenye thamani kubwa zilitoka Israeli kwa ajili ya zile sura zenye kuhusu Uyuda na imani ya Baha’i. Mashahidi katika nchi za Kiislamu walichunguza kwa uangalifu yaliyomo katika ile sura ihusuyo Uislamu. Maoni asilia yenye mafaa yalitoka India juu ya Wahindu, Wasiki (Wakalasinga), na Wajeni. Wahudumu katika Mashariki walihakikisha kwamba ile sura ihusuyo Ushinto ilikuwa sahihi, na pia wakatoa ushauri juu ya Ubuddha, Utao, na Ukonfyushasi.

Kwa sababu ya mazungumzo ya uangalifu ya kitabu hicho kuhusu kila dini, wale walio nacho katika lugha yao wataweza kuanza mafunzo ya Biblia katika sura ifaayo malezi ya kidini ya kila mtu. Halafu huenda wakataka kuhamia sura nyingine inayoshughulika na kutokea kwa Ukristo wa mapema na sababu za kuamini kwamba Kristo ndiye Mwakilishi wa kweli wa Mungu, yule aliyetumiwa kuvuta ainabinadamu kuelekea Mungu. Kuna sura zielezazo jinsi uasi-imani ulivyotokea, ukatokeza migawanyiko na yale mafarakano mengi ya Jumuiya ya Wakristo. Sura mbili za mwisho zaonyesha jinsi ibada ya kweli imerudishwa katika siku za mwisho hizi na yale yangojayo Babuloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini bandia ya Shetani, kwenye wakati ujao ulio karibu. Baada ya hapo, ulimwengu mpya na tumaini la Biblia la ufufuo ni mambo yakaziwayo.—Yohana 5:28, 29; 12:44-46; 14:6; Ufunuo 21:1-4.

Kwa kweli hiki ni kichapo kipasacho kusaidia wengi kotekote ulimwenguni wamkaribie Mungu, kama vile Yakobo alivyosema katika sura ya 4 ya barua yake, mstari wa 8: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.” Ndiyo, kama vile Isaya asemavyo: “Mtafuteni BWANA [Yehova, NW], maadamu anapatikana, mwiteni, maadamu yu karibu.”—Isaya 55:6; Yohana 6:44, 65.

Acheni sisi sote tuendelee kugeukia upande ufaao, kuelekea Bwana Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote mzima, Yehova Mungu. Na kwa msaada wa kichapo hiki, Mankind’s Search for God, acheni tusaidie maelfu zaidi wamwabudu Yehova “katika roho na kweli.” (Yohana 4:23, 24) Na tudumu katika kuwatafuta watafutaji wa ukweli na kuwaeleza juu ya Mungu wa kweli, kwa maana, kwa kweli, yeye aweza kupatikana!

[Maelezo ya Chini]

a “Mtao” hutamkwa m-dao; msikiko wa matamshi wakaribiana na nao.

[Picha katika ukurasa wa 17]

Binadamu amemtafuta Mungu katika njia nyingi

[Picha]

Wakatoliki wenye moyo mweupe hugeukia Mariamu

[Picha]

Wahindu huheshimu mno ule mto Ganges

[Hisani]

Harry Burdich, Transglobe Agency, Hamburg

[Picha]

Wayahudi fulani wenye kujitoa sana huzivaa hirizi zenye vifungu vya maandiko

[Hisani]

GPO, Jerusalem

[Picha]

Wanaume Waislamu huhiji kwenda

Meka

[Hisani]

Camerapix

[Picha]

Wengi humpa Buddha heshima ya ibada

[Picha katika ukurasa wa 18]

Yesu alitumia mifano ya maneno kusaidia watu wampate Mungu wa kweli

[Hisani]

Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.

[Hisani]

Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.

[Hisani]

Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki