Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/92 uku. 1
  • Uhitaji wa Ainabinadamu wa Kutafuta-Tafuta Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uhitaji wa Ainabinadamu wa Kutafuta-Tafuta Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Utangulizi wa Kitabu Mankind’s Search for God
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Jitihada Ya Ainabinadamu Kutafuta-tafuta Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kutolea Ushahidi “Watu wa Namna Zote”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Itikio kwa ”Mankind’s Search for God”
    Amkeni!—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 6/92 uku. 1

Uhitaji wa Ainabinadamu wa Kutafuta-Tafuta Mungu

1 Katika karne hii ya 20, wengi sana wamekuwa wakihama kwa sababu ya vita, uonevu, na misongo ya kiuchumi. Na kwa kuwa usafiri na uwasiliano ni mwepesi zaidi, ulimwengu unaonekana kana kwamba unaendelea kuwa mdogo. Hilo limefanya vikundi mbalimbali vya kidini kuwa karibu-karibu. Hivyo, mara nyingi dini inazungumzwa sana katika habari kuwa inaathiri maisha za watu kila mahali.

2 Kazi yetu ya kuhubiri imeathiriwa pia. Si jambo lisilo la kawaida tena kuwapata watu wa dini tusizozijua.

3 Ili kutusaidia tuwe na uelewevu mzuri zaidi wa dini nyinginezo na historia yazo, tumeandaliwa kitabu Mankind’s Search for God. Kinajibu mamia ya maswali kuhusu itikadi za msingi za dini kubwa za ulimwengu. Katika mwezi Juni tutatumia kitabu hiki hudumani. Ni habari zipi tunazoweza kukazia katika kitabu hicho chenye msaada wa thamani ili kuwatia moyo wale walio na moyo mweupe wajifunze zaidi kuhusu Mungu?

4 Swali moja la msingi ambalo limeshughulikiwa katika kitabu chote ni: Je! mwanadamu ana nafsi isiyoweza kufa inayoendelea kuishi baada ya kifo chake na kuendelea kuwapo katika maisha ya baada ya kifo? Kwa namna moja au nyingine, karibu kila dini hufundisha fundisho hilo. Maswali mengine yanayojibiwa katika kitabu hicho ni: Je! kuna mahali pa mateso ambapo nafsi huteswa? Ni nini tumaini la kweli la wafu? Je! kuna Mungu mmoja, au kuna miungu mingi? Fikira zaweza kuelekezwa kwenye maswali yaliyo katika kurasa 17-18 za kitabu hicho. Hata tunapoongea na mtu asiyeamini kuwako kwa Mungu au mwagnosti (anayeamini kwamba ya Mungu hayajulikani), maswali ya 4 na 5 yaweza kuvuta fikira zake na labda yatokeze mazungumzo ya maana.

5 Ainabinadamu yote inahitaji kutafuta-tafuta Mungu na kujitahidi kupata kibali chake sasa. Matukio ya ulimwengu yanaonyesha kwamba Har–Magedoni inazidi kukaribia kwa kasi. Huu ni wakati wa utendaji wenye bidii. Ni pendeleo lililoje tulilo nalo la kuwahimiza wengine wamtafute Yehova sasa, wakati angali aweza kupatikana! (Isa. 55:6, 7) Kitabu Mankind’s Search for God kinasaidiaje watu katika kutafuta-tafuta kwao Mungu? Kinaandaa habari zenye kuchochea fikira kwa watu wa malezi mbalimbali. Kwa mfano, fungu la 26 katika ukurasa 297 linawaeleza Waislamu kwamba Ukristo wa kweli haufundishi fundisho la Utatu. Ona jinsi fungu la 43 katika ukurasa 229 linavyoweza kuchochea kupendezwa kwa Wayahudi kuhusiana na utumizi wa jina la Mungu.

6 Tuna kila sababu ya kuwa wenye idili tunapotoa kitabu hicho. Ikiwa tunajua vizuri yale yaliyomo ndani yacho, tutapata fursa za kuamsha kupendezwa kwa watu wenye mioyo myeupe wa dini mbalimbali. Na tuonyeshe bidii katika utumishi huo.

7 Yehova ni Mungu mwenye ukarimu na rehema. Mwaliko wake wa kujifunza juu yake ni wenye fadhili jinsi gani! Huenda kukawa na wengi zaidi watakaokuwa wenye kumsifu Yehova. Wakati wa Juni, kwa msaada wa kitabu Mankind’s Search for God, tutaweza kusaidia wengi katika Jumuiya ya Wakristo pamoja na wale walio na malezi yasiyo ya Kikristo au ya kutomcha Mungu waanze kumwabudu Yehova “katika roho na kweli.” (Yn. 4:23, 24) Na tuendelee kwa bidii kuwatafuta watafutaji kweli na kuimarisha uhusiano wao na Mungu wa kweli. Yeye aweza kupatikana!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki