Kuchukua Furushi Letu Wenyewe la Daraka
1 Wazo la kuwa na daraka huonekana kuwa mzigo kwa watu leo. Wengi hujaribu kuepa daraka. Tokeo ni kwamba, waume huwaacha wake zao, mama huwatupa watoto wao, vijana huacha shule, na raia huepa kulipa kodi. Orodha ya matendo ya kuepa daraka ni ndefu sana. Mtu mwenye kuchukua daraka ni yule mwenye kutumainika, anayetaka na anayeweza kutoa jibu kwa mwenendo wake. Kwa hiyo, Neno la Mungu husema wazi kuhusu Wakristo kwamba “kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.” (Gal. 6:5) Jinsi inavyofaa kwamba kichwa cha kusanyiko letu la mzunguko la mwaka wa utumishi 1992 ni “Kuchukua Furushi Letu Wenyewe la Daraka”! Mfululizo huo utaanza Julai. Sisi sote twapaswa tufanye mipango hususa ya kuhudhuria.
2 Kupitia hotuba, miigizo, maonyesho, yaliyoonwa, na mahoji, programu hiyo ya kusanyiko la mzunguko itaonyesha wazi madaraka mbalimbali ambayo sisi sote tunayo tukiwa Wakristo. Jumamosi alasiri, hotuba yenye mfululizo wa sehemu nne itatolewa nayo itaeleza jinsi sisi sote tunavyoweza kushughulikia madaraka yetu kwa furaha. Vijana wetu wana daraka la kuchukua, na hotuba ya Jumamosi alasiri itakayotolewa na mwangalizi wa mzunguko itaelekezwa kwao hasa. Jumamosi kutakuwa pia na fursa ya wale waliojiweka wakfu karibuni kuweza kubatizwa. Wote wanaopangia kubatizwa kwenye kusanyiko la mzunguko wamjulishe mwangalizi msimamizi mapema vya kutosha ili kwamba matayarisho yafanywe kwa ajili ya ubatizo.
3 Jumapili asubuhi hotuba nyingine yenye mfululizo wa sehemu nne itakazia daraka letu la Kikristo la kuhubiri. Halafu, Jumapili alasiri, hotuba ya watu wote yenye kichwa “Ulimwengu Mpya wa Mungu—Ni Nani Atastahili Kuingia?” itatolewa na mwangalizi wa wilaya. Uwe macho kualika wapya wote wanaopendezwa wasikie hotuba hiyo.
4 Sisi sote na tupange mambo yetu ili tuwe miongoni mwa wale watakaohudhuria na kunufaika kikamili kutokana na programu hiyo nzuri ya siku mbili. Mwangalizi wa mzunguko wenu atawajulisha juu ya mahali na tarehe zilizopangiwa kundi lenu.