Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
1 Kuanzia 1996, kichwa cha makusanyiko ya mzunguko kitakuwa “Sikiliza na Ujifunze Kutenda Neno la Mungu.” Kichwa hicho kinachotegemea Kumbukumbu la Torati 31:12, 13, huandaa msingi ufaao kwa programu nzima ili kukazia masomo tunayohitaji kujifunza na kutumia.
2 Ingawa leo watu walio wengi husikiliza mafundisho yaliyopuliziwa yenye kuongoza vibaya, kuna uhitaji muhimu kwa kila mmoja wetu kusikiliza Neno la Mungu na kujifunza kulitenda. (Luka 11:28; 1 Tim. 4:1) Tukiwa na jambo hili akilini, programu ya kusanyiko la mzunguko imekusudiwa kuandaa kitia-moyo na msaada kwa wahubiri, familia, wazee na mapainia. Jumamosi, kutakuwa na mfululizo wenye sehemu nne juu ya habari “Kukabiliana na Matatizo Yetu—Kwa Kusikiliza Neno la Mungu.” Na Jumapili asubuhi, kutakuwa na mfululizo wenye kichwa “Jinsi Maandiko Yanavyotutia Nidhamu kwa Uadilifu.” Programu nzima itatoa kitia-moyo cha kiroho ambacho wewe na familia yako hampaswi kukosa.
3 Siku zote mbili Jumamosi na Jumapili, madokezo yenye kutumika ya huduma ya shambani yatatolewa na kufanywa maonyesho. Mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo na yenye kufundisha yatatolewa pia. Hivyo, kwa kuwapo na kusikiliza ukiwa na nia ya kutumia unayojifunza, utaweza ifaavyo kuzitekeleza kikamili amri za Neno la Mungu.
4 Mojawapo mambo makuu ya kusanyiko la mzunguko litakuwa ubatizo wa ndugu na dada waliojiweka wakfu hivi karibuni. Basi kabla ya tangazo la peupe la wakfu wao, wataka-kubatizwa wapaswa kumwambia mwangalizi-msimamizi tamaa yao ya ubatizo ili apange wazee wakutane nao.
5 Hotuba ya watu wote ya huu mfululizo wa kusanyiko la mzunguko ina kichwa “Kwa Nini Uongozwe na Biblia?” Alika watu wenye kupendezwa wahudhurie. Kwa kutarajia kitia-moyo kingi kinachohitajika sana na msaada ambao wewe na familia yako mtapokea, fanya mipango dhahiri mwepo katika programu nzima.